Wasomi wamrushia JK kombola; aache ulalamishi...

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
JK achochea moto


*Wasomi, wanasiasa wasema naye amegeuka kuwa mlalamikaji
*Wadai angeeleza serikali itakavyokabili genge la wahuni


Tumaini Makene na Grace Michael

HOTUBA ya Rais Jakaya Kikwete ya kuadhimisha miaka 34 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi imechochea moto na
mijadala nchini, huku kauli kuwa hakuna uharaka wa kuilipa Kampuni ya Dowans sh. bilioni 94 ikiibua maswali zaidi kuliko majibu.

Wasomi na wasiasa waliozungumza na Majira jana walisema Rais Kikwete ameungana na wananchi wa kawaida na kuwa mlalamikaji, badala ya kutoa mwongozo wa nini cha kufanya kuondokana na suala hilo na kueleza jinsi ya kulikabili 'genge la wahuni wanaotafubna rasilimali za nchi na kuteka mamlaka ya taifa'.

Miongoni mwa waliozungumaia hotuba hiyo, ni Mhadhiri Msaidizi Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Chuo Kikuu Dar es Salaam, Bw. Bashiru Ally alisema kuwa hotuba ya rais ilipaswa kujikita katika kuzungumzia masuala yanayolikabili taifa kwa upana wake, kwani Dowans ni dalili tu ya tatizo kubwa nchini.

Alisema mathalani badala ya kuzungumzia Dowans, kwani kama alivyokiri mwenyewe tayari ilishazungumziwa na wasaidizi wake, rais alipaswa kuliambia taifa kupitia sherehe hizo za CCM, kuwa serikali yake itakabiliana vipi na genge la watu wachache walioteka mamlaka za nchi.

Alisema kuwa hotuba ya juzi ya kutimiza miaka 34 ya CCM ilipaswa kujikita katika kuangalia malengo makuu ya chama hicho kikongwe, masuala ya itikadi, sera na mwelekeo wa taifa, badala ya kuangalia maslahi ya muda mfupi kama vile kushinda uchaguzi, kila baada ya miaka mitano.

"Kwangu mimi issue si kulipa au kuilipa Dowans, Dowans ni dalili ya ugonjwa mzito unaolikabili taifa...ugonjwa wa kutowajibika, kikundi cha watu wachache kujilimbikizia mali, mfumo wa sheria kutofanya kazi, tatizo la kuuza na kununua kura, watu wanachukua posho zinazozidi mishahara yao.

"Hivyo hotuba ya jana (juzi) ilijikita zaidi katika kuangalia ushindi wa hali ya uchaguzi, msukosuko ambao CCM inapata kutoka kwa wapinzani kwenye uwanja wa CCM, kuwatia moyo wana-CCM na suala la kufanya mageuzi ndani ya chama...hivyo kulikuwa na imbalance (hakukuwa na uwiano sawa) na mambo mengine ya mtazamo mpana juu ya mweleko wa taifa.

"Hata ukisema chama kinafanya mageuzi, unajiuliza mageuzi kutoka wapi, CCM imepita katika vipindi mbalimbali, malengo makuu ya CCM zamani haikuwa kushinda uchaguzi, ilikuwa ni kujenga taifa huru, lenye usawa na heshima kwa watu, uzalendo, maadili. Taifa ambalo lilikuwa linazungumzia juu majirani na Bara la Afrika zima kwa ujumla.

"Kuna changamoto ya kuangalia masuala ya itikadi, sera na mwelekeo wa taifa, chama si mashine ya kutafutia kura, ni uongozi, na uongozi ni dira...masuala ya kushinda uchaguzi ni malengo ya muda mfupi sana, hakuna dira ya miaka mitano, la sivyo CCM nacho kitakuwa kimetumbukia katika mtazamo finyu," alisema Bw. Ally.

"Kwa kweli badala ya kuzungumzia Dowans tu kwa sababu Pinda na Chiligati walishasema kama alivyosema, basi rais alipaswa kuzungumzia bigger picture (mtazamo mpana) si smaller picture, juu ya matatizo yetu, angetuhakikishia namna gani serikali yake imejipanga katika mapambano dhidi ya ufisadi.

"Itapambanaje na genge la wahuni wanaotumia fursa zao za kiuchumi kuteka mamlaka ya nchi...ufisadi unaoangamiza sekta karibu zote, energy (nishati), ardhi, huduma za jamii, mfumo wa utawala, ufujaji wa rasrimali za umma," alisema Bw. Ally kwa kirefu.

Aliongeza kuwa hotuba hiyo ingeweza kueleza mwelekeo wa taifa katika wakati huu ambapo makatibu wakuu au wakurugenzi wa idara, wanajitwalia fedha na marupurupu mengi, huku wakitembelea magari ya kifahari, wakati wanafunzi vyuoni na shuleni hawana uhakika wa chakula.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), Bw. John Mnyika alisema kuwa Rais Kikwete hawezi kuepuka mzigo wa tuhuma dhidi ya Dowans. Pia anapaswa kuwaeleza Watanzania jinsi serikali ilivyoweza kuingia mkataba na kampuni feki, ambayo hatimaye iliuhamishia kwa mtu mwingine.

"Rais hapaswi kulalamika kama anavyolalamika mwananchi wa kawaida...Katika hotuba ya jana, Rais Kikwete kakiri mwenyewe kuwa Richmond ilikuwa kampuni feki, yeye mwenyewe anasema kuwa alikuwa ameishtukia, sasa ilikuwaje kampuni hiyo ikaendelea kufanya kazi na hata ikaweza kuhamisha mkataba wake kwenda Dowans.

"Ilikuwaje serikali yenye vyombo vyenye mamlaka...vyombo vya dola vilivyokuwa na taarifa kuwa Richmond ni kampuni feki, ziliruhusu kampuni hiyo iingie mkataba na serikali, kisha vyombo hivyo vikaruhusu kampuni hiyo feki ikahamisha mkataba kwenda kampuni nyingine...atuambie iwapo uhamishaji wa mkataba huo ulipitia katika baraza la mawaziri, ambalo yeye ni mwenyekiti wake.

"Lakini pia Rais Kikwete anapaswa kutuambia ni lini hasa mkataba ulihamishwa kwenda Dowans, tarehe ngapi na mwezi gani...na upande wa pili wa serikali (TANESCO) walipewa taarifa na kuridhia lini. Maana katika mkataba wa Richmond na TANESCO ilikubaliwa kuwa mkataba huo hauwezi kuhamishwa kwenda kampuni nyingine bila makubaliano ya pande hizo mbili.

"Lakini kulingana na taarifa zilizopo kutoka vyanzo mbalimbali zinaonesha kuwa Richmond na Dowans walifikia makubaliano ya kuhamisha mkataba kabla hata upande wa pili wa serikali (TANESCO) haujaridhia suala hilo...sasa rais atuambie ni lini mkataba ulihamishiwa Dowans na lini TANESCO waliridhia kuhamishwa kwa mkataba huo.

"Kwa sababu kuhamisha mkataba wa Richmond na TANESCO kwenda kwa mtu mwingine bila pande hizo mbili kukubaliana kama ilivyokubaliwa katika mkataba, kisheria ni batili...sasa ilikuwaje mamlaka zikaruhusu kuhamisha mkataba ambao tayari ulisema lazima kuwe na makubaliano ya pande mbili.

Naye Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David Kafurila amesema kuwa maelezo hayo yameongeza utata, hatua inayolazimu suala hilo kurejeshwa bungeni kujadiliwa upya.

Akizungumza na Majira jana kwa njia ya simu, Bw. Kafurila alisema kuwa hotuba ya rais aliyoitoa akiwa mjini Dodoma katika sherehe za maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imezidi kuongeza utata katika sakata la malipo yanayodaiwa na Dowans.

"Maelezo ya Rais yamezidi kutuonesha kuwa kuna umuhimu sasa wa suala hilo kujadiliwa bungeni...hawezi akatuambia eti hawajui kabisa wamiliki wa Dowans huku akitaka wanasheria waangalie uwezekano wa kupunguza deni hilo au kulikwepa kabisa, wanapunguziana deni na nani huyo ambaye hajulikani? alihoji Bw. Kafurila.

Alizidi kuhoji kuwa inakuwaje Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) asimjulishe rais wamiliki wa kampuni hiyo baada ya kupitia hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC) iliyoitaka TANESCO kulipa fedha hizo, mpaka ifikie hatua Rais anasimama mbele ya maelfu ya Watanzania na kusema kuwa hawajui wamiliki hao.

"Mwanasheria Mkuu baada ya kupitia hukumu alishauri walipwe, na siku chache baadaye Waziri wa Nishati na Madini Bw. Willium Ngeleja alitaja wamiliki wa kampuni hiyo, hivyo tutaaminije kama hao waliotajwa ndio wamiliki halali na wakati Rais anasema hawajui?" alihoji.

Bw. Kafurila alisema kuwa haiwezekani rais aeleze kutowafahamu wamiliki wa Dowans na wakati serikali ilikuwa ikiwalipa fedha wakati wakizalisha umeme hapa nchini.

"Rais ni Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri na tangu Dowans ianze kuzalisha umeme hadi leo ni lazima suala hilo liwe limepitia kwenye Baraza la Mawaziri hivyo hakuona kweli umuhimu wa kuwafahamu wamiliki hao?" alisema.

Kutokana na utata huo, Bw. Kafurila alisema kuwa malipo hayo yalipwe au yasilipwe lakini serikali haiwezi kukwepa kuwajibika katika suala hilo kwa kuwa Watanzania wamengia gharama kubwa ya kujadili jambo hilo huku serikali ikiwa kimya lakini pia kutumia gharama kuwalipa mawakili na kuendesha kesi hiyo.

Alizidi kuihoji Serikali kuwa imeshindwaje katika kesi hiyo na kampuni ambayo hata wamiliki wake hawajulikani lakini mbali na kutojulikana kampuni hiyo ni feki na yenye mkataba batili.

"Serikali katika hili haiwezi ikajitoa kwenye kitanzi hiki ni lazima iwajibike kwa namna yoyote kwani suala hili limechukua muda wetu mwingi katika kulijadili badala ya kushughulikia mambo mengine," alisema Bw. Kafurila.

 
Kikwete aamsha hasira za wabaya wa Dowans Sunday, 06 February 2011 22:30

MBOWE, KAFULILA WAMSHANGAA KUTOFAHAU WAMILIKI WA KAMPUNI HIYO
Boniface Meena naRaymond Kaminyoge
HOTUBA ya Rais Jakaya Kikwete imeibua mjadala mpana baada ya baadhi ya wanasiasa, wasomi na wanaharakati kumpongeza huku wengine wakimkosoa kutokana na kile walichokiita ni kauli yake tata ya kutowafahamu wamiliki wa Dowans na kutaka aitishe kikao cha Baraza la Mawaziri na kutangaza kutoilipa kampuni hiyo tata.

Juzi akizungumza na wana-CCM wakati wa maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe Afrika, pamoja na kuelezea mlolongo mrefu kuanzia Richmond aliyoiita "Phantom Company,' Rais Kikwete aliweka bayana, "Sina hisa Dowans, wala wamiliki wake siwajui na hawajawahi kuniita kwasababu hawanihitaji."

Hata hivyo, msimamo huo wa Rais kujivua tuhuma hizo za kuwa mmoja wa wamiliki wa Dowans zilizoelekezwa kwake na Dk Willibrod Slaa, bado haujamnasua baada ya mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kushangaa kauli hiyo wakati Serikali ya Awamu ya Nne ndiyo iliyoingia mkataba na kampuni hiyo.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, alifafanua kwamba kitendo hicho cha Rais Kikwete ni hadaa kwa wananchi akifikiri wanataka kujua uhusiano wake na wamiliki hao.

"Ni kazi ngumu sana kulinda uongo, Rais anasahau kwa jinsi gani Richmond na Dowans zilivyoisumbua Serikali yake hivyo kama anasema hajui basi hafai kuwa Rais wa nchi,"aliweka bayana Mbowe.

Mbowe alisisitiza kwamba, Rais wa nchi si mtu anayepaswa kulalamika bali ni mtu wa kuchukua hatua.

"Ni aibu kwake kunung'unika badala ya kuchukua hatua, ni lazima ajue anapozungumza kwenye vikao vya CCM ajue bado ni Rais wa nchi,"alisema Mbowe.

Kuhusu onyo la Rais kuhusu wanaochochea migomo na maandamano kwa kudai kile alichokiita madaraka waliyokosa kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, Mbowe alisema mkuu huyo wa nchi aache madai hayo akimtaka atambue kila mtu ana haki ya kudai kile anachoona ni haki yake.

Mwenyekiti huyo wa Chadema aliongeza kwamba, kuandamana ni haki ya watu hivyo kama Rais hataki kuwepo kwa maandamano afute haki hiyo ili wananchi wajue haipo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kituo cha Taarifa kwa Wananchi (TCID), Deus Kibamba alisema kauli aliyoitoa Rais Kikwete juzi ilikuwa ni maoni yake binafsi.

"Tunataka Rais Kikwete aitishe kikao cha Baraza la Mawaziri, ili kitoe msimamo mmoja wa Serikali wa kukataa kuilipa kampuni ya Dowans," alisema.

Alisema kauli ya Rais kwamba, ni mmoja kati ya watu wanaotaka Tanesco isiilipe kampuni ya Dowans, ilikuwa ni maoni yake binafsi.

"Tunataka msimamo wa Serikali, tunataka uamuzi wa Baraza la Mawaziri, mawaziri wamepingana kuhusu Dowans kwa sababu hakuna kikao kilichowahi kufanyika,"alirejea kauli na msimamo huo uliowahi kutolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.

Kibamba alifafanua kwamba, baada ya kikao hicho, ndipo mawaziri na wanasheria wanatakiwa kuweka mikakati ya namna wanavyoweza kuinusuru nchi na ulipaji wa fidia hiyo.

Tayari kauli ya Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa na kusimamia Serikali kuwaadhibu waliohusika Richmond na kisha kuvunja mkataba wa Dowans, inapingana na msimamo wa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliyetangaza kwamba, Serikali lazima iilipe kampuni ya Dowans fidia ya Sh 94 milioni.

Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG) Frederick Werema, naye aliangukia katika kundi hilo la Ngeleja akisema deni hilo halikwepeki kauli ambayo ilipingwa si tu na Sitta, bali pia Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe huku wanaharakati kwa upande wao wakifungua kesi Mahakama Kuu kutaka shauri hili litolewe uamuzi nchini na kuanisha hoja 16 za kwanini kampuni hiyo isilipwe.

Kafulila adai JK hawajui Dowans, Ngeleja anawajua

Kwa upande wa mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

"Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,"alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.

Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.

"Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua," alisema Kafulila na kuongeza:

Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?

Alisema katika sakata hili ataendelea kupigana hadi ijulikane nani amefikisha taifa katika hali hii. "Serikali ilipe isilipe ni lazima iwajibike maana hoja ya msingi hapa tumefikishwaje hapa hadi kushindwa kesi," alihoji Kafulila

Mwanasheria maarufu, Profesa Abdallah Safari alisema Serikali inazidi kuwachanganya wananchi kwa namna vigogo wanavyotofautiana kuhusu suala hilo.

"Rais kuwa upande wa wanaopinga kuilipa kampuni hiyo ni jambo jema, lakini inasikitisha kuona mawaziri wanapingana hadharani, hakuna msimamo wa pamoja, Baraza la Mawaziri likae ili kutoa msimamo wa Serikali.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema ni jambo la busara kutafuta njia mbalimbali za kisheria ili fidia hiyo isilipwe.

"Kuna mambo mawili ya kuangalia tunapojadili suala hili..., ni vizuri tukitafuta njia za kutuokoa kulipa fedha hizi, lakini tukumbuke tukishindwa tutatozwa fedha zaidi ambazo ni asilimia 7.5,"alisema.

Kuanzia siku hukumu ilivyotoka, faini ya Dowans imeongezeka hadi kufikia Sh97 bilioni kutokana na riba ya Sh20milioni kwa siku.


Mkataba wa Dowans na Tanesco ulivunjwa Agosti 31 mwaka juzi, baada ya Bunge kuagiza uvunjwe baada ya kuibuka sakata la Kampuni ya kufua umeme ya Richmond mwaka 2008, l ililomfanya Edward Lowassa kujiuzulu Uwaziri Mkuu na Baraza la Mawaziri likavunjwa.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Comments




0 #11 nelson kaserwa 2011-02-07 08:00 sina la zaidi ila wanaccm mnajionea wenyewe kwa jinsi gani kanga na kofia na fulana zenu zilizomchagua raisi wetu mtukufu mpendwa dr.jk
Quote









0 #10 sauti ya umma 2011-02-07 07:30 mbona kikwete unajikaanga kwa mafuta yako mwenyewe achia ngazi mapema maana siku zinavyoendelea unazidi kudhihirisha huna nia nzuri kwa watanzani na unakaribia kutamka wazi kuwa wewe ndio mmiliki wa dowans.
Quote









+1 #9 Zinga 2011-02-07 07:28 Mh. Rais Kikwete. Mpendwa wetu na chaguo la Mungu wetu. Nimesikitishwa sana na kauli zako. Inabidi utuombe samahani watanzania kwani inajulikana wazi kabisa kwamba umetudanganya. Mpendwa Rais, Chaguo la Mungu wa kweli alisemi uongo hivyo udanganyifu huu unanifanya niamini kuwa wewe ni chaguo la Mungu wa Kuzimu. Mpendwa Rais, kwa kutimiza matakwa ya Mungu wako umeamua kuipeleka Tanzania yote kuzimu bila kujali kuwa bado tupo watanzania wachache tunao mtii na kumcha Mungu wa kweli. Tafadhali tusikie ugeuke ili uponye nafsi yako na zetu pia. DOWANS unawajua!!
Quote









0 #8 yusuf 2011-02-07 07:21 Rais wetu hiyo Dowans hawezi kuikwepa.Hebu jaribu hili zoezi dogo,piga namba yako ya simu kwenye hiyo hiyo simu,halafu sikiliza kama itaita.Kikwete hawezi kujipigia mwenyewe,ndiyo haijui Dowans.Kanuni ya kawaida ya kinga ya mwili ni kwamba hiyo kinga haiwezi kupingana na mwili ambamo hiyo kinga imo.Dowans ni ya ikulu,kwa hiyo ikulu haiwezi kujipinga yenyewe.
Quote









+1 #7 Mwanaweja 2011-02-07 06:34 ukweli utabakia hapalele maana kauli za jk,ngereja, warema, zinakinzana.je, tz tumwamini na nani? cha ajabu sana naomba kumuuliza jk maswali yafuatayo
1.alipokuwa anaomba kura alihandaa wananchi au alijua hatunaakili?
2. CC ilipokuwa ina kaa yeye alikuwa mwenyekiti kwa hiyo hakujua mmiliki halali wa Richmond/Dowans na kuanzia kusainiwa yeye kama mkuu wa nchi hajui mmiliki wake je walikujaje tz bila yeye kujua basi naamini yeye ndiye Dowans
3.utueleze unajihuzuru lini maana umesha sema hauwezi kuendeleza wala kututoa hapo tulipo kwenda sehemu nyingine kimaendeleo maana uwezo wako wa kufikiria umefikia mwisho.
4. nakutaka usijilinganishe na watangulizi wako Nyerere, mzee wa ruksa, mkapa hawakutoa malighafi yetu kwenda nje kama wewe unavyo tuibia bila huruma
5. je lini tutajitegemea kila siku unajisifu kupewa misaada ndio kusema watanzania wote ni akina matonya? hao wanakupatia misaada ndio hao wanasababisha kuendelea sisi kuwa maskini.
mwisho naomba tu usome nyakati maana kila siku hadhi yako inashuka tena kwa kasi kubwa chunga hao washauri wako maana ninamashaka na bongo zao wanakushauri uongo na wala siukweli nchi iliko.

Quote









0 #6 daniel shirima 2011-02-07 05:30 ninashindwa kuamini nilichokisoma kama kweli kimetolewa na RAIS wa nchi, hivi alitamka mwenyewe haya kwa kinywa chake au kuna mtu alitamka kwa niaba yake? Kwa namana yeyote ile kama ametamkiwa au ametamka mwenyewe amejidhalilisha na kuidhalilisha nafasi hiyo kubwa kuliko zote katika utawala wa nchi. Ni vema rais akumbuke hata akiwa kuwa rais ni rais tu haijlishi yuko kwene sherehe ya harusi, kwene sherehe ya chama, kwene, msiba au kwene ukumbi wa burudani. Taunataka tamko rasmi kuhusu dowans na siyo hoja za kukinzana kutoka kwa waziri huyu na yule.
Quote









+1 #5 Ralp J. Kimbisa 2011-02-07 03:31 Kamati kuu ya CCM ambayo Kikwete ndiye mwenyekiti wake ilikwishasema DOWANS walipwe. Waziri wake wa madini na mwanasheria wake mkuu walikwisharidhi a malipo hayo. Baraza lake la mawaziri lilikwishagawan yika kwa sababu ya Dowans. Ni mazingaombwe gani haya! Ama kweli rais wa Tanzania!
Quote









+2 #4 paka shume 2011-02-07 02:11 Tuna rais ambaye uwezo wake wa kuelewa mambo nimdogo sana na alikurupukia tu kazi ya urai hakujua ugmu wake sasa anantapatapa tu anaonekana tu kwenye misiba akiingia tu ofisini cha kwanza kuuliza leo nani kafa
Quote









+2 #3 laggosa mwamba 2011-02-07 02:09 JK ANAWADANGANYA WADANGANYIKA,RA IS WA NCHI KUDAI KWAMBA HAWAJUI WAMILIKI WA DOWNS NI UONGO WA MCHANA KWEUPE.SASA KAMA HAWAJUI KWANINI WAZIRI WAKE NA MWANASHERIA MKUU,PAMOJA NA CHAMA CHAKE WAMESEMA DOWNS ILIPWE..HIVI CC ILIPOKUWA INAKUTANA NA KUFIKIA UAMUZI WA KULIPA DOWNS NANI ALIKUWA MWENYEKITI? MWONGO HUSAHAU HARAKA.JK YOU ARE TRYING TO CONFUSE PEOPLE SO THAT YOU CAN GET FAVOR DON'T EXPECT THAT.
Quote









+1 #2 msemakweli 2011-02-07 01:51 "Huyu ndiye kiwete wa CCM ambaye walisema ni chaguo la mungu. Anauwezo mdogo saaaaana kiuongozi. Jamani nchi inaangamia.Hatuna rais tena. Mungu tusaidie.
Quote









+2 #1 Najaribu 2011-02-07 01:24 Huyu ndiye Rais wa nchi ya Tanzania. JK huwajui wamiliki wa Dowans? Ngeleja anafanya kazi aliyotumwa na nani basi kama si wewe? Mbona yeye anawahamu? Jamani, tumefika hapo? Tuna Rais kweli? Rais asiyefahamu nchi inakwenda wapi? Rais ambaye hahitaji kuwafahamu wamiliki wa kampuni inayosadikiwa kuiibiwa nchi mchana kweupe? Ushauri wa bure - kama JK unashindwa mwenyewe kuondoka Ikulu kwa sababu ya aibu, basi itisha kura ya maoni ili angalau usingizie wananchi walikuondoa.
Quote
 
Kikwete aamsha hasira za wabaya wa Dowans Sunday, 06 February 2011 22:30

MBOWE, KAFULILA WAMSHANGAA KUTOFAHAU WAMILIKI WA KAMPUNI HIYO
Boniface Meena naRaymond Kaminyoge
HOTUBA ya Rais Jakaya Kikwete imeibua mjadala mpana baada ya baadhi ya wanasiasa, wasomi na wanaharakati kumpongeza huku wengine wakimkosoa kutokana na kile walichokiita ni kauli yake tata ya kutowafahamu wamiliki wa Dowans na kutaka aitishe kikao cha Baraza la Mawaziri na kutangaza kutoilipa kampuni hiyo tata.

Juzi akizungumza na wana-CCM wakati wa maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe Afrika, pamoja na kuelezea mlolongo mrefu kuanzia Richmond aliyoiita "Phantom Company,' Rais Kikwete aliweka bayana, "Sina hisa Dowans, wala wamiliki wake siwajui na hawajawahi kuniita kwasababu hawanihitaji."

Hata hivyo, msimamo huo wa Rais kujivua tuhuma hizo za kuwa mmoja wa wamiliki wa Dowans zilizoelekezwa kwake na Dk Willibrod Slaa, bado haujamnasua baada ya mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kushangaa kauli hiyo wakati Serikali ya Awamu ya Nne ndiyo iliyoingia mkataba na kampuni hiyo.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, alifafanua kwamba kitendo hicho cha Rais Kikwete ni hadaa kwa wananchi akifikiri wanataka kujua uhusiano wake na wamiliki hao.

"Ni kazi ngumu sana kulinda uongo, Rais anasahau kwa jinsi gani Richmond na Dowans zilivyoisumbua Serikali yake hivyo kama anasema hajui basi hafai kuwa Rais wa nchi,"aliweka bayana Mbowe.

Mbowe alisisitiza kwamba, Rais wa nchi si mtu anayepaswa kulalamika bali ni mtu wa kuchukua hatua.

"Ni aibu kwake kunung'unika badala ya kuchukua hatua, ni lazima ajue anapozungumza kwenye vikao vya CCM ajue bado ni Rais wa nchi,"alisema Mbowe.

Kuhusu onyo la Rais kuhusu wanaochochea migomo na maandamano kwa kudai kile alichokiita madaraka waliyokosa kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, Mbowe alisema mkuu huyo wa nchi aache madai hayo akimtaka atambue kila mtu ana haki ya kudai kile anachoona ni haki yake.

Mwenyekiti huyo wa Chadema aliongeza kwamba, kuandamana ni haki ya watu hivyo kama Rais hataki kuwepo kwa maandamano afute haki hiyo ili wananchi wajue haipo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kituo cha Taarifa kwa Wananchi (TCID), Deus Kibamba alisema kauli aliyoitoa Rais Kikwete juzi ilikuwa ni maoni yake binafsi.

“Tunataka Rais Kikwete aitishe kikao cha Baraza la Mawaziri, ili kitoe msimamo mmoja wa Serikali wa kukataa kuilipa kampuni ya Dowans,” alisema.

Alisema kauli ya Rais kwamba, ni mmoja kati ya watu wanaotaka Tanesco isiilipe kampuni ya Dowans, ilikuwa ni maoni yake binafsi.

“Tunataka msimamo wa Serikali, tunataka uamuzi wa Baraza la Mawaziri, mawaziri wamepingana kuhusu Dowans kwa sababu hakuna kikao kilichowahi kufanyika,”alirejea kauli na msimamo huo uliowahi kutolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta.

Kibamba alifafanua kwamba, baada ya kikao hicho, ndipo mawaziri na wanasheria wanatakiwa kuweka mikakati ya namna wanavyoweza kuinusuru nchi na ulipaji wa fidia hiyo.

Tayari kauli ya Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa na kusimamia Serikali kuwaadhibu waliohusika Richmond na kisha kuvunja mkataba wa Dowans, inapingana na msimamo wa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliyetangaza kwamba, Serikali lazima iilipe kampuni ya Dowans fidia ya Sh 94 milioni.

Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG) Frederick Werema, naye aliangukia katika kundi hilo la Ngeleja akisema deni hilo halikwepeki kauli ambayo ilipingwa si tu na Sitta, bali pia Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe huku wanaharakati kwa upande wao wakifungua kesi Mahakama Kuu kutaka shauri hili litolewe uamuzi nchini na kuanisha hoja 16 za kwanini kampuni hiyo isilipwe.

Kafulila adai JK hawajui Dowans, Ngeleja anawajua

Kwa upande wa mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

“Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,”alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.

Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.

“Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua,” alisema Kafulila na kuongeza:

Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?

Alisema katika sakata hili ataendelea kupigana hadi ijulikane nani amefikisha taifa katika hali hii. “Serikali ilipe isilipe ni lazima iwajibike maana hoja ya msingi hapa tumefikishwaje hapa hadi kushindwa kesi,” alihoji Kafulila

Mwanasheria maarufu, Profesa Abdallah Safari alisema Serikali inazidi kuwachanganya wananchi kwa namna vigogo wanavyotofautiana kuhusu suala hilo.

“Rais kuwa upande wa wanaopinga kuilipa kampuni hiyo ni jambo jema, lakini inasikitisha kuona mawaziri wanapingana hadharani, hakuna msimamo wa pamoja, Baraza la Mawaziri likae ili kutoa msimamo wa Serikali.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema ni jambo la busara kutafuta njia mbalimbali za kisheria ili fidia hiyo isilipwe.

“Kuna mambo mawili ya kuangalia tunapojadili suala hili..., ni vizuri tukitafuta njia za kutuokoa kulipa fedha hizi, lakini tukumbuke tukishindwa tutatozwa fedha zaidi ambazo ni asilimia 7.5,”alisema.

Kuanzia siku hukumu ilivyotoka, faini ya Dowans imeongezeka hadi kufikia Sh97 bilioni kutokana na riba ya Sh20milioni kwa siku.


Mkataba wa Dowans na Tanesco ulivunjwa Agosti 31 mwaka juzi, baada ya Bunge kuagiza uvunjwe baada ya kuibuka sakata la Kampuni ya kufua umeme ya Richmond mwaka 2008, l ililomfanya Edward Lowassa kujiuzulu Uwaziri Mkuu na Baraza la Mawaziri likavunjwa.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites

Comments




0 #11 nelson kaserwa 2011-02-07 08:00 sina la zaidi ila wanaccm mnajionea wenyewe kwa jinsi gani kanga na kofia na fulana zenu zilizomchagua raisi wetu mtukufu mpendwa dr.jk
Quote









0 #10 sauti ya umma 2011-02-07 07:30 mbona kikwete unajikaanga kwa mafuta yako mwenyewe achia ngazi mapema maana siku zinavyoendelea unazidi kudhihirisha huna nia nzuri kwa watanzani na unakaribia kutamka wazi kuwa wewe ndio mmiliki wa dowans.
Quote









+1 #9 Zinga 2011-02-07 07:28 Mh. Rais Kikwete. Mpendwa wetu na chaguo la Mungu wetu. Nimesikitishwa sana na kauli zako. Inabidi utuombe samahani watanzania kwani inajulikana wazi kabisa kwamba umetudanganya. Mpendwa Rais, Chaguo la Mungu wa kweli alisemi uongo hivyo udanganyifu huu unanifanya niamini kuwa wewe ni chaguo la Mungu wa Kuzimu. Mpendwa Rais, kwa kutimiza matakwa ya Mungu wako umeamua kuipeleka Tanzania yote kuzimu bila kujali kuwa bado tupo watanzania wachache tunao mtii na kumcha Mungu wa kweli. Tafadhali tusikie ugeuke ili uponye nafsi yako na zetu pia. DOWANS unawajua!!
Quote









0 #8 yusuf 2011-02-07 07:21 Rais wetu hiyo Dowans hawezi kuikwepa.Hebu jaribu hili zoezi dogo,piga namba yako ya simu kwenye hiyo hiyo simu,halafu sikiliza kama itaita.Kikwete hawezi kujipigia mwenyewe,ndiyo haijui Dowans.Kanuni ya kawaida ya kinga ya mwili ni kwamba hiyo kinga haiwezi kupingana na mwili ambamo hiyo kinga imo.Dowans ni ya ikulu,kwa hiyo ikulu haiwezi kujipinga yenyewe.
Quote









+1 #7 Mwanaweja 2011-02-07 06:34 ukweli utabakia hapalele maana kauli za jk,ngereja, warema, zinakinzana.je, tz tumwamini na nani? cha ajabu sana naomba kumuuliza jk maswali yafuatayo
1.alipokuwa anaomba kura alihandaa wananchi au alijua hatunaakili?
2. CC ilipokuwa ina kaa yeye alikuwa mwenyekiti kwa hiyo hakujua mmiliki halali wa Richmond/Dowans na kuanzia kusainiwa yeye kama mkuu wa nchi hajui mmiliki wake je walikujaje tz bila yeye kujua basi naamini yeye ndiye Dowans
3.utueleze unajihuzuru lini maana umesha sema hauwezi kuendeleza wala kututoa hapo tulipo kwenda sehemu nyingine kimaendeleo maana uwezo wako wa kufikiria umefikia mwisho.
4. nakutaka usijilinganishe na watangulizi wako Nyerere, mzee wa ruksa, mkapa hawakutoa malighafi yetu kwenda nje kama wewe unavyo tuibia bila huruma
5. je lini tutajitegemea kila siku unajisifu kupewa misaada ndio kusema watanzania wote ni akina matonya? hao wanakupatia misaada ndio hao wanasababisha kuendelea sisi kuwa maskini.
mwisho naomba tu usome nyakati maana kila siku hadhi yako inashuka tena kwa kasi kubwa chunga hao washauri wako maana ninamashaka na bongo zao wanakushauri uongo na wala siukweli nchi iliko.

Quote









0 #6 daniel shirima 2011-02-07 05:30 ninashindwa kuamini nilichokisoma kama kweli kimetolewa na RAIS wa nchi, hivi alitamka mwenyewe haya kwa kinywa chake au kuna mtu alitamka kwa niaba yake? Kwa namana yeyote ile kama ametamkiwa au ametamka mwenyewe amejidhalilisha na kuidhalilisha nafasi hiyo kubwa kuliko zote katika utawala wa nchi. Ni vema rais akumbuke hata akiwa kuwa rais ni rais tu haijlishi yuko kwene sherehe ya harusi, kwene sherehe ya chama, kwene, msiba au kwene ukumbi wa burudani. Taunataka tamko rasmi kuhusu dowans na siyo hoja za kukinzana kutoka kwa waziri huyu na yule.
Quote









+1 #5 Ralp J. Kimbisa 2011-02-07 03:31 Kamati kuu ya CCM ambayo Kikwete ndiye mwenyekiti wake ilikwishasema DOWANS walipwe. Waziri wake wa madini na mwanasheria wake mkuu walikwisharidhi a malipo hayo. Baraza lake la mawaziri lilikwishagawan yika kwa sababu ya Dowans. Ni mazingaombwe gani haya! Ama kweli rais wa Tanzania!
Quote









+2 #4 paka shume 2011-02-07 02:11 Tuna rais ambaye uwezo wake wa kuelewa mambo nimdogo sana na alikurupukia tu kazi ya urai hakujua ugmu wake sasa anantapatapa tu anaonekana tu kwenye misiba akiingia tu ofisini cha kwanza kuuliza leo nani kafa
Quote









+2 #3 laggosa mwamba 2011-02-07 02:09 JK ANAWADANGANYA WADANGANYIKA,RA IS WA NCHI KUDAI KWAMBA HAWAJUI WAMILIKI WA DOWNS NI UONGO WA MCHANA KWEUPE.SASA KAMA HAWAJUI KWANINI WAZIRI WAKE NA MWANASHERIA MKUU,PAMOJA NA CHAMA CHAKE WAMESEMA DOWNS ILIPWE..HIVI CC ILIPOKUWA INAKUTANA NA KUFIKIA UAMUZI WA KULIPA DOWNS NANI ALIKUWA MWENYEKITI? MWONGO HUSAHAU HARAKA.JK YOU ARE TRYING TO CONFUSE PEOPLE SO THAT YOU CAN GET FAVOR DON'T EXPECT THAT.
Quote









+1 #2 msemakweli 2011-02-07 01:51 "Huyu ndiye kiwete wa CCM ambaye walisema ni chaguo la mungu. Anauwezo mdogo saaaaana kiuongozi. Jamani nchi inaangamia.Hatuna rais tena. Mungu tusaidie.
Quote









+2 #1 Najaribu 2011-02-07 01:24 Huyu ndiye Rais wa nchi ya Tanzania. JK huwajui wamiliki wa Dowans? Ngeleja anafanya kazi aliyotumwa na nani basi kama si wewe? Mbona yeye anawahamu? Jamani, tumefika hapo? Tuna Rais kweli? Rais asiyefahamu nchi inakwenda wapi? Rais ambaye hahitaji kuwafahamu wamiliki wa kampuni inayosadikiwa kuiibiwa nchi mchana kweupe? Ushauri wa bure - kama JK unashindwa mwenyewe kuondoka Ikulu kwa sababu ya aibu, basi itisha kura ya maoni ili angalau usingizie wananchi walikuondoa.
Quote
 
JK alifanyia siasa sakata la Dowans
• Akana kuwa na hisa katika kampuni hiyo

na Mwandishi wetu


amka2.gif
RAIS Jakaya Kikwete ameungana na wananchi wanaopinga hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC) inayolitaka Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kuilipa Kampuni ya Dowans fidia ya dola za Marekani milioni 94 kwa kosa la kuvunja mkataba.
Kikwete alitoa kauli hiyo yenye mwelekeo wa kupoza hasira za makundi mbalimbali ya kijamii na kisiasa yanayoendelea kujitokeza kupinga hukumu hiyo ambayo utekelezaji wake unaweza ukaanza siku chache zijazo iwapo juhudi za kuzuia kusajiliwa kwake zitagonga mwamba.
"Nataka kuwahakikishia kuwa na mie ni miongoni mwa wale wasiotaka TANESCO ilipe, hivyo kauli za kuhusika na Dowans zinanishangaza, maana nisingeamua hivyo katika Kamati Kuu na Kamati ya Wabunge wa CCM. Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi," alisema Kikwete.
Awali kabla ya kutoa hitimisho hilo, Kikwete alitoa kauli iliyoonyesha kuielezea Dowans kama kampuni ambayo ilifanikiwa kuleta mitambo ya kuzalisha umeme ambayo baada ya kuwasili nchini ilisaidia kupunguza makali ya tatizo la mgawo wa umeme.
"Baada ya hapo Kampuni ya Richmond ikauza mkataba wake kwa Kampuni ya Dowans ambayo ilileta mitambo na uzalishaji wa umeme ukafanyika na kupunguza kabisa makali ya mgawo," alisema.
Kikwete ambaye alikuwa akihutubia wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema tayari wameshawaelekeza wanasheria kushirikiana na wale wa TANESCO kutafuta namna ya kukwepa kulipa kiasi hicho kikubwa cha fedha.
Alisema uamuzi wake wa kulizungumzia suala hilo la Dowans umekuja baada ya kuwapo kwa watu wengi ambao wamekuwa wakihoji juu ya ukimya wake.
Akizungumzia madai kwamba amekuwa kimya kwa kuwa kampuni hiyo inahusishwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakumtaja, Kikwete alisema hilo lisingeweza likamfanya akashindwa kuchukua hatua.
"Sina ajizi wala kigugumizi cha kuchukua hatua kwa sababu ya rafiki yangu au hata kama angekuwa ndugu yangu kahusika… "Maamuzi yaliyofanywa na Kamati Kuu na Kamati ya Chama ya Wabunge wa CCM yalifanywa chini ya uongozi wangu. Ni uthibitisho tosha wa ukweli huo. Waliokuwepo kwenye vikao hivyo wanajua ukweli wa haya ninayosema. Ningekuwa na masilahi au hofu tusingefanya uamuzi ule," alisema.
Alitumia fursa hiyo kueleza historia ya sakata zima la Dowans kuanzia katika Kampuni ya Richmond ambayo ilishindwa kutimiza mkataba hata kulazimika kuuza.
Pasipo kuingia kwa undani, Kikwete alisema kabla ya mkataba ulioipa ushindi Richmond kupita taratibu za kisheria za ukodishwaji wa mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura zilifuatwa na serikali ikaombwa kugharamia ukodishwaji huo.
Akisimulia kuhusu kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa pasipo kumtaja kwa jina, Rais Kikwete alisema tuhuma zilizoelekezwa kwake kwamba ndiye mwenye kampuni hazikuthibitika.
Alisema Lowassa alilazimika kujiuzulu kwa sababu yeye ndiye aliyetoa kauli ya kukubali Richmond ipewe tenda ili kuepusha nchi isiwe gizani.
Akizungumzia madai ya Katiba mpya, Rais Kikwete alisema mchakato wa kuitazama upya katiba ya sasa ili kuihuisha na kupata kile alichokiita "Katiba mpya", utaanzishwa mwaka huu.
Kwamba hivi sasa matayarisho yanaendelea serikalini ili kupeleka bungeni muswada wa sheria wa kuanzisha mchakato huo, ikijumuisha pia kuundwa kwa tume ya kuongoza mchakato huo.
"Napenda kuwahakikishia wananchi wenzangu kuwa sisi katika serikali na CCM ni miongoni mwa wadau wakubwa wanaotaka Katiba ihuishwe kukidhi mahitaji ya wakati tulionao na matarajio yetu ya baadaye.
"Sisi sote ni wadau wa mabadiliko ya Katiba yetu ya sasa…niwaombe kuwa wakati huo ukifika Wana CCM na wananchi tujitokeze kwa wingi katika kutoa maoni na katika kupiga kura ya maoni itakayoidhinisha Katiba hiyo", alisema.
Hata hivyo, mtindo huo wa kuihuisha au kuiboresha katiba ya sasa tayari umepingwa na wasomi, wanaharakati na wananchi mbalimbali wanaotaka katiba iandikwe upya.
Akizungumzia wimbi la maandamano na migomo inayoendelea nchini, Rais Kikwete alisema hali hiyo inasababishwa na kuwepo kwa mipango ya makusudi ya uvunjifu wa amani kwa kutumia njia hiyo, huku akigusia vurugu zilizotokea jijini Arusha kati ya polisi na wananchi kama mfano wa mipango hiyo aliyodai inasukwa na wanasiasa ili kujitafutia ushindi mwaka 2015.
Hata hivyo, maelezo hayo yameonekana kutofautiana na hali halisi ya migomo na maandamano hayo, kwani ajenda yake kuu imekuwa ni kudai haki na maslahi, yakiwamo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, walimu na wafanyakazi wa mashirika ya umma au ya vyama vya siasa na wananchi kupinga ukiukwaji wa demokrasia kama ilivyotokea katika uchaguzi wa umeya jijini Arusha.
Tafiti za wasomi na taasisi mbalimbali zisizo za kiserikali nchini zimethibitisha kuwa uvunjifu wa amani umekuwa ukifanywa zaidi na Jeshi la Polisi linapojaribu kusambaratisha maandamano ya haki na ya amani yanayofanywa na wananchi.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete alisema kuwa nguvu ya vyama vya upinzani imeongezeka na kusababisha ruzuku ya CCM ipungue, hivyo aliwataka Wana CCM kubuni vyanzo vingine zaidi vya mapato ili kuiimarisha kiuchumi.
Aidha, alikiri kuwa Wana CCM wamekuwa wakitishwa na kunyong'onyezwa na mafanikio ya CHADEMA iliyoyapata katika Uchaguzi Mkuu uliopita.
Sanjari na kukiri hilo, Rais Kikwete alitumia sehemu ya hotuba yake hiyo kurejea tena matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kwa kutoa maelezo ya kuwatia moyo Wana CCM, akiwataka wasiwe wanyonge kwani bado chama chao kilijitahidi kupata ushindi mkubwa.
Akionekana kuiacha CUF na kuishambulia zaidi CHADEMA huku akitumia maneno yenye husuda ya kisiasa ndani yake, Rais Kikwete alisema: "Nadhani tunatishwa na kelele na propaganda za chama fulani na bwana Fulani, ambazo zinajenga hisia kama vile wako wengi sana na wamepata ushindi mkubwa sana hata kuliko CCM. "Hilo si kweli, ingawaje safari hii wamepata viti vingi kuliko uchaguzi uliopita.
"Kwa nini tujisikie wanyonge baada ya kupata ushindi mnono kiasi hicho?" alisema Rais Kikwete.
 
PHP:
Kafulila adai JK hawajui Dowans, Ngeleja anawajua
 
Kwa upande wa mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.
 
"Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,"alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.
 
Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi. 
 
"Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua," alisema Kafulila na kuongeza:

Kafulila is a leader to watch...................................he can read between the dotted lines...........................
 

JK: Tutazingatia ushauri wa wabunge kuhusu Dowans

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 5th February 2011 @ 23:57

HATIMAYE Rais Jakaya Kikwete amelitolea ufafanuzi suala la Kampuni ya kufua umeme ya Dowans akisema Serikali itazingatia ushauri wa Kamati ya Wabunge wa CCM iliyokaa hivi karibuni.

Akihutubia wanachama wa CCM wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 34 ya chama hicho zilizofanyika kitaifa Dodoma jana, Rais Kikwete alisema Serikali yake iko makini kutafuta ufumbuzi wa tatizo la Dowans ambao hautaleta madhara makubwa kwa wananchi.

Akitoa historia juu ya kilichosababisha nchi kutafuta ufumbuzi wa haraka, Rais Kikwete alisema alipoingia madarakani, miongoni mwa changamoto zilizojitokeza, ni ukame uliosababisha kukauka kwa vyanzo vya maji na hatimaye nchi kuingia gizani.

Alisema mavuno ya chakula yalikuwa mabaya na kukawa na njaa kali ambapo watu 3,776,000 walilazimika kuhudumiwa na Serikali. Aidha, mito mikubwa na midogo ikapungukiwa sana maji na mingine kukauka kabisa.

Alisema jitihada zilifanyika na moja ya hatua ilikuwa ni kutafuta kampuni ambayo ingeweza kupata suluhisho la haraka na ndipo mchakato ulipofanyika wa kumpata mzabuni ambaye angefanya kazi hiyo.

"Mimi nilitilia shaka nilipoambiwa kwamba Kampuni ya Richmond iko tayari, lakini wanataka tuwalipe kwanza dola milioni 10.

Niliwambia walete hiyo mitambo, kisha sisi tuwalipe. Shaka yangu ilikuwa ni ya kweli, kwani badala ya kuleta mitambo, wakauza mkataba huo kwa Dowans," alisema Rais Kikwete na kuongeza:

"Hawa Dowans ni kweli walileta mitambo na umeme ukapatikana, lakini suala likaja, je hawa walioingia mikataba nao si ilikuwa kampuni ya mfukoni?

Ndipo Bunge likalazimika kuunda tume na ikagundulika kwamba Richmond kweli ni kampuni ya mfukoni".

Hata hivyo, Rais Kikwete alisema badala ya watu kutafuta jinsi ya kutatua tatizo lililopo mbele yao, wakawa wanamhusisha kuhusika na Kampuni hiyo ya Dowans.

"Yapo maneno mengi eti mbona Rais yuko kimya sana, hatujamsikia kusema chochote? Niseme nini zaidi na hao wote wameshasema kwa niaba yangu? Wapo wanaosema niko kimya kwa sababu nahusika na Downs, na eti ndiye mwenyewe hasa.

Wapo wanaosema niko kimya au nashindwa kuchukua hatua, kwa sababu marafiki zangu wamehusika, nawalinda, " alisema Rais Kikwete na kuongeza:

"Jambo ninalotaka kulizungumzia sasa sikutaka kulizungumza, kwa sababu Waziri Mkuu alishalifafanua baada ya semina ya wabunge wa CCM na hata John Chiligati, Katibu wa Siasa na Uenezi Taifa alishalizungumzia.

Sikuona umuhimu wa kufanya hivyo kwa sababu viongozi wenzangu hao wameelezea kwa ufasaha uamuzi wa Kamati Kuu na ule wa kikao cha pamoja cha wabunge wa CCM".

Akiweka msimamo juu ya kutohusika kwake na Dowans, Rais Kikwete alisema: "Napenda kuwahakikishia wana-CCM na wananchi wenzangu, kuwa sina uhusiano wowote wa kimaslahi kwa namna yoyote ile na Kampuni ya Dowans.

Sina hisa zozote wala manufaa yoyote yale. Pia sina ajizi wala kigugumizi cha kuchukua hatua kwa sababu ya rafiki yangu au hata kama angekuwa ndugu yangu kahusika".

Alisema uamuzi uliofanywa na Kamati Kuu na Kamati ya Chama ya Wabunge wa CCM ulifanywa chini ya uongozi wake na hivyo; " ni uthibitisho tosha wa ukweli huo.

Waliokuwepo kwenye vikao hivyo wanajua ukweli wa haya ninayosema. Ningekuwa na maslahi au hofu tusingefanya uamuzi ule."

Alisema anachobaini katika sakata hili ni yeye kukubaliana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kwa wakati huo ambalo liliiomba Serikali igharamie ukodishaji wa mitambo kutoka nje, jambo ambalo alisema lilikubaliwa kulingana na hali halisi.

Aliongeza: "Ili kukabiliana na tatizo hilo, ushauri ulitolewa na Tanesco nasi tukaukubali kuwa wakodishe mitambo ya kuzalisha umeme kutoka nje.

Serikali tukaombwa kugharamia ukodishaji huo. Taratibu za kisheria zikafanywa, tenda zikatangazwa na washindi wakapatikana Aggreco, Richmond na Alstom.

Kampuni za Aggreco na Alstom zilileta mitambo yao kwa wakati, lakini Richmond ikawa
inasuasua.

"Wakati huo huo maneno mengi yakawa yanazagaa kuhusu Richmond kutostahili kupewa tenda kwa sababu ya kutokuwa na uwezo na kutokuwa hai.

"Ikadaiwa kuwa wamepewa tenda kwa sababu ya kubebwa na baadhi ya viongozi serikalini. Maneno hayo yalifanya Wizara ya Fedha isite kutoa fedha za kuanzia kwa kampuni hiyo.

"Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati ule alipokuja kuniomba niingilie kati ili kampuni hiyo ilipwe malipo ya awali nikakataa na kumwambia Waziri aachane nao kwani kampuni hiyo ni ya shaka".

Rais Kikwete alisema hata hivyo Richmond haikulipwa malipo hayo kwa kushindwa kutimiza mkataba, ingawa alisema maneno yalizidi kadri makali ya kukosa umeme yalivyoendelea kuuma.

Aliongeza kwamba baada ya hapo Kampuni ya Richmond ikauza mkataba wake kwa Dowans ambayo ilileta mitambo na uzalishaji umeme ukafanyika na kupunguza kabisa makali ya mgawo.

 
JK achochea moto


*Wasomi, wanasiasa wasema naye amegeuka kuwa mlalamikaji
*Wadai angeeleza serikali itakavyokabili genge la wahuni


Tumaini Makene na Grace Michael

HOTUBA ya Rais Jakaya Kikwete ya kuadhimisha miaka 34 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi imechochea moto na
mijadala nchini, huku kauli kuwa hakuna uharaka wa kuilipa Kampuni ya Dowans sh. bilioni 94 ikiibua maswali zaidi kuliko majibu.

Wasomi na wasiasa waliozungumza na Majira jana walisema Rais Kikwete ameungana na wananchi wa kawaida na kuwa mlalamikaji, badala ya kutoa mwongozo wa nini cha kufanya kuondokana na suala hilo na kueleza jinsi ya kulikabili 'genge la wahuni wanaotafubna rasilimali za nchi na kuteka mamlaka ya taifa'.

Miongoni mwa waliozungumaia hotuba hiyo, ni Mhadhiri Msaidizi Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Chuo Kikuu Dar es Salaam, Bw. Bashiru Ally alisema kuwa hotuba ya rais ilipaswa kujikita katika kuzungumzia masuala yanayolikabili taifa kwa upana wake, kwani Dowans ni dalili tu ya tatizo kubwa nchini.

Alisema mathalani badala ya kuzungumzia Dowans, kwani kama alivyokiri mwenyewe tayari ilishazungumziwa na wasaidizi wake, rais alipaswa kuliambia taifa kupitia sherehe hizo za CCM, kuwa serikali yake itakabiliana vipi na genge la watu wachache walioteka mamlaka za nchi.

Alisema kuwa hotuba ya juzi ya kutimiza miaka 34 ya CCM ilipaswa kujikita katika kuangalia malengo makuu ya chama hicho kikongwe, masuala ya itikadi, sera na mwelekeo wa taifa, badala ya kuangalia maslahi ya muda mfupi kama vile kushinda uchaguzi, kila baada ya miaka mitano.

"Kwangu mimi issue si kulipa au kuilipa Dowans, Dowans ni dalili ya ugonjwa mzito unaolikabili taifa...ugonjwa wa kutowajibika, kikundi cha watu wachache kujilimbikizia mali, mfumo wa sheria kutofanya kazi, tatizo la kuuza na kununua kura, watu wanachukua posho zinazozidi mishahara yao.

"Hivyo hotuba ya jana (juzi) ilijikita zaidi katika kuangalia ushindi wa hali ya uchaguzi, msukosuko ambao CCM inapata kutoka kwa wapinzani kwenye uwanja wa CCM, kuwatia moyo wana-CCM na suala la kufanya mageuzi ndani ya chama...hivyo kulikuwa na imbalance (hakukuwa na uwiano sawa) na mambo mengine ya mtazamo mpana juu ya mweleko wa taifa.

"Hata ukisema chama kinafanya mageuzi, unajiuliza mageuzi kutoka wapi, CCM imepita katika vipindi mbalimbali, malengo makuu ya CCM zamani haikuwa kushinda uchaguzi, ilikuwa ni kujenga taifa huru, lenye usawa na heshima kwa watu, uzalendo, maadili. Taifa ambalo lilikuwa linazungumzia juu majirani na Bara la Afrika zima kwa ujumla.

"Kuna changamoto ya kuangalia masuala ya itikadi, sera na mwelekeo wa taifa, chama si mashine ya kutafutia kura, ni uongozi, na uongozi ni dira...masuala ya kushinda uchaguzi ni malengo ya muda mfupi sana, hakuna dira ya miaka mitano, la sivyo CCM nacho kitakuwa kimetumbukia katika mtazamo finyu," alisema Bw. Ally.

"Kwa kweli badala ya kuzungumzia Dowans tu kwa sababu Pinda na Chiligati walishasema kama alivyosema, basi rais alipaswa kuzungumzia bigger picture (mtazamo mpana) si smaller picture, juu ya matatizo yetu, angetuhakikishia namna gani serikali yake imejipanga katika mapambano dhidi ya ufisadi.

"Itapambanaje na genge la wahuni wanaotumia fursa zao za kiuchumi kuteka mamlaka ya nchi...ufisadi unaoangamiza sekta karibu zote, energy (nishati), ardhi, huduma za jamii, mfumo wa utawala, ufujaji wa rasrimali za umma," alisema Bw. Ally kwa kirefu.

Aliongeza kuwa hotuba hiyo ingeweza kueleza mwelekeo wa taifa katika wakati huu ambapo makatibu wakuu au wakurugenzi wa idara, wanajitwalia fedha na marupurupu mengi, huku wakitembelea magari ya kifahari, wakati wanafunzi vyuoni na shuleni hawana uhakika wa chakula.



Nakubaliana kabisa na Bashiru Ally kuwa hayo ndiyo yalistahili kuzungumzwa na Rais lakini kwa sababu watanzania tumewaweka wenye upeo mdogo wawe watawala wetu, mara nyingi tutakuwa tukisimuliwa hadithi badla ya kusikia hotuba.
 
The way it goes sitaki kuamini kabisa kama raisi (as a CEO) badala ya kutoa maamuzi na mwongozo nae analalamika kama wananchi.
You guys unajua hili linashangaza sana. Is this Guy fit mentally, hivi amesahau kuwa yeye ni Raisi, has he forgoten kabisa?

Mhhh
 
PHP:
Nakubaliana kabisa na Bashiru Ally kuwa hayo ndiyo yalistahili kuzungumzwa na Rais lakini kwa sababu watanzania tumewaweka wenye upeo mdogo wawe watawala wetu, mara nyingi tutakuwa tukisimuliwa hadithi badla ya kusikia hotuba.

You are a keen observer.................
 
PHP:
[B] [IMG]https://www.jamiiforums.com/images/icons/icon1.png[/IMG] Re: Wasomi wamrushia JK kombola; aache ulalamishi... [/B]

    kama hukupiga kura tusikusikie wala kukuona ukilalamika!!

Umasikini wa hii hoja ni dhana potofu inayoibeba ya kuwa uchaguzi ulikuwa ni huru na haki jambo ambalo siyo kweli hata kidogo....................................wengi wetu tulipiga kura na JK tulimkataa ila TISS na NEC ndiyo walimsimika JK kinyume na sheria ya katiba yetu.............
 
Back
Top Bottom