warning to CHADEMA

SILENT GUNNER

Member
Jan 23, 2012
22
9
Jamani kama mwanachama wa chadema na mwenye mapenzi mema na chadema,nimemsikiliza shibuda akihojiwa na radio one katika kipindi cha nipashe asubuhi na nimeamini kweli ana kusudia kugombea urais,pamona na lengo lake nimemsikia akiwa na mtazamo wa kukikandia chama et ni cha kidictator na ukabila. jamani hamna namna ya kuliengua hili gamba? najisikia hasira nikikumbuka uwepo wa jitu kama hili chadema. Anawezaje kulala chadema kula ccm? na kwann aombe msaada jk amsaidie kama sio jitu lililotumwa na magamba? Lets he careful kupokea mtu na kumpa madaraka
 
Huyu ni wa kupiga Pichi ili aungane na wakina Kafurila, Rashidi Mohamed katika Ubunge wa Mahakama, najua akipigwa chini atachonga sana, ila ni wa kupiga chini tu, na CHADEMA wahakikishe 2015 hakanyagi Bungeni kwamwe ni Bora kilikosa Jimbo kabisa lakini asikanyage Bungeni kwa Tiketi ya Chama chochote kile, Ndo dawa yake,
 
Jamani kama mwanachama wa chadema na mwenye mapenzi mema na chadema,nimemsikiliza shibuda akihojiwa na radio one katika kipindi cha nipashe asubuhi na nimeamini kweli ana kusudia kugombea urais,pamona na lengo lake nimemsikia akiwa na mtazamo wa kukikandia chama et ni cha kidictator na ukabila. jamani hamna namna ya kuliengua hili gamba? najisikia hasira nikikumbuka uwepo wa jitu kama hili chadema. Anawezaje kulala chadema kula ccm? na kwann aombe msaada jk amsaidie kama sio jitu lililotumwa na magamba? Lets he careful kupokea mtu na kumpa madaraka

Chadema needs high technicalities to get rid of this stupid guy!! wasikurupuke, atakwenda mahakamani atawashinda kama hawajamwekea mtego wa kisheria/kichama wa/kikatiba ya CDM kumnasa na kumtema. Si vizuri jitu kama hili kwenda mahakamani likakushinda!!! Historia hufunza , si tunaona akina Hamad Rashid et al wote wako mahakamani, wakifanya ubunge wa mahakama!!!
 
Shibuda ni mzigo ata alipokuwa CCM nako alikuwa ni mzigo unao kera......ni mtu anayepanda kuropoka na kujifanya anakijua sana kiswahili na nahau zake,ila ameingia kingi,amewakuta Chadema wako so smart,wana msikilizia tu na kumcheki kwenye darubini.....elimu yake ni form IV...hatafika mbali.....!
 
We ndo umestuka leo! mi tangu ameangushwa kura za maoni kule Maswa na lilivyokimbilia CDM nililitambua mapema sana.
cha kufanya ni kulipuuza na kulifanya lifanye ubunge wake kama wa John Cheyo. Kwa kulitafutia zengwe au ku ague nalo ni kutafuta balaa kutoka kwenye magazeti uchwara kama Uhuru,Mzalendo na Habari leo.
 
SI-HA-SA msishangae anaweza kuwa anaropoka ili kujua msimamo wa upande wa pili
 
Shibuda kachanganyikiwa anajua ubunge ndiyo kwaheri hiki ni kipindi chake cha mwisho. Anajua fika cdm haitampitisha hata ccm anakojikomba hawamhitaji. Ninaloweza kumshauri akae na majimarefu amfundishe masuala ya uganga ili asife njaa kuanzia 2016. Elimu, upeo na fikra zake hazimruhusu tena kuwa hata diwani chama chochote ikiwemo magamba.
 
Ila napongeza CHADEMA kwa kuliona hili mapema make kuna kipindi alikuwa awe Mwenyekiti wa CHADEMA MKOA WA SHINYANGA NA HAPO NDO INGEKUWA BALAA SANA, Kwa sasa zaidi ya Ubunge hana cheo kingine CHADEMA so hata akipigwa chini au akakimbilia CCM atakuwa wakawaida tu,

Huyu ni zaidi ya Kinyonga, nakumbuka wakati alipigwa chini CCM kwenye kura za maoni aliichuria CCM ile mbaya, na shangaa juzi kuanza kuwasifia, na hata huko CCM KUNA ANACHO TAFUTA,
 
Tafakarini zaidi!! Ikiwa ametumwa(cdm walishaligundua hili) mjue ana suport kubwa nyuma yake toka magamba, tukimpuga bila vigezo imara atatusumbua, ukizingatia mahakama ni zao!!

