Wasomi UDOM waandamana kumuunga mkono JK kuwa mgombea pekee CCM, akerwa na Zitto!

Hii ni hatari kweli. Lkn pia sishangai kusikia kuwa wsomi uchwara wa Udom wanamfagilia huyu mbayuwayu. ikumbukwe kuwa udom ni chuo kilichoanzishwa katika mazingir ya siasa. KAma watu tunaodhani kuwa watatoa mwanga kwa wale waliogizani ndio wa kwanza kutuhadaa na kutupoteza unadhani nini kimebaki? Malipo ni hapa hapa DUNIANI. KAMA ULIMCHAGUA MBAYUWAYU KWA SABABU ZA KISHABIKI AU KWA SABABU NZURI TU TUVUMILIE KWA SABABU TUNAPOKEA MSHAHARA WA MAWAZO YETU KUWA FINYU. Watu hawaelewi maana ya siasa wala hatuna utashi wa siasa. Tuna kukuruka tu. Mara utasikia: huyu ni kijana mwenzetu au mzuri bwana au kichaa wangu; hatuangalii maslahi ya nchi na watu wake. Vijana hatupigi kura tunashabikia siasa tu kwa nje. Akina mama wanapiga kura kwa wingi wakifuatiwa na wazee lkn vijana NONE of OUR BUSINESS. Vijana ni taifa la leo, sisi ndio tuamue nani tunayemhitaji na tushiriki katika hatua zote za uchaguzi. Sisi tuonyeshe kuwa tunakerwa na hii hali kuwa wazee tu ndo wanaweza. Hakuna kitu kama hicho sisi ndo wahitaji zaidi na tutawale kwani ni kipindi chetu kutawala. Kwa nini wazee watutawale na hali kipindi chao kimepita? Wao watupe mawazo na hekima ya kutawala."Lets take action as of today". Tuache blablaa nyingi wakati wa uchaguzi. Tujiandikishe kwa wingi zaidi sisi pamoja wenzi wetu. Tuwashauri wazee na wazazi wetu watuunge mkono kwa sababu nao wanatutegemea kwa sasa. Sasa kwa kukosa kazi wanaitwa Karimjee kumshangilia mbayuwayu. Hawana kazi.Kila kheri watu wangu.
 
Kuna makala mwezi may iliandika kuwa wakati wa uchaguzi vyuo vitakua vimefungwa kama kweli sio ndio ingekuwa hoja apo jamani bse hawatapiga kura
 
Wakuu,

Mimi kwa mtazamo wangu, nadhani wanafunzi kuandamana kumuunga mkon JK ni haki ya kikatiba; kwani inawezekana ni wanachama wenye imani na chama,tafauti na wengi wetu humu.

However, my only concerns kwao, ni kuwa je hawaoni haya yalitokea na yanayoendelea kutokea!! Surely serikali imekuwa inaendeshwa kisanii full blast!! Sasa kama wasomi wanashindwa kunusuru haya (maana wanategemewa kuwa na uelewa wa juu nani atayakemea/atayaondoa). Haingii akilini kama wameshindwa kuelewa kuwa JK hana uwezo wa kuongoza nchi kabisaaaaaa. Yeye amekalia sifa tu, mizaha na utani...

Kazi ipo...
 
Zitto,zitto,zittooo na jakaya hapa si kama tyson na matumla. Hivi ilikua sahihi kweli jk kumjibu zitto kwa swala alilouliza bungeni? Sasa atajibu mangapi? Na sisi humu jamvini tuna muuliza au tunauuliza hao watoto waliokuchangia pesa wametoa wapi?kama raisi mbona hujauliza, douuuu ccm inatoa damu mpaka maiti

Asante mkuu hapo penye red haswaaaa
 
Wadau hebu tuchambue mambo kwa mapana...!!! Kuwalaumu baadhi ya wasomi wa UDOM nafikiri si sahihi...!!! Kuna Kundi kubwa tu la wanafunzi hawajaandamana...!!! ...wapinzani bado hawajajipanga kutumia fursa za wanafunzi...!!

So far hata pesa walizotoa...ni sawa na Mzazi aliekwenda Kanisani au msikiti kutoa sadaka....badala yeye kutoa sadaka ile, anampa mtoto wake akaitoe ile sadaka....the same kwa hilo la UDOM....!!!...kusema wanafunzi wamekamuliwa haiingii akilini....!!

So far wasomi wachache waliopo Upinzani hawapewi nafasi...!! Waende wapi...?
 
Mkandara (Sijui kama ni Rwekaza)

Kwa suala la VC wa UDSM kuwa kibaraka wa CCM hilo halihusiani na waliyoyafanya wadogo zetu wa UDOM, point yangu ni kuwa,mbona wanakuwa so cheap!!!!juzi juzi walitaka kugoma kwa madai hawana boom,leo 1.2M wametoa wapi?

Zaidi ya hayo, naweza kwenda mbali zaid na kusema kuwa inawezekana hata hizo fedha hazijatoka mifukon mwao, wamepandikiziwa tu ili CCM watuoneshe kuwa wanaungwa mkono na jamii ya wasomi, off course huo ni mchezo mchafu, tumeona Wazee waliochoka kimaisha wa Igunga wakifanya vivyo hivyo, so hilo sio chaguo lao ila tu njaa zao ndo zinawafanya wadharauliwe na sisi wasomi wenzao ila mimi sio wa UDOM (Nilikuwa na qualifications nzuri sana)

Mhhh
Mimi hoja yako naona sieelewi, hebu tuambie ipi kati ya udsm na udom wanafunzi wake walianza kuandamana na kuiunga ccm na jk? unakumbuka vizuri lakini?

Hata hivyo nafikiri hatujui maana ya demokrasia.Teh teh teh teh.
Nafikiri Demokrasia ni uamuzi wa kupenda na kuchagua na kufanya maamuzi bila kuingilia mipaka ya mwenzako.

Na msifikiri mnavyowaza ninyi ama wewe ndo sahihi, kama unafikiri ndo hivyo POLE SANAAAAAAAAAAA. Na ukifikiria vizuri kabisa utatambua wewe ndo hujui Demokrasia, yani unalazimisha unachotaka wewe na mwenzako akifanye. Hao jamaa wanachofanya ndo demokrasia yenyewe.
 
Labda swali lianzie kama ni mantiki kwa wasomi kuwa wanachama wa CCM jinsi ilivyo sasa au ,tuende mbali zaidi, chama chocote siasa? Kwa sababu mara unapojitambulisha na chama basi unajipunguzia uhuru wa uchambuzi. Hao wa DOM, kama walivyosema wengi humu, ni wanachama wa CCM na sote hivi sasa tunajua CCM ni ya watu wa aina gani.
 
Labda swali lianzie kama ni mantiki kwa wasomi kuwa wanachama wa CCM jinsi ilivyo sasa au ,tuende mbali zaidi, chama chocote siasa? Kwa sababu mara unapojitambulisha na chama basi unajipunguzia uhuru wa uchambuzi. Hao wa DOM, kama walivyosema wengi humu, ni wanachama wa CCM na sote hivi sasa tunajua CCM ni ya watu wa aina gani.

Nafikiri hapa hatuongei chama ya namna gani bali tunaongelea demokrasia. Bado nafikiri watu tunachanganya mambo. Dunia hii unavyoiona is not REAL. Usifikiri jinsi unavyokiona kikombe fulani kina rangi ya zamarau basi na mwenzako atakiona vilevile. Ndio maana mnaweza bishana kwamba ile gari ilikua ya blue na mwezako anakwambia hapana ilikua nyekundu. Uwezo wa macho yako wakunyang'anau pixel ni tofauti na wa mwenzako , ndiyo maana kitu kile kile kila lakini jinsi unavyokiona rangi yake si sawa na mwenzako anavyokiona. Na mwisho inabidi mkubaliane tu hivyo hivyo.

Mfano mbwa angekua anaongea ndo ungesikia makuu. kwa kifupi mbwa yeye hana rangi machoni kwake yeye kila kitu anakiona kama white ama black SASA angekuwa mbwa anaongea na ukamwambia rangi hii ni blue nafikiri angekuona MJUHA usiye na upeo sahihi na demokrasia huujiu , mbwa angeendelea maana kama ungelikua unajua maana ya demokrasia na nini kinaonekana hapo basi usingeweza sema hiyo rangi ni blue.

Samahani kwa mfano huo, natumai hutokwazika bali utachukulia ujumbe ndani.
 
KUtokana na hali ngumu ya maisha ya wanachuo, wanafunzi hao wa vyo vikuu Dodoma wameandamana ili wapewe mikopona si vinginevyo.
 
Nafikiri hapa hatuongei chama ya namna gani bali tunaongelea demokrasia. Bado nafikiri watu tunachanganya mambo. Dunia hii unavyoiona is not REAL. Usifikiri jinsi unavyokiona kikombe fulani kina rangi ya zamarau basi na mwenzako atakiona vilevile. Ndio maana mnaweza bishana kwamba ile gari ilikua ya blue na mwezako anakwambia hapana ilikua nyekundu. Uwezo wa macho yako wakunyang'anau pixel ni tofauti na wa mwenzako , ndiyo maana kitu kile kile kila lakini jinsi unavyokiona rangi yake si sawa na mwenzako anavyokiona. Na mwisho inabidi mkubaliane tu hivyo hivyo. ...

Samahani kwa mfano huo, natumai hutokwazika bali utachukulia ujumbe ndani.

Mfano huo haujanikwaza ila umenipumbaza kiasi. Ni kama vile unasema tunaishi katika dunia isiyo halisi bali virtual. Kila kitu kinategemeana na jinsi ufahamu wa mtu ulivyoelekezwa (calibrated) - wewe unapoona embe mwenzio anaona chungwa na wote mnakuwa sahihi! This is a new dimension! Kwa ufafanuzi ulioutoa hapo basi hakuna hata haja ya mijadala wala kupeana mawazo mbadala kwani kila anachokiona mtu ni sahihi kulingana na mfumo wake wa ufahamu. Anayeona rushwa ni muafaka asiambiwe tofauti kwani ndivyo brain cells zake zilivyoelekezwa kufikiri! Anayeona ujamaa au ubepari ni sera bora kuliko zote asidokezwe madhara yake. A stunningly interesting concept!
 
Back
Top Bottom