Kibunago
JF-Expert Member
- Jan 11, 2008
- 300
- 122
Kuna Washiriki fulani wanaojirudia rudia kila kipindi cha Malumbano ya Hoja ITV kama vile, Ibrahim Dimoso (aka mwananchi wa kawaida), Ole, ndg. Aweda, ndg. Ngowi n.k. Je, ina maana hao ndio role models wa malumbano ya nguvu au kwamba wao ndio wenye ujuzi mpana wa kila aina ya mada na uzoefu (jack of all trades) au nayo imekuwa forum fulani ya kuuza sura?
Mtu anaweza kuwa mzuri katika eneo fulani lakini akachafua sana kwa kuchangia katika eneo asilokuwa na utaalamu nalo kwa undani. Mfano Dimoso kukataa kuwa kondomu si chochote katika kinga dhidi ya ukimwi ni mchango unaoweza kuwa janga la upotoshwaji sana kwa Taifa.
Hali halisi iko wazi juu ya uambukizwaji magonjwa ya zinaa (STIs) kama Kaswende n.k kati ya miakaya 1980 na kurudi nyuma na zile za miaka ya 1990 kwenda mbele.
Ni kweli, hatutegemei kuwa na watu wajuzi tu katika kipindi kama hicho cha malumbano lakini pia hatutegemei kuwa na washiriki fulani ambao wapo karibu kila kipindi bila sababu za msingi!
Mtu anaweza kuwa mzuri katika eneo fulani lakini akachafua sana kwa kuchangia katika eneo asilokuwa na utaalamu nalo kwa undani. Mfano Dimoso kukataa kuwa kondomu si chochote katika kinga dhidi ya ukimwi ni mchango unaoweza kuwa janga la upotoshwaji sana kwa Taifa.
Hali halisi iko wazi juu ya uambukizwaji magonjwa ya zinaa (STIs) kama Kaswende n.k kati ya miakaya 1980 na kurudi nyuma na zile za miaka ya 1990 kwenda mbele.
Ni kweli, hatutegemei kuwa na watu wajuzi tu katika kipindi kama hicho cha malumbano lakini pia hatutegemei kuwa na washiriki fulani ambao wapo karibu kila kipindi bila sababu za msingi!