Wasomi wa Tanzania wametoa mchango gani kwenye Taifa letu mpaka sasa?

Wana wa Tanzania wenzangu; tumejaaliwa kuwa na wasomi na wataalam wa fani tofautitofauti katika taifa letu. Tuna ma Profesa, Dakta, Injinia, pamoja na wengine wengi tu..! Swali ni je, kwa ujumla wao wanalisaidiaje taifa kutatua ama kukabiliana na changamoto mbambali zinazolikabili taifa? Je; ni mimi peke yangu ndio sioni mchango wao au hiyo michango yao tafiti, ugunduzi ama nasaha zao ndio haiko wazi ili kila mtanzania yeyote aweze kuona kile wanachokifanya na kuondoa walakini juu ya wasomi wetu? Katika nchi za wenzetu hususan Ulaya, Asia na America, tunasikia na kusoma kwenye vitabu; mara msomi flani kagundua hiki, mwingine kile nk, nk. Kila mmoja kwa nafasi yake anataka kuacha historia hata siku akitangulia mbele ya haki jina lake liendelee kuishi daima kutokana na kile ama mchango wake kwa taifa lake na dunia kwa ujumla. Hadi mtu unahisi raha na kujivunia wasomi wa taifa lako. Pengine mimi ndio sijui ama sielewi, naomba tujadili pamoja wana jamvi wote.
 
Wana wa Tanzania wenzangu; tumejaaliwa kuwa na wasomi na wataalam wa fani tofautitofauti katika taifa letu. Tuna ma Profesa, Dakta, Injinia, pamoja na wengine wengi tu..! Swali ni je, kwa ujumla wao wanalisaidiaje taifa kutatua ama kukabiliana na changamoto mbambali zinazolikabili taifa? Je; ni mimi peke yangu ndio sioni mchango wao au hiyo michango yao tafiti, ugunduzi ama nasaha zao ndio haiko wazi ili kila mtanzania yeyote aweze kuona kile wanachokifanya na kuondoa walakini juu ya wasomi wetu? Katika nchi za wenzetu hususan Ulaya, Asia na America, tunasikia na kusoma kwenye vitabu; mara msomi flani kagundua hiki, mwingine kile nk, nk. Kila mmoja kwa nafasi yake anataka kuacha historia hata siku akitangulia mbele ya haki jina lake liendelee kuishi daima kutokana na kile ama mchango wake kwa taifa lake na dunia kwa ujumla. Hadi mtu unahisi raha na kujivunia wasomi wa taifa lako. Pengine mimi ndio sijui ama sielewi, naomba tujadili pamoja wana jamvi wote.

Wamebaki kujisifia tu wana vyeti kibao na kuongea kiswanglish kuwakoga watu, lakini hao ndio wanaingia mikataba ya kipumbavu na huko maofisini ndio mabingwa wa kutengeneza risiti fake, na kujipangia semina zisizo na tija. Kichekesho ni pale msomi anapopewa mradi ausimamie hapo ndio utacheka, kitu cha kwanza ni kuanzisha kikundi cha majungu na kwenda kwa waganga ili asipoteze cheo chake. Akifukuzwa kazi hata ufahamu wa kujiajiri hana anaishia kutembea na mavyeti kibao mpaka soli ya kiatu kinaenda upande.
 
Jana wakati wa mdahalo wa Nkurumah ni wazi Prof.Tibaijuka alijenga hoja hafifu sana ktk uwasilishaji wake. Na hii si mara ya kwanza kwa Prof.Tibaijuka kufanya mambo chini ya kiwango ukilinganisha na elimu aliyonayo. (refer siku alipowasilisha bajeti ya wizara yake).

Though wapo Maprofesa wachache wanaofanya vizuri kama Prof.Mpangala, Prof.Shivji, Prof.Baregu Mwesiga, na Prof.Lipumba (huyu amesaidia nchi nyingi sn duniani kujikwamua kiuchumi + WB & IMF huwa wanamtumua mara kwa mara).

Lakini wengi waliobaki ni sub-standard hasa wale waliojiingiza kwenye siasa. Hivi watu kama:

1.Prof.Kapuya, (uprofesa wake kaupeleka AKUDO impact). Sisemi maprofesa wasiwekeze, lakini waangalie na mahali pa kuwekeza.

Hivi profesa mzima unamikiki bendi ya muziki, kila weekend unakata mauno "samaki ana vipande vingapi....?" Na wewe unajibu "vitatu..." pembeni una vimwana kadhaa na chupa ya vodka. Mi nadhani uprofesa hapo unakua kushney.!

2.Prof.Maghembe, huyu ni Profesa wa nyuki lakini sidhani kama ana mchango wowote kwny sekta ya ufugaji nyuki nchini. Yeye ni kula bata tu mjini wakati alitakiwa awe anazalisha asali mbichi Tabora.!

3.Prof.Muhongo huyu ndo sitaki hata kumuongelea.

4.Prof.Tibaijuka nasikia huyu ukimuuliza mbona hawezi kujenga hoja, huwa anajitetea "mm nilikua UN, kawaulize UN watakueleza habari zangu"

Hawa ni baadhi tu ya Maprofesa waliojiingiza kwny suasa na wameshindwa kuisaidia nchi hii. Lakini hata wale ambao hawajajiingiza kwenye siasa still hakuna la maana walilofanya kama alama ya elimu yao.

Sasa naomba kuhoji "Maprofesa wa nchi hii wana faida gani kwa maendeleo ya taifa zaidi ya kufundisha vyuoni??" Karibuni kwenye mjadala, na tafadhali jenga hoja sio matusi.
 
Jana wakati wa mdahalo wa Nkurumah ni wazi Prof.Tibaijuka alijenga hoja hafifu sana ktk uwasilishaji wake. Na hii si mara ya kwanza kwa Prof.Tibaijuka kufanya mambo chini ya kiwango ukilinganisha na elimu aliyonayo. (refer siku alipowasilisha bajeti ya wizara yake).

Though wapo Maprofesa wachache wanaofanya vizuri kama Prof.Mpangala, Prof.Baregu Mwesiga, Prof.Lipumba etc. Lakini wengi waliobaki ni sub-standard hasa wale walioingia kwenye siasa. Hivi watu kama Prof.Kapuya, Prof.Maghembe, Prof.Muhongo etc wamesaidia nini nchi hii?

Lakini hata wale ambao hawajajiingiza kwenye siasa still hakuna la maana walilofanya kama alama ya elimu yao.

Sasa naomba kuhoji "Maprofesa wa nchi hii wana faida gani kwa maendeleo ya taifa zaidi ya kufundisha vyuoni??" Karibuni kwenye mjadala, na tafadhali jenga hoja sio matusi.

Neno Prof. siku hizi halina maana sana hasa baada ya kuingiliwa na vilaza hata ile maana ya Professor haionekani tena. Huyu mama kwa kweli kabisa hana uwezo ila tu anatembelea CV ya UN alikofanya. Alipowasilisha bajeti yake alichemka mpaka niamua kuzima TV ilikuwa aibu sana.
 
Hebu twambie wewe ungepewa nafasi ungeongea nini kizuri na cha maana zaidi ya alichokiongea Prof Tibaijuka? au kwa kuwa alitoa hali halisi na hatua kubwa waliyopiga wanawake kupitia hoja zao mezani ?
 
Tatizo la Tanzania si wasomi. Tatizo ni wanasiasa. Ukiangalia balaa zote zilizotukumba chanzo chake ni wanasiasa. Kuanzia IPTL, Net Solutions, Richmonduli, wasomi walitoa ushauri lakini wanasiasa wakaingilia kati. Na ukitofautiana na utashi wa wanasiasa unaundiwa zengwe, unahamishwa au kuachishwa kazi.

Wasiasa na wasomi waliokimbia siasa ndiyo chanzo cha matatizo. Nchi inayoongozwa kwa unafiki wa kisiasa and ufisadi nafikiri maendeleo endelevu ni ndoto. Tafiti nyingi zimefanyia na kushauri kila sekta nini cha kufanya lakini utekelezaji unategemea serikali ambayo inaongozwa na wanasiasa wasiojali wananchi au wapiga kura wao. Sheria at times inafanya kazi kwa kupendelea.
 
