nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Hellen Ngoromera na Irene Mark
UMOJA wa wanachama wa Chama cha Mapinduzi kutoka vyuo vikuu nchini, umesema hatua ya CCM kujivua gamba kwa kufanya mabadiliko ya kiutendaji haitoshi kwani ndani ya chama hicho na serikali yake kuna magamba (mafisadi) zaidi ya 100 yanayotakiwa kuondoshwa.
Kauli ya wasomi hao imekuja huku Mjumbe wa Mkutano Mkuu UVCCM wilaya ya Moshi Mjini, Paul Makonda, akibainisha kuwa uongozi wa kitaifa wa jumuiya hiyo nao unapaswa kungolewa kwani nao unafanya ufisadi wa kutumiwa na mafisadi ambao unazidi kukiua chama hicho na jumuiya yake.
Makonda alisema kinachofanyika ni kuhakikisha mafisadi wote ndani ya chama wanaondoka kwa kuunda UVCCM Maadili na kukiondoa UVCCM Maslahi chini ya uongozi wa Benno Malisa na ushawishi wa Hussein Bashe.
Umoja huo pia umetangaza kufanya operesheni maalumu nchini kumsaidia Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, kuwaondoa mafisadi ndani ya chama hicho.
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Katibu wa Umoja huo Leoni Mboya na Mwenyekiti wake Nestory Chilumba, walimpongeza Mwenyekiti wao Jakaya Kikwete kwa ujasiri aliouonyesha wa kufanya mabadiliko hayo na kutaka mfumo mzima ndani ya chama hicho kubadilishwa.
Sisi kama vijana wasomi tunaamini kwamba CCM kujivua gamba si tu kujiuzulu kwa sekretarieti wala kufukuza wanachama wanaokipotezea umaarufu bali kufanya mabadiliko ya mfumo mzima wa chama kuanzia mwenyekiti taifa hadi shina pamoja na katiba ya chama.
CCM kuna magamba zaidi ya 100 hivyo kuna haja ya kutoa gamba moja hadi jingine, wembe uliotumika kwa sekretarieti utumike kwa watu wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi ndani ya chama tumechoshwa na kelele za wapinzani, alisema Chilumba.
Alisema wao kama wana CCM wapenda maendeleo wanamwakikishia mwenyekiti wao kuwa watakuwa bega kwa bega naye kwa kila hatua anazochukua ndani ya chama hicho ili kukiwezesha kuwa na wanachama wenye maadili, uadilifu na nidhamu.
Aliishauri sekretarieti kuu ya chama hicho kutekeleza ahadi yake ya kuwashughulikia wanachama mafisadi na kusema wana matumaini nayo katika kukiletea chama hicho mabadiliko makubwa.
Kuhusu kutaka uongozi wa umoja wa vijana wa chama hicho (UVCCM) kujiuzulu kutokana na kushindwa kazi, Chilumba alisema kwa kuwa kuna sekretarieti mpya wameona ni busara wakaonane nayo ili kuona njia za busara zinazofaa katika kuhakikisha UVCCM inajisafisha.
Wanachama hao hai wa CCM walisema kwa sauti moja kuwa hawao
gopi nguvu yoyote ya mafisadi na kama wana pesa nyingi waanzishe chama chao.
Akizungumzia kuhusu operesheni kokoro ambayo wamepanga kuifanya hivi karibuni Katibu, Leoni Mboya, alisema itakuwa na lengo la kuwaondoa mafisadi wote.
Tunataka umma uelewe kuwa kuna operesheni kokoro inakuja, hii itakuwa maalumu kwa ajili ya kumsaidia mwenyekiti wetu kuyaondoa mayai na mapapa ndani ya CCM ikiwa hawatafanya hivyo wenyewe, alisema Mboya.
Kwa upande wake Makonda alisema mfumo mbovu wa utawala na kusubiri vikao ndani ya chama hutoa mwanya kwa matajiri wachache wenye maslahi binafsi kukiharibu chama na jumuiya zake.
Katika hilo alipongeza uamuzi wa mwenyekiti wao Kikwete kubadili uongozi wa sekretarieti na kutoa changamoto kwa viongozi wapya chini ya Katibu Mkuu Wilson Mukama kuunda mfumo bora wa uongozi ili kukiimarisha chama na kurejesha imani ya wananchi kwa chama hicho.
Inahitaji utashi na uamuzi mgumu kubadili uongozi katikati ya safari haijawahi kutokea tangu kuanza kwa CCM, baada ya mabadiliko hayo naamini sasa changamoto kubwa ipo kwa hiyo sekretarieti mpya ihakikishe inabadili mfumo, itoke kwenye sera za kitamaduni tulizorithi ikipeleke chama kwenye sera za kisasa.
Sekretarieti iliyopita ilikuwa inasubiri vikao na taratibu bila kujali madhara yanayokikumba chama kwa kuchelewa kutoa maamuzi kwa wakati. Ilifika kipindi chama kinafanya mabadiliko kutokana na kauli ya wapinzani.
Naishauri sekretarieti mpya kurejesha heshma na imani ya chama tunategemea mabadiliko makubwa sasa, alisema Makonda huku akiongeza kwamba kinachotakiwa ni kubadili mfumo.
Alisema UVCCM maadili ipo kwenye mchakato wa kuunda umoja mpya utakaosaidia kukuza na kukiimarisha chama huku akibainisha kwamba wanaruhusiwa kufanya hivyo kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho.
