KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,139
Najua wapo watu hii hawatapenda kuisikia zitto alihusika kwa kiasi kikubwa kufanikisha hili....lakini ndio hali halisi,lazima tuiseme .
Wadau mi nadhani baadhi yetu wakati umefika sasa tubadili mitazamo yetu kuhusu ZITTO KABWE;kiukweli kijana anaonyesha ukomavu wa kisiasa kila kukicha tofauti na vijana wengi ambao wanakimbilia posho tu; Zitto kumbe anafanya mambo mengi bila kupiga mayowe wala kuita wapiga picha...hili nalisema kufuatia kugundua kuwa Mh. zitto kabwe kuwa chanzo cha mazungumzo maarufu yanayoendelea ikulu kati ya chadema na Rais kikwete,mambo yako hivi.....
Safari ilianza hivi; baada ya kuona mwenendo wa mijadala na mwelekeo wa baadhi ya viongozi wenzake, hasa katika siku ambazo CHADEMA kilikuwa kinatangaza kwamba kingeitisha maandamano nchi nzima kupinga mchakato wa katiba mpya uliokuwa umewasilishwa na Serikali bungeni, baadhi ya wanaCHADEMA na wengine miongoni mwa umma, walihisi kuwako kwa hatari ya kweli ya vurugu kuibuka nchini, ambayo isingekisaidia chama hicho au kundi jingine lolote, hivyo Zitto alifunga safari kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam ili kuteta na Dk. Slaa.
Katika mazungumzo yao, vyanzo kadhaa vya habari vimesema, hoja ilikuwa ni umuhimu wa kuchukua njia ya mazungumzo katika suala la mchakato wa katiba mpya, kuliko njia ya maandamano. Lakini Dk. Slaa amekaririwa akiashiria kwamba ilikuwa vigumu zaidi kuanzisha njia ya mazungumzo kwake kuliko njia ya shinikizo kupitia maandamano.
Raia Mwema limeambiwa kwamba kutokana na ugumu huo, Dk. Slaa amekaririwa kumueleza Zitto kuwa wanaweza, katika kufikia kupata muda wa kukutana na Rais Jakaya Kikwete, kuwatumia wazee wenye utulivu na busara, wasio na misimamo mikali ya kisiasa, wenye kutanguliza mbele maslahi ya nchi na wanaosimamia zaidi nguvu ya hoja, ambao miongoni mwao ni Dk. Salim na Jaji Warioba.
Habari zinasema, tatizo kubwa alilokuwanalo Dk. Slaa katika kuwafikia wazee hao ni kwamba hakuwa na ukaribu wa kiasi hicho nao na Raia Mwema limeelezwa kwamba katika mazingira hayo ndipo Zitto alipoahidi kuwatafuta wahusika na kuwaeleza mtazamo huo na kisha kusikiliza mawazo yao.
"Zitto alikwenda kuwaona Jaji Warioba na Dk. Salim na wakati huo, vikao vya Bunge vilikuwa vikiendelea Dodoma. Kule wale wazee walimsikiliza Zitto na kuona mapendekezo yao yana mantiki na kwa hiyo, Zitto akarudi kumweleza Dk. Slaa na baadaye wakapanga kukutana na Warioba na Salim.
"Walizungumza sana, wakafanya uchambuzi wa kina na njia bora zaidi ya kuweza kufikisha suala hilo kwa Rais Kikwete. Jaji Warioba aliombwa afanye kazi hiyo kuwa kiunganishi na taarifa zinasema baada ya kujiridhisha na hali ya mambo naye aliwasiliana na Ikulu na mchakato ukaanza.
Ndani ya Kamati Kuu CHADEMA
Habari za uhakika zinasema baada ya Dk. Slaa na Zitto kukubaliana na akina Warioba, kibarua kigumu kwao kilikuwa kuwasilisha mawazo yao mbele ya Kamati Kuu ya CHADEMA.
Taarifa hizo zinaelezwa kuwa Zitto hakuwa amehudhuria kikao hicho cha Kamati Kuu na hivyo, mzigo ulibaki kwa Dk. Slaa. Wakati huo, Zitto alikuwa amerejea kutoka India alikokuwa akitibiwa na hivyo hakuweza kushiriki kikao cha Kamati Kuu kwa sababu ya hali yake kiafya kutoimarika.