Nina hasira na viongozi, kila nikiwaona viongozi hasa wa dini na wa serikali natamani kuwanyuka makofi ya kutosha maana hao ndio tatizo
 
Ndg! WaTanzania naamini ya kwamba, wale wote munaojifanya eti niwasomi, mtukajeli sana, mtatukana sana lakini ukweli utabaki kuwa pale pale.

kwanza kabisa mimi naweza kusema Tanzania hakuna wasomi bali kuna watu wanaokaririshwa na uongo wa maandisha ya nchi za magharibi.

ni sawa tunao watu wanaojiita wadegree, wengine maprofeser

maswali ya kujiuliza hawa wenye degree na maprofeser wameifanyia nini nchi yao.

tufauti na kukariri maadishi za nchi za wenzetu. kwa mfano wanafunzi wetu hapa nchini wanadanganywa kuhusu nadharia sahihi ya chazo cha ukimwi,

pili, viongozi pamoja na watu wenye hela wakiumwa wanaenda kutibiwa nyije ya nchi, kwa nini?.

kama kuna mtu anajidai amesoma ajitokeze hapa,,!
 
Tunapoelekea katika uchaguzi mkuu watz wenzangu ni bora tukakumbushana haya. Tuliwaamini sana wasomi tukajua ni watu makini na wana uwezo wa kutumia elimu yao kutuvusha kutoka hatua moja kwenda nyingine ya juu zaidi.

Lakini haijawa ivyo. ukiangalia binge huwezi kutofautisha hao wasomi ni wapi na wasio wasomi ni wapi. hata sisi ambao hatukwenda shule yaani tunashangaa wanayoyafanya.

Maamuzi yanayotolewa hata kama ni ya kipuuzi namna gani ila watapeana sapoti kulingana na chama. Yaani hakuna msaada wowote tunaopata kulingana na elimu zao tulizowasomesha kwa kodi zetu.

Binge lijalo ni bora tukawapewa nafasi vijana wa vijiweni, wapiga debe, makondakta wa daladala wasanii, wacheza mpira na wengine lakini sio hao wasomi tuliowaamini hawana jipya lolote.
 
Ndugu zangu watanzania, moja ya nguzo mhimu katika ujenzi wa taifa imara ni Elimu. Pamoja na definition ya Elimu kuwa pana, naitazama zaidi formal education kama ndiyo elimu ninayotaka kuizungumuzia hapa na hapa ndipo naona kuna haja ya kuangalia mchango wa wasomi wetu katika kukuza taifa letu. Kifupi, yapo mambo yanayofanywa na wasomi wa taifa hili mpaka yanasikitisha na ninajiuliza nani katuloga sisi ama elimu yetu imerogwa?.

Mfano; Kumekuwepo na vikundi vingi vya kitafiti vikiegemea zaidi upande wa maswla ya kijamii na siasa na machapisho ya vikundi hivi mara nyingi huibua maswali zaidi kuliko kujibu maswali yanayolikabili taifa. Baadhi ya vikundi hivi vinasimamiwa na wasomi wakubwa (phD holders) na wanaotambulika sana na taasisi za ki-elimu hapa nchini. Hapa napata shida kuelewa mchango wa wasomi wetu; kwanini wanapofanya tafiti zao (e.g. kuhusu maswala ya kisiasa), zinaibua maswali kuliko kutoa majibu ya maswali yanayolitatiza taifa?. Na hata kama watatowa majibu, lazima katikati ya jamii kutaibuka minong'ono kuwa taifiti zao hazina ukweli kwani wengine wanadai zimepikwa.

Nadhani kuna haja ya kuangalia elimu yetu na mchango wa wasomi wetu katika maendeleo ya taifa
 
Ndugu zangu watanzania, moja ya nguzo mhimu katika ujenzi wa taifa imara ni Elimu. Pamoja na definition ya Elimu kuwa pana, naitazama zaidi formal education kama ndiyo elimu ninayotaka kuizungumuzia hapa na hapa ndipo naona kuna haja ya kuangalia mchango wa wasomi wetu katika kukuza taifa letu. Kifupi, yapo mambo yanayofanywa na wasomi wa taifa hili mpaka yanasikitisha na ninajiuliza nani katuloga sisi ama elimu yetu imerogwa?.

Mfano; Kumekuwepo na vikundi vingi vya kitafiti vikiegemea zaidi upande wa maswla ya kijamii na siasa na machapisho ya vikundi hivi mara nyingi huibua maswali zaidi kuliko kujibu maswali yanayolikabili taifa. Baadhi ya vikundi hivi vinasimamiwa na wasomi wakubwa (phD holders) na wanaotambulika sana na taasisi za ki-elimu hapa nchini. Hapa napata shida kuelewa mchango wa wasomi wetu; kwanini wanapofanya tafiti zao (e.g. kuhusu maswala ya kisiasa), zinaibua maswali kuliko kutoa majibu ya maswali yanayolitatiza taifa?. Na hata kama watatowa majibu, lazima katikati ya jamii kutaibuka minong'ono kuwa taifiti zao hazina ukweli kwani wengine wanadai zimepikwa.

Nadhani kuna haja ya kuangalia elimu yetu na mchango wa wasomi wetu katika maendeleo ya taifa

Kweli mkuu
 
Nawataja wachache ambao watawakilisha wengine.

Prof. Lipumba, Dr. Willibroud Slaa(dr. Mihogo), prof. Juma kapuya, Prof. Sospeter Mhongo(mzee wa gesi).

Hawa watu kitaaluma za darasani ni wazuri ila wanayoyafanya ni hasara dunia kuwa na watu kama hawa.

Huwa najiuliza, hao wote mbali na udhaifu wao kisiasa lakini pia wana matatizo ktk maisha yao ya mapenzi, kapuya kakutwa na tuhuma za kubaka na kuambukiza ukimwi katoto ka watu. Lipumba nae hama hata mimba ya kusingiziwa. Dr. Wa Mihogo nae anapelekwa na yule mama wa kukopa kama trekta bovu.

Ukienda kisiasa ndo kabisa, hawa jamaa unaweza kumkosea Mungu kwa kujiuliza kwa nini aliwaleta duniani. Ni hasara kwa kweli.

Hivi kwa nini hawa ma Prof. na ma Dr.? Wana nini vichwani?
 
Tumebalikiwa kuwa na Wasomi wenye kujitapa kuwa wabobezi wa Mambo! Kuna Maprofesa, Dakta nakadhalika.
Hivi ninyi watu lini tutaona mchango wenu katka kukemea ukandamizi wa sheria zetu? Yaani Chombo cha habari kinapigwa fine wakati hakuna kosa?
Mfano Kuna tukio la Kufungia gazeti la MSETO na Waziri wa habari, Sanaa na Utamaduni Nape Nnauye. Waziri amefuta gazeti hili na mengine mengi kwa kauli yake. Sasa hamuoni kuwa hii sheria imepitwa na wakati kwa kumfanya Waziri awe Mahakama? Je, Sauti yenu ni ipi katika hili? Je, mnaridhika na sheria kandamizi kama.
Wanasheria wa Watanzania na Wasomi wengine nawauliza hayo, na Leo mlikuwa Arusha mnaacha kuanzisha movement za kupinga sheria kandamizi kama hizi Je, mchango wenu ni upi? Au taifa hili ndiyo ile laana ya Uoga na Kujipendekeza imetamalaki?
Waandishi wa habari na ninyi pia mmeshindwa kupaza Sauti zenu katka hili kwa ujumla wenu? Leo kwa Wale kesho kwenu, vinginevyo Iwe hivyo hivyo Muamriwe cha Kuandika/Kutangaza na Serikali iliyopo madarakani.
Badilike Wasome Wetu tunataka mchango chanya katka Taifa hili Tanzania.
 
Back
Top Bottom