Wassira: Dk Slaa Si Msafi!

Wassira aliwahi kukamatwa mbugani Serengeti pale Saronera baada magemu kudhania SOKWE kavalishwa nguo anatoroshwa, dereva wake alipata wakati mgumu sana. Mpaka jioni ndo magemu wakajua sio sokwe ni Wasira.
Huyu mzee kummaliza ni kuiweka hadharani ile picha yake ya usingizini bungeni na kuja na ajenda ya msichague mlalaji mwingine.
Huyu mzee alipopigwa chini na Mrema pale nccr alichoka mbaya akawa anatembelea baiskeli huku akiwa na suruali mbili tu. Kaja kuokolewa na JK kwa kuwa wote walikuwa na bifu na Nyerere na Warioba
 
Wassira ni vuvuzela wa magamba tuu,maana wanamwamin kwa uropokaj.yuko arumeru kulinda kitumbua chake na vipaumbele vyake ni;
1.usingiz na kutokuwa na muda wa kujenga hoja hata kama issue ni sensitive kwa maslah ya taifa chini ya wizara yake.
2.uropokaji na upayukaji usio na maana wala evidence yakinifu kisayansi.
3.kudandia mahouse girl wake pamoja na vimwana wengine out,kisa aonekane handsome kumbe ni zinjanthropus, gorrila & chimpanzee.
4.yuko kwa magamba kwa kuwa ananyonya la sivyo angekua upinzani. maana kuna muda aliasi ccm na kwenda upinzan lakin baada ya kuahidiwa keki aliamua kurudi kuvaa magamba. nb. hivyo ni mtu msaliti asiyekuwa na msimamo na anauwezo wa kuwasalit magamba endapo hawatampa kitumbua.
5.awaambie wananchi wa arumeru watawafanyia nini endapo watawachagua na si kuleta porojo zake zisizo na mantiki.
6.kwamba wanunua shahada za wananchi ni wao magamba na si chadema, hivyo anyooshe maelezo ni kwa jinsi gani watanunua na kuiba hizo shahada pamoja na kuiba kura za wananchi watakaomchagua nassari,mgombea ubunge wa chadema.
 
ok kweli amenena.na alipoacha upadri mbona ccm mlimpokea kwa mikono miwili?au mlitaka awape gawio?nadhani tukimtangaza vizuri wasira nje ya nchi watalii watafurika nchini.apelekwe makumbusho ya taifa
 
Duh!!! Slaa mpaka leo ana mchumba tu. Jizee la miaka sitini na kuendelea! Kweli Watanzania mna mambo. Si aoe tu. Bado wanaendelea na zinaa?

Kua na mchumba ina athiri nini utendaji wake?je na huyo anaezaa zaa hovyo kama panya?hv haujui pia huyo Wassira anaishi kiuchumba na mama Ndege aliyekuaga N.d.c!ni nini kilichopelekea kumuacha mkewe wa ndoa na kumrukia mama Ndege?
 
Wasira yasije yakakutokea piano mama mkapa ukalalamika. Haipendezi kuropoka vitu ambavyo havijengi.
 
Kua na mchumba ina athiri nini utendaji wake?je na huyo anaezaa zaa hovyo kama panya?hv haujui pia huyo Wassira anaishi kiuchumba na mama Ndege aliyekuaga N.d.c!ni nini kilichopelekea kumuacha mkewe wa ndoa na kumrukia mama Ndege?

Uchumba na mke wa mtu?
 
Mzee wa kulala angemalizia tu kuwa Dr slaa si Msafi kuliko huyu Mkwe mgombea!! labda angeeleweka. sasa anaposema si msafi mbona hamalizii si msafi kuliko nani?
 
kwani ufisadi wa CCM unawanyima usingizi CHADEMA? cha msingi jibu hoja ili kama Dr. ambaye nami nampenda na kumkubali kama kiongozi mwadilifu tujue madhaifu yake na kama vipi ashauriwe vizuri ili asichafue tulipofikia
Dr kama angekuwa amefukuzwa na kanisa katoliki ninalolijua mimi basi madhambi yake yangeanikwa hadharani badala yake anapewa sapoti ya kutosha sana.Mwenye kumbukumbu arejee mazungumzo ya iliyokuwa TvT zamani katika kipindi cha Wako Wapi? aone docta alieleza nini alipoulizwa kuwa kwanini alitoka kanisani na je uhusiano wake na kanisa upoje kwa sasa?Atapata majibu yote.
 
wassira mtaalam wa kulaka bungeni amekurupuka wapi? Mwambie atuwekee ushahidi la sivyo itakuwa majungu.com

nafahamu wengi hamtapenda lakini ndivyo dunia ilivyo ukimwaga ugali watu wanamwaga mboga lakini katika viongozi wa sasa wa vyama vyote vikuu hakuna aliyekuwa msafi tofauti ni kwamba kundi fulani liko jikoni la kundi lingine liko sebuleni waliko jikoni wananafasi kubwa ya kula msosi wanavyotaka lakini ikitokea nafasi ya kundi lililoko sebuleni kuingia jikoni tatizo litakuwa lile lile kwani nao si wasafi ebu soma hii stori ya katibu mkuu wa magwanda akiwa na umri wa miaka sitini na tisa akini bado ana mchumba:....

Kashfa ya katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema),Dk Willibrod Slaa imewekwa hadharani kwamba kiongozi huyo alifukuzwa upadri baada ya kutafuna mamilioni ya fedha zilizochangwa kwa ajili ya ujio wa hapa nchini wa Kiongozi wa Kanisa katoliki nchi duniani papa katika miaka ya tisini

Tuhuma hizo zimemwagwa na Waziri Steven Wassira katika mikutano ya kampeni za ccm kumnadi mgombea wa chama hicho sioi Solomon sumari katika Jimbo la Arumeru mashariuki

tuhuma hizo zinakuja wakati vyama hivyo viwili vikubwa nchini vikirusiana vijembe na makombora mazito mazito

kashfa hiyo imetolewa katika vijiji vya kata Kikwe katika Jimbo hilo la Arumeru Mshariki Mkoani Arusha.

Wassira alisema kwamba Dk Slaa ambaye pia aliwahi kuwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu nchini(TEC) kabla ya kukumbwa na kashfa hizo za kutafuna mamilioni hayo ya fedha zilizochangwa na waumini wa katoliki kutoka vigango na parokia mbalimbali nchini ili kufaniisha ujio wa Papa miaka ya tisini kitendo kilichopelekea kufukuzwa kazi ya upadri.

amesisitizas kwamba kiongozi huyo hana kifua cha kupambana na ufisadi kwa kuwa hata yeye alitafuna fedha za kanisa.

Aliwataka wakazi wa kata ya Kikwe kumuuliza Dk Slaa chanzo cha kufukuzwa upadri pindi atakapotia mguu ndani ya kata yao na kuwataka wakazi hao kutosikiliza sera za kiongozi huyo kwa kuwa si msafi wa kujipambanua kwamba anapambana na ufisadi nchini.

Alimtuhumu Dk Slaa Pia katika hatua nyingine anatuhumiwa kumfukuza kazi mhasibu wa chama hicho ngazi ya taifa kwa kosa la kukataa kutekeleza maagizo yake amlipe shilingi milioni 10 mchumba wake,Josephine Mushumbushi kitendo kinachotia mashaka ya uadilifu wa kiongozi huyo.

Hata hivyo,alishangaa kitendo cha Dk Slaa kuishi maisha ya uchumba wakati akiwa na umri wa miaka zaidi ya 60 na kudai kitendo hicho kinashangaza umma wa watanzania pamoja na wafuasi wa vyama vya siasa nchini.

Wakati huo huo,Wassira ambaye pia ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM alisema kwamba mgombea ubunge wa Chadema,Joshua Nassari hafai kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa kuwa ni kijana mkorofi na mara kwa mara baba yake mzazi amekuwa akimsihi kuachana na ukorofi tangu wakati akiwa chuo kikuu cha Dar es salaam.

Alisema kwamba baba wa mgombea huyo ambaye ni kiongozi wa dini amekuwa akimsihi kuachana na ukorofi ikiwa ni pamoja na kuoa ili aweze kutulia lakini cha ajabu Nassari amekuwa akionekana na bibi wa kizungu mwenye umri wa zaidi ya miaka 60 akizunguka naye mitaani.