"Zitto aliitwa na Dk. Slaa kwenye Kamati Kuu amsaidie kueleza suala hilo, tulimwona alikuwa ametoka kuumwa alijitahidi sana kujieleza. Lakini kabla ya hapo, uchokozi wa wazo hilo uliibuliwa na Regia Mtema, ambaye alisema tukamwone Rais Kikwete ili tuzungumze naye....wajumbe karibu wote wakaguna wakimpinga na kumwona msaliti, wengine wakisema eti katumwa.
"Baada ya Zitto kuitwa na Dk. Slaa, ndipo alianza kutoa maelezo na hatimaye wajumbe wakaridhia. Na baadaye Mbowe akaandika barua kwenda kwa Rais kuomba kukutana naye ili kuwasilisha mapendekezo ya chama," kinaeleza chanzo chetu cha habari.
Warioba ‘messanger' mtiifu
Habari zinasema baada ya Mbowe kuandika barua ya kuomba kukutana na Rais Kikwete, Jaji Warioba ndiye aliyekuwa ‘wakala' wa mawasiliano kati ya pande hizo mbili, yaani CHADEMA na Rais Kikwete.
"Barua ile alipewa Jaji Warioba naye binafsi kwa mkono wake aliifikisha Ikulu moja kwa moja kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye baadaye alifanya mazungumzo na Kikwete pamoja na Dk. Salim na kisha kukubali ombi hilo la CHADEMA.
"Warioba akarejea tena kwa viongozi wa CHADEMA kwa ajili ya kutoa majibu kama ‘mjumbe' na akaeleza kuwa Rais hana tatizo kukutana na ujumbe wa CHADEMA kwa sababu hili ni suala la kitaifa, si la kwake pekee," anaeleza mtoa taarifa huyo.
Waziri Mkuu Pinda arudi Dar
Kutokana na kuanza kwa mchakato huo wa ‘kimya kimya' vyanzo vyetu vya habari kutoka bungeni vinaeleza kuwa mjadala wa sheria hiyo ulikuwa ukisogezwa mbele kwa maelezo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ili kutoa nafasi kwa mchakato huo wa CHADEMA, Dk. Salim, Jaji Warioba na Rais Kikwete, ambao mpaka wakati huo haukuwa rasmi, ushike kasi.
Vyanzo vingine vya habari vimesema kuna wakati Waziri Mkuu Pinda alikwenda Dar es Salaam kutoka Dodoma kwa ajili ya mazungumzo kuhusu suala hilo na baada ya mjadala wa sheria hiyo kusogezwa mbele kujadiliwa bungeni kwa mara kadhaa, ilibidi mjadala uruhusiwe.
Milango ya Ikulu yafunguliwa
Baada ya kazi hiyo ya ‘kimya kimya' na baada ya Bunge kujadili, kurekebisha na hatimaye kupitisha muswada huo, ujumbe wa CHADEMA ulikaribishwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya mazungumzo.
Makaribisho hayo yaliwekwa bayana na Ikulu kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano na kuanza rasmi Novemba 27, mwaka jana, na kurejewa tena siku iliyofuata, Novemba 28, kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuipa nafasi Serikali iweze kutafakari mapendekezo ya CHADEMA kuhusu sheria hiyo.
"Katika mkutano huo, pande zote mbili zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu sana kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na umoja wa kitaifa," inaeleza taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu iliyotolewa baada ya duru la kwanza la mazungumzo hayo.
Kamati Kuu CCM yatia neno
Hata hivyo, wakati CHADEMA wakiwa wameomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya mazungumzo, Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilikuwa inaendelea na kikao chake mjini Dodoma, ambako ilimshauri Rais Kikwete kutanua wigo kwa kukutana na wadau wengine, ambao ni pamoja na vyama vingine vya siasa, ambavyo hata hivyo, tayari vimeonana na kuzungumza na Kikwete. Vyama hivyo ni Chama cha Wananchi (CUF) na NCCR-Mageuzi.
Kwa upande mwingine, ushauri huo wa Kamati Kuu ya CCM ulizua mjadala mpya katika jamii, wengine wakiupinga na kuukosoa, wengine wakiuunga mkono lakini mwishowe, Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho kikongwe nchini, aliuzingatia.
Viongozi wanne waibuka vinara
Kama suala hili litafikia hatua nyingine katika hali isiyokuwa na malumbano tofauti na dalili za awali zilivyokuwa zikiashiria, basi, vinara wa kutuliza hali hiyo ni pamoja na Rais Kikwete binafsi ambaye aliridhia kukutana na wawakilishi wa makundi tofauti licha ya muswada kupitishwa na Bunge naye mwenyewe kuutia saini kuwa sheria.
"Angeweza kugoma na kutumia ubabe wa dola kulazimisha mambo, lakini hakufanya hivyo," kinaeleza chanzo chetu cha habari na kuongeza kuwa; "Shukurani za kipekee ziwaendee Dk. Slaa, Zitto, Dk. Salim na Jaji Warioba, wameonyesha upeo mkubwa wa kiuongozi."
Muswada kufanyiwa marekebisho
Taarifa zaidi zinabainisha kuwa mazungumzo hayo pamoja na ya vyama vingine yamezingatiwa na Rais Jakaya Kikwete na kwa hiyo, katika mkutano ujao wa Bunge unaonza wiki ijayo mjini Dodoma, sheria hiyo ya mchakato wa Katiba mpya nchini itafanyiwa marekebisho.
Miongoni mwa mapendekezo hayo ni kurejesha uwezekano wa viongozi wanasiasa, wakiwamo wabunge kuweza kuteuliwa kuwa wajumbe wa Tume ya Katiba ambao watateuliwa na Rais, kinyume cha ilivyokuwa awali, wanasiasa wakizuiwa kuteuliwa wajumbe.
Marekebisho hayo yatawasilishwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani kabla ya mkutano huo kwisha na zipo taarifa nyingine kuwa huenda Rais Jakaya Kikwete akakutana na wabunge wa Chama cha Mapinduzi au kile alichopaswa kuzungumza nao kikafikishwa kwao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Inatarajiwa kuwa wabunge hao wataelezwa hatua kwa hatua kuhusu kilichojiri kati ya mkutano wa Rais Kikwete na vyama vya upinzani kuhusu muswada walioupitisha ambao hatimaye naye aliutia saini kuwa sheria.
Wadau mi nadhani baadhi yetu wakati umefika sasa tubadili mitazamo yetu kuhusu ZITTO KABWE;kiukweli kijana anaonyesha ukomavu wa kisiasa kila kukicha tofauti na vijana wengi ambao wanakimbilia posho tu; Zitto kumbe anafanya mambo mengi bila kupiga mayowe wala kuita wapiga picha...hili nalisema kufuatia kugundua kuwa Mh. zitto kabwe kuwa chanzo cha mazungumzo maarufu yanayoendelea ikulu kati ya chadema na Rais kikwete,mambo yako hivi.....
Safari ilianza hivi; baada ya kuona mwenendo wa mijadala na mwelekeo wa baadhi ya viongozi wenzake, hasa katika siku ambazo CHADEMA kilikuwa kinatangaza kwamba kingeitisha maandamano nchi nzima kupinga mchakato wa katiba mpya uliokuwa umewasilishwa na Serikali bungeni, baadhi ya wanaCHADEMA na wengine miongoni mwa umma, walihisi kuwako kwa hatari ya kweli ya vurugu kuibuka nchini, ambayo isingekisaidia chama hicho au kundi jingine lolote, hivyo Zitto alifunga safari kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam ili kuteta na Dk. Slaa.
Katika mazungumzo yao, vyanzo kadhaa vya habari vimesema, hoja ilikuwa ni umuhimu wa kuchukua njia ya mazungumzo katika suala la mchakato wa katiba mpya, kuliko njia ya maandamano. Lakini Dk. Slaa amekaririwa akiashiria kwamba ilikuwa vigumu zaidi kuanzisha njia ya mazungumzo kwake kuliko njia ya shinikizo kupitia maandamano.
Raia Mwema limeambiwa kwamba kutokana na ugumu huo, Dk. Slaa amekaririwa kumueleza Zitto kuwa wanaweza, katika kufikia kupata muda wa kukutana na Rais Jakaya Kikwete, kuwatumia wazee wenye utulivu na busara, wasio na misimamo mikali ya kisiasa, wenye kutanguliza mbele maslahi ya nchi na wanaosimamia zaidi nguvu ya hoja, ambao miongoni mwao ni Dk. Salim na Jaji Warioba.
Habari zinasema, tatizo kubwa alilokuwanalo Dk. Slaa katika kuwafikia wazee hao ni kwamba hakuwa na ukaribu wa kiasi hicho nao na Raia Mwema limeelezwa kwamba katika mazingira hayo ndipo Zitto alipoahidi kuwatafuta wahusika na kuwaeleza mtazamo huo na kisha kusikiliza mawazo yao.
"Zitto alikwenda kuwaona Jaji Warioba na Dk. Salim na wakati huo, vikao vya Bunge vilikuwa vikiendelea Dodoma. Kule wale wazee walimsikiliza Zitto na kuona mapendekezo yao yana mantiki na kwa hiyo, Zitto akarudi kumweleza Dk. Slaa na baadaye wakapanga kukutana na Warioba na Salim.
"Walizungumza sana, wakafanya uchambuzi wa kina na njia bora zaidi ya kuweza kufikisha suala hilo kwa Rais Kikwete. Jaji Warioba aliombwa afanye kazi hiyo kuwa kiunganishi na taarifa zinasema baada ya kujiridhisha na hali ya mambo naye aliwasiliana na Ikulu na mchakato ukaanza.
Ndani ya Kamati Kuu CHADEMA
Habari za uhakika zinasema baada ya Dk. Slaa na Zitto kukubaliana na akina Warioba, kibarua kigumu kwao kilikuwa kuwasilisha mawazo yao mbele ya Kamati Kuu ya CHADEMA.
Taarifa hizo zinaelezwa kuwa Zitto hakuwa amehudhuria kikao hicho cha Kamati Kuu na hivyo, mzigo ulibaki kwa Dk. Slaa. Wakati huo, Zitto alikuwa amerejea kutoka India alikokuwa akitibiwa na hivyo hakuweza kushiriki kikao cha Kamati Kuu kwa sababu ya hali yake kiafya kutoimarika.
"Zitto aliitwa na Dk. Slaa kwenye Kamati Kuu amsaidie kueleza suala hilo, tulimwona alikuwa ametoka kuumwa alijitahidi sana kujieleza. Lakini kabla ya hapo, uchokozi wa wazo hilo uliibuliwa na Regia Mtema, ambaye alisema tukamwone Rais Kikwete ili tuzungumze naye....wajumbe karibu wote wakaguna wakimpinga na kumwona msaliti, wengine wakisema eti katumwa.
"Baada ya Zitto kuitwa na Dk. Slaa, ndipo alianza kutoa maelezo na hatimaye wajumbe wakaridhia. Na baadaye Mbowe akaandika barua kwenda kwa Rais kuomba kukutana naye ili kuwasilisha mapendekezo ya chama," kinaeleza chanzo chetu cha habari.
Warioba ‘messanger' mtiifu
Habari zinasema baada ya Mbowe kuandika barua ya kuomba kukutana na Rais Kikwete, Jaji Warioba ndiye aliyekuwa ‘wakala' wa mawasiliano kati ya pande hizo mbili, yaani CHADEMA na Rais Kikwete.
"Barua ile alipewa Jaji Warioba naye binafsi kwa mkono wake aliifikisha Ikulu moja kwa moja kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye baadaye alifanya mazungumzo na Kikwete pamoja na Dk. Salim na kisha kukubali ombi hilo la CHADEMA.
"Warioba akarejea tena kwa viongozi wa CHADEMA kwa ajili ya kutoa majibu kama ‘mjumbe' na akaeleza kuwa Rais hana tatizo kukutana na ujumbe wa CHADEMA kwa sababu hili ni suala la kitaifa, si la kwake pekee," anaeleza mtoa taarifa huyo.
Waziri Mkuu Pinda arudi Dar
Kutokana na kuanza kwa mchakato huo wa ‘kimya kimya' vyanzo vyetu vya habari kutoka bungeni vinaeleza kuwa mjadala wa sheria hiyo ulikuwa ukisogezwa mbele kwa maelezo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ili kutoa nafasi kwa mchakato huo wa CHADEMA, Dk. Salim, Jaji Warioba na Rais Kikwete, ambao mpaka wakati huo haukuwa rasmi, ushike kasi.
