Warioba: Huu ndio ukweli kuhusu Mwananchi Gold

- So far tumesikia one side ya WArioba peke yake on this ishu, sasa tunasubiri upande mwingine najua soon atatokea wa kumjibu, lakini tumeshamsikia ila maneno yake sio final katika hii ishu ya Mwananchi Gold.

Mkuu FMES, heshima kwako.

Ni kweli kuwa tumemsikia Warioba pekee akielezea kuhusu uundwaji wa Mwananchi Gold (amefanya hivyo hadharani). Angefanya hivyo kwenye vikao vya siri na/au kwa kuomba asiandikwe ingekuwa tofauti. Ukweli unabaki kuwa yeye ndie anaejua zaidi kuhusu uanzishwaji wa Mwananchi Gold kuliko si ajabu mtu mwingine yeyote. Ninayo kila sababu ya kuamini kuwa alichokisema ni ukweli mtupu (kwa kuzingatia utu uzima wake, heshima yake, na nafasi yake katika Mwananchi Gold). Mpaka hapo atakapojitokeza mtu anaeweza kutuhakikishia kuwa anaijua zaidi Mwananchi Gold zaidi yake (na hivyo kupinga kauli ya Warioba), sina shaka na wala sidhani kama ni jambo sahihi kudhani kuna wowote katika kauli zake hizo. Naamini si rahisi mtu mwingine kuja na kupinga maneno ya Warioba kuhusiana na Mwananchi Gold.

Mkuu, Taifa hili lina watu na viongozi wengi wenye uoga wa kuthubutu (labda hii inaweza kuwa sababu ya kushindwa kwetu katika kila jambo). Serikali ilijitahidi kupingana na ukweli huu kwa kuthubutu kufanya jambo la maana sana kuanzisha mradi huu. Inaelekea uoga huo huo wa kuthubutu ndio ulioifanya serikali kurudi nyuma na kuanza kuukwepa (ikidhani ni mradi mbaya). Nadhani ni vyema mTanzania yeyote mwenye mapenzi mema na nchi hii hasa mwenye kutaka maendeleo ya kudumu na kuzuia ubadhilifu unaofanywa/unaoweza kufanywa katika kuhujumu madini yetu akaangalia upya suala la Mwananchi Gold. Si lazima iwe ni kampuni ya Warioba (kama mwekezaji tu), ila mtu yeyote mwenye uwezo, na nia ya kuikomboa nchi hii. Ni vyema tukapenda uwekezaji wa ndani kuliko wa watu wa nje. Maana wao wana kwao, nako kunahitaji kujengwa vile vile. Hivyo miradi kama hii ni vyema ikawa ya waTanzania pekee. Ni miradi nyeti kwa ustawi wa Taifa letu.
 
Jasusi,

Kuwa waziri mkuu na kuwa mwenyekiti wa board wa kampuni kubwa kama hiyo ni vitu tofauti. Ndio maana mashirika yetu yote yamekufa shauri ya kutumia watu kama hao.

Nikiona hata anavyojitetea, inaonyesha wazi Warioba hakuwa na hana uwezo wa kusimamia kampuni kama hiyo. Ukitaka kampuni kama hiyo ipate faida lazima uwe na watendaji wanaoelewa biashara sio hao wanasiasa wanaofikiri solution ni kutumbukiza more money.

Hiyo kampuni ilikuwa doomed for failure toka siku inaanzishwa.

BTW mbona sasa Warioba haongelei kuhusu hiyo kampuni kumilikiwa na CCM?

Ndugu yangu Mtanzania, sudhani kuwa mashirika yetu yalikufa kwakuwa Warioba alikuwa anayaongoza ama kwa kuwa yalikuwa yanaongozwa na wanasiasa (wala haikuwa hivyo). Labda kama unataka kusema mashirika yetu yanatakiwa kuongozwa na malaika.

Labda nijaribu kukupa sababu chache za kufa kwa mashirika yetu; Mashirika yetu mengi yalikufa kwa sababu kubwa tatu.
1. Serikali kuingilia katika maamuzi na usimamizi wa mashirika hayo (kiutaratibu). Na mapato makubwa yaliyotengenezwa na mashirika hayo yalikwenda Hazina na kutumiwa na serikali katika mipango ya maendeleo na mingineyo kadiri serikali ilivyotaka.

2. Serikali ilikuwa ikiweka pesa kidogo sana (ama hakuna) katika kuendeleza mashirika hayo (capital investment). Mifano ni NBC, TCC, TBL, Hotel zilizokuwa za serikali, n.k.

3. Uchakavu wa mitambo, au technolojia iliyokuwa ikitumika.

Ndugu yangu Mtanzania, hakuna kitu kibaya kama kuamini kuwa hatuna uwezo. Maana ukishaamini hivyo, inakuwa ni sawa na bondia aliepigwa konde na kuanguka chini, halafu akaogopa (si kushindwa) kunyanyuka. Maana atakuwa ameshindwa kwa knock-out, hata kama angenyanyuka mwenzie angeanguka baada ya kupigwa konde jepesi.
 
Jaji Warioba
....

Sasa katika hilo kama Serikali haitaki kumiliki hisa nyingi, na haitaki mtu wa nje awe na nyingi, ilibidi watafutwe wengine kuingia ili katika kampuni hiyo na wakaamua hao wengine wawe wa hapa ndani.

Ziwe ni kampuni ndogo ndogo za hapa, ziingie mle, hiyo ndiyo iliyoleta kuundwa kwa kampuni ya pili inayoitwa Mwananchi Trust, hii ilikuwa mwavuli wa kampuni ndogo ndogo za hapa. Baada ya kukubaliana kwa hilo, wakakubaliana kuwa mfumo wa hisa uwe Serikali ingechukua asilimia 35, na ziligawanywa Benki Kuu ichukue 20 na NDC 15, mwekezaji wa nje angechukua 20% kwa hiyo jumla inafika 55%. Zilizobaki 45 zilikuwa ndani ya Mwananchi Trust.

.....

Mimi nionavyo ni kuwa mkanganyiko wote huu ni kwa sababu walioko serikalini hawana maslahi binafsi kwenye mradi huo kwa sasa. Mzee Warioba anakiri kuwa walifuatwa kama mawakili katika kuanzisha kampuni hii, anakubali pia kuwa kuna asilimia 45 ambazo zinamilikiwa na wawekezaji wa ndani kwa kutumia Mwananchi Trust. La kujiuliza hao wawekezaji wa ndani ni akina nani? Angetaja orodha ya hao wamiliki ndio unaweza kuona kwa nini inapigwa vita. Kwangu mimi inawezekana kabisa hawa ndio wanopigwa vita kwa sababu mbalimbali za kisiasa ama za kimaslahi binafsi. Pia sikuona mahali aliposema kama yeye pia ni mwanahisa kwenye hiyo Mwanachi Trust. Angesema wazi ili kuweka kumbukumbu sawa.
 
Ndugu yangu Mtanzania, hakuna kitu kibaya kama kuamini kuwa hatuna uwezo. Maana ukishaamini hivyo, inakuwa ni sawa na bondia aliepigwa konde na kuanguka chini, halafu akaogopa (si kushindwa) kunyanyuka. Maana atakuwa ameshindwa kwa knock-out, hata kama angenyanyuka mwenzie angeanguka baada ya kupigwa konde jepesi.

Duu, hii imenikumbusha ngumi za Mohammad Ali na Joe Frazier, pambano lililoitwa The Thriller in Manila, lililofanyika Manila, Philippines, tarehe 1Oktoba , 1975. Pambano hili la round 15, huku joto la ndani likiwa 40 degree, lilikwenda hadi round ya 14 na hapo maboss wa Joe wakarusha taulo. Ali akasimama kwa furaha kuashiria kuwa kashinda na akaangua na kupoteza fahamu huku Joe akiwa kapatwa hasira ya "kwa nini nimekimbia ushindi? Huyu kweli alikuwa wa kusukumwa na anakwenda chini".

Jingine ni lile la Kichaa Badri Hari na Ruslan Karaev kwenye mashindano ya K-1. Kwenye pambano hilo, Badri Hari alichukua konde akaenda chini. Kahesabiwa na akasimama. Kipigo kikapadilika kwani wote hupigana bila kujikinga kama afanyavyo flying Gentleman, Remmy Bonjasky. Ila safari hii Badri Hari akawa faster, akamtandika Karaev na ikawa Knock-out.