UMOJA wa wanachama wa Chama cha Mapinduzi kutoka vyuo vikuu nchini, umesema hatua ya CCM kujivua gamba kwa kufanya mabadiliko ya kiutendaji haitoshi kwani ndani ya chama hicho na serikali yake kuna magamba (mafisadi) zaidi ya 100 yanayotakiwa kuondoshwa.
Kauli ya wasomi hao imekuja huku Mjumbe wa Mkutano Mkuu UVCCM wilaya ya Moshi Mjini, Paul Makonda, akibainisha kuwa uongozi wa kitaifa wa jumuiya hiyo nao unapaswa kungolewa kwani nao unafanya ufisadi wa kutumiwa na mafisadi ambao unazidi kukiua chama hicho na jumuiya yake.
Makonda alisema kinachofanyika ni kuhakikisha mafisadi wote ndani ya chama wanaondoka kwa kuunda UVCCM Maadili na kukiondoa UVCCM Maslahi chini ya uongozi wa Benno Malisa na ushawishi wa Hussein Bashe.
Umoja huo pia umetangaza kufanya operesheni maalumu nchini kumsaidia Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, kuwaondoa mafisadi ndani ya chama hicho.
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Katibu wa Umoja huo Leoni Mboya na Mwenyekiti wake Nestory Chilumba, walimpongeza Mwenyekiti wao Jakaya Kikwete kwa ujasiri aliouonyesha wa kufanya mabadiliko hayo na kutaka mfumo mzima ndani ya chama hicho kubadilishwa.
Sisi kama vijana wasomi tunaamini kwamba CCM kujivua gamba si tu kujiuzulu kwa sekretarieti wala kufukuza wanachama wanaokipotezea umaarufu bali kufanya mabadiliko ya mfumo mzima wa chama kuanzia mwenyekiti taifa hadi shina pamoja na katiba ya chama.
CCM kuna magamba zaidi ya 100 hivyo kuna haja ya kutoa gamba moja hadi jingine, wembe uliotumika kwa sekretarieti utumike kwa watu wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi ndani ya chama tumechoshwa na kelele za wapinzani, alisema Chilumba.
Alisema wao kama wana CCM wapenda maendeleo wanamwakikishia mwenyekiti wao kuwa watakuwa bega kwa bega naye kwa kila hatua anazochukua ndani ya chama hicho ili kukiwezesha kuwa na wanachama wenye maadili, uadilifu na nidhamu.
Aliishauri sekretarieti kuu ya chama hicho kutekeleza ahadi yake ya kuwashughulikia wanachama mafisadi na kusema wana matumaini nayo katika kukiletea chama hicho mabadiliko makubwa.
Kuhusu kutaka uongozi wa umoja wa vijana wa chama hicho (UVCCM) kujiuzulu kutokana na kushindwa kazi, Chilumba alisema kwa kuwa kuna sekretarieti mpya wameona ni busara wakaonane nayo ili kuona njia za busara zinazofaa katika kuhakikisha UVCCM inajisafisha.
Wanachama hao hai wa CCM walisema kwa sauti moja kuwa hawao
gopi nguvu yoyote ya mafisadi na kama wana pesa nyingi waanzishe chama chao.
Akizungumzia kuhusu operesheni kokoro ambayo wamepanga kuifanya hivi karibuni Katibu, Leoni Mboya, alisema itakuwa na lengo la kuwaondoa mafisadi wote.
Tunataka umma uelewe kuwa kuna operesheni kokoro inakuja, hii itakuwa maalumu kwa ajili ya kumsaidia mwenyekiti wetu kuyaondoa mayai na mapapa ndani ya CCM ikiwa hawatafanya hivyo wenyewe, alisema Mboya.
Kwa upande wake Makonda alisema mfumo mbovu wa utawala na kusubiri vikao ndani ya chama hutoa mwanya kwa matajiri wachache wenye maslahi binafsi kukiharibu chama na jumuiya zake.
Katika hilo alipongeza uamuzi wa mwenyekiti wao Kikwete kubadili uongozi wa sekretarieti na kutoa changamoto kwa viongozi wapya chini ya Katibu Mkuu Wilson Mukama kuunda mfumo bora wa uongozi ili kukiimarisha chama na kurejesha imani ya wananchi kwa chama hicho.
Inahitaji utashi na uamuzi mgumu kubadili uongozi katikati ya safari haijawahi kutokea tangu kuanza kwa CCM, baada ya mabadiliko hayo naamini sasa changamoto kubwa ipo kwa hiyo sekretarieti mpya ihakikishe inabadili mfumo, itoke kwenye sera za kitamaduni tulizorithi ikipeleke chama kwenye sera za kisasa.
Sekretarieti iliyopita ilikuwa inasubiri vikao na taratibu bila kujali madhara yanayokikumba chama kwa kuchelewa kutoa maamuzi kwa wakati. Ilifika kipindi chama kinafanya mabadiliko kutokana na kauli ya wapinzani.
Naishauri sekretarieti mpya kurejesha heshma na imani ya chama tunategemea mabadiliko makubwa sasa, alisema Makonda huku akiongeza kwamba kinachotakiwa ni kubadili mfumo.
Alisema UVCCM maadili ipo kwenye mchakato wa kuunda umoja mpya utakaosaidia kukuza na kukiimarisha chama huku akibainisha kwamba wanaruhusiwa kufanya hivyo kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho.