Washabiki wa Abdoulaye Wade washangilia mitaani; Kikwete amejifunza nini?

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Maajabu!!!!!
Wakati aliyekuwa Rais wa Senegal amekubali kushindwa Urais na mpinzani wake Macky Sall, wale wote waliokuwa wakimshabikia Wade, wamejitokeza mtaani kushangilia ushindi wa Sall. Hii ukiiangalia kwa haraka, unaweza kuchanganyikiwa. Sababu unaweza kuona watu wamekuja kwa wingi kukusikiliza, kula nawe, na kushangilia, ukadhani hao wanakuunga mkono kumbe wapi... Inawezekana wanashangilia kwa vile kuna faida wanayoipata kwa kupiga makofi hata kama ni ya muda mfupi.

Watu hao hao walishiriki kupiga kura! mara ya kwanza, wagombea wakashindwa kufikia idadi ya kura. Kura zikarudiwa, Wade aliendelea kupata watu wengi wanaomshangilia kwa bidii. Siku ya kura ikafika, zikapigwa na matokeo yakaonesha Sall ameshinda kwa kura 30,000 wakati Wade amepata kura 11,000. Kumbuka waliokuwa wanamshangilia ndio waliopiga Kura. Jua kuwa wakati uchaguzi unafanywa, Alikuwa bado na madaraka yote na dola ilitumika lakini hayo yote hayakuweza kuizuia nguvu ya Umma kufanya kazi.

Sasa kwa JK ambapo maroli hutumika kusomba wananchi ili wamsikilize hata wakati ambao siyo wa Uchaguzi, hali itakuwaje? Mwezi Feb Rais Kikwete alikuwa Mwanza kwenye sherehe ya CCM kutimiza miaka 35 ya kuanzishwa kwake alipochinja ng'ombe 55 wakati watu wanakufa muhimbili, wananchi wakiona haya yote. Siku hiyo maroli yaliyosomba wananchi kuwaleta Kirumba kula, hayahesabiki. Kwa hiyo utaona wananchi wengi kwa sababu ya Lift, fedha na chakula!

Asije akashangaa mwaka 2015 ya wade yakimpata!

Quality


:scared:
 
Lini tutaanza kuheshimu matokeo ya uchaguzi kama yalivyo? Senegal wameonyesha mfano!
 
Maajabu!!!!!
Wakati aliyekuwa Rais wa Senegal amekubali kushindwa Urais na mpinzani wake Macky Sall, wale wote waliokuwa wakimshabikia Wade, wamejitokeza mtaani kushangilia ushindi wa Sall. Hii ukiiangalia kwa haraka, unaweza kuchanganyikiwa. Sababu unaweza kuona watu wamekuja kwa wingi kukusikiliza, kula nawe, na kushangilia, ukadhani hao wanakuunga mkono kumbe wapi... Inawezekana wanashangilia kwa vile kuna faida wanayoipata kwa kupiga makofi hata kama ni ya muda mfupi.

Watu hao hao walishiriki kupiga kura! mara ya kwanza, wagombea wakashindwa kufikia idadi ya kura. Kura zikarudiwa, Wade aliendelea kupata watu wengi wanaomshangilia kwa bidii. Siku ya kura ikafika, zikapigwa na matokeo yakaonesha Sall ameshinda kwa kura 30,000 wakati Wade amepata kura 11,000. Kumbuka waliokuwa wanamshangilia ndio waliopiga Kura. Jua kuwa wakati uchaguzi unafanywa, Alikuwa bado na madaraka yote na dola ilitumika lakini hayo yote hayakuweza kuizuia nguvu ya Umma kufanya kazi.

Sasa kwa JK ambapo maroli hutumika kusomba wananchi ili wamsikilize hata wakati ambao siyo wa Uchaguzi, hali itakuwaje? Mwezi Feb Rais Kikwete alikuwa Mwanza kwenye sherehe ya CCM kutimiza miaka 35 ya kuanzishwa kwake alipochinja ng'ombe 55 wakati watu wanakufa muhimbili, wananchi wakiona haya yote. Siku hiyo maroli yaliyosomba wananchi kuwaleta Kirumba kula, hayahesabiki. Kwa hiyo utaona wananchi wengi kwa sababu ya Lift, fedha na chakula!

Asije akashangaa mwaka 2015 ya wade yakimpata!

Quality


:scared:

Irrelevant, JK hagombei 2015, umeandika vizuri mwanzoni ila umemalizia hovyo, these are distinguishable cases
 
Samahani mkuu mleta mada. Mshindi kapata kura 30,000???? au umekosea. Hii nchi ni kama Jimbo la Ubungo pekee.
 
Two different Scenarios, labda ingekuwa kipindi cha uchaguzi wa Dr Salmin Amour Vs Maalim Seif ungeweza kusema hayo...
 
Maajabu!!!!!

Siku ya kura ikafika, zikapigwa na matokeo yakaonesha Sall ameshinda kwa kura 30,000 wakati Wade amepata kura 11,000.