Nafikiri kwa hili wote hata Mtanzania anakubaliana kuwa hatutakiwi KU-Gave up. Lazima tusimamme na tuendeleza pambano. Ila sema jinsi ya kuendeleza pambano hapo ndipo tunapishana. Wengine wanataka serikali (BoT) wajitoe na waachiwe watu binafsi. Wengine wanataka BoT iendelee. Kuna umuhimu wa kuliSHABIKIA hili. Kila Mwuungwana/ Ngereja na Pinda wakionekana lazima washambuliwe kwa kulitelekeza hili na kuwaambia kuwa WALIRUDISHE haraka mara tu wakirekebisha MAMBO TATA. Tukomae nao tu mwaka huu, soon KITAELEWEKA.
 
Kwa mazingira ya tawala zetu zamani na sasa, iliwezekana kabisa mtu kupata cheo kikubwa ingawa anachofanya hakionekani.
Tanzania yetu, kwa mtazamo wangu mpaka leo, hatupeani vyeo kulingana na uwezo wetu wa kufanya mambo, ila inategemea unajulikana vipi na watu walioko kwenye system.Kwa mfano, kwa background ya Obama kwenye siasa za Marekani, ingelikuwa ni Tanzania hata kama ni mahiri kiasi gani asingeweza kuwa raisi mana hajakulia kwenye circles of the elite, ambao wanapenda kuona wanalindana.
Kwa mtazamo huo, Warioba si lazima angefanya maajabu kwenye mwananchi gold kama mradi huu ungefanikiwa. Kwa mtazamo wangu angelikuwa ni conduit nyingine ya kuvuja fedha za umma.
I am glad times change....I wonder why evil doers like mafia learn and know that fact, lakini waheshimiwa wanasiasa wetu wengi hawalioni hilo.
Tunataka investment nyingi nnchi lakini sio za kisanii sanii kama hizi...inavyoonekana amekamatwa kubaya this time....aangalie asiadhirike
 
Kwa mazingira ya tawala zetu zamani na sasa, iliwezekana kabisa mtu kupata cheo kikubwa ingawa anachofanya hakionekani.
Tanzania yetu, kwa mtazamo wangu mpaka leo, hatupeani vyeo kulingana na uwezo wetu wa kufanya mambo, ila inategemea unajulikana vipi na watu walioko kwenye system.Kwa mfano, kwa background ya Obama kwenye siasa za Marekani, ingelikuwa ni Tanzania hata kama ni mahiri kiasi gani asingeweza kuwa raisi mana hajakulia kwenye circles of the elite, ambao wanapenda kuona wanalindana.
Kwa mtazamo huo, Warioba si lazima angefanya maajabu kwenye mwananchi gold kama mradi huu ungefanikiwa. Kwa mtazamo wangu angelikuwa ni conduit nyingine ya kuvuja fedha za umma.
I am glad times change....I wonder why evil doers like mafia learn and know that fact, lakini waheshimiwa wanasiasa wetu wengi hawalioni hilo.
Tunataka investment nyingi nnchi lakini sio za kisanii sanii kama hizi...inavyoonekana amekamatwa kubaya this time....aangalie asiadhirike
Hujaelewa alichokisema Warioba.
 
Kwa maoni yangu binafsi nasema zidumu fikra sahihi kuwa SISI NDIVYO TULIVYO.

Ndugu Warioba anasema kwamba serikali ilianza kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo wadogo (mchezo huo ukashindwa). Baadaye wakaanzisha Meremeta (mchezo huo ukashindwa). Na baada Mwananchi Gold.

Kisheria kuna uwezekano mkubwa Warioba and others hawana makosa. Lakini kutumia sheria za nchi kuanzisha entities ambazo zinalikamua taifa, ni PONZI scheme at best.
 
Warioba pamoja na maelezo yake yote hajajibu hoja nzito zilizomo kwenye sakata hili.

ThisDay

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/132-mengi-vs-warioba-2.html

point, nazaidi ya hapo, kama ilikuwa uamuzi wa serikali, kuna institution mbili tanzania ambazo zingeweza kufanya hivyo, kwa kumshirikisha huyo mwekezaji wa nje , nazo ni ndc, na stamico, na stategic investor ambaye amepatikana kihalali, then watu binafsi iwe Warioba/ Mushi etc tungeuziwa share through DSE, hiyo ndio nji muuafaka na iliyo wazi kwa waTz wote. na kila share holder angetoa huo mtaji wake upon establishment ya hiyo institution, na sio BOT itoe mkopo, kwa share holders wote kwa mgongo wa serikali kuwa mojawapo, wa wamiliki? na stategic Investor mtaji wake ni Brief case, maana proper evaluation ya contribution yake ni siri au privy to certain people then unasema hii institution ni ya Umma
 
Naona Tanzania Wapare wengi. Kesi ya KUKU, yuko tayari auze NG'OMBE ili ASHINDE.

Hiyo Mitambo inazidi kuoza. Warioba sanasana atafungwa. Then what next????!!!!!

Here we talk about TIME and more wastage of Pen'ga aka Money and Madini.
 
Ndugu yangu Mtanzania, sudhani kuwa mashirika yetu yalikufa kwakuwa Warioba alikuwa anayaongoza ama kwa kuwa yalikuwa yanaongozwa na wanasiasa (wala haikuwa hivyo). Labda kama unataka kusema mashirika yetu yanatakiwa kuongozwa na malaika.

Labda nijaribu kukupa sababu chache za kufa kwa mashirika yetu; Mashirika yetu mengi yalikufa kwa sababu kubwa tatu.
1. Serikali kuingilia katika maamuzi na usimamizi wa mashirika hayo (kiutaratibu). Na mapato makubwa yaliyotengenezwa na mashirika hayo yalikwenda Hazina na kutumiwa na serikali katika mipango ya maendeleo na mingineyo kadiri serikali ilivyotaka.

2. Serikali ilikuwa ikiweka pesa kidogo sana (ama hakuna) katika kuendeleza mashirika hayo (capital investment). Mifano ni NBC, TCC, TBL, Hotel zilizokuwa za serikali, n.k.

3. Uchakavu wa mitambo, au technolojia iliyokuwa ikitumika.

Ndugu yangu Mtanzania, hakuna kitu kibaya kama kuamini kuwa hatuna uwezo. Maana ukishaamini hivyo, inakuwa ni sawa na bondia aliepigwa konde na kuanguka chini, halafu akaogopa (si kushindwa) kunyanyuka. Maana atakuwa ameshindwa kwa knock-out, hata kama angenyanyuka mwenzie angeanguka baada ya kupigwa konde jepesi.

Recta,
Ni nani hao hawana uwezo? Kusema Warioba alikuwa hana uwezo wa kuongoza shirika kama hilo haina maana kwamba hata Watanzania wengine hawana uwezo. Ninavyosoma anavyoongea mzee Warioba, nikiwa investor nitakiwa mjinga kweli kutumbukiza hata senti tano yangu kwenye hilo shirika.

Unaweza kuwa mwanasiasa mtupu kama Bush na kuzungukwa na washauri 20, kwenye dunia ya manyan'gau kwenye private sector huna luxury kama hiyo.

Mashirika yetu ya umma yalikufa shauri ya poor management. Kuingiza wanasiasa hata kwenye maamuzi ya kiuchumi. Hizo sababu unazozisema ni mengineyo tu. Kama mitambo imechakaa kwanini wasinunue mipya? Utasema NBC ilikuwa haina mtaji huku wafanyakazi nchi nzima walikuwa ni wateja wake? Angalia TTCL na na yule mwanasiasa/balozi.

Uamuzi tu wa kutaka kujenga hicho kiwanda Dar ilikuwa ni tayari wameongoza gharama kwa asilimia kubwa tu.

Hicho kiwanda cha akina Warioba kilikuwa cha kuchotea pesa za walalahoi tu na wala sio biashara. Kama ni biashara si wakakope pesa bank waendeleze biashara yao? Wana majina makubwa, kama biashara ina faida, watapata faida tu.
 
Naona Tanzania Wapare wengi. Kesi ya KUKU, yuko tayari auze NG'OMBE ili ASHINDE.

Hiyo Mitambo inazidi kuoza. Warioba sanasana atafungwa. Then what next????!!!!!

Here we talk about TIME and more wastage of Pen'ga aka Money and Madini.