Kumbukeni mtu wa namna hii anakuwa anafanya hayo kwa umakini mkubwa wa ki-sheria, anajipanga maana anajua alifanyalo!!

CHADEMA tunatakiwa kumg'oa mtu huyu kabla ya 2014, lakini kwa umakini mkubwa!! Shetani ni shetani tu hapatani na utakatifu!!
 
Chadema needs high technicalities to get rid of this stupid guy!! wasikurupuke, atakwenda mahakamani atawashinda kama hawajamwekea mtego wa kisheria/kichama wa/kikatiba ya CDM kumnasa na kumtema. Si vizuri jitu kama hili kwenda mahakamani likakushinda!!! Historia hufunza , si tunaona akina Hamad Rashid et al wote wako mahakamani, wakifanya ubunge wa mahakama!!!
Nakubaliana na wewe kuwa hata akifukuzwa uanachama, bado ataendelea na ubunge kwa amri ya mahakama pengine hadi uchaguzi mwingine 2015. Kuna haja ya kuangalia sheria hii. Hivi ikija kuthibitika mahakamani kuwa Kafulila au Hamad walifukuzwa uanachama kihalali, hii mishahara na posho wanazoendelea kulipwa watazirudisha hazina? Wanasheria tusaidieni katika hili.
 
Mimi nasubiri nione mchezo utavyochezwa na hapo ndipo CDM watakuwa wamejiongezea umaarufu kichama. MUNGU IBARIKI 'CDM'
 
Huyu ni wa kupiga Pichi ili aungane na wakina Kafurila, Rashidi Mohamed katika Ubunge wa Mahakama, najua akipigwa chini atachonga sana, ila ni wa kupiga chini tu, na CHADEMA wahakikishe 2015 hakanyagi Bungeni kwamwe ni Bora kilikosa Jimbo kabisa lakini asikanyage Bungeni kwa Tiketi ya Chama chochote kile, Ndo dawa yake,
Bwana Komandoo na wengine msiwe na wwasi wasi na hkuna sababu ya kumpiga chini bw Shibuda. CHADEMA ni chama makini na kila mtu ndani ya chama ana uhuru wake ila chama kina taratibu zake. Hata watoto wa familia moja hawafanani lakini wote ni watoto wa alio nao.
 
...
Huyu ni zaidi ya Kinyonga, nakumbuka wakati alipigwa chini CCM kwenye kura za maoni aliichuria CCM ile mbaya, na shangaa juzi kuanza kuwasifia, na hata huko CCM KUNA ANACHO TAFUTA,
CDM ndio wanatakiwa kujifunza. Huyu alipopigwa chini kura za maoni, alisema wazi kuwa anatafakari aende wapi, lakini pia akasema kuna vyama zaidi ya vitatu vimemuomba ajiunge navyo. Pengine kwa kiu ya kuongeza viti au kuogopa kuwahiwa na vyama vingine, CDM kupitia kwa Zitto (Atanisamehe kama sivyo) ndio waliokwenda kumuomba ajiunge nao.
Matunda yake tumeyaona, na wengine tuliposikia nyimbo za wabunge 70 na mawaziri kutaka kujiunga CDM tulihisi kama tuna viongozi walevi huko juu.
 
Ndio maana William@Mzakwe-Dodoma ametangaza leo kuwa Shibuda ni KENGE aliye kwenye msafara wa mamba!
Nakubaliana naye 100%!
 
Shibuda ni wa kuogopa kuzidi ukoma,mtengeni kabisa kama mchawi anavyotengwa kijijini,msimuhusishe na shuguli zozote z chama,wala kwenye vikao msimkaribishe,muacheni aendelee kujishushia heshima katika jamii,na dont argue with a fool ,people might not see the difference.Muacheni abwabwaje,ni upepo tu utapita.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom