VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Yale mambo ya zomeazomea yaliyowakumba makada wa CCM na UDP,Prince Bagenda na John Momose Cheyo pale katika Ukumbi wa Nkrumah-UDSM,jana yaliwakumba Makada wawili wa CCM:Jaji Joseph Sinde Warioba na Tambwe Hiza pale katika Ukumbi wa Karimjee-Dar es Salaam.Walitaka kuubeba Muswada mbovu kuliko yote Tanzania uliosomwa kwa mara ya kwanza Bungeni uhusuo mabadiliko ya Katiba.Zomeazomea zote hizo zinahusu makongamano ya kujadili Katiba mpya ya Tanzania hasa 'Muswada wa Marekebisho ya Katiba' badala ya 'Muswada wa Baraza la Katiba' unaotakiwa.Poleni sana mliozomewa na tunawaahidi kuwa tutaendelea kuwazomea pindi mtakapoendelea kuongea pumba zenu.CCM mnaelekea mahali ambapo hamtakuwa na mtu wa kumhutubia zaidi ya 'Press Conference'.