Jamani hapo hakuna cha mitambo wala nini. Nakwambia ni usanii mtupu. Mzee wa watu hakujua wenzake wanamtumia kupanda ngazi na kuchota. wengine wakachukua madolari na kwenda DRC kununua dhahabu hawajarudi na dhahabu wala fedha na Wariona anajua. halafu wakaja wawekezaji wakataka kununua huo mradi lakini baada ya Mahalu kuona mwenyeji wa hao wageni ni mmoja wa wabaya wake, akaweka ngumu jamaa wakatimua zao. Sasa tunapozungumzia mitambo inaoza hakuna kitu pale labda wawekeze tena. Hadi sasa kwanza mishahara inalipwa na BoT na mengineyo!!! kina warioba na wenzake nadhani hata vikao vya bodi hawajajilipa maana wanaona haya.

Inawezekana kabisa (naamini hivyo) kwamba Warioba kama yeye binafsi hajapata manufaa yoyote na hakuwa anajua mambo ya "kisasa" ya uchotaji na anajitahidi kuwafanya wengine tuamini kwamba wenzake nao ni safi kama yeye jambo ambalo litatulazimisha na yeye achafuke (kama bado).
 
Halisi, jaji warioba ni mtu mzima ambaye sidhani kama yeye na vyanzo vyote aje hadharani kutudanganya? Ukweli ndio huo aliouweka hadharani sasa ni fix serikali ikatae kuwa hakuna hicho anachopkisema mkuu warioba.

Hapo kuna siasa za makundi imeingia ktk project matokeo yake wanapoteza mapesa yetu ili baada ya 5yrs tuambiwe bomu jipya!!!!

Project iko pale mkuu nenda kaiangalie wewe kama alivyofanya invisible ktk isue ya liyumba. Kula watu wanakula lakini wengine ni wastaarabu ktk kula mkuu, unanawa kabla na baada ya kula.
 
FDR.Jr,
Mkuu nimekukubali kabisa kwa sababu haiwezekani mtu mmoja tu ndioye awe kila siku akisema hili ama lile na tusipate jibu wala upinzani toka upande wa pili, tunazungumzia mwezi mzima toka habari hii imekuwa habari...

Haya, Mtanzania anahoji kwa nini Warioba hakugusia CCM wakati anajua kabisa siasa za Bongo.. Na kama akisoma vizuri ataona kuna sehemu kasema...I quote:- La kwanza tulilofanya kwa kuwa walikuwa na haraka, wanataka mambo fulani fulani yafanywe mapema, tuliunda trust company kwa kutumia watu wetu hapa."

Hapa ni changa la macho kabisa... na mzee kafanya staha safari hii baada yaaa!..hao waliokuwa na haraka na wakataka mambo fulani fulani YAFANYWE MAPEMA - ni kina nani?...mkuu karata ndio hizo, mzungu kalala...
Kisha tunapozungumzia viongozi wetu kuongoza mashirika tunasahau kwamba Tanzania ni nchi pekee yenye wataalam ambao wameingia siasa kwa sababu ya maslahi.. toka kina Mwapachu hadi Mwakyosa hawa wote ni wataalam ambao wameingia siasa tu kwa sababu serikali yetu ilikuwa na mfu8mo wa Kijamaa ambapo kila kitu ktk Uchumi wa nchi yetu kilikuwa chini ya serikali kuu.
Sasa ni ajabu kabisa kusikia mtu akisema, Warioba ambaye alikuwa waziri mkuu ati hana uwezo wa kuendesha shirika la kusafisha dhahabu.. tena linaitwa KUBWA wakati huo huo linaitwa pia halina faida kwa mwananchi..
Jamani hizi siasa zetu tujaribu sana kuzitenganisha inapofikia maslahi ya Taifa. Warioba ni mtu mmoja tu ambaye hawezi kutusumbua akili zetu wote hapa, isipokuwa kuna zaidi ya haya tunayoyafahamu...
Na serikali kama kweli ina malengo mazuri kwetu ni lazima swala hili lifikiwe suluhu ambayo italiwezesha shirika hili kusimama kwani nchi yetu inategemea zaidi madini ktk uchumi wake bila shaka shirika hili ni muhimu sana tena kwa figures za Warioba inaonyesha wazi kuwa hakuna gharama kubwa sana kusimamisha kitu cha uhakika..
Tatizo linakuja tu pale utakapo tazama mikataba iliyopita, mikataba ambayo inasomba madini yetu kama kokoro kisha yanapelekwa nje kama mchanga mchafu na tunategemea figures za Barricks baada ya kusafisha huko nje ambako sisi hatuna sheria yoyote..Kwa hiyo wakituambia zimetoka Tani 2 hatuna hila isipokuwa kukubaliana nao...

Fellas, tuambiwe kitu gani sisi Wadanganyika tuweze kufikiria nje ya haya mapazia ya ya baadhi viongozi wasiowajibika!.. come one now!
 
Jamani ehh,
Naomba ile KAMATI (Sijui niite hivyo) ya Wachumi wa Tanzania wanaoitakia mema nchi hii, wafuatilie huo mpango kwa karibu na tusikie maoni yao. Pia Waandishi wa habari, hebu fuatilieni hiyo mitambo, muwaone na wale vijana waliopelekwa kusomea kusafisha dhahabu, maboss wao zaidi ya Warioba na mje mtupatie habari ya uhakika. Nafikiri hii itauwa mzizi wa fitina. Maana Warioba anasema mitambo ipo na ya kisasa, Halisi anasema HAMNA KITU. Sasa mmoja hapa anadanganya.
 
ninaomba tutengenishe nia nzuri na uvunjaji wa sheria au kuwaendea kinyume wananchi wa tanzania
1. huyu mzee analipwa pensheni ya viongozi mpaka mwisho wa maisha yake, hivyo kwa upande bado ni muajiriwa wetu, pili hiyo pensheni inmwezesha kuishi vizuri tu , hivyo aache hizo tamaa.
2 alikuwa ni mwana sheria mkuu wa serikali hivyo anajua, jinsi mashirika ya umma nk yanavyo anzishwa na utafutwaji wa hao stategic investors.na pia waziri kuu hivyo lwenye cabinet wamejadili mambo mengi tu ya uwekezaji nk , na faida zake na hasara ya different strategy
3 anajua sheria ya uanzishwaji wa bot na majukumu yake, katika kulinda na kutetea maslahi ya taifa.na jinsi serikali invyo pata mitaji katika miradi yake
4. anaelewa past experience ya bot katika kununua dhahabu na hasara walizo pata.
5 anajua uwepo wa stamico na kuwepo kwa ndc katika jukumu la kuendeleza viwanda na madini.
sasa leo hii kilicho msababisha ashindwe kuyaanisha haya yote, na kuweka maslahi ya taifa mbele, mpaka kutaka kuiweka bot katika biashara ya kusafisha dhahabu ni nini?
kwani stamico-ndc wakifanya hiyo biashara taifa hali faidiki?
kwani stamico hawana hao wataalamu wa madini mpaka wao mwananchi trust wakapeleka watu wao?
ambao hata walivyokuwa selected mimi na wewe hatujui?sijiui watoto wao au ndugu wa karibu etc etc
 
Last edited:
Jamani ehh,
Naomba ile KAMATI (Sijui niite hivyo) ya Wachumi wa Tanzania wanaoitakia mema nchi hii, wafuatilie huo mpango kwa karibu na tusikie maoni yao. Pia Waandishi wa habari, hebu fuatilieni hiyo mitambo, muwaone na wale vijana waliopelekwa kusomea kusafisha dhahabu, maboss wao zaidi ya Warioba na mje mtupatie habari ya uhakika. Nafikiri hii itauwa mzizi wa fitina. Maana Warioba anasema mitambo ipo na ya kisasa, Halisi anasema HAMNA KITU. Sasa mmoja hapa anadanganya.

Sikonge,

Hivi unategemea mzee Warioba ndio atuambie kama ni mitambo ya kisasa? Ujuzi wa kutuambia hayo anautoa wapi? Yeye angeenda kwenye hiyo press conference na mtaalamu wao na ndiye akasema hayo anayosema Warioba sasa.

Hivi lini ulisoma matangazo ya vijana kutakiwa kwenda kusoma nje ili kuongeza ujuzi kwenye kusafisha dhahabu? Ni nani wamepeleka hao vijana? Waliwapataje hao vijana?

Hivi kampuni kubwa kama hiyo si inakuwa na CEO pamoja na management nzima? Je wako wapi na ni akina nani?

