HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Habari za leo Wana JF?
Binafsi si mpenzi wa kuandika nyaraka lakini nimejikuta nalazimika kuandika waraka huu kwa uchungu mkubwa kutokana na mambo ambayo nimeyasikia na kuyashuhudia kupitia vyomba vya habari juu ya mpasuko mkubwa wa kimahusiano ambao umeanza kujitokeza kati ya baadhi ya waumini wa dini za Kiislam na Kikristo.
Kwa siku za hivi karibuni tumesikia vurugu nyingi kati ya waumini wa dini fulani na polisi, waumini fulani na kuchomeana majengo ya ibada, waumini fulani na udhalilishaji wa vitabu vya dini nyingine nk. Hili si jambo la kuchekewa hata kidogo maana halina mwisho mzuri. Inawezekana likawa limepandikizwa na baadhi ya watu kwa manufaa yao binafsi na ndiyo maana nimeamua kurudi hapa kuomba viongozi wa dini zetu wafanye jambo mapema kutunusuru na kutupa amani ya kudumu.
Kudumisha amani napendekeza wapenda amani wote na viongozi wetu wa dini kutufundisha sisi waumini wao mambo yafuatayo
Nawashukuru baadhi ya viongozi wa dini hasa wa Kiislam ambao wamediriki kutoa matamko ya wazi ya kudumisha amani na kuvumilia, nawatakia kheri kwa msimamo wao wa kujali na kuheshimu imani na amani ndani ya nchi.
Pia nawapongeza baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristo kwa kuhubiri amani wazi wazi na kuwafundisha waumini wao kuwa wavumilivu na kutokushambulia wengine.
Watanzania, tuwe makini na watu wanaotaka kutugawa, tukumbuke kuwa hakuna nchi hata moja iliyowahi kuendelea au kufaidika kwa chuki na ugomvi wa kidini, na pia hakuna nchi iliyofanikiwa kuifuta dini nyingine ndani ya nchi na kupata amani.
Mwisho ningependa watu wote wausome waraka huu wakiwa na mtazamo wa kuisaidia nchi ikae kwa amani na siyo kuleta malumbano ya kidini yasiyo na tija ndani ya uzi huu, SIPENDI!
Nawapenda Watanzania wote na napenda tuishi kwa amani na upendo,
Nawakilisha,
HorsePower Kufakunoga.
October, 2012
******** Naomba usichangie, soma kwa faida yako *****
Binafsi si mpenzi wa kuandika nyaraka lakini nimejikuta nalazimika kuandika waraka huu kwa uchungu mkubwa kutokana na mambo ambayo nimeyasikia na kuyashuhudia kupitia vyomba vya habari juu ya mpasuko mkubwa wa kimahusiano ambao umeanza kujitokeza kati ya baadhi ya waumini wa dini za Kiislam na Kikristo.
Kwa siku za hivi karibuni tumesikia vurugu nyingi kati ya waumini wa dini fulani na polisi, waumini fulani na kuchomeana majengo ya ibada, waumini fulani na udhalilishaji wa vitabu vya dini nyingine nk. Hili si jambo la kuchekewa hata kidogo maana halina mwisho mzuri. Inawezekana likawa limepandikizwa na baadhi ya watu kwa manufaa yao binafsi na ndiyo maana nimeamua kurudi hapa kuomba viongozi wa dini zetu wafanye jambo mapema kutunusuru na kutupa amani ya kudumu.
Kudumisha amani napendekeza wapenda amani wote na viongozi wetu wa dini kutufundisha sisi waumini wao mambo yafuatayo
- Kuheshimu dini na imani za watu wengine
- Kila muumini na afundishwe namna ya kuvumilia wafuasi wa imani nyingine na kutumia vyombo vya sheria kuchukua hatua kwa matukio ambayo yanaonekana yana lengo la kudhalilisha imani nyingine
- Kufundisha mafundisho ya namna ya kumsaidia muumini kuishi maisha ya kumpendeza muumba wake badala ya mafundisho ya chuki dhidi ya watu wa imani tofauti
- Waumini tufundishwe kuwa vurugu, chuki, mapigano, vita, hasira na mengineyo mengi yanayofanana na hayo kwa namna yeyote ile hayataweza kutusaidia kuondokana na tatizo tulilonalo sasa na badala yake hujenga chuki zaidi na mbaya zaidi kwa watoto wetu ambao ndio taifa la kesho. Hapa kuna hatari ya kujenga taifa lenye chuki, lisilo na amani na kukosa upendo.
- Kwa namna yeyote ile, hakuna dini inayoweza kuiondoa dini nyingine ndani ya nchi hata kama kutatokea vita ya miaka hamsini na zaidi, hivyo kupigana vita, kuchomeana nyumba za ibada na pengine hata kuuana ni kudhulumu uhai na nafsi za watu zisizo na hatia na kujiweka kwenye umasikini ambao hauna tija ya namna yeyote.
- Migogoro ya kidini huishia kwenye kuitia nchi kwenye umaskini badala ya kupata suluhu ya dini maana mwisho wa siku suala la imani halihitaji nguvu, linahitaji convincing power.
- Tujifunze kutoka kwenye nchi zenye migogoro ya kivita tuone kama kuna imani moja imefanikiwa kuiondoa imani nyingine au ni faida gani waliyoipata katika hivyo vita kama siyo kupoteza ndugu zao na kujitupia kwenye shimo la umaskini!!! Tujifunze toka Nigeria na nchi nyingine jamani!
- Kupiga marufuku mikutano ya wazi inayofanywa na wafuasi wa dini nyingine kuchambua vitabu vya dini nyingine na pia malumbano yeyote yale baini ya dini mbili tofauti.
Nawashukuru baadhi ya viongozi wa dini hasa wa Kiislam ambao wamediriki kutoa matamko ya wazi ya kudumisha amani na kuvumilia, nawatakia kheri kwa msimamo wao wa kujali na kuheshimu imani na amani ndani ya nchi.
Pia nawapongeza baadhi ya viongozi wa dini ya Kikristo kwa kuhubiri amani wazi wazi na kuwafundisha waumini wao kuwa wavumilivu na kutokushambulia wengine.
Watanzania, tuwe makini na watu wanaotaka kutugawa, tukumbuke kuwa hakuna nchi hata moja iliyowahi kuendelea au kufaidika kwa chuki na ugomvi wa kidini, na pia hakuna nchi iliyofanikiwa kuifuta dini nyingine ndani ya nchi na kupata amani.
Mwisho ningependa watu wote wausome waraka huu wakiwa na mtazamo wa kuisaidia nchi ikae kwa amani na siyo kuleta malumbano ya kidini yasiyo na tija ndani ya uzi huu, SIPENDI!
Nawapenda Watanzania wote na napenda tuishi kwa amani na upendo,
Nawakilisha,
HorsePower Kufakunoga.
October, 2012
******** Naomba usichangie, soma kwa faida yako *****