Vyanzo vingine vya habari vimesema kuna wakati Waziri Mkuu Pinda alikwenda Dar es Salaam kutoka Dodoma kwa ajili ya mazungumzo kuhusu suala hilo na baada ya mjadala wa sheria hiyo kusogezwa mbele kujadiliwa bungeni kwa mara kadhaa, ilibidi mjadala uruhusiwe.
Milango ya Ikulu yafunguliwa
Baada ya kazi hiyo ya ‘kimya kimya' na baada ya Bunge kujadili, kurekebisha na hatimaye kupitisha muswada huo, ujumbe wa CHADEMA ulikaribishwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya mazungumzo.
Makaribisho hayo yaliwekwa bayana na Ikulu kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano na kuanza rasmi Novemba 27, mwaka jana, na kurejewa tena siku iliyofuata, Novemba 28, kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuipa nafasi Serikali iweze kutafakari mapendekezo ya CHADEMA kuhusu sheria hiyo.
"Katika mkutano huo, pande zote mbili zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu sana kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na umoja wa kitaifa," inaeleza taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu iliyotolewa baada ya duru la kwanza la mazungumzo hayo.
Kamati Kuu CCM yatia neno
Hata hivyo, wakati CHADEMA wakiwa wameomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya mazungumzo, Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilikuwa inaendelea na kikao chake mjini Dodoma, ambako ilimshauri Rais Kikwete kutanua wigo kwa kukutana na wadau wengine, ambao ni pamoja na vyama vingine vya siasa, ambavyo hata hivyo, tayari vimeonana na kuzungumza na Kikwete. Vyama hivyo ni Chama cha Wananchi (CUF) na NCCR-Mageuzi.
Kwa upande mwingine, ushauri huo wa Kamati Kuu ya CCM ulizua mjadala mpya katika jamii, wengine wakiupinga na kuukosoa, wengine wakiuunga mkono lakini mwishowe, Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho kikongwe nchini, aliuzingatia.
Viongozi wanne waibuka vinara
Kama suala hili litafikia hatua nyingine katika hali isiyokuwa na malumbano tofauti na dalili za awali zilivyokuwa zikiashiria, basi, vinara wa kutuliza hali hiyo ni pamoja na Rais Kikwete binafsi ambaye aliridhia kukutana na wawakilishi wa makundi tofauti licha ya muswada kupitishwa na Bunge naye mwenyewe kuutia saini kuwa sheria.
"Angeweza kugoma na kutumia ubabe wa dola kulazimisha mambo, lakini hakufanya hivyo," kinaeleza chanzo chetu cha habari na kuongeza kuwa; "Shukurani za kipekee ziwaendee Dk. Slaa, Zitto, Dk. Salim na Jaji Warioba, wameonyesha upeo mkubwa wa kiuongozi."
Muswada kufanyiwa marekebisho
Taarifa zaidi zinabainisha kuwa mazungumzo hayo pamoja na ya vyama vingine yamezingatiwa na Rais Jakaya Kikwete na kwa hiyo, katika mkutano ujao wa Bunge unaonza wiki ijayo mjini Dodoma, sheria hiyo ya mchakato wa Katiba mpya nchini itafanyiwa marekebisho.
Miongoni mwa mapendekezo hayo ni kurejesha uwezekano wa viongozi wanasiasa, wakiwamo wabunge kuweza kuteuliwa kuwa wajumbe wa Tume ya Katiba ambao watateuliwa na Rais, kinyume cha ilivyokuwa awali, wanasiasa wakizuiwa kuteuliwa wajumbe.
Marekebisho hayo yatawasilishwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani kabla ya mkutano huo kwisha na zipo taarifa nyingine kuwa huenda Rais Jakaya Kikwete akakutana na wabunge wa Chama cha Mapinduzi au kile alichopaswa kuzungumza nao kikafikishwa kwao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Inatarajiwa kuwa wabunge hao wataelezwa hatua kwa hatua kuhusu kilichojiri kati ya mkutano wa Rais Kikwete na vyama vya upinzani kuhusu muswada walioupitisha ambao hatimaye naye aliutia saini kuwa sheria.