washikaji yamenikuta...isssue yenyewe ni kwamba nimekuwa na girl friend wangu katika uhusiano mzuri sana kwa miaka miaka, na kweli nilikuwa na imani naye sana kiasi kwamba hata mara moja sikuwahi kuhisi kuwa anaweza kuwa na mshikaji mwingine. NIlipopaswa kwenda masomoni, alinipa viapo ambavyo hata mimi vilinifanya niwe mwaminifu huku niliko kwa kumkumbuka yeye. Tumekuwa vile na mambo yalikuwa shwari kabisa. One tukiwa out, nislishtuka kuona anapokea simu zinazo mshitua, and then nikachukua simu yake na kuona message eti CHUPI INAFICHA MAMBO MENGI SANA, HATA MIMI NAKUPENDA SANA TENA SANA TU...niliishiwa nguvu na sikuweza kumwuliza chochote kwa kuchanganyikiwa. then once nilipomuuliza alikuwa na kila sababu ya kujitetea, lakini mimi nilipumbaa na kuzidi kumwamini. BAada ya kuwa likizio tena nilimtembelea katika kituo chake cha kazi naye akawa ananitambulisha kwa washikaji zake et mimi ni kaka yake, kitu ambacho sikuweza kukielewa kabisa, na akawa na tabia ya ajabu, kwa mfano hakutaka hata mara moja kunibusu hadhalani nk. Nikaona makubwa na kuamua kuongea naye seriously, bado hakutaka kuniambia ukweli, then nikwambwambia dear if things must be like this then we better stop our relationship, akajidai kulia nk, na kuomba tuendelee kuwa na uhusiano ingawa hataki kunieleza kulikoni, cha ajabu zaidi sasa ni mwezi umepita simpati kwa simu, nahisi kabadili namba namba. naomba ushauri wenu washikaji nifanyeje mimi na kiumbe huyu??