Waraka wangu kwa viongozi wa CHADEMA

Hiki ndo nachokikataa mimi na ninapogundua kuwa we ni mtu wa namna gani katika kunena lakini ukashindwa kuonesha unachokinena kwa matendo ni ushahidi tosha kuwa ni mtu mnafiki.
Ngoja nikwambie kwa nini nimesema hivyo; waraka wako uko wazi kwa kusisitiza umuhimu wa kuwa mtu wa watu wote kama kiongozi. Na tafsiri ya uongozi hapa ni kuwa kila binadamu mwenye akili timamu ana sifa za uongozi. Umetuo ushauri wa kiuongozi lakini umeshindwa kuonesha tabia za kiungozi.

Katika jibu lako hilo umebagua, umesema una watu wako kwamba uliyemjibu sio sehemu ya kusudio lako maana kuna watu umewalenga. Sasa utawezaje kuhubiri kitu kuhusu kuthaminiana wakati wewe hujathamini?!
Teh teh teh Tanzania bhana.

Kwa ufupi, waraka wako una madhaifu mengi. Nayafanyia kazi halafu nitakujibu.
Sikuelewi hapa. Nilichosema siwezi kuandika kwa uchache ili kila mtu asome wakati waraka wangu umelenga kuyasema yote yalokuwa kichwani kwangu. Kwa nini nifiche? au niyakatishe pasipo kutoyatoa fully. Kwa nini JF wayakate maelezo yangu vipande kwa sababu kuna watu hawana muda wa kuyasoma yote, wakati wapo wanaopenda kuyasoma yote? kosa ni lipi mkuu wangu...

Nicholas
,
Mkuu wangu mimi nimeandika waraka huu kwa uchunguzi wangu niloufanya na wewe umechukulia unayoyafahamu kuwa ndio kinga ya Chama hivyo waendelee na haya wanayoyafanya pasipo kuzingatia yangu kwa imani kwamba watakao athirika ni CCM na CUF, hii ni dhana tu huwezi kuweka dhamana juu yake.
Mimi nasema hivi haya ni mawazo yako na unasema upendavyo kwa sababu hujui lolote kuhusu CCM wala CUF na mbinu wanazozijenga na kuzitumia ktk mashambulizi yao. Hujui athari yake kwa chama unless utawafikia wananchi wenyewe wapiga kura na kufanya utafiti..

Sasa nakuomba hivi:- Wasimamishe watu njiani (one oon one) na waulize imani zao kwa Chadema, nini wasiwaisi wao na wapi wanaona bado chama kinashindwa kuwapa majibu sahihi na kama watakichagua chama hiki mkuongoza mwaka 2015 au itategemea nini?. Nakuhakikishia watu wengine hawana imani kama chadema inaweza kuwa tofauti, wameaminishwa mengi sana usiyoyaona wewe na kibaya zaidi utagundua kwamba Waislaam wengi hawana imani na chama hiki kutokana na Tuhuma za CCM na CUF ambazo hazina majibu.

Unachoshindwa kuelewa ni kwmba Chadema leo hii inashambuliwa na vyama karibu vyote utafikri nwapo madarakani na wasipo jiweka sawa kulinda huu umaarufu wa muda, trust me tutasema mengine hapa kijiweni ifikapo January 2016..
 
Mheshimiwa Mwenyekiti, katibu mkuu wa chama, viongozi wa chama ngazi ya Taifa, mikoa na wajumbe wa mabaraza yote ya chama ngazi zote..

Waheshimiwa,
Kama tulivyowahi kuzungumz awali kuhusu nafasi ya Chadema ktk utawala na maandalizi ya chama kugombea mwaka 2015, bado nina imani kubwa na chama lakini bado kabisa chama chetu kimeshindwa kupasua ngome ya CCM ipaswavyo na kujenga imani za wananchi wa chama hiki. Kinachotokea ni kujaribu kwa chama chetu kuwavuta wanachama wa CCM zaidi ya kuwavuta wananchi kuichagua Chadema. Kauli mbiu kama VUA GAMBA naa GWANDA ni moja ya kauli nyingi zilizoonyesha wazi vita ya chama hiki ni kupambana na uongozi wa CCM badala ya kupambana na sera za CCM zilizotufikisha hapa tulipo.

Ebu tutazame Mchambuzi ktk mada yake utagundua kwamba Chadema inajaribu sana kufanya wajibu wake ‘Do the right thing’ kukemea Ufisadi, utawala wa mabavu, mapungufu ya JK na kadhalika lakini tumeshindwa kuyafanya ipaswavyo ‘Do things right’ hivyo tunashindwa kujenga uaminifu kwamba Chama hiki kitaweza kurekebisha kero za wananchi.

Waheshimiwa, sio mwanachama atakaye tupa ushindi mwaka 2015, bali mwananchi mlalahoi anayetakiwa kwenda ktk sanduku la kupiga kura siku ya Uchaguzi na kutupa imani yake kwenye kipande cha karatasi kama tumaini lake kwa miaka mitano ya uongozi wa nchi hii..


Na kwa nini basi tumeshindwa kuwa na ngao ktk mashambuliz makali yanayoelekezwa kwetu?. Jibu nalipata kwa Mchambuzi tena akisema hivi:- Leo hii masuala ya Uongozi na siasa yametawaliwa sana na misingi ya UKANDA, UKABILA na UDINI. Mheshimiwa hili tupende tusipende ndivyo watanzania watawahukumu viongozi wetu kwa sababu ndivyo siasa za nchi hii zimejikita iwe kutokana kupoteza dira ya Kitaifa, kuwepo kwa vyama vingi ama hisia na wajibu wa viongozi wenyewe kuwajibika ktk makundi ya watu wanaowawakilisha.

Hivyo, Tuache UNAFIKI, tuache kujidanganya kwa unafiki wa wapambe wa vyama wanaotumia siasa kaa uwanja wa kujuana. Sisi sote ktk nafasi tulizopo na kutambua kwamba Utanzania wetu unajumuisha tofauti zetu za maumbile, makabila na imani za dini na yeyote atakaye jaribu kumdharau hata mmoja wetu ni kielelezo cha Ubaguzi ambao hautakiwi kupewa nafasi bali kuupiga vita. Hizi ndio ngao zetu, ndizo zinazo tu identify kama jamii ya Kitanzania na lazima tuzilinde dhidi ya siasa za chuki na uutengano. Bila utayari wa kuwajumuisha watu wote kwa tofauti zao kama sehemu ya Utanzania wetu itakuwa vigumu sana kupata ushindi mwaka 2015 maana CCM wanaifanya kazi yao ipaswavyo – Kushambulia nasi ktk kujilinda lazima tuwe na kinga zetu kwa kufanya vitu sawa – Doing things right !

Nawakilisha..

Mkuu Mkandara, asante sana kwa mada hii, kwa kuanzia naomba mimi niziunganishe hizo sentensi nilizo bold ili nipate para para zangu 5 za kuanzia
" Chadema ktk utawala na maandalizi ya chama kugombea mwaka 2015, bado nina imani kubwa na chama lakini bado kabisa chama chetu kimeshindwakupasua ngome ya CCM. Kauli nyingi zilizoonyesha wazi vita ya chama hiki ni kupambana na uongozi wa CCM badala ya kupambana na sera za CCM zilizotufikisha hapa tulipo.

Chadema inajaribu sana kufanya wajibu wake ‘Do the right thing’ kukemea Ufisadi, utawala wa mabavu, mapungufu ya JK na kadhalika lakini tumeshindwa kuyafanya ipaswavyo ‘Do things right’ hivyo tunashindwa kujenga uaminifu kwamba Chama hiki kitaweza kurekebisha kero za wananchi.

Waheshimiwa, sio mwanachama atakaye tupa ushindi mwaka 2015, bali mwananchi mlalahoi anayetakiwa kwenda ktk sanduku la kupiga kura siku ya Uchaguzi na kutupa imani yake kwenye kipande cha karatasi kama tumaini lake kwa miaka mitano ya uongozi wa nchi hii..


Tumeshindwa kuwa na ngao ktk mashambuliz makali yanayoelekezwa kwetu?. Leo hii masuala ya Uongozi na siasa yametawaliwa sana na misingi yaUKANDA, UKABILA na UDINI. Tupende tusipende ndivyo watanzania watawahukumu viongozi wetu.

Tuache UNAFIKI, tuache kujidanganya kwa unafiki wa wapambe wa vyama siasa za chuki na uutengano. Bila utayari wa kuwajumuisha watu wote kwa tofauti zao kama sehemu ya Utanzania wetu itakuwa vigumu sana kupata ushindi mwaka 2015.

Na nikiunganisha hizo red, nitapata para moja ifuatayo.

" Chadema kimeshindwa kupasua ngome ya CCM. Chadema tumeshindwa kuyafanya ipaswavyo ‘Do things right’ hivyo tunashindwa kurekebisha kero za wananchi.Tumeshindwa ktk mashambulizi ya siasa yametawaliwa na misingi ya UKANDA, UKABILA na UDINI. Tuache UNAFIKI, tuache kujidanganya kwa unafiki itakuwa vigumu sana kupata ushindi mwaka 2015"

Angalau maneno hayo, umeyatamka wewe!, hayo ni maneno ya msingi sana na sio ya kupuuzwa hata kidogo!. Japo mimi sio mwanachama, mfuasi, wala mshabiki wa chama chochote, mara nyingi nimekuwa nikitoa maoni yangu mbalimbali kwa Chadema, mfano niliwahi kuwaeleza hivi Chadema kwenye mada yangu, "CCM Imechokwa, Chadema Haijajipanga".
Wanabodi,
Hakuna ubishi, Chadema imenyanyuka, toka wabunge 5 mpaka 22 wa kuchaguliwa tena majimbo ya haja, huku sio kukua bali ni kupaa, tatizo kubwa la Chadema, bado hawajipanga.

Kichama, wanachadema mkubali msikubali, chama chenu japo kipo juu, lakini bado hamjajipanga kwa sura ya kitaifa.
Kwa vile CCM imekaa mkao wa kifo, hii ndio opportunity yenu kujipanga muwe na sura ya kitaifa, Watanzania wawamini wawakabidhi nchi mwaka 2015!.

Nilipata majibu haya,
PASCO,
Mwanajamvi nimefurahi sana kujitambulisha kama Political analyst. Ningelifurahi sana kusaidia Taifa lako kama analist kama ungelitusaidia yafuatayo:

i) Utafiti unaonyesha nini duniani kuhusu Leader of the Opposition katika mifumo ya mabunge yaliyoko Duniani. Kwa mtu yeyote anayefanya analysis angelitegemea kuona American Model na WestMinster Model zinaeleza nini. Analysis yako ime base kwa personalities badala ya Model na analysis ya aina hii kwa maoni yangu ni ya hatari sana kwa kuwa inakosa misingi ya kisayansi. Politics is science and should never be reduced to anything less than empirical analysis to be scientific.

ii) Analysis yako imetoa Conclusions kabla ya kujenga plausible major and minor. Scientific and logical conclusion can only be based on a well founded "major and minor". Ili tunaofuatilia tuweze kunufaika na analysis yako ningelitegemea a properly constitued logical arugement inayofuata clasical logical construction ambayo ndio msingi wa analysis yoyote ambayo ni credible.

Natanguliza shukrani za dhati, na ninategemea kupata objective political analysis ya mapendekezo yako.

Mungu Ibariki Tanzania.


Leo kwa vile wewe umejitanabaisha ni Chadema, mimi nayasubiria majibu yao kwa hamu na pia nakusikilizia kama na wewe utavurumishiwa makombora kama tunavyovurumishiwa akina siye!.

Pasco.

 
Mkuu Mkandara kwa miaka mingi sasa nimekuwa nasikia hizi propaganda zinazofanywa na magamba kwamba CHADEMA ni chama cha kikabila na kidini lakini hadi hii leo sijaona mifano yoyote ile ambayo imewahi kutolewa ili kuthibitisha kwamba kweli CHADEMA ni chama cha Wakristo na Wachaga.

Tukiangalia ndani ya CHADEMA viongozi wajuu kama Dr Slaa, Lissu, Zitto na wengineo si wachagga na pia Zitto si mkristo. Tukiangalia Wabunge wa CDM walichaoguliwa katika uchaguzi wa 2010 pia tunaona Wabunge wa CDM wametoka katika mikoa mbali mbali si Kilimanjaro pekee hili pia linathibitisha kwamba Watanzania wamekikubali CDM na hivyo kutoona kama kuna matatizo yoyote ya kuwapigia kura wagombea wake wa nafasi ya Ubunge. Mpaka sasa hivi katika sera zote za CDM sijaona sera yoyote ile ambayo imekaa kikabila au kidini.

Ndani ya CDM pia kuna wanachama wengi na wafuasi wa CDM ambao ni Waislamu na wamekikubali chama hicho pamoja na propaganda za nguvu zinazofanywa nchini ili kukionyesha chama cha CHADEMA kama ni cha Wakristo.

Hivi karibuni hapa jamvini nimesoma bandiko la mwenzetu mmoja aitwaye mohamed Mtoi kwa kweli lilinifariji sana na kunithibitishia tena kwamba CDM si chama cha kidini kama vile ambavyo magamba wanataka tuamini.

Bandiko la Mohamed ni hili hapa:

Mimi huwa namshangaa sana Ritz! Hata kama ni muislamu wa siasa kali uislamu wetu hauna chuki na upande wa pili namna hiyo! Kwanza muislamu yoyote uislamu wake hauwezi kukamilika kama hakiri kutambua uwepo wa ukristo kama jinsi ukristo unavyotambua uwepo wa uislamu! Uelewa mdogo ndio unamfanya Ritz anakuwa mbumbumbu wa mambo ya dini kiasi hiki!

Hapa leo anawatetea ccm na kusahau kuwa ccm ndio waliichafua cuf kuwa ni chama cha udini na kigaidi, baadae haohao wakasema chadema ni chama cha wakristo lakini wao hawasemi kuwa ni chama cha dini gani! Sasa ukija hapa ukimuona jinsi ritz anavyotoa povu la udini unajua kabisa aidha uelewa wake ni mdogo au yuko hapa kwa kazi maalum ya kipato kutoka Lumumba.

Mimi ni muislamu lakini napingana sana na misimamo ya Ritz! Alisha diriki kuniambia Mohamedi na chadema wapi na wapi?! Huu ni upovu iliopiitiliza na tangu siku ile niliamua kumsamehe bure na kumkabidhi Mungu maana nimeona ni mtu ambae ana uabisha hata uislamu wenyewe.


Hapa chini sijakuelewa. Pale ulipoandika kuwakwaza wananchi kuabudu na kupingana na mawazo ya kiimani. Je, una maana CDM inawakwaza wananchi kuabudu na pia inapingana na mawazo ya kiimani? Naomba ufafanue tafadhali kama muda wako unakuruhusu kufanya hivyo.

"Nchi yetu halina dini kwa maana kwamba milihili ya utawala wa nchi yetu haitakiwi kuundwa ama kujenga policies zinazotokana na imani ya dini moja isipokuwa serikali inawawezesha wananchi wenye ibada zao. Kuwakwaza wananchi kuabudu kama walivyofanya China na Urusi. Kupingana na mawazo ya kiimani kwa kutunga sheria moja kwa wote itatafsirika tu kama exclusive ama sheria ya kuwatenga wao hivyo kuzaa underground movement kupingana na sheria hiyo. Imetokea sana nchi zilizowakwaza waumini wa dini au kuwayenga makabila kama Wayahudi nchi za Ulaya."

Natanguliza shukrani


BAK. Asante sana kwa mada nzuri. Hapo nilipoweka kijani ni aibu sana kwa chama tawala kutamka jambo hili la udini kususu vyama vya upinzani. Huu ni ukiukwaji wa katiba ya nchi na CCM imeivunja maana yake ni nini? Mihimili ya Bunge na Mahakama zinafanya nini kulinda sheria? Weledi wao kulinda sheria zisivunjwe uko wapi sasa? Tumtegemee nani? Inaudhi sana. Vyama vya upinzani vijihadhari visifanye makosa kama ya sasa ya kutoheshimu sheria. Kuendesha taasisi yoyote (hasa serikali) kwa kufuata sheria zilizowekwa katika utaratibu wa kuwasikiliza wadau (wananchi) husika ndiyo njia pekee ya kuleta haki na usawa hapa Tanzania vinginevyo ni vurugu tupu kama zinavyoanza kujitokeza kutokana na CCM na serikali yake kutoheshimu sheria za nchi.
 
Mkuu Mkandara!

Shukrani sana na Uchambuzi huu, Kuna msemo "working hard or hard working" CCM are working hard kuichafua CDM. Sasa CDM have hard work kukabiliana na propaganda za CCM. Now its time kwa CDM to work Smart (DO THINGS RIGHT).

Hakuna haja ya kujibu hoja za Ukanda za CCM, bali wafunge kambi kutafuta watu wenye elimu na misimamo kutoka Kusini na Pwani ambao watafanya kazi ya Chama katika mikoa hiyo.

Mfano hapa Bagamoyo, CCM wanaamini ni Ngome yao. Lakini kama CDM ikawapata wazawa wa hapa wenye Elimu kuzungumzia matatizo ya hapa, CCM wamekwisha. Sawa na Mkuranga, Kibiti, Mafia, Kilwa na Rufiji ambazo CCM wana take for granted kama Ngome zao. Kuna msemo "wao wanakuja kutuletea vurugu zao" who is wao?

Naomba kusema hivi WORKING SMART ni bora kuliko WORKING HARD
 
Sikuelewi hapa. Nilichosema siwezi kuandika kwa uchache ili kila mtu asome wakati waraka wangu umelenga kuyasema yote yalokuwa kichwani kwangu. Kwa nini nifiche? au niyakatishe pasipo kutoyatoa fully. Kwa nini JF wayakate maelezo yangu vipande kwa sababu kuna watu hawana muda wa kuyasoma yote, wakati wapo wanaopenda kuyasoma yote? kosa ni lipi mkuu wangu...

Nicholas
,
Mkuu wangu mimi nimeandika waraka huu kwa uchunguzi wangu niloufanya na wewe umechukulia unayoyafahamu kuwa ndio kinga ya Chama hivyo waendelee na haya wanayoyafanya pasipo kuzingatia yangu kwa imani kwamba watakao athirika ni CCM na CUF, hii ni dhana tu huwezi kuweka dhamana juu yake.
Mimi nasema hivi haya ni mawazo yako na unasema upendavyo kwa sababu hujui lolote kuhusu CCM wala CUF na mbinu wanazozijenga na kuzitumia ktk mashambulizi yao. Hujui athari yake kwa chama unless utawafikia wananchi wenyewe wapiga kura na kufanya utafiti..

Sasa nakuomba hivi:- Wasimamishe watu njiani (one oon one) na waulize imani zao kwa Chadema, nini wasiwaisi wao na wapi wanaona bado chama kinashindwa kuwapa majibu sahihi na kama watakichagua chama hiki mkuongoza mwaka 2015 au itategemea nini?. Nakuhakikishia watu wengine hawana imani kama chadema inaweza kuwa tofauti, wameaminishwa mengi sana usiyoyaona wewe na kibaya zaidi utagundua kwamba Waislaam wengi hawana imani na chama hiki kutokana na Tuhuma za CCM na CUF ambazo hazina majibu.

Unachoshindwa kuelewa ni kwmba Chadema leo hii inashambuliwa na vyama karibu vyote utafikri nwapo madarakani na wasipo jiweka sawa kulinda huu umaarufu wa muda, trust me tutasema mengine hapa kijiweni ifikapo January 2016..

mkandara unadhani hata nina shida kushambulia unachoamini basi....!mimi nina shida na analysis yako kam avile unavyoweza kuwa na yangu.Mi wala sihitaji kusimamisha mtu,ila kila ukipanda basi, ukiwa shuleni, ukiwa polisi,ukiwa katik vikao vya vijiji, ukiwa baa, ukiwa theatre(mahospital mengine yana TV), ukiwa bank, wakati bunge linaendelea,ukiwa mahofisini kote huko ukiwasikiliza walivyo determined ni kwamba utaoana upepo upo vipi. Sasa unachoongelea wewe ni zile clusters zenye watu specifics aabpo utakuta ni cuf tuu au CCM tuu.Kama ndipo ulipo naweza pata picture wewe ni nani na unafanya nini katik hiii thread.

okay:

Hujanijibu mkuu: kwanini unajibu hivi?kwenye thread hapo juu unajaribu brainswash-response ya kwanza unatongoza watu wakubali ushawishi wako na kuonyesha dalili za vitisho- response ya pili unaamua kuifanya kuwa personal opinion.
 
Mkuu Mkandara! Shukrani sana na Uchambuzi huu, Kuna msemo "working hard or hard working" CCM are working hard kuichafua CDM. Sasa CDM have hard work kukabiliana na propaganda za CCM. Now its time kwa CDM to work Smart (DO THINGS RIGHT)
Hakuna haja ya kujibu hoja za Ukanda za CCM, bali wafunge kambi kutafuta watu wenye elimu na misimamo kutoka Kusini na Pwani ambao watafanya kazi ya Chama katika mikoa hiyo. Mfano hapa Bagamoyo, CCM wanaamini ni Ngome yao. Lakini kama CDM ikawapata wazawa wa hapa wenye Elimu kuzungumzia matatizo ya hapa, CCM wamekwisha. Sawa na Mkuranga, Kibiti, Mafia, Kilwa na Rufiji ambazo CCM wana take for granted kama Ngome zao. Kuna msemo "wao wanakuja kutuletea vurugu zao" who is wao? Naomba kusema hivi WORKING SMART ni bora kuliko WORKING HARD
Shukran sana yaani ningepata Wanachadema wachache tu wanaofikiria kama wewe hasa baada ya kunisoma basi bila shaka Chama kingeweza kupenyeza sehemu ambazo hazipenyeki.. Lakini nasikitika tu kwamba kuna watu wanaamini kuishambulia CCM, JK na mafisadi wake kunaweza kujenga uamnifu wa watu kwao. Jamani sisi tumeposema Unafiki wa Watanzania ni kwamba tunajuana sana. Mtu yeyote anayekuponda wewe kwa mkeo na hasa akiwa mwanaume mara nyingi hutaka kuivunja ndoa na ukisha ivunja hutamwona akikusaidia.

Chadema jisogeze kwa wananchi na sio kujitangaza kwa wananchi, tangaza utayari wa kufanya mema na ushirikiano, tangaza sera zako na jinsi utakavyoweza kuwaunganisha wananchi waliogawanywa. Ukimya siku zote sio ngao bali ni udhaifu wa ngome yako na CCM na CUF wataendelea kurushia makombora hapo hapo..
Pasco,
Mkuu sidhani kama kuna chama kimewahi kupata ushauri hapa JF kama Chadema lakini inashangaza sana hasa baada ya kuwa chama mbadala cha Upinzani kuna kitabia fulani kinaniogopesha kama kweli hawa ndio watu wale wale tulokuwa nao miaka ya nyuma au?..
 
Mkuu Mkandara, asante sana kwa mada hii, kwa kuanzia naomba mimi niziunganishe hizo sentensi nilizo bold ili nipate para para zangu 5 za kuanzia
" Chadema ktk utawala na maandalizi ya chama kugombea mwaka 2015, bado nina imani kubwa na chama lakini bado kabisa chama chetu kimeshindwakupasua ngome ya CCM. Kauli nyingi zilizoonyesha wazi vita ya chama hiki ni kupambana na uongozi wa CCM badala ya kupambana na sera za CCM zilizotufikisha hapa tulipo.

Chadema inajaribu sana kufanya wajibu wake ‘Do the right thing’ kukemea Ufisadi, utawala wa mabavu, mapungufu ya JK na kadhalika lakini tumeshindwa kuyafanya ipaswavyo ‘Do things right’ hivyo tunashindwa kujenga uaminifu kwamba Chama hiki kitaweza kurekebisha kero za wananchi.

Waheshimiwa, sio mwanachama atakaye tupa ushindi mwaka 2015, bali mwananchi mlalahoi anayetakiwa kwenda ktk sanduku la kupiga kura siku ya Uchaguzi na kutupa imani yake kwenye kipande cha karatasi kama tumaini lake kwa miaka mitano ya uongozi wa nchi hii..


Tumeshindwa kuwa na ngao ktk mashambuliz makali yanayoelekezwa kwetu?. Leo hii masuala ya Uongozi na siasa yametawaliwa sana na misingi yaUKANDA, UKABILA na UDINI. Tupende tusipende ndivyo watanzania watawahukumu viongozi wetu.

Tuache UNAFIKI, tuache kujidanganya kwa unafiki wa wapambe wa vyama siasa za chuki na uutengano. Bila utayari wa kuwajumuisha watu wote kwa tofauti zao kama sehemu ya Utanzania wetu itakuwa vigumu sana kupata ushindi mwaka 2015.

Na nikiunganisha hizo red, nitapata para moja ifuatayo.

" Chadema kimeshindwa kupasua ngome ya CCM. Chadema tumeshindwa kuyafanya ipaswavyo ‘Do things right’ hivyo tunashindwa kurekebisha kero za wananchi.Tumeshindwa ktk mashambulizi ya siasa yametawaliwa na misingi ya UKANDA, UKABILA na UDINI. Tuache UNAFIKI, tuache kujidanganya kwa unafiki itakuwa vigumu sana kupata ushindi mwaka 2015"

Angalau maneno hayo, umeyatamka wewe!, hayo ni maneno ya msingi sana na sio ya kupuuzwa hata kidogo!. Japo mimi sio mwanachama, mfuasi, wala mshabiki wa chama chochote, mara nyingi nimekuwa nikitoa maoni yangu mbalimbali kwa Chadema, mfano niliwahi kuwaeleza hivi Chadema kwenye mada yangu, "CCM Imechokwa, Chadema Haijajipanga".

Nilipata majibu haya,


Leo kwa vile wewe umejitanabaisha ni Chadema, mimi nayasubiria majibu yao kwa hamu na pia nakusikilizia kama na wewe utavurumishiwa makombora kama tunavyovurumishiwa akina siye!.

Pasco.


teh teh..mbona hiyo paragra[h ina pasonality mbili?..kuna tu-kama sisi, ki-kama chama.

