Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Katika chaguzi nyingi kuanzia za ujumbe wa nyumba kumi,serikali za mitaa ubunge na Uraisi wasomi waliobobea sana wamekuwa wakibwagwa na wasiosoma sana.
Nakumbuka Raisi Nyerere aliwahi kuulizwa miaka ya nyuma sababu ya yeye kuwa na mawaziri wengi ambao sio wasomi na waelewa sana akajibu kuwa tatizo sielewi kawaulize wananchi ni kwa nini msomi sana akigombea na mtu asiyesoma sana na asiye mwelewa sana wananchi wanampa kura yule mwenye elimu ya chini na uelewa mdogo..Nyerere akasema wale anaoletewa na wananchi kupitia kura ndio hao anaowateua kuwapa uwaziri yaliyobaki watajaza wananchi waliowachagua.
Hivi nauliza wananchi kukataa kuwachagua wasomi sana wengi kwenye chaguzi mbalimbali kwa wingi ni hasira ya wananchi kwa kuwa wasomi wakubwa hawatimizi matakwa yao au ni kwa sababu wanaona wasomi sana hawaitumii elimu yao kwa faida ya wote bali kwa faida zao binafsi zaidi? Nini tatizo hasa hadi wananchi wasiwaone wasomi sana kama ni wenzao na wawape ushindi wa kishindo dhidi ya wasomi kidogo au wasiosoma?
Nakumbuka Raisi Nyerere aliwahi kuulizwa miaka ya nyuma sababu ya yeye kuwa na mawaziri wengi ambao sio wasomi na waelewa sana akajibu kuwa tatizo sielewi kawaulize wananchi ni kwa nini msomi sana akigombea na mtu asiyesoma sana na asiye mwelewa sana wananchi wanampa kura yule mwenye elimu ya chini na uelewa mdogo..Nyerere akasema wale anaoletewa na wananchi kupitia kura ndio hao anaowateua kuwapa uwaziri yaliyobaki watajaza wananchi waliowachagua.
Hivi nauliza wananchi kukataa kuwachagua wasomi sana wengi kwenye chaguzi mbalimbali kwa wingi ni hasira ya wananchi kwa kuwa wasomi wakubwa hawatimizi matakwa yao au ni kwa sababu wanaona wasomi sana hawaitumii elimu yao kwa faida ya wote bali kwa faida zao binafsi zaidi? Nini tatizo hasa hadi wananchi wasiwaone wasomi sana kama ni wenzao na wawape ushindi wa kishindo dhidi ya wasomi kidogo au wasiosoma?