Huo utakuwa na equivalent na uchaguzi wa DIWANI kwa Tangayika au WAWAKILISHI kwa upande wa Zanzibar.
Rais anachaguliwa kwa kura 30,000 tu! Urais mwingine ni sawa na urais wa TFF tu!
 
Mimi kwa hapa kwetu sina imani na tume ya uchaguzi kabisaaa hata huyu jaji lubuva, ngoja tuone kwanza arumeru kama watatenda haki na chaguzi nyingine zijazo kabla ya 2015 kwani nina imani magamba yataendelea kupukutika tu
 
yule bwana Wade alitaka kubadili katiba aendelee kuongoza lakini Jk ni kipindi chake cha pili kikatiba ni wapi anatakiwa kujifunza wakati mazingirza ya mvutano wa kisiasa wa senegal na Tanzania ni tofauti?

Kikwete yuko kikatiba ajifunze nini huko?
 
Lini tutaanza kuheshimu matokeo ya uchaguzi kama yalivyo? Senegal wameonyesha mfano!

Matokeo ya chaguzi yataheshimika pale ambapo kutoyaheshimu kutakapoonekana kama kumwagia petrol kwenye moto. Hizi nchi wanaoheshimu matokeo usidhani ilikuwa rahisi, kuna mazingira ya kuyaheshimu yamejengwa. Nina jamaa yangu wa karibu sana ni raia wa Ghana, ananiambia Ghana haiibiwi hata kura moja, watu wanahesabu kura na kujumlisha hata kabla ya tume kutangaza wanakuwa wamejua nani mshindi, Tume ikifanya tofauti tu panachimbika, utamaduni huo umejenga uangalizi wa kura kuwa kama vile ku-handle bomu la nyukilia lisiwalipukie.
 
Hilo ni funzo kwa pande zote mbili,wapo waloshabikia wagombea flani ili wasitengwe kwenye nyumba za Ibada,wapo waloshabikia ili wasipoteze Ajira,wapo waloshabikia wapate madaraka lakini jambo la msingi linalochelewesha mabadiliko ni unafiki wa watanzania mnchana makelele kibao jion moja kabla ya uchaguzi wanakodisha kadi zao kwa buku kumi! hapo hata kama tutawalaumu wakodishaji tunapaswa pia kujadili kwa kina Unafiki wa hawa "wakodishaji wa shahada",mara kadhaa viongozi wa upinzani wakiwa hapa wanaulizwa waeleze kwa ufasaha wanaibiwa vipi kura wanashindwa kujieleza,angalau Maalim Seif wakati flani aliweza kushawishi nchi wahisani kuelewa kilio chake,wengine wanakuja na majibu ya mitaani eti kuna kura za kichina!.CCM bado haijachokwa na Watanzania
 
Maajabu!!!!!
Wakati aliyekuwa Rais wa Senegal amekubali kushindwa Urais na mpinzani wake Macky Sall, wale wote waliokuwa wakimshabikia Wade, wamejitokeza mtaani kushangilia ushindi wa Sall. Hii ukiiangalia kwa haraka, unaweza kuchanganyikiwa. Sababu unaweza kuona watu wamekuja kwa wingi kukusikiliza, kula nawe, na kushangilia, ukadhani hao wanakuunga mkono kumbe wapi... Inawezekana wanashangilia kwa vile kuna faida wanayoipata kwa kupiga makofi hata kama ni ya muda mfupi.

Watu hao hao walishiriki kupiga kura! mara ya kwanza, wagombea wakashindwa kufikia idadi ya kura. Kura zikarudiwa, Wade aliendelea kupata watu wengi wanaomshangilia kwa bidii. Siku ya kura ikafika, zikapigwa na matokeo yakaonesha Sall ameshinda kwa kura 30,000 wakati Wade amepata kura 11,000. Kumbuka waliokuwa wanamshangilia ndio waliopiga Kura. Jua kuwa wakati uchaguzi unafanywa, Alikuwa bado na madaraka yote na dola ilitumika lakini hayo yote hayakuweza kuizuia nguvu ya Umma kufanya kazi.

Sasa kwa JK ambapo maroli hutumika kusomba wananchi ili wamsikilize hata wakati ambao siyo wa Uchaguzi, hali itakuwaje? Mwezi Feb Rais Kikwete alikuwa Mwanza kwenye sherehe ya CCM kutimiza miaka 35 ya kuanzishwa kwake alipochinja ng'ombe 55 wakati watu wanakufa muhimbili, wananchi wakiona haya yote. Siku hiyo maroli yaliyosomba wananchi kuwaleta Kirumba kula, hayahesabiki. Kwa hiyo utaona wananchi wengi kwa sababu ya Lift, fedha na chakula!

Asije akashangaa mwaka 2015 ya wade yakimpata!

Quality


:scared:
Kwani JK amekwambia anataka kubadilisha Katiba agombee mara ya tatu 2015? Acha hizo!
 
Back
Top Bottom