Waraka wa Tambwe Hizza kwa watanzania

Hoja ya msingi :
1:kwanini chadema ilishidwa vibaya kwa kupata viti 23 kati ya 239 kwenye uchaguzi uliopita?

2:Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite?

3:Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini?

4:Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye?

5:Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao?

6:Je walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo Tundu Lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa CCM, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana CCM huko Sumbawanga na Igunga.

Hizi ni hoja za msingi sana ambazo hazijajibiwa so far zaidi zaidi naona watau wanatapa tapa tu na kumshambulia mtoa hoja binafsi badala ya hoja zake,ondokeni kwenye denial and anger jibuni hoja

hizo ndio hoja za kitoto,
Labda utueleze kikosi cha kutuliza ghasia kilienda kutuliza ghasia gani, zilizoripotiwa kufanywa na nani.

kwa mafunzo waliyoyapata ccp, polisi walishindwaje kuwakamata wafanya ghasia pamoja na kuwa na zana za kisasa kutuliza ghasia.

Hatukuonyeshwa watu wakifanya ghasia, lakini inakuwaje lengo kuu la kutuliza ghasia linakuwa kuua.

Kanuni ya kijeshi inaelekeza kuwa "ukimkamata mateka unawajibika kumlinda" kwa maneno mengine huruhusiwi kumuua, huyu Mwangosi RIP
alikuwa ameshikiliwa na polisi wasiopungua sita, wamemuuaje tena mbele ya makamanda wawili, kamuhanda na kamanda wa kikosi cha kutuliza ghasia.

Cha kujadili hapa ni;
Amri ya kuua ilitolewa na nani kati ya hao makamanda wawili.

Ikiwa muuaji alitekeleza mauaji bila amri ya senior polisi officers, ni vipi hao senior polisi officers hawakulaani mauaji hayo with immediate effect, na kumshitaki kwenye mahakama ya kijeshi immediately.

Kwa kuwa mazingira yanatuelekeza kuwa makamanda walitoa amri ya kuua, ndiyo maana wakachukua hatua ya kumtetea na kumkingia kifua muuaji,

kwa mwendelezo huo huo na nchimbi katumbukia kwenye kosa la kuwatetea wauaji sawasawa na kamuhanda,
Na ccm inamtetea nchimbi, anayewatetea kamuhanda & kamanda wa kikosi cha kutuliza ghasia, wanaomtetea askari muuaji.

Hatudanganywi kwa waraka wa MTU ALALAYE NA MAMA YAKE KAMA ALAVYO NA MKEWE, kama alivyouhakikishia umma kwa ahadi ya kurudi ccm.
 
Hapana ambavyo nataka kufahamu ni hivi:

1:kwanini chadema ilishidwa vibaya kwa kupata viti 23 kati ya 239 kwenye uchaguzi uliopita?

2:Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite?

3:Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini?

4:Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye?

5:Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao?

6:Je walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo Tundu Lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa CCM, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana CCM huko Sumbawanga na Igunga.

Nakujibu moja moja:

1:kwanini chadema ilishidwa vibaya kwa kupata viti 23 kati ya 239 kwenye uchaguzi uliopita?

Sijui ni uchaguzi upi unao uzungumzia na sielewi uchaguzi unahusianaje na thread?

2:Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite?

CHADEMA walizuiwa kufanya mikutano ya hadhara na wao wakaamua kufanya vikao vya ndani na wakapigwa mabomu wakiwa ndani(kielelezoo naambatanisha)
ofisi%2Bya%2BChadema%2BNyololo%2Bikifuk%2Bmoshi%2B%2Bwa%2Bmabomu.JPG


3:Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini?

Fafanua CHADEMA walikaidi nini(refer #2)...na kwa nini mara kwa mara?

4:Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye?

Wangewaacha tu kwa kuwa hawakuwa wanafanya mkutano wa hadhara

5:Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao?

Hapo sijui una maana gani
 
ok sawa tukubali hiyo,haya tuje upande wa pili kwa nini chadema ilikiuka amri ya jeshi la polisi ambalo walikwenda kuliomba kibali likawakatalia ili kupisha shughuli ya kitaifa?mbona waislam walipogomea shughuli hiyo tuliwazomea humu,kwanini chadema walilazimisha kufanya yale yale ya waislam lakini katika style tofauti???na mbona polisi hiyo hiyo ndio imekua ikiwakubalia kila walipoomba kwanini nao wasionyeshe fair play kwa kuikubalia polisi kwa angalau hiyo mara moja?tena chadema ina bahati kila wakati ikiomba kibali inapewa cuf enzi za mahita nadhani mnakumbuka ilivyokua ngumu mpaka wakawa wanaforce na nganagari yao ndio wanapewa

Acha uvivu wa kufikiri ,suala sio CDM na CCM .Hapa cha kujadili ni Kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa kiasi kile mpaka kupelekea mauti ya Mwongoso. Usitake kupaka ukweli wa mambo rangi kwa mashairi yasiyo na vina ,beti wala mizani kwa kuhalalisha kilichofanywa na polisi kuwa ni sahihi.Zipo njia za kupambana na wanaovunja taratibu/ maagizo ya serikali .Usihalalishe uharamia ule kwa chuki na ushabiki wa kivyama,makala hii imeegemea kiushabiki zaidi na si uhalisia/ukweli.
 
na richard tambwe hizza

wiki hii waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali nchini waliandamana kulaani kuuawa kwa mwandishi wa habari wa kituo cha chanel 10 huko iringa, kifo cha mwandishi huyu kwa bahati mbaya na kwa mara nyingine tena kimewagawa wananchi katika makundi yanayotofautiana kifikra kuhusu chanzo na hatimaye kufariki kwake.

Wapo wanaoona na kuamini polisi wametumia nguvu kubwa katika kukabiliana na tatizo lililokuwepo, wapo wanaoamini kwamba jeshi la polisi lilikuwa linatimiza wajibu wake na madhara haya makubwa yaliyotokea yanatokana na chadema kuendeleza ghasia katika nchi na kujaribu kuifanya isitawalike kama walivyoahidi baada ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu uliopita (walishinda viti 23 kati ya majimbo 239).

Hata hivyo, kabla ya kuingia katika tafakuri pana zaidi zinazotokana na msiba huu sina budi kutoa pole kwa familia ya mwangosi, waandishi waliokuwa karibu naye katika kufanikisha majukumu yake ya uandishi wa habari, kituo cha channel 10 na watanzania wote kwa ujumla, kwa kuondokewa na mwananchi mwenzetu katika mazingira ambayo wote hatukuyategemea.

Tumeshuhudia wakati taifa likiwa katika simanzi nzito kutokana na msiba huu, wapo wenzetu walioamua kuutumia kama turufu ya kuleta chuki baina ya jeshi la polisi na waandishi na zaidi umma wa watanzania ambao usalama wao na mali zao unategemea sana uwepo wa jeshi hilo. Kuna mambo mengi ambayo nimekuwa najiuliza na ningependa watanzania wote tujiulize, hivi ghasia zilizosababisha msiba huu zilisababishwa na nini/nani?

Je kulikuwa na ulazima kwa chadema kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite? Je, ukaidi wa chadema siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini? Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia chadema kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye? Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao? Na je, uhalali wa uwepo wa jeshi hilo ungeendelea kuwepo?

Wananchi wote tunapaswa kuheshimu sheria na polisi wana jukumu la kutulazimisha kufuata sheria tunapozikiuka vikiwemo vyama vya siasa, najua sheria ya vyama vya siasa inavipa fursa vyama kufanya maandamano na mikutano baada ya kutoa taarifa polisi, lakini sheria hiyo hiyo inasema vitafanya hivyo endapo tu kama havitapata amri pingamizi kutoka polisi (sheria ya vyama vya siasa 1992 kifungu cha 11).

Tujiulize kulikuwa na ulazima gani kwa chadema ambao mwaka mzima wamekuwa wakiruhusiwa kufanya mikutano na maandamano kulazimisha kufanya mkutano uliosababisha kifo baada ya kupata amri pingamizi? Kama waliona polisi hawakuwafanyia haki je ilikuwa vyema kuandaa mapambano dhidi ya polisi? Jje walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo tundu lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa ccm, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana ccm huko sumbawanga na igunga.

Naamini ili jeshi la polisi liweze kuendelea kulinda amani ndani ya nchi ni lazima tuliamini na lazima tujue kwamba lipo, likizuia jambo kwa mujibu wa sheria wote tuheshimu vinginevyo litakuwa halina sababu ya kuwepo. Si mara moja au mbili mamlaka za umma na vyombo vya sheria viliamua mambo muhimu katika maendeleo ya taifa, lakini yalipata upinzani hadi pale polisi ilipotumia nguvu kuhakikisha sheria inafuatwa na utekelezaji wake unatimia.

Je, kumfukuza waziri katika hafla ya kulaani mauaji na kumkaribisha mwana-chadema dk. Lweitama kuhutubia na kuilaani serikali ni sawa? Je, ni sawa kulilaumu jeshi zima la polisi kwa tatizo lililojitokeza sehemu moja ya nchi tena katika kutimiza wajibu wao? Kitendo cha kutowalaani walioanzisha uvunjaji wa sheria uliosababisha ndugu yetu mwangosi kupoteza maisha katika umri mdogo kinaashiria nini kutoka katika taasisi zetu za habari?

Hapa ndiyo maswali mengine yasiyo na majibu yanapoanza, kwa nini tamko lililotolewa na chadema na lile la wanahabari yanashabihiana. Kwa nini wanahabari hawakuilaumu chadema hata mara moja kwa kutokutii sheria na kuanzisha ghasia zilizosababisha maafa ya ndugu yetu. Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi. Je wametumwa? Wana hasira? Au nao wameanza kushirikishwa katika ajenda za siri dhidi ya serikali na vyombo vyake?

Wote tumesikitishwa na msiba huu sidhani kama ni vyema kuendelea kushambulia jeshi la polisi bali kuangalia nani ameanzisha sokomoko ili awajibishwe kisheria, kama ikibainika aliyeua ni raia wa kawaida sheria ichukue mkondo wake, pia ikibainika muuaji ni askari akiwa katika kutimiza majukumu yake ni vyema taratibu za kijeshi na mahakama zitumike badala ya kuendeleza chuki zisizo na msingi.

Tusijisahau wote tunawahitaji polisi kama ambavyo tulikuwa tunamhitaji ndugu yetu mwangosi nikiwemo mimi niliyeshirikiana naye katika shughuli mbalimbali. Tusiwe na hasira maana wahenga walisema hasira hasara. Tutafute suluhisho la yanayotokea yasijirudie.
koma kabisa mi usalama wangu hata hautegemei hao policcm wako mi usalama wangu ni juu yangu na mungu wangu, kama jeshi la polisi kweli linatimiza majukumu yake je lingeuwa watu wasio na hatia na kuwaacha majambazi? Mbona benk imeibiwa juzi tu afu halijafanya chochote, kama wanaweza si wangezuia ule ualifu, narudia tena usala wangu ni juu yangu na mungu wangu, nimeibiwa mara mbili mbaka leo hata dalili za kuwakamata watuhumiwa siajaziona, na mara ya mwisho n8iliwaambia hata mtu ninayemhisi wakanitoza hela za mafuta na za kuwapa askari lakini hawakufanya chochote, hawana maana kwanza mbele yao mi ndo naona usalama unapotea zaidi bora livunjwe tu. Ilivunjwa kgb sembuse na hiki kijeshi chetu cha wahalifu, mapusha, wakodisha silaha kwa majambazi, walinzi wa mafisadi? Wafe tu
 
mbona unakwepa kutumia maneno chadema walivunja sheria kama ulivvyofanya kwa polisi?au ndio ule usemi mkubwa hakombi mboga akikomba tunaondoa ukali wa maneno kwa kusema kaipenda?tuwe wakweli tuache unafiki na ushabiki kupita kiasi

Naona hujanipata vizuri, sitaki kumtetea mtu wala kumuonena mtu. Kuhusu Chadema kuvunja sheria bado ni debatable kwa sababu wao wanasema ule ulikuwa mkutano wa ndani na yale hayakuwa maandamano wala mkutano wa hadhara.

Ila makosa ya polisi yapo clear, hamna debate. Mwandishi kapigwa bomu la machozi tumboni!! Wapi ambapo polisi wanaelekezwa hizi mbinu??

Ninachotaka kusisitiza ni kwamba two wrongs dont make no right, CHADEMA kuvunja sheria hakuwezi kuwa kisingizio cha polisi kuvunja sheria. Na kama kosa lilikuwa la CHADEMA mbona askari ndio ana kesi mahakamani?? Polisi wakubali tu kwamba wali-mess katika hili swala, kuendelea kuilaumu CHADEMA kutawafanya wao waonekane kama tawi la CCM.
 
daah jamani njaa mbaya huyu jamaa wakati yupo cuf alikuwa msumbufu kwa serikali na polisi haohao anaowatetea leo,hata mauaji ya kule ZENJI aliyalaani tena sana ila leo yupo NYINYIEMU anawasifia polisi eti walikuwa wanatekeleza majukumu yao,mh napata shida sana kuamini anayoyasema kwani sidhani kama majukumu ya polisi ni KUUA,ila kamwe simlaumu kwani aliporudi nyinyiemu alipewa cheo cha KISHKAJI eti MKURUGENZI WA PROPAGANDA waliposhindwa kule TARIME kwenye uchaguzi mdogo ndo ukawa mwisho wa mimi kumsikia huyu mtu ndo nakutana na UOZO wake huu leo humu kwenye JF.labda anajaribu kuwaonnesha magamba kuwa bado anaweza kazi ya PROPAGANDA ambayo hivi sasa amepewa mropokaji NEPI,nahofu kuwa huenda hata JF ikaja kudharauliwa kama watu wenye kuweka mada humu ni wa aina hii,IS HE A GREAT THINKER????????????????
MODS please hawa watu wanachafua hili jukwaa msiwape nafasi kuweka MAUOZO yao humu ili jukwaa liendelee kuheshimika.
 
Kitengo cha propaganda kilivunjwa ndani ya CCM baada ya kukulaghai kisiasa, sasa, Hiza, rudi CUF uwaombe msamaha.
 
...aaah Hiza,naona ushammisi Mwarabu wako aliyekuwa anakupumulia mgongoni. Tumepata habari kuwa alisharudi Uarabuni,naona sasa mnduku unakuwasha maana umekosa basha mbadala.
 
CCM inabidi msome nyakati, kizazi hiki si cha kudanganya kirahisi. Mbona BUBUBU na KAGERA shughuli za CCM zilikuwa zinaendelea wakati wa sensa? Mbona NCCR Mageuzi, CUF nao mmewahi kuwaona wabaya kipindi fulani, mbona CHADEMA sasa? chama kipi chema kwenu?

acha propaganda za enzi za mwalimu, this is new generation bwana
 
Tambe ni mzigo hata ndani ya ccm hilo linajulikana kapoteza uwezo wake toka hakiame chama cha CUF Shame on you
 
Haki ya mungu maswali ya kumuuliza Tambwe ni mengi Mno tena mno lakini kwa ninavyo mfahamu ngoja nimuulize dogo tu,

Hivi kumbe Mwangosi alikuwa kiongozi au mwanachama wa chadema aliyekiuka hiyo inayoitwa amri halali ya polisi?
 
chama kimebakiwa na mabomu tupu yanalipuka bila kuwa na target which is more than dangerous
 
Nilikuwa simfahamu Tambwe hiza, nikabahatika kumuona siku ccm wamefanya mkutano jangwani na kigali fulani hata hukiwa dereva taxi utakosa watu kama una kigali kama anachotumia Tambwe Hiza, KAZI yake propaganda wajanja ndo wanafaidi ccm
 
NA RICHARD TAMBWE HIZZA

WIKI hii waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali nchini waliandamana kulaani kuuawa kwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Chanel 10 huko Iringa, kifo cha mwandishi huyu kwa bahati mbaya na kwa mara nyingine tena kimewagawa wananchi katika makundi yanayotofautiana kifikra kuhusu chanzo na hatimaye kufariki kwake.

Wapo wanaoona na kuamini polisi wametumia nguvu kubwa katika kukabiliana na tatizo lililokuwepo, wapo wanaoamini kwamba jeshi la polisi lilikuwa linatimiza wajibu wake na madhara haya makubwa yaliyotokea yanatokana na CHADEMA kuendeleza ghasia katika nchi na kujaribu kuifanya isitawalike kama walivyoahidi baada ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu uliopita (walishinda viti 23 kati ya majimbo 239).

Hata hivyo, kabla ya kuingia katika tafakuri pana zaidi zinazotokana na msiba huu sina budi kutoa pole kwa familia ya Mwangosi, waandishi waliokuwa karibu naye katika kufanikisha majukumu yake ya uandishi wa habari, Kituo cha Channel 10 na Watanzania wote kwa ujumla, kwa kuondokewa na mwananchi mwenzetu katika mazingira ambayo wote hatukuyategemea.

Tumeshuhudia wakati taifa likiwa katika simanzi nzito kutokana na msiba huu, wapo wenzetu walioamua kuutumia kama turufu ya kuleta chuki baina ya jeshi la polisi na waandishi na zaidi umma wa Watanzania ambao usalama wao na mali zao unategemea sana uwepo wa jeshi hilo. Kuna mambo mengi ambayo nimekuwa najiuliza na ningependa Watanzania wote tujiulize, hivi ghasia zilizosababisha msiba huu zilisababishwa na nini/nani?

Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite? Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini? Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye? Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao? Na je, uhalali wa uwepo wa jeshi hilo ungeendelea kuwepo?

Wananchi wote tunapaswa kuheshimu sheria na polisi wana jukumu la kutulazimisha kufuata sheria tunapozikiuka vikiwemo vyama vya siasa, najua sheria ya vyama vya siasa inavipa fursa vyama kufanya maandamano na mikutano baada ya kutoa taarifa polisi, lakini sheria hiyo hiyo inasema vitafanya hivyo endapo tu kama havitapata amri pingamizi kutoka polisi (sheria ya vyama vya siasa 1992 kifungu cha 11).

Tujiulize kulikuwa na ulazima gani kwa CHADEMA ambao mwaka mzima wamekuwa wakiruhusiwa kufanya mikutano na maandamano kulazimisha kufanya mkutano uliosababisha kifo baada ya kupata amri pingamizi? Kama waliona polisi hawakuwafanyia haki je ilikuwa vyema kuandaa mapambano dhidi ya polisi? Jje walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo Tundu Lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa CCM, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana CCM huko Sumbawanga na Igunga.

Naamini ili jeshi la polisi liweze kuendelea kulinda amani ndani ya nchi ni lazima tuliamini na lazima tujue kwamba lipo, likizuia jambo kwa mujibu wa sheria wote tuheshimu vinginevyo litakuwa halina sababu ya kuwepo. Si mara moja au mbili mamlaka za umma na vyombo vya sheria viliamua mambo muhimu katika maendeleo ya taifa, lakini yalipata upinzani hadi pale polisi ilipotumia nguvu kuhakikisha sheria inafuatwa na utekelezaji wake unatimia.

Je, kumfukuza waziri katika hafla ya kulaani mauaji na kumkaribisha mwana-CHADEMA Dk. Lweitama kuhutubia na kuilaani serikali ni sawa? Je, ni sawa kulilaumu jeshi zima la polisi kwa tatizo lililojitokeza sehemu moja ya nchi tena katika kutimiza wajibu wao? Kitendo cha kutowalaani walioanzisha uvunjaji wa sheria uliosababisha ndugu yetu Mwangosi kupoteza maisha katika umri mdogo kinaashiria nini kutoka katika taasisi zetu za habari?

Hapa ndiyo maswali mengine yasiyo na majibu yanapoanza, kwa nini tamko lililotolewa na CHADEMA na lile la wanahabari yanashabihiana. Kwa nini wanahabari hawakuilaumu CHADEMA hata mara moja kwa kutokutii sheria na kuanzisha ghasia zilizosababisha maafa ya ndugu yetu. Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi. Je wametumwa? Wana hasira? au nao wameanza kushirikishwa katika ajenda za siri dhidi ya serikali na vyombo vyake?

Wote tumesikitishwa na msiba huu sidhani kama ni vyema kuendelea kushambulia jeshi la polisi bali kuangalia nani ameanzisha sokomoko ili awajibishwe kisheria, kama ikibainika aliyeua ni raia wa kawaida sheria ichukue mkondo wake, pia ikibainika muuaji ni askari akiwa katika kutimiza majukumu yake ni vyema taratibu za kijeshi na mahakama zitumike badala ya kuendeleza chuki zisizo na msingi.

Tusijisahau wote tunawahitaji polisi kama ambavyo tulikuwa tunamhitaji ndugu yetu Mwangosi nikiwemo mimi niliyeshirikiana naye katika shughuli mbalimbali. Tusiwe na hasira maana wahenga walisema hasira hasara. Tutafute suluhisho la yanayotokea yasijirudie.

***** mtupu nauliza huyu mtu ana elimu gani na umri gani?naombeni msaada
 
NA RICHARD TAMBWE HIZZA
..........................................................................................

Hapa ndiyo maswali mengine yasiyo na majibu yanapoanza, kwa nini tamko lililotolewa na CHADEMA na lile la wanahabari yanashabihiana. Kwa nini wanahabari hawakuilaumu CHADEMA hata mara moja kwa kutokutii sheria na kuanzisha ghasia zilizosababisha maafa ya ndugu yetu. Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi. Je wametumwa? Wana hasira? au nao wameanza kushirikishwa katika ajenda za siri dhidi ya serikali na vyombo vyake?.................................................................................

SWALI LA MUHIMU NI MOJA TU, NALO NI:
Je, ni sheria ipi ambayo CDM hawakuitii ambayo CCM na vyama vyingine viliitii, ikumbukwe kwamba CCM walifanya mikutano ya hadhara siku hiyo hiyo ya utii wa sheria ili hali CDM walikuwa na mkutano wa ndani...?????

Nimekubali moja tu katika uliyoandika kwamba
"Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi." japo na yenyewe haiko sawa sema unahitaji sio tunahitaji.

Umeandika ukiwa umejifunika boksi kichwani (kama sio gamba) au umeazima ubongo wa Tendwa.

Jitafakuri halafu uandike upya...!!

 
Wewe acha ushabiki, jadili waraka wa tambwe hiza na sio slaa na mbowe. Upo nje ya bit,behave mkuu ata kama ni ushabiki wewe umepitiliza.

Zomba yuko sahihi. Na CCM mnaichukia kwa sababu mwenyekiti wake ni mwislamu!!! Siku mwenyekiti akiwa mkisto wooooote mtaipenda CCM!
 
NA RICHARD TAMBWE HIZZA

WIKI hii waandishi wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali nchini waliandamana kulaani kuuawa kwa mwandishi wa habari wa Kituo cha Chanel 10 huko Iringa, kifo cha mwandishi huyu kwa bahati mbaya na kwa mara nyingine tena kimewagawa wananchi katika makundi yanayotofautiana kifikra kuhusu chanzo na hatimaye kufariki kwake.

Wapo wanaoona na kuamini polisi wametumia nguvu kubwa katika kukabiliana na tatizo lililokuwepo, wapo wanaoamini kwamba jeshi la polisi lilikuwa linatimiza wajibu wake na madhara haya makubwa yaliyotokea yanatokana na CHADEMA kuendeleza ghasia katika nchi na kujaribu kuifanya isitawalike kama walivyoahidi baada ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu uliopita (walishinda viti 23 kati ya majimbo 239).

Hata hivyo, kabla ya kuingia katika tafakuri pana zaidi zinazotokana na msiba huu sina budi kutoa pole kwa familia ya Mwangosi, waandishi waliokuwa karibu naye katika kufanikisha majukumu yake ya uandishi wa habari, Kituo cha Channel 10 na Watanzania wote kwa ujumla, kwa kuondokewa na mwananchi mwenzetu katika mazingira ambayo wote hatukuyategemea.

Tumeshuhudia wakati taifa likiwa katika simanzi nzito kutokana na msiba huu, wapo wenzetu walioamua kuutumia kama turufu ya kuleta chuki baina ya jeshi la polisi na waandishi na zaidi umma wa Watanzania ambao usalama wao na mali zao unategemea sana uwepo wa jeshi hilo. Kuna mambo mengi ambayo nimekuwa najiuliza na ningependa Watanzania wote tujiulize, hivi ghasia zilizosababisha msiba huu zilisababishwa na nini/nani?

Je kulikuwa na ulazima kwa CHADEMA kukaidi amri ya polisi ya kusubiri sensa ipite? Je, ukaidi wa CHADEMA siyo chanzo cha maafa yaliyotokea na yanayotokea mara kwa mara nchini? Je, ingekuwa sawa kwa jeshi la polisi kuwaachia CHADEMA kufanya shughuli ambayo walikwisha wazuia wasiifanye? Je, polisi ingewaachia kufanya jambo ambalo walikwishawazuia wangekuwa wanatimiza sheria na wajibu wao? Na je, uhalali wa uwepo wa jeshi hilo ungeendelea kuwepo?

Wananchi wote tunapaswa kuheshimu sheria na polisi wana jukumu la kutulazimisha kufuata sheria tunapozikiuka vikiwemo vyama vya siasa, najua sheria ya vyama vya siasa inavipa fursa vyama kufanya maandamano na mikutano baada ya kutoa taarifa polisi, lakini sheria hiyo hiyo inasema vitafanya hivyo endapo tu kama havitapata amri pingamizi kutoka polisi (sheria ya vyama vya siasa 1992 kifungu cha 11).

Tujiulize kulikuwa na ulazima gani kwa CHADEMA ambao mwaka mzima wamekuwa wakiruhusiwa kufanya mikutano na maandamano kulazimisha kufanya mkutano uliosababisha kifo baada ya kupata amri pingamizi? Kama waliona polisi hawakuwafanyia haki je ilikuwa vyema kuandaa mapambano dhidi ya polisi? Jje walichukua hatua yoyote ya kisheria dhidi ya polisi au hawana imani na vyombo vya kisheria kama ambavyo Tundu Lissu anavyoziponda mahakama zetu bila kuheshimu kwamba zilimpa ushindi yeye binafsi katika kesi yake ya uchaguzi aliyofunguliwa na mgombea wa CCM, na zile zilizokipa ushindi chama chake zilizowