Wastaafu - Je ni halali wananchi wabebe mzigo wa kutunza viongozi wabadhirifu??

Morani75

JF-Expert Member
Mar 1, 2007
613
19
Heshima kwa wanaJambo wenzangu. Nimekuwa nikifuatilia hili swala la serikali (through jasho la wananchi) kuendelea kuwatunza viongozi waliostaafu. Sina shida na wale waliostaafu sababu hata jeshini hawa wanatunzwa pia. Lakini nina hoja ambayo ningeomba kama wanaJambo watu wenye uchungu wa nchi na jasho la wananchi (ambao ndio sisi) tuijadili,

Hoja yenyewe ni:

"Je kiongozi aliyejiuzulu kutokana na kashfa inayohusishwa na rushwa, ni halali kuendelea kulipwa mafao na kupata huduma zote yeye na familia yake kwa maisha yao yote kwa gharama za wananchi ambao walidhulimiwa mali zao na kiongozi husika??"

Tukiwa katika hilo pia tunagalie pande zote, upande wa kwanza ni uraiani (ambapo sheria ya matunzo haiongelei kuhusu wale viongozi waliojuiuzulu kutokana na ubadhirifu) na upande wa pili ni kwenye jeshi ambapo ingaw viongozi wastaafu wanatunzwa na jeshi lakini wale waliokuwa "Dishonourably discharged" sidhani kama wanapata maslahi na matunzo kama wenzao!

Ka ajili ya kujua gharama za matunzo hayo, naomba tuangalie kwenye hii ThisDay ya leo kwa kubofya hapa chini:
http://www.thisday.co.tz/News/3511.html

Naomba kuwakilisha.......
 
Back
Top Bottom