Wassira amuunga mkono Lowassa suala la vijana

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797


[h=2][/h]JUMAPILI, SEPTEMBA 16, 2012 08:16 NA MWANDISHI WETU, MEATU

SERIKALI imeunga mkono wazo la Waziri Mkuu (mstaafu), Edaward Lowassa kwa kukiri kuwa endapo hakutakuwa na mkakati thabiti wa kushughulikia tatizo la ajira kwa kundi la vijana kuna hatari kubwa ya kuleta machafuko katika siku zijazo.

Kauli hiyo ilitolewa na juzi wilayani Meatu na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu Stephen Wassira alipozungumza na viongozi wa wilaya hiyo ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake mkoani Simiyu.

Wassira alitoa matamshi hayo huku kukiwa na kauli kadhaa ambazo zimekuwa zikitolewa na Lowassa kuwa tatizo la ajira kwa vijana ni sawa na bomu.

Akizungumza na viongozi wa Meatu mbele ya wajumbe wa kamati ya ulinzi wakiongozwa na Mwenyekiti wake Rossemary Kirigini, Wassira alisema tatizo la ajira kwa kundi la vijana ni kubwa na linatishia amani hivi sasa.

“Asilimia 60 ya Watanzania ni vijana na hawana ajira hivi unategemea nini ndiyo maana wakiambiwa kuna maandamano wao hawaulizi maandamano hayo ni ya nini wanachouliza yanaanzia wapi.

“Hatuwezi kuwa taifa huku kundi kubwa la watu ambao ni vijana halina kazi hivyo kama viongozi lazima sasa tuchukue hatua mbalimbali kwa kutumia fursa tulizo nazo tuhakikishe tunapambana na changamoto hii,” alisema Wassira.

Kwa sababu hiyo alitaka kupitia Tasaf awamu ya tatu pamoja na kulenga kuwezesha familia masikini kwa ajili ya kuwaongezea kipato kupambana na umasikini.

Pia alishauri halmashauri nchini kote zihakikishe zinahamasisha uundwaji wa vikundi vya vijana vya uzalishaji mali ambavyo vitawezeshwa ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na changamoto hiyo.

Alisema serikali imechukua hatua mbalimbali ambazo zitawezesha kukabiliana na tatizo hilo la ajira kwa vijana hasa kwa kutumia mkakati wa Kilimo Kwanza.

Kwa mkakati huo vijana kujiunga katika vikundi watawezeshwa kupata zana za kisasa za kilimo kumudu kulima kisasa na kuzalisha kwa tija na kupata kipato kwa ajili ya kupambana na umasikini.

 
Hii ni Sera ambayo Umoja wa VIJANA wa CCM; Wangepaswa kuiweka kuwa ndio HOJA yao KUU katika UCHAGUZI wa

VIONGOZI WAPYA kukiwakilisha ndani ya NEC ya CCM; Lakini Inaoyesha tokea PRINCE ajiingize HOJA yao KUU NI

KUKISHUTUMU CHADEMA kwa KUUA; Nani WATAUNGA MKONO URAIS 2015 zaidi ya JINSI ya kusaidia VIJANA wengi

WASIO NA AJIRA NCHINI; Wangepinga MPANGO wa kuruhusu WAKENYA kupata VIBALI rahisi VYA KAZI ili kuchukua KAZI

ZA VIJANA WASOMI WA CCM... WANGEPATA KURA NZURI KWA KUINUFAISHA CCM...
 
Mwenye macho yoyote anaweza kuona hali ilivyo ktk nchi hii. Ukianzia huduma za jamii, elimu, afya, nk. Hali ni ovyo ovyo ukilinganisha na ahadi zilizotolewa na wanasiasa; hivyo haihitajiki ubashiri wowote ule, kinachohitajika ni 'man in action to deal with the situation'.
Waziri kutangaza tatizo badala ya mikakati ya kutatua tatizo ni tatizo zaidi ya tatizo lenyewe ambalo jamii inakabiliana nalo. Alomteua atafakari!
 
shua wassira ameongea neno employment opportunities must be created ili angalau ibaki asilimia chache ya unemployed ila kwa sasa noma
 
Wasira ni upepo - kwani alikuwa halijui hilo hadi lowassa kaliongelea aliuwa wapi ukizingati kuwa bado ana cheo kikubwa mno ndani ya serikali ya sasa.
sasa aunge mkono na hili la pili kwamba elimu kwanza badala ya kilimo kwanza ambacho Lowassa kasema ni kuwahadaa wananchi mchana kweupe.

Badala ya kutatua matatizo ya wananchi yeye muda mwingi anawaza CDM wanaandamana wapi na wamefungua matawi mangapi hili ndiyo tatizo la watendaji wengi wa serikali yetu - Hongera Lowassa uwapasha live.
 
Hii ni Sera ambayo Umoja wa VIJANA wa CCM; Wangepaswa kuiweka kuwa ndio HOJA yao KUU katika UCHAGUZI wa

VIONGOZI WAPYA kukiwakilisha ndani ya NEC ya CCM; Lakini Inaoyesha tokea PRINCE ajiingize HOJA yao KUU NI

KUKISHUTUMU CHADEMA kwa KUUA; Nani WATAUNGA MKONO URAIS 2015 zaidi ya JINSI ya kusaidia VIJANA wengi

WASIO NA AJIRA NCHINI; Wangepinga MPANGO wa kuruhusu WAKENYA kupata VIBALI rahisi VYA KAZI ili kuchukua KAZI

ZA VIJANA WASOMI WA CCM... WANGEPATA KURA NZURI KWA KUINUFAISHA CCM...

I SALUTE U nguu
 
attachment.php


Mh. Wassira
 
Back
Top Bottom