Kweli CDM kama honeybadger, wanaweza indure maultiple attacks...JF nayo ni kiboko kwa kunusa traces za vitu haramu.
 
mkandara unadhani hata nina shida kushambulia unachoamini basi....!mimi nina shida na analysis yako kam avile unavyoweza kuwa na yangu.Mi wala sihitaji kusimamisha mtu,ila kila ukipanda basi, ukiwa shuleni, ukiwa polisi,ukiwa katik vikao vya vijiji, ukiwa baa, ukiwa theatre(mahospital mengine yana TV), ukiwa bank, wakati bunge linaendelea,ukiwa mahofisini kote huko ukiwasikiliza walivyo determined ni kwamba utaoana upepo upo vipi. Sasa unachoongelea wewe ni zile clusters zenye watu specifics aabpo utakuta ni cuf tuu au CCM tuu.Kama ndipo ulipo naweza pata picture wewe ni nani na unafanya nini katik hiii thread.

okay:

Hujanijibu mkuu: kwanini unajibu hivi?kwenye thread hapo juu unajaribu brainswash-response ya kwanza unatongoza watu wakubali ushawishi wako na kuonyesha dalili za vitisho- response ya pili unaamua kuifanya kuwa personal opinion.
Mkuu wangu labda nikwambie tu ya kwamba watu wengi wamechoka na utawala wa Kikwete na sio CCM. watu wengi bado wana imani na chama hiki kama akipatikana kiongozi wamtakaye. Subiri kama watamsimamisha Mwandosya au Rose Migiro utaona jinsi upepo utakavyo badilika. Hii ni tahadhari tu mkuu wangu tusijikite ktk kushambulia watu badala ya sera za CCM. Pili, tujihadhari na propaganda za CCM na CUF tayari zimeisha ingia watu vichwani iwe wakristu au waislaam halafu what about those who are not Christians or Muslims wao wamesimama wapi? nini nafasi yao - hakuna mshindi hapa.. Chuki tayari imeshajenga na huwezi kuiondoa majukwaani..
 
.
Uvumi siku zote ndio hujenga imani za watu, wanasema Chadema ni chama cha Ukanda au udini, wewe huzioni, mimi zisioni na vile vile kumbuka hata mtu wa CUF anaamini hivyo hivyo. Na sidhani kama tunaweza kuonyesha Udini wa CUF lakini Je ni watanzania wangapi wanaamini CUF sio chama cha Waislaam au Wazanibar?..wamepewa majibu gani?.. maana ukweli ni kwamba CUF wenyewe hawana ngao, hawana majibu wala defence mechanism inayo onekana isipokuwa wao wenyewe wanajiingiza zaidi ktk ukimya.. Je ktk hali hiyo unafuu na credit zinakwenda wapi - CCM, uongo! I have done my study mkuu wangu na nakuhakikishia najua nilichokiandika..

Nimekukubali mkuu, kukaa kimya kunahalalisha misconceptions ambazo zinaendelea kuwaweka magamba madarakani.
Inabidi zijibiwe promptly and aggressively.
 
Mkuu wangu labda nikwambie tu ya kwamba watu wengi wamechoka na utawala wa Kikwete na sio CCM. watu wengi bado wana imani na chama hiki kama akipatikana kiongozi wamtakaye. Subiri kama watamsimamisha Mwandosya au Rose Migiro utaona jinsi upepo utakavyo badilika. Hii ni tahadhari tu mkuu wangu tusijikite ktk kushambulia watu badala ya sera za CCM. Pili, tujihadhari na propaganda za CCM na CUF tayari zimeisha ingia watu vichwani iwe wakristu au waislaam halafu what about those who are not Christians or Muslims wao wamesimama wapi? nini nafasi yao - hakuna mshindi hapa.. Chuki tayari imeshajenga na huwezi kuiondoa majukwaani..

Mkuu sijui sample yako uliichukulia wapi, ila nadhani una undermine CDM, na si wewe mwenyewe.ndio maana nimeweka thread inayowafanisha na "honyebadgers". Igunga palikuwa pagumu ila CDM waliingia kirahisi sana.Meru walimchafua Lema na tangazo la kizushi toka kwa wazee kuwa "Lema angeenda anguwawa" kwa hiyo asikanyage lema aliingia.Na kama si Busara Msiba wa Sumari Sr. ungekuwa doa.Lema alifunika convoy yote ya CCM, kusimama kwake tuu palilipuaka shangwe mpaka aibu.Pengine Nape ali downplay kwa kusema kuwa CDM walifanya siasa na Media hazikuweka sawa.Lema ilibidi aondoke kwa gari lingine na familia kutumia lingine.

Kwa hili la Ukanda limeshakaa vibaya kwa CCM mukama alichemsha katika msiba wa Bob na CUF wakitumia yoyote kati ya haya (Ukanda, Udini) inakula kwao. Wakitumia ukabila watajikuta wakitaja makabila nchi nzima halafu kujiweka katika kundi la waongo, au vibaraka wa CCM na CDM watawamalizia kwa kuwakebehi kwa jina la CCM B.

Ima sure kwa jinsi CCM walivyojiweka pabaya ndani aya chama na nje.CDM wanaweza mbana nape katika midahalo ya TV siku moja kwa maswali ya hapo kwa hapo.Na kumuuliza "Upi ushahidi kuwa CDM ni chama cha Kikanda, kikabila au hata kidini", hatochomoka katik huo mdahalo kwani wamekuwa wakijidanganya sana mpaka wakaamini uongo wao na hadly ataweza kuwa na hata sentence yenye maana.
 
Nimekukubali mkuu, kukaa kimya kunahalalisha misconceptions ambazo zinaendelea kuwaweka magamba madarakani.
Inabidi zijibiwe promptly and aggressively.
Shukuran maana lazima ukweli usemwe. Mimi hujiuliza sana maswali kama vile CUF ilisingiziwa kuwa chama cha Waislaam na Ukanda lakini pamoja na tuhuma zile walishindwa ama walizuiwa vipi kuingia ktk ngome za Wakristu na wenye imani za jadi? Hivi kweli CUF ilianguka yenyewe kwa kukosa umaarufu bara au wananchi wapiga kura waliamini tuhuma hizo na kutokipa kura zao ktk uchaguzi ulofuata. Halafu pamoja na wanachama wengi waliokuwa nao, washabiki, walalahoi na vibaka wote walipotelea wapi ghafla? na ilikuwaje washindwe hata kushika jimbo bara miaka yote walotuhumiwa Udini.
- Chadema Je wamejiandaa vipi, leo hii tuna majibu gani... Hili nalo neno..
 
Mkuu sijui sample yako uliichukulia wapi, ila nadhani una undermine CDM, na si wewe mwenyewe.ndio maana nimeweka thread inayowafanisha na "honyebadgers". Igunga palikuwa pagumu ila CDM waliingia kirahisi sana.Meru walimchafua Lema na tangazo la kizushi toka kwa wazee kuwa "Lema angeenda anguwawa" kwa hiyo asikanyage lema aliingia.Na kama si Busara Msiba wa Sumari Sr. ungekuwa doa.Lema alifunika convoy yote ya CCM, kusimama kwake tuu palilipuaka shangwe mpaka aibu.Pengine Nape ali downplay kwa kusema kuwa CDM walifanya siasa na Media hazikuweka sawa.Lema ilibidi aondoke kwa gari lingine na familia kutumia lingine.

Kwa hili la Ukanda limeshakaa vibaya kwa CCM mukama alichemsha katika msiba wa Bob na CUF wakitumia yoyote kati ya haya (Ukanda, Udini) inakula kwao. Wakitumia ukabila watajikuta wakitaja makabila nchi nzima halafu kujiweka katika kundi la waongo, au vibaraka wa CCM na CDM watawamalizia kwa kuwakebehi kwa jina la CCM B.

Ima sure kwa jinsi CCM walivyojiweka pabaya ndani aya chama na nje.CDM wanaweza mbana nape katika midahalo ya TV siku moja kwa maswali ya hapo kwa hapo.Na kumuuliza "Upi ushahidi kuwa CDM ni chama cha Kikanda, kikabila au hata kidini", hatochomoka katik huo mdahalo kwani wamekuwa wakijidanganya sana mpaka wakaamini uongo wao na hadly ataweza kuwa na hata sentence yenye maana.
That was 2010 tunaelekea 2015 mambo yanaweza kubadilika haraka sana kama hatukuzingatia tulipofika leo hii 2012..Kisha mkuu wangu mimi wala sintopingana na wewe kwa sababu nimezoea kupingwa. Mara nyingi sana huwa napokea kukubali kutokubaliana na wajibu wako maana ndipo ukomo wa kufikiri kwako na mimi huzama zaidi kutafuta yasiyoonekana kwa macho wala hisia za kibinadamu. Hujitenga nafsi hii na kuwa nje ya sanduku la Uchadema nikaitazama picha nzima kwa ukaribu zaidi.. Mwisho wa siku nina hakika hutokea nayoyaamini halafu utakuja niona mchawi.. Zingatia ile hadithi za Abunuasi na juha alokuwa akikata tawi alokalia..
 
That was 2010 tunaelekea 2015 mambo yanaweza kubadilika haraka sana kama hatukuzingatia tulipofika leo hii 2012..Kisha mkuu wangu mimi wala sintopingana na wewe kwa sababu nimezoea kupingwa. Mara nyingi sana huwa napokea kukubali kutokubaliana na wajibu wako maana ndipo ukomo wa kufikiri kwako na mimi huzama zaidi kutafuta yasiyoonekana kwa macho wala hisia za kibinadamu. Hujitenga nafsi hii na kuwa nje ya sanduku la Uchadema nikaitazama picha nzima kwa ukaribu zaidi.. Mwisho wa siku nina hakika hutokea nayoyaamini halafu utakuja niona mchawi.. Zingatia ile hadithi za Abunuasi na juha alokuwa akikata tawi alokalia..

lets assume upo deep nami nipo shallow.Then tuangalie tupo katika kitu gani....huwezi niambia upo deep kwa vitu unrealistic halafu utake tulazimisha kumeza.No wonder kuwa unasisitiza kuwa umezoea kupingwa.Hapa naona upo very sensitive sana kwa utakaloaminisha watu."nimekuwa nikihighlight hiyo shift ila hutoi majibu".humu ndani kila mtu hupingwa hadi aweke mambo clear, na wengine hupingwa forever na watu wenye imani zao na malengo yao humu ndani.Hapa wewe ndio una malengo yako,yaani unakomaa kuwa CDM ina shida,watu wanakupa mifano hai kukuonyesha kuwa CDM wameruka yote hayo ila bado unahama katik hisia za kujibu.

Hujanijibu shift yako ya "msisitizo inavyohama" naona sasa umehamia kuniamisha kuwa fikra zangu zimekomea hapo.Ingawa ni dharau,ila sijali sana kwa vile unapush kuongeza uzito katik usemalo.Umekuwa nortorius katika kujibu kwa ukali, kutwist theme kwa ku introduce unnecessary things ili kukuchomoa katika pressure,kuseduce silently, kueudisha mada kuwa personal na mwishowe kama hili jibu la mwisho unataka aminisha watu kuwa wengine wamefikia mwisho wa kufikiri.Pengine your school of thoughts ilikuwa na walimu waliokuaminisha kuwa your the best na mtu akipingana na hizo vew zako atakuwa wrong.najaribu kuangalia kama tofauti hapa ni perspectives ila naon ahakuna kwani nimegusia sample zako ulichukua wapi katik distribution ya watanzania wenye kufuatilia siasa,naona hukuona hilo.Umeamishia katika hisia.
Well, unaweza brain wash walio wako,ila im a true radical kama hujaniconvice kwa idea huwezi nisilence kwa hisia zozote.
 
Mkuu wangu labda nikwambie tu ya kwamba watu wengi wamechoka na utawala wa Kikwete na sio CCM. watu wengi bado wana imani na chama hiki kama akipatikana kiongozi wamtakaye. Subiri kama watamsimamisha Mwandosya au Rose Migiro utaona jinsi upepo utakavyo badilika. Hii ni tahadhari tu mkuu wangu tusijikite ktk kushambulia watu badala ya sera za CCM. Pili, tujihadhari na propaganda za CCM na CUF tayari zimeisha ingia watu vichwani iwe wakristu au waislaam halafu what about those who are not Christians or Muslims wao wamesimama wapi? nini nafasi yao - hakuna mshindi hapa.. Chuki tayari imeshajenga na huwezi kuiondoa majukwaani..
Mkandara,
Naomba nitofautiane na wewe. Watu hawajachoshwa tu na utawala wa Kikwete, bali wamechoshwa na utawala wa CCM. Period. Sasa hivi hata akisimamishwa Magufuli, au Mwandosya, wimbi la uchovu wa CCM halitapukutika. Watu wameshafikia pale Mwalimu aliposema kuwa ikiwa CCM itashindwa kutoa uongozi bora watautafuta kwingineko. Tupo hapo sasa. CCM haiaminiki kabisa, bna ndiyo maana wameelekeza nguvu zao katika propaganda za kukivunja Chadema.
 
Mkuu Pasco CDM imeweza kuipasua ngome ya magamba ndio maana sasa hivi wanaweweseka na kuhaha huku na kule katika jitihada za kujaribu kuidhibiti CDM.

Mwanzoni magamba walianza na propaganda zao uchwara kwamba "CDM ni chama cha kikabila na pia cha kidini" juhudi ambazo hazikufua dafu na hivyo CDM kuendelea kuchanja mbuga na kujizolea umaarufu mkubwa katika kona mbali mbali za nchi yetu. Pia kumbuka katika bunge lilivyoisha hivi karibuni jinsi Makinda na Ndugai walivyokuwa wanaweweseka ndani ya Bunge ili kuidhibiti CDM ambao hoja zao nyingi zilikuwa zinaungwa mkono na Watanzania walio wengi. Pia tumesikia kauli za mpumbavu Mwigulu kwamba Jeshi limewakikishia magamba ulinzi.

Magamba hawakutaka Watanzania tupate katiba mpya, wao walitaka kuongeza viraka tu katika katiba ya zamani na kusonga mbele. Sera ya katiba mpya ilikuwa ni ya CDM na CDM wakasimama kidete mpaka magamba wakawa hawana jinsi ila kukubali kuunda tume ya kukusanya maoni ya Watanzania ili kuunda katiba mpya.

Kumbuka pia malipo ta Dowans magamba walisharidhia kwamba yanastahili yafanywe. Kauli zilitolewa na Pinda, Werema, Ngeleja na kama sikosei kamati kuu ya magamba nayo ilikutana na kuridhia kwamba malipo yale ya $96 millioni ni malipo halali hivyo ni lazima yafanyike. CDM kwa kusimama imara na Watanzania kuhoji uhalali wa malipo yale iliweza kusimamisha malipo hayo ambayo yalitakiwa yafanyike tangu December, 2010.

Magamba baada ya kuona propaganda zao uchwara za "CDM ni chama cha kikabila na kidini" kugonga ukuta ndio wakaamua kutumia vyombo vya dola na kuanza kufanya mauaji mbali mbali ndani ya nchi yetu. Mauaji hayo yaliyofanywa na vyombo vya dola ili kuithibiti CDM yalitokea kule Arusha, Tarime, Mbeya, Igunga, Morogoro na ya hivi karibuni kule Iringa.

Wiki chache zilizopita Nape alitoa kauli kwamba "CCM haitakuwa tayari kukabidhi madaraka kwa wahuni wa CDM." Kwa hiyo ukiangalia ushahidi ambao nimeuweka hapo juu utaona ni dhahiri kwamba CDM imefanikiwa kuipasua ngome ya magamba na ndiyo maana sasa hivi wanahaha kwa kiwango cha juu kabisa ili kuidhibiti CDM.

Pia tukumbuke kwamba CDM ni chama cha upinzani. Pamoja na sera zake nyingi kuungwa mkono na Watanzania kamwe hakiwezi kupunguza kero za Watanzania mpaka pale kitakapofanikiwa kushika dola. Na kuungwa mkono kwa sera hizi na Watanzania walio wengi ndio kumesababisha CDM iendelee kujizolea umaarufu katika mikoa mbali mbali nchini.

Kwa maoni yangu CDM imefanikiwa katika kuzuia upotoshaji wa propaganda uchwara za magamba kuhusu misingi ya UKABILA, UDINI na UKANDA ndiyo maana hata kule Lindi na Mtwara ambako hivi karibuni kampeni ya M4C ilifanyika Viongozi wa CDM waliotembelea mikoa hiyo katika juhudi za kukitangaza chama na pia kupata wanachama wapya walipata mapokezi makubwa sana na mapicha yaliwekwa hapa kama ushahidi wa umaarufu wa CDM katika mikoa hiyo ya kusini.

Kwa kumalizia napenda kusema zipo kasoro ndani ya CDM lakini ukilinganisha na mafanikio waliyoyapata hadi sasa kwa kweli uongozi wa CDM inabidi kupongezwa sana kwamba pamoja na kufanya kazi katika mazingira magumu mno lakini bado wameweza kukijenga chama na wanaendelea kukijenga kwa juhudi kubwa sana usiku na mchana katika kila pembe za nchi yetu.

Juhudi hizi za M4C zikiendelea kati ya sasa na 2015 basi kama uchaguzi ujao utafanyika kwa kutumia katiba mpya na Watanzania kuwa macho ili kulinda kura za Watanzania hivyo kuhakikisha Serikali DHAIFU, magamba wakishirikiana na vyombo vya dola washindwe kufanya uchakachuaji wa matokeo ya uchaguzi basi naamini kabisa CDM itachukua dola katika uchaguzi huo wa 2015.

Mkuu Mkandara, asante sana kwa mada hii, kwa kuanzia naomba mimi niziunganishe hizo sentensi nilizo bold ili nipate para para zangu 5 za kuanzia

" Chadema kimeshindwa kupasua ngome ya CCM. Chadema tumeshindwa kuyafanya ipaswavyo ‘Do things right' hivyo tunashindwa kurekebisha kero za wananchi.Tumeshindwa ktk mashambulizi ya siasa yametawaliwa na misingi ya UKANDA, UKABILA na UDINI. Tuache UNAFIKI, tuache kujidanganya kwa unafiki itakuwa vigumu sana kupata ushindi mwaka 2015"

Nilipata majibu haya,


Leo kwa vile wewe umejitanabaisha ni Chadema, mimi nayasubiria majibu yao kwa hamu na pia nakusikilizia kama na wewe utavurumishiwa makombora kama tunavyovurumishiwa akina siye!.

Pasco.

 
lets assume upo deep nami nipo shallow.Then tuangalie tupo katika kitu gani....huwezi niambia upo deep kwa vitu unrealistic halafu utake tulazimisha kumeza.No wonder kuwa unasisitiza kuwa umezoea kupingwa.Hapa naona upo very sensitive sana kwa utakaloaminisha watu."nimekuwa nikihighlight hiyo shift ila hutoi majibu".humu ndani kila mtu hupingwa hadi aweke mambo clear, na wengine hupingwa forever na watu wenye imani zao na malengo yao humu ndani.Hapa wewe ndio una malengo yako,yaani unakomaa kuwa CDM ina shida,watu wanakupa mifano hai kukuonyesha kuwa CDM wameruka yote hayo ila bado unahama katik hisia za kujibu.

Hujanijibu shift yako ya "msisitizo inavyohama" naona sasa umehamia kuniamisha kuwa fikra zangu zimekomea hapo.Ingawa ni dharau,ila sijali sana kwa vile unapush kuongeza uzito katik usemalo.Umekuwa nortorius katika kujibu kwa ukali, kutwist theme kwa ku introduce unnecessary things ili kukuchomoa katika pressure,kuseduce silently, kueudisha mada kuwa personal na mwishowe kama hili jibu la mwisho unataka aminisha watu kuwa wengine wamefikia mwisho wa kufikiri.Pengine your school of thoughts ilikuwa na walimu waliokuaminisha kuwa your the best na mtu akipingana na hizo vew zako atakuwa wrong.najaribu kuangalia kama tofauti hapa ni perspectives ila naon ahakuna kwani nimegusia sample zako ulichukua wapi katik distribution ya watanzania wenye kufuatilia siasa,naona hukuona hilo.Umeamishia katika hisia.
Well, unaweza brain wash walio wako,ila im a true radical kama hujaniconvice kwa idea huwezi nisilence kwa hisia zozote.
Umesema wewe sio mwanachama wa Chadema kinachokuuma nini hasa kama sio Udini wako. Chama changu mimi wewe kinakuhusu nini haswa? bro ebu jitulize kidogo kanywe maji maana hata sikuelewi unachozungumza. Ebu nambie swali lako ni nini haswa?Umeaminishwa kwamba Chadema ni chama cha wakristu nini?
 
Umesema wewe sio mwanachama wa Chadema kinachokuuma nini hasa kama sio Udini wako. Chama changu mimi wewe kinakuhusu nini haswa? bro ebu jitulize kidogo kanywe maji maana hata sikuelewi unachozungumza. Ebu nambie swali lako ni nini haswa?Umeaminishwa kwamba Chadema ni chama cha wakristu nini?

1.Sio mwanachama,kinachoniuma ni kwamba unapotosha watu.....

2. Mimi sio mdini.

3.Chama si chako.

4. Hivi ulikuwa ukibishana usijokijua?

5.Sijui kama nimekuaminisha hivyo(kuwa chadema ni chama cha KIkristu),kwani halikuwa lengo langu.

Teh teh...Hembu tuambie hiyo logic ya ulichopost umefikia vipi hizo conclusion zako?NImejibu kwa mstari ili nikuone umeunganishaje logically no.1 ukapata 2, namba 4 kupata 5? nitashukuru sana.Kama ni ngumu pitia red zote katika posting zangu hapa.
 
BAK, nakubalina na wewe sana tu lakiji mwenyewe umekiri kuwepo kwa mapungufu. lakini sijakuona ukiya orodhesha. Halafu kulingana na Mchambuzi hizi ndio ngome yao, nakuomba uninyeshe ni wapi tumeweza kubomoa..


  1. CCM ndio iliyoongoza mageuzi ya kiuchumi (political reforms) Tanzania;
  2. Umiliki na Udhibiti wa Vyombo Vya habari;
  3. Uchumi Mkubwa Wa CCM;
  4. Ujamaa Bado ni Relevant (unaendana) na Maisha ya Wengi Vijijini;
  5. CCM imejenga Coalition na Taasisi zote nchini zenye nguvu kiuchumi, kijamii na kijeshi;
  6. Katiba ya Sasa ya nchi inaipa CCM nguvu kubwa kisiasa;
  7. Mbinu za upinzani zinazotumiwa na Chadema Hazipo Consistent na Coherent;
  8. Tanzania inakabiliwa na Udhaifu mkubwa wa Civil Society; na
  9. Political Culture ya Tanzania ina matatizo..
 
1.Sio mwanachama,kinachoniuma ni kwamba unapotosha watu.....

2. Mimi sio mdini.

3.Chama si chako.

4. Hivi ulikuwa ukibishana usijokijua?

5.Sijui kama nimekuaminisha hivyo(kuwa chadema ni chama cha KIkristu),kwani halikuwa lengo langu.

Teh teh...Hembu tuambie hiyo logic ya ulichopost umefikia vipi hizo conclusion zako?NImejibu kwa mstari ili nikuone umeunganishaje logically no.1 ukapata 2, namba 4 kupata 5? nitashukuru sana.Kama ni ngumu pitia red zote katika posting zangu hapa.
Haya mkuu wangu mwelevu wewe tena ulikuwa wapi siku zote.. laa una akili sana weye..
 
Mkandara,
Naomba nitofautiane na wewe. Watu hawajachoshwa tu na utawala wa Kikwete, bali wamechoshwa na utawala wa CCM. Period. Sasa hivi hata akisimamishwa Magufuli, au Mwandosya, wimbi la uchovu wa CCM halitapukutika. Watu wameshafikia pale Mwalimu aliposema kuwa ikiwa CCM itashindwa kutoa uongozi bora watautafuta kwingineko. Tupo hapo sasa. CCM haiaminiki kabisa, bna ndiyo maana wameelekeza nguvu zao katika propaganda za kukivunja Chadema.
Yawezekana ilikuwa hivyo kwa muda lakini bro kuna vita kubwa sana ambayo huwezi kuiona hapa jukwaani. Unajua ni rahisi sana kuvutiwa na umati wa watu wanasema wamechoshwa na CCM lakini hawa hawa fahamu ni watu wa aina gani na sipendi kutumia neno langu maana nitakuwa nawatukana watanzania wenzangu lakini what You see ukiwapa mgongo watakumaliza. Nimekutana na watu ana kwa ana na kuwatupia maswali na trust me wengi wao wameichoka CCM kwa sababu ya JK maana wapo wengine kwa ujinga wao wanasema afadhali Mkapa angerudi na wengine kama angekuwa Lowassa isingekuwa hivi. Hawa ni watanznia wapiga kura ambao hawataki kuitazama Chadema kama chama mbadala isipokuwa kile walicholishwa.

Wapo wanasema wazi hawana imani na Chadema kwa sababu wameaminishwa Udini na kibaya zaidi kuna wahuni kama hawa wa JF ambao kwao wanaona deal kubwa sana kuzungumzia tofauti zao ktk kujikuza. Watanzania wengi wanaamini Udini upo na wengine wamefikia kuamini vyama vya Upinzani vinatumiwa na vyombo vya dini wala sio hila za CCM. Kwa Chadema kukosa kujibu mashambulizi kama haya, kuwaonyesha wananchi kwamba wapo kwa wananchi wote na hata kukubali kujibu maswali magumu yanayohusu tuhuma hizi inaongezea kupanua hisia mbaya za watu hasa wakati kama huu.

Mkuu wangu wewe na Mbowe mnanifahamu vizuri sana na hata marafiki na vijiwe vyangu kiasi kwamba hizi info wewe huwezi kupewa. Na hakuna kitu kibaya zaidi ikiwa Chama changu kina mapungufu ktk mawasiliano na wadau wa pande zote isipokuwa kujikita ktk mashambulizi wakati ngome yake inalika. Sisemi tunafanya vibaya kushambulia lakini nachotaka kuona ni ngome zetu wenyewe zimezatitiwa kiasi gani maana CCM na CUF wanapenya kirahisi sana kama vile hatuna ngome wakati hii ndio ngao yetu. Kama mchezo wa Draft mtu akisha ingia King atakumaliza haraka sana.
 
Back
Top Bottom