Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #41
Nadhani kuna kitu bado tunakimiss kwenye mjadala huu.. na Pundit na Sahara mmekigusia kwa mbali...
Wazungu (includes Wajapan) wanasikilizwa zaidi kwa sababu ya 'ngozi' yao siyo elimu. Miaka fulani nikiwa kwenye semina niliuona ukweli huu. Watu waliokuwa wanaendesha semina hiyo kwenye ukumbi wa then Nyegezi Social, walikuwa wanatoka Dar wizara fulani.
Basi semina tukawa tumegawanyika kwenye makundi na watu wakawa wanatoa maoni juu ya kutatua jambo fulani. Sasa kwenye majumuisho kundi kubwa la waswahili wenzangu toka kijijini wakawa wamependekeza jambo fulani ambalo naamini lilikuwa na mantiki. Wenye semina wakalipinga kwa visingizio kadhaa kuwa halitekelezeki bla bla bla.. Na tena walionesha kama kebehi ya aina fulani kwamba "tulithubutuje kufikiria jambo kama hilo huko kijijini".
Uzuri wake ni kuwa tulikuwa na Padre Mmoja toka Bariadi (nakumbuka jina lake Fr. Gappa) amekaa Tanzania kwa karibu miaka thelani na ana kimwaga kisukuma utadhani ni ngosha! basi yeye hakuwa kwenye kundi letu; basi akasimama na kutoa pendekezo lile lile; wakuu wa semina wakalikubali! Sasa inawezekana kulikuwa na sababu nyingine lakini tuliokuwapo tulihisi kitu kimoja tu hatukusikilizwa kwa sababu hatukuwa wazungu siyo wasomi...
Sasa naamini wataalam wa kizungu wakituambia kuwa Takakata ni mbaya mtaani tutasimama kusafisha; lakini akija mbondei mwenzetu na kusema Takataka ni mbaya tutamkodolea macho na kumpuuza!!
Hivi kweli mnafikiri Tanzania ingetaka kupata net milioni tano kwa kila Mtanzania tungeshindwa? Kwanini hiyo impromptu idea ya Bush ilishangaliwa?
Wazungu (includes Wajapan) wanasikilizwa zaidi kwa sababu ya 'ngozi' yao siyo elimu. Miaka fulani nikiwa kwenye semina niliuona ukweli huu. Watu waliokuwa wanaendesha semina hiyo kwenye ukumbi wa then Nyegezi Social, walikuwa wanatoka Dar wizara fulani.
Basi semina tukawa tumegawanyika kwenye makundi na watu wakawa wanatoa maoni juu ya kutatua jambo fulani. Sasa kwenye majumuisho kundi kubwa la waswahili wenzangu toka kijijini wakawa wamependekeza jambo fulani ambalo naamini lilikuwa na mantiki. Wenye semina wakalipinga kwa visingizio kadhaa kuwa halitekelezeki bla bla bla.. Na tena walionesha kama kebehi ya aina fulani kwamba "tulithubutuje kufikiria jambo kama hilo huko kijijini".
Uzuri wake ni kuwa tulikuwa na Padre Mmoja toka Bariadi (nakumbuka jina lake Fr. Gappa) amekaa Tanzania kwa karibu miaka thelani na ana kimwaga kisukuma utadhani ni ngosha! basi yeye hakuwa kwenye kundi letu; basi akasimama na kutoa pendekezo lile lile; wakuu wa semina wakalikubali! Sasa inawezekana kulikuwa na sababu nyingine lakini tuliokuwapo tulihisi kitu kimoja tu hatukusikilizwa kwa sababu hatukuwa wazungu siyo wasomi...
Sasa naamini wataalam wa kizungu wakituambia kuwa Takakata ni mbaya mtaani tutasimama kusafisha; lakini akija mbondei mwenzetu na kusema Takataka ni mbaya tutamkodolea macho na kumpuuza!!
Hivi kweli mnafikiri Tanzania ingetaka kupata net milioni tano kwa kila Mtanzania tungeshindwa? Kwanini hiyo impromptu idea ya Bush ilishangaliwa?