Wassira amewataka wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanatunza shada zao ili kuepuka kuporwa na wafuasi wa chadema

Amesema tayari chama cha chadema kimeanza mchezo mchafu kwa kusambaza waraka pamoja na vijana kwa ajili ya kununua shahada
 
Mnyama wa msitu wa gombe katuingiza mkenge, kapiga dili wamechota mihela kupitia KAULI MBIU kirimo kwanza, wameshirikiana na wafanyabiashara kupiga dili la power tiller. wameshakomba hela nowadays kelele za kilimo kwanza/power tiller wameachiwa vyombo vya habari, wanacalculate jinsi ya kuzitia kibindoni fasta chenji ya rada. pamoja na mambo mengine rekodi zinaonyesha wassira ni mgomvi.
 
Huyu mzee naona aliongea baada ya kutoka usingizini ambao ni kawaida yake...Kanisa Katoliki siyo NGO kama anavyotaka kutuaminisha na wala upadre si cheo ndani ya Kanisa kama anavyotaka tuamini...Kanisa lina taratibu zake za kushughulikia matatizo yake...na moja ya mambo ambayo hayawezi kumuondolea mtu sakramenti ya upadre ni pamoja na huo ubadhirifu anaoutaja Wasira..Vinginevyo pasingelikuwa na Sakramenti ya Kitubio ndani ya Kanisa Katoliki...Watu wanaiba(Kuvunja amri ya 7) na wanatubu na kuondolewa dhambi hiyo na tena mwenye mamlaka hayo ni Padre mwenyewe...Sitaki kuingia kwa undani zaidi...ila huyu mzee hajui anachokiogea na wala hana uelewa wowote juu ya mfumo mzima wa Kanisa Katoliki na yeye anajielewa na ndiyo maana kayatamuka haya kijijini amabako wananchi uwezo wao wa kuelewa mambo ni mdogo.Ila ningewashauri viongozi wa CCM wakaachana na chokochoko za udini...Imagine ikitokea sasa Kanisa Katoliki Likakanusha tuhuma hizo dhidi ya SLAA na kutoa ufafanuzi tofauti huyo mzee ataficha wapi sura yake?Au ndiyo wataanza tena malalamiko yao ya CDM chama cha Kikatoliki?....Viongozi wa CCM tumieni busara zaidi kusaka si njia yoyote ile...nyingine zingine athari zake zina kuwa ni hasi kwa jamii au makundi mbalimbali ya kijamii.
 
Atuambie kwanini alifukuzwa upadri. Kama uongo anayosema Wasira ampeleke mahakamani, anangoja nini?

Kwa hiyo ishu ya mkaahapa kuhusu baba wa taifa asipoenda mahakamani kumshtaki dogo steve basi ni kweli? ww Ribo usiwe kama robot. Pima tuhuma hizi na athari zake kwa jamii usiendekeze siasa za matope
 
Kua na mchumba ina athiri nini utendaji wake?je na huyo anaezaa zaa hovyo kama panya?hv haujui pia huyo Wassira anaishi kiuchumba na mama Ndege aliyekuaga N.d.c!ni nini kilichopelekea kumuacha mkewe wa ndoa na kumrukia mama Ndege?

Maadili ya mtu mzima? Kiongozi hutakiwi kuwa na hawara na kuzaa nje ya ndoa hususan kwa mwenye dini.
 
Print picha yake kuuuuuubwa aliyolala mjengoni...peleka pale kijiji...hapo utakuwa umemaliza kila kitu.
 
Kwa hiyo ishu ya mkaahapa kuhusu baba wa taifa asipoenda mahakamani kumshtaki dogo steve basi ni kweli? ww Ribo usiwe kama robot. Pima tuhuma hizi na athari zake kwa jamii usiendekeze siasa za matope

Mkapa hajakosea, Steve babake sio Juliasi.

Slaa aseme kwanini kafukuzwa upadri?
 
binafsi ziwez poteza mda kumjadili sokwe like wasira mzee wa vibinti vidogo vodogo. shame on him.....
 
Hata kama ingekuwa hayo alosema yote kweli! Yanawasaidiaje Arumeru? Ukizoa porini lazima ya mjini yakushinde
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom