Waraka wa wazi kwa mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania

mwamola

Senior Member
May 28, 2012
109
15
Kwanza, heshima yako na pole kwa majukumu ya kila ya ujenzi wa taifa hili.\

Pili, Uniwie radhi kama nitakayosema yatakuwa mambo ya kawaida sana kiasi chakutostahili waraka huu. Hata hivyo nimeona yaweza kuwa ni ya muhimu kwangu/kwetu wahanga wa tatizo hili.

Mheshimiwa Rais mimi na wenzangu wafanyakazi wa UDOM tulikuwa promoted November 2010 na November 2011 kutoka ngazi moja ya utumishi kwenda nyingine. Kwa wale wa November 2010 tulikaa pasipo kulipwa mshahara wa ngazi mpya ya mshahara kwa miezi 13 pasipo kulipwa mshahara huo mpya hadi hapo December 2011 tulipolipwa.

Baada ya kulipwa tulijaza salary arrears claim forms mwezi February 2012 lakini hadi leo hatujalipwa malimbikizo hayo. Cha kusikitisha zaidi ni pale tulipokuwa tunajaza form hizo tuliambiwa tujaze mshahara wa chini ya stahili yetu kwa maelezo kuwa Hazina wangetulipa pasipo kujali kile tulichojaza (stahili yetu).

Naandika waraka huu kukuomba mawili;
i) Kuomba utusaidie tulipwe mapunjo (arrears) yetu kwakuwa imechukua muda mrefu sasa.
ii) Kuomba ofisi yako kupitia utumishi utupeleke kwenye ngazi stahili ya mshahara yaani PUTS 2/3 badala ya PUTS 2/1 ambayo tumekuwa tukilipwa tangu November, 2010

Tuna imani ofisi yako itatusadia kupata haki yetu hii cheleweshwa ama tuliyopunjwa kwa muda mrefu sasa.

Ndimi katika ujenzi wa taifa
Mtumishi katika nchi hii.
 
Fuatilia ngazi husika mkuu, si kila jambo latatuliwa na rais. Nna hakika hata ngazi ya wizara hutaifikia na hiyo ishu itakuwa solved easily.
 
Fuatilia ngazi husika mkuu, si kila jambo latatuliwa na rais. Nna hakika hata ngazi ya wizara hutaifikia na hiyo ishu itakuwa solved easily.
Nchi hii ina urasimu kaka, utakuta hata hwenye board husika hizo hela watu wanagawana na ukionekana unafuatilia basi huenda kibarua kikaota mbawa, hii ndo Tanzania bwana, sio UDOM tu hata ofisi zingine za Umma hayo mambo yapo, tena wale wenye kuchapa kazi vizuri ndo wanaodidimizwa sijui ni kwanini. kwa hiyo naomba binafsi kama rais ameliona hilo alifanyie kazi kwani watu siku hizi hawafanyi kazi zao kiuadilifu mpaka wasukumwa aibu sana hii.
 
Kama mnataka kulipwa vizuri, acheni kazi muende huko mnapopaamini- by JK

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kama ulilipwa hiyo ngazi mpya ya mshahara shukuru Mungu, kawaulize walimu wa sekondari na shule za msingi wanamadai ya kuanzia lini na wamejaza CLAIM FORMS mara ngapi......! Shukuru kwa japo hilo serikali na hazina haina hela hata za kulipa/kurejesha mabilioni yaliyokopwa PPF,NSSF, PSPF ili kukijenga chuo cha UDOM. Na ndio maana wamepitisha waraka kupitia SSRA kuzuia ulipwaji wa mafao hadi 60yrs kwa kua kufanya hivyo mifuko itafilisika mwaka 2013.

Agalizo ni kupima uwezo wa utendaji wa serikali ya CCM na kuchukua hatua 2015. Karubu kundini tumtafute kondoo aliepotea tangu uhuru mwaka 1961.......
 
Kibaya ni kwamba Rais wako huwa hasomi waraka ndani ya JF. Umeingia chaka! Vinginevyo mambo mazito yanachambuliwa humu yangesikilizwa hii nchi isingefika hapa tulipo!
 
Kibaya ni kwamba Rais wako huwa hasomi waraka ndani ya JF. Umeingia chaka! Vinginevyo mambo mazito yanachambuliwa humu yangesikilizwa hii nchi isingefika hapa tulipo!

Myopic thinking! unafikiri RAIS ni mtu mmoja? URAIS NI TAASISI, make no mistake kila siku wasaidizi/washauri wa RAIS husoma michango ya JF and when neccessary humpatia briefing.

Kwa mfano suala SSRA na mafao yetu, kelele za JF zimeshafika IKULU na RAIS ameshakuwa briefied. Inategemea tu pressure yetu itakuwaje wafanyakazi.

kama wewe unai underate JF kwanini kila siku inasemwa Bungeni? Mama Rwakatale, Dr. Nkya na jana Ngamia.

FYI, mitandao ya kijamii ndiyo iliratibu Arab springs ktk nchi za Algeria, Egypt, Libya!
 
Fuatilia kweneye ngazi husika na kuwa na subra ndugu, haki ya mtu haipotei.
Kuna watumishi wamedai muda mrf sana lkn baaade wakalipwa.
 
Fuatilia kweneye ngazi husika na kuwa na subra ndugu, haki ya mtu haipotei. Kuna watumishi wamedai muda mrf sana lkn baaade wakalipwa.
Wafanyakazi hawa wamefuatilia sana tena kwakupitia vikao halali vya ndani ya chuo vingi kadiri ilivyowezekana na kumekuwa na lugha mbalmbali tangu july 2011 kwa kupitia barua mbalimbali za PFA na Director HRM kuwa serikali imefikia pazuri na uongozi na muda wowote tutalipwa. Cha ajabu ni kuwa hadi sasa hatujalipwa na nimeomba ofisi ya Rais na kwa uwezo wa Rais mwenyewe watumishi hawa walipwe hii ni kutokana na kauli za waziri wa utumishi kuwa zikishajazwa tu hizo claim forms watalipwa lakini leo ndoto hizo zimezima. Zaidi ni kwamba hazina, utumishi na wizara ya elimu zimekuwa zikitajwa na maafsa wa UDOM kuwa ndio wakwamishaji wakubwa wa malipo haya. nimemwomba rais kwa kuwa yu zaidi ya wizara zote
 
Pole sana Mkuu, kama umeishafuatilia kwa HR, Wizarani na Utumishi ikashindikana, nakushauri uandike barua kwa Rais na kuambatisha mawasiliano ambayo yamekuwa yakifanyika. Maana hapa JF huwezi taja wewe ni nani kwa majina.
 
Pole sana Mkuu, kama umeishafuatilia kwa HR, Wizarani na Utumishi ikashindikana, nakushauri uandike barua kwa Rais na kuambatisha mawasiliano ambayo yamekuwa yakifanyika. Maana hapa JF huwezi taja wewe ni nani kwa majina.


Naunga mkono hoja!
 
Kwanza, heshima yako na pole kwa majukumu ya kila ya ujenzi wa taifa hili.\

Pili, Uniwie radhi kama nitakayosema yatakuwa mambo ya kawaida sana kiasi chakutostahili waraka huu. Hata hivyo nimeona yaweza kuwa ni ya muhimu kwangu/kwetu wahanga wa tatizo hili.

Mheshimiwa Rais mimi na wenzangu wafanyakazi wa UDOM tulikuwa promoted November 2010 na November 2011 kutoka ngazi moja ya utumishi kwenda nyingine. Kwa wale wa November 2010 tulikaa pasipo kulipwa mshahara wa ngazi mpya ya mshahara kwa miezi 13 pasipo kulipwa mshahara huo mpya hadi hapo December 2011 tulipolipwa.

Baada ya kulipwa tulijaza salary arrears claim forms mwezi February 2012 lakini hadi leo hatujalipwa malimbikizo hayo. Cha kusikitisha zaidi ni pale tulipokuwa tunajaza form hizo tuliambiwa tujaze mshahara wa chini ya stahili yetu kwa maelezo kuwa Hazina wangetulipa pasipo kujali kile tulichojaza (stahili yetu).

Naandika waraka huu kukuomba mawili;
i) Kuomba utusaidie tulipwe mapunjo (arrears) yetu kwakuwa imechukua muda mrefu sasa.
ii) Kuomba ofisi yako kupitia utumishi utupeleke kwenye ngazi stahili ya mshahara yaani PUTS 2/3 badala ya PUTS 2/1 ambayo tumekuwa tukilipwa tangu November, 2010

Tuna imani ofisi yako itatusadia kupata haki yetu hii cheleweshwa ama tuliyopunjwa kwa muda mrefu sasa.

Ndimi katika ujenzi wa taifa
Mtumishi katika nchi hii.
Wewe Jambo la kumalizwa n a UDOM unapeleka kwa Rais? hana muda huo na siyo kazi yake. kama management ya chuo imeshindwa kukusaidia appeal kwenye bodi ya chuo. I mean kwa Charman of board of Directors.
 
Wafanyakazi hawa wamefuatilia sana tena kwakupitia vikao halali vya ndani ya chuo vingi kadiri ilivyowezekana na kumekuwa na lugha mbalmbali tangu july 2011 kwa kupitia barua mbalimbali za PFA na Director HRM kuwa serikali imefikia pazuri na uongozi na muda wowote tutalipwa. Cha ajabu ni kuwa hadi sasa hatujalipwa na nimeomba ofisi ya Rais na kwa uwezo wa Rais mwenyewe watumishi hawa walipwe hii ni kutokana na kauli za waziri wa utumishi kuwa zikishajazwa tu hizo claim forms watalipwa lakini leo ndoto hizo zimezima. Zaidi ni kwamba hazina, utumishi na wizara ya elimu zimekuwa zikitajwa na maafsa wa UDOM kuwa ndio wakwamishaji wakubwa wa malipo haya. nimemwomba rais kwa kuwa yu zaidi ya wizara zote
umeonana na katibu wa wizara mara nagpi kuhusu jambo hili? au mwenyekiti wa bodi? au mkurugenzi wa wizara anayeshughulika na HR za vyuo?
 
Mambo ya huko UDOM yanatisha. Unaweza ukaajiriwa ukamaliza hata mwaka mzima bila kuthibitishwa kazini wakati sheria za kazi zinasema ukimaliza miezi 6 uthibitishwe!
 
Back
Top Bottom