Waandishi Wetu, Dodoma| Mwananchi | 19, Juni 2012
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Esther Bulaya, juzi walizozana katika kile kinachoonekana kuwa ni kuwania madaraka katika Jimbo la Bunda mkoani Mara, katika uchaguzi mkuu 2015.
Sakata hilo lilitokea nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao juzi usiku, ambapo Wassira alimfuata Bulaya na kumhoji kwamba kwanini alitoa maneno ya kuipinga bajeti ya Serikali.
Wassira ambaye pia ni Mbunge wa Bunda (CCM) alimwambia Bulaya: "Mimi ndiye Mbunge wa Bunda, wewe huwezi kujifanya ndiye uliyetumwa na wananchi kuja kusema maneno ya uwongo hapa, eti unaipinga bajeti ya Serikali, ni nani aliyekutuma?"
Waziri huyo alikwenda mbali na kumwambia mbunge huyo kijana kwamba, "wewe tunakufahamu una pande mbili (upinzani na CCM) na kila siku unashirikiana na Halima Mdee (Kawe-Chadema), tunakujua kwamba uko CCM na Chadema."
Kutokana na kauli hizo, Bulaya alijibu mapigo akimwambia Wassira kwamba yeye akiwa mbunge wa CCM ana wajibu wa kukikosoa chama chake na hakuwa mtu wa kwanza kukataa kuunga mkono bajeti hadi hapo marekebisho yatakapokuwa yamefanywa.
"Mimi nina haki ya kuzungumza ndani ya Bunge na kusema kile ninachokiamini kama mbunge, wala hakuna mtu wa kuniwekea mipaka. Halafu kama ni uhusiano na wabunge wengine mbona wabunge wengi tu wa CCM wanashirikiana na upinzani?" alihoji Bulaya.
Wakati hayo yakiendelea Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na mbunge mwingine wa Viti Maalum (CCM), Rosemary Kirigini walikuwa wakishuhudia.
Nahodha alitumia dakika chache kumsihi Bulaya kutojibu mashambulizi ya Wassira.
Msingi wa mvutano
Msingi wa mvutano huo ni mchango wa Bulaya alipochangia hotuba ya bajeti ya Serikali na kuhoji sababu ya kutotengwa kwa fedha za kuwalipa fidia wananchi wa Bunda waliohama katika maeneo yao kupisha utekelezaji wa mradi wa maeneo maalum ya uwekezaji (EPZ).
"Nitahitaji majibu sahihi katika hili, kwani wananchi wa Bunda wamenituma na bila majibu sina haja ya kuunga mkono hoja," alisema Bulaya.
Mbali na suala hilo, mbunge huyo pia aliiponda bajeti ya Serikali kwamba haina jipya kutokana na kushindwa kuandaliwa kwa vipaumbele, ambavyo vitasaidia maendeleo ya Watanzania, badala yake bajeti hiyo, bado imetenga fedha nyingi kwa matumizi ya kawaida, imeendeleza misamaha ya kodi na kukuwa kwa deni la Taifa.
Akichangia hotuba ya bajeti ya Serikali, Bulaya alisema bado hajaridhishwa na serikali kutenga fedha nyingi katika matumizi ya kawaida na kwenda kinyume na mpango wa serikali wa miaka mitano ambao ulieleza wazi fedha za maendeleo zitaongezeka walau kwa asilimia 35 kila mwaka.
Mbunge huyo alisema ni lazima Serikali iwe na vipaumbele vichache ili iweze kutekeleza kwa fedha za ndani, kuliko kuwa na vipambele vingi ambavyo haviwezi kutekelezeka.
Bulaya alisema pia inahitajika mchanganuo wa deni la Taifa kwani bado linaongezeka mwaka hadi mwaka na sasa limefikia trilioni 20.
Alisema pia inashangaza wakati fedha za maendeleo zinapunguzwa matumizi mengineyo katika wizara yameongezeka hadi kufikia 583 fedha ambazo ni nyingi sana.
"Haiwezekani zikatengwa Sh583 bilioni kwa ajili ya kula katika wizara, wakati miundombinu muhimu kama Reli ya Kati inahitaji zaidi ya Sh1.3 trilioni kuboreshwa na wizara nzima imepangiwa trilioni 3.8," alisema Bulaya na kuongeza:
"Nina mhurumia sana Waziri wa Uchukuzi, Dk Mwakyembe (Harrison) kwani hawezi kutekeleza mipango yake kwa bajeti hii," alisema.
Mgogoro wahamia bungeni
Katika kile kinachoonekaka kwamba ni mvutano wa kisiasa baina ya Wassira na Bulaya, suala lao liliibuka kwa sura nyingine katika kipindi cha maswali na majibu jana asubuhi.
Bulaya aliuliza swali kuhusu wananchi 164 katika Wilaya ya Bunda waliosubiri kulipwa fidia kwa ajili ya kupisha utekelezaji wa mradi wa maeneo maalum ya uwekeza (EPZ).
Katika majibu yake, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Gregory Teu alisema wananchi hao watalipwa fedha zao mwezi ujao.
Akijibu swali la nyongeza la Bulaya, Teu alisema, "napenda kumpongeza Mbunge wa Bunda, Mheshimiwa Wassira kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia suala hili, kwa kweli amekuwa akifuatilia sana ili kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanalipwa."
Kauli yake hiyo ilizua miguno na minong'ono ya chinichini kwa baadhi ya wabunge, wakiashiria kile kinachoonekana ni vita baina ya Wassira na Bulaya.
Kuhusu mchakato wa malipo hayo, Teu alisema malipo ya fidia yalilipwa kwa awamu mbili kupitia akaunti ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ambapo mwaka 2009 jumla ya Sh1 bilioni zililipwa kama awamu ya kwanza kwa hundi kutoka EPZ.
"Awamu ya pili ya malipo ya Sh100 milioni ililipwa mwaka 2010 kwa hundi namba 6064316 kutoka EPZ, hadi sasa katika awamu hizo mbili, jumla ya watu 116 wameshalipwa,'' alisema Teu.
Naibu Waziri alisema fedha zilizobaki, Sh 1,042,852,910, tayari zimetengwa na hazina na inatarajiwa kulipwa Julai 2012 kwa wahusika 164 waliobakia, ili kukamilisha idadi ya watu 280 waliostahili kulipwa.
Alisema mwaka 2007, wizara kupitia Mamlaka ya EPZ na kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ilitenga eneo la hekta 2,316 katika kijiji cha Tairo Bunda ikijumuisha vitongoji vitatu kwa ajili ya uwekezaji wa EPZ.
Teu alibainisha kuwa katika mpango huo, jumla ya Sh3.4 bilioni zilihitajika ili kulipa wananchi wanaomiliki maeneo hayo, lakini kutokana na gharama kuwa kubwa EPZ kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara walikubaliana kupunguza na kubakiza kitongoji kimoja cha Kirumi.
Hata hivyo, Naibu Waziri alisema kuwa malipo yatayotolewa katika kipidni cha sasa, yatakuwa katika bei ya soko la sasa, na kwamba serikali imekwisha wa kuangalia namna ya kufidia deni hilo.
Habari hii imeandaliwa na Neville Meena, Mussa Juma na Habeli Chidawali
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Esther Bulaya, juzi walizozana katika kile kinachoonekana kuwa ni kuwania madaraka katika Jimbo la Bunda mkoani Mara, katika uchaguzi mkuu 2015.
Sakata hilo lilitokea nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao juzi usiku, ambapo Wassira alimfuata Bulaya na kumhoji kwamba kwanini alitoa maneno ya kuipinga bajeti ya Serikali.
Wassira ambaye pia ni Mbunge wa Bunda (CCM) alimwambia Bulaya: "Mimi ndiye Mbunge wa Bunda, wewe huwezi kujifanya ndiye uliyetumwa na wananchi kuja kusema maneno ya uwongo hapa, eti unaipinga bajeti ya Serikali, ni nani aliyekutuma?"
Waziri huyo alikwenda mbali na kumwambia mbunge huyo kijana kwamba, "wewe tunakufahamu una pande mbili (upinzani na CCM) na kila siku unashirikiana na Halima Mdee (Kawe-Chadema), tunakujua kwamba uko CCM na Chadema."
Kutokana na kauli hizo, Bulaya alijibu mapigo akimwambia Wassira kwamba yeye akiwa mbunge wa CCM ana wajibu wa kukikosoa chama chake na hakuwa mtu wa kwanza kukataa kuunga mkono bajeti hadi hapo marekebisho yatakapokuwa yamefanywa.
"Mimi nina haki ya kuzungumza ndani ya Bunge na kusema kile ninachokiamini kama mbunge, wala hakuna mtu wa kuniwekea mipaka. Halafu kama ni uhusiano na wabunge wengine mbona wabunge wengi tu wa CCM wanashirikiana na upinzani?" alihoji Bulaya.
Wakati hayo yakiendelea Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na mbunge mwingine wa Viti Maalum (CCM), Rosemary Kirigini walikuwa wakishuhudia.
Nahodha alitumia dakika chache kumsihi Bulaya kutojibu mashambulizi ya Wassira.
Msingi wa mvutano
Msingi wa mvutano huo ni mchango wa Bulaya alipochangia hotuba ya bajeti ya Serikali na kuhoji sababu ya kutotengwa kwa fedha za kuwalipa fidia wananchi wa Bunda waliohama katika maeneo yao kupisha utekelezaji wa mradi wa maeneo maalum ya uwekezaji (EPZ).
"Nitahitaji majibu sahihi katika hili, kwani wananchi wa Bunda wamenituma na bila majibu sina haja ya kuunga mkono hoja," alisema Bulaya.
Mbali na suala hilo, mbunge huyo pia aliiponda bajeti ya Serikali kwamba haina jipya kutokana na kushindwa kuandaliwa kwa vipaumbele, ambavyo vitasaidia maendeleo ya Watanzania, badala yake bajeti hiyo, bado imetenga fedha nyingi kwa matumizi ya kawaida, imeendeleza misamaha ya kodi na kukuwa kwa deni la Taifa.
Akichangia hotuba ya bajeti ya Serikali, Bulaya alisema bado hajaridhishwa na serikali kutenga fedha nyingi katika matumizi ya kawaida na kwenda kinyume na mpango wa serikali wa miaka mitano ambao ulieleza wazi fedha za maendeleo zitaongezeka walau kwa asilimia 35 kila mwaka.
Mbunge huyo alisema ni lazima Serikali iwe na vipaumbele vichache ili iweze kutekeleza kwa fedha za ndani, kuliko kuwa na vipambele vingi ambavyo haviwezi kutekelezeka.
Bulaya alisema pia inahitajika mchanganuo wa deni la Taifa kwani bado linaongezeka mwaka hadi mwaka na sasa limefikia trilioni 20.
Alisema pia inashangaza wakati fedha za maendeleo zinapunguzwa matumizi mengineyo katika wizara yameongezeka hadi kufikia 583 fedha ambazo ni nyingi sana.
"Haiwezekani zikatengwa Sh583 bilioni kwa ajili ya kula katika wizara, wakati miundombinu muhimu kama Reli ya Kati inahitaji zaidi ya Sh1.3 trilioni kuboreshwa na wizara nzima imepangiwa trilioni 3.8," alisema Bulaya na kuongeza:
"Nina mhurumia sana Waziri wa Uchukuzi, Dk Mwakyembe (Harrison) kwani hawezi kutekeleza mipango yake kwa bajeti hii," alisema.
Mgogoro wahamia bungeni
Katika kile kinachoonekaka kwamba ni mvutano wa kisiasa baina ya Wassira na Bulaya, suala lao liliibuka kwa sura nyingine katika kipindi cha maswali na majibu jana asubuhi.
Bulaya aliuliza swali kuhusu wananchi 164 katika Wilaya ya Bunda waliosubiri kulipwa fidia kwa ajili ya kupisha utekelezaji wa mradi wa maeneo maalum ya uwekeza (EPZ).
Katika majibu yake, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Gregory Teu alisema wananchi hao watalipwa fedha zao mwezi ujao.
Akijibu swali la nyongeza la Bulaya, Teu alisema, "napenda kumpongeza Mbunge wa Bunda, Mheshimiwa Wassira kwa jinsi ambavyo amekuwa akifuatilia suala hili, kwa kweli amekuwa akifuatilia sana ili kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanalipwa."
Kauli yake hiyo ilizua miguno na minong'ono ya chinichini kwa baadhi ya wabunge, wakiashiria kile kinachoonekana ni vita baina ya Wassira na Bulaya.
Kuhusu mchakato wa malipo hayo, Teu alisema malipo ya fidia yalilipwa kwa awamu mbili kupitia akaunti ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ambapo mwaka 2009 jumla ya Sh1 bilioni zililipwa kama awamu ya kwanza kwa hundi kutoka EPZ.
"Awamu ya pili ya malipo ya Sh100 milioni ililipwa mwaka 2010 kwa hundi namba 6064316 kutoka EPZ, hadi sasa katika awamu hizo mbili, jumla ya watu 116 wameshalipwa,'' alisema Teu.
Naibu Waziri alisema fedha zilizobaki, Sh 1,042,852,910, tayari zimetengwa na hazina na inatarajiwa kulipwa Julai 2012 kwa wahusika 164 waliobakia, ili kukamilisha idadi ya watu 280 waliostahili kulipwa.
Alisema mwaka 2007, wizara kupitia Mamlaka ya EPZ na kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, ilitenga eneo la hekta 2,316 katika kijiji cha Tairo Bunda ikijumuisha vitongoji vitatu kwa ajili ya uwekezaji wa EPZ.
Teu alibainisha kuwa katika mpango huo, jumla ya Sh3.4 bilioni zilihitajika ili kulipa wananchi wanaomiliki maeneo hayo, lakini kutokana na gharama kuwa kubwa EPZ kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara walikubaliana kupunguza na kubakiza kitongoji kimoja cha Kirumi.
Hata hivyo, Naibu Waziri alisema kuwa malipo yatayotolewa katika kipidni cha sasa, yatakuwa katika bei ya soko la sasa, na kwamba serikali imekwisha wa kuangalia namna ya kufidia deni hilo.
Habari hii imeandaliwa na Neville Meena, Mussa Juma na Habeli Chidawali