Huyo mwekezaji toka Italy yuko wapi? Kwanini hachukui hatua baada ya BOT au serikali kuvunja mkataba? Je yeye alichangia pesa ngapi na ziko wapi? Nani aliamua hicho kiwanda kijengwe Dar na kwanini?

Watanzania kwa kuliwa tumezidi, hii kampuni ilikuwa mrija wa kunyonyea Watanzania kama ule mgodi wa Kiwira, Richmond, IPTL na mingine.

Nashangaa warioba aliingia mkenge kwenye kitu ambacho kiko wazi kama hiki.

Binafsi ni mpenzi wa miradi yetu kumilikiwa na Watanzania lakini sio mradi kama huu ambao usingelileta faida yoyote kwa mlipa kodi na hata hao wachimbaji wadogo wadogo.

Serikali imefanya la maana kujitoa mapema. Kama mradi una faidi basi watafute backers kutoka mashirika ya fedha. Ukiangalia pesa ambazo zimepotea kwa miradi kama hii kwa kutumia BOT ni nyingi mno. Miradi yote ilikuwa inaongozwa na wanasiasa na kufunguliwa na rais Mkapa. Mfano ni ule mradi wa Mzindakaya na kiwanda cha nyama.
 
Mtanzania,
Shukran kwa maswali yako ambayo ni sehemu ya kujifunza...
Ila nadhani hakuna shirika hata moja la serikali ambalo wewe na mimi tunaweza kujibu maswali haya isipokuwa yale yaliyoanzishwa toka wakati wa Nyerere..

Lakini pamoja na yote haya ningeomba unambie ni kutokana na vitu gani umefikia kusema - 'Binafsi ni mpenzi wa miradi yetu kumilikiwa na Watanzania lakini sio mradi kama huu ambao usingelileta faida yoyote kwa mlipa kodi na hata hao wachimbaji wadogo wadogo.'

Kumbuka tu hapa hatuzungumzii tena warioba isipokuwa mradi wenyewe!..nipe sababu zilizokusukuma hadi kusema hivyo - naomnba darasa!
 
August,
Mkuu nimeona hapo juu maswali yako mengi sana kuhusiana na Warioba, kisha umejenga hoja ambazo zimewaingiza Stamico kama shirika la serikali..
Kifupi mkuu wangu hufahamu lolote kuhusiana na Stamico ambao hivi sasa wameingia na Ubia na mashirika feki ya Canada kama Tan Range Exploration ambalo mhusika wake mkubwa ni Sinclair - uchafu wake unaujua vizuri..nasema feki kwa sababu hawana record wala ujuzi kama shirika ktk exploration zaidi ya kuwatumia vijana wetu.. hapakuwepo na sababu ya kuwatumia hata kidogo ikiwa lengo la Stamico ni kuboresha maisha ya machimbaji wadogo wadogo..

Binafsi, natazama picha nzima kabla sijawakilisha hoja zangu.. swala hapa sio Warioba isipokuwa ni sababu zilizotumika au zinazotumika kuivunja Mwananchi Gold kwani nikitazama hao Stamico ambao wanapokea fedha za serikali vilevile ktk exploration zao kisha sijui kama Sinclair ameingia na mtaji wowote ktk ubia huo zaidi ya kutumia mtaji na rasilimali zetu wenyewe, halafu nikijumlisha na habari za Barricks na mashirika mengine ya nje bila shaka jibu lake ni rahisi sana... Mwananchi Gold ni tishio kwa wezi wa rasilimali zetu kwani kusafishwa kwa dhahabu na madijni mengine nchini kunaweza kuondoa pande kubwa la faida wanazovuta leo hii..
Guys haihitaji Phd kuweza kuona swala hili na warioba is not an issue hata kidogo kwa sababu anaweza kuondolewa na akawekwa mwingine mwenye kuaminika au uzalendo zaidi yake..Hizi habari za BoT kujiingiza ktk biashara, sisi hatujafikia Ubepari uliokamilika yaani sisi wananchi tuna uwezo wa kuwekesha ktk miradi mikubwa kama hii na pia Uzalendo kwa Taifa letu chini ya Ubepari bado ni somo tunalojifunza..
 
Back
Top Bottom