Lah! Masatu umetokea wapi tena? Sijakusoma kwa muda mrefu sana nikadhani labda ulisweka kunakohusika; si unaijua tena nchi yetu. well karibu tena JF.
Swali lako: ninataka kuprove kuwa (a) Wasira Massato (somo yako) amechoka sana. Yeye alidai vijana ni wavuta bangi, lakini inaelekea kuwa yeye ndiye anayezidiwa zaidi na madawa ya mafua. (b) Alifanya makosa kulishambulia gazeti la mwananchi lilipotoa picha yake akiwa amelala, kwani kumbe hiyo ni ada yake.
Port nipo ila mbio za kukimbiza shilingi zimezidi muda unakuwa hautoshi.
Back to Wassira, vigezo unavyotumia kumhukumu Wassira sio sahihi, kusinzia (sio kulala) ni involuntary action sio lazima iwe inatokana na uzee, ni maumbile tu hata vijana husinzia/hulala.
Wassiira ni miongoni mwa mawaziri wachache katika baraza la JK walio watendaji mahili.
Kuzidiwa na dawa za mafua hakuna uhusiano na uzee, na zaidi hilo halimnyimi haki ya kukemea vitendo vibaya vya kuvuta bangi.