Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,297
- 33,082
Majambazi saba wakiwa na mashine za ukweli (bunduki), wameteka basi na kupora mali na fedha...huku wakiwashusha abiria hao mmoja mmoja na kuwaamuru kusaula viwalo na kubaki kama walivyozaliwa.
Katika songombingo hilo Suka (Dereva) wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Ahmed Hilali, alibandikwa risasi kichwani na kujeruhiwa ile kinoma.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Celina Kaluba amelitaja basi lililotekwa na majambazi hao kuwa ni mali ya kampuni ya Sunset ya mjini Singida na lilikuwa likitokea katika kijiji cha Iyumbu kwenda Singida Town.
Afande Kaluba amesema kabla ya kuliteka basi hilo, majambazi hayo yalifyatua risasi iliyovunja kioo kikubwa cha mbele kwa lengo la kulisimamisha...risasi ambayo ilimpata suka kichwani
Akifafanua Afande Kaluba alisema majambazi hayo yaliamuru abiria wote na wafanyakazi wa basi hilo kuteremka na kuvua nguo kabla ya kuanza kuwapora fedha na mali nyingine.
Hata hivyo mama mmoja alifanikiwa kuokoa fedha zake zaidi ya Sh. milioni 1.8, baada ya kufanikiwa kuzificha ndani ya basi, wakati wa purukushani ya kuteremka chini na kuvua nguo.
Katika songombingo hilo Suka (Dereva) wa basi hilo aliyejulikana kwa jina la Ahmed Hilali, alibandikwa risasi kichwani na kujeruhiwa ile kinoma.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida, Celina Kaluba amelitaja basi lililotekwa na majambazi hao kuwa ni mali ya kampuni ya Sunset ya mjini Singida na lilikuwa likitokea katika kijiji cha Iyumbu kwenda Singida Town.
Afande Kaluba amesema kabla ya kuliteka basi hilo, majambazi hayo yalifyatua risasi iliyovunja kioo kikubwa cha mbele kwa lengo la kulisimamisha...risasi ambayo ilimpata suka kichwani
Akifafanua Afande Kaluba alisema majambazi hayo yaliamuru abiria wote na wafanyakazi wa basi hilo kuteremka na kuvua nguo kabla ya kuanza kuwapora fedha na mali nyingine.
Hata hivyo mama mmoja alifanikiwa kuokoa fedha zake zaidi ya Sh. milioni 1.8, baada ya kufanikiwa kuzificha ndani ya basi, wakati wa purukushani ya kuteremka chini na kuvua nguo.