Wasichana wote waliofaulu wachaguliwa kidato cha tano!

corlpole

Member
Nov 21, 2010
11
0
Habari hii ni ya ushindi wa malengo ya elimu, au huzuni kwa wanazuoni?
Habari jamvini!
Mimi nimeisoma hii kwenye mwananchi jana, na nimesikitika sana. Nini maana yake, tuna shule nyingi za A level kiasi chakututosha wote, au ufaulu umeshuka kupita wakati wowote katika historia ya elimu?
Nafikiri ukiweka mizani katika hili utapata jawabu.
Ombi langu kwa serikali na wizara ya elimu, tuweke mkazo zaidi katika kuboresha mazingira ya elimu, ukijumuisha walimu, majengo na elimu kwa vitendo.
Nitasikitika zaidi pindi mtakaposema mmefanikiwa malengo yenu kwani sitaelewa malengo yapi yamefanikiwa!
Mwaka jana 2010 42.33%
mwaka huu 100%
na hamna hata shule moja iliyoongezwa!
Jamani tuwe makini na hili, hawa ndio viongozi, wafanyakazi, wafanyabiashara wa TZ ya kesho!
Wapi tunaenda??!
 
Back
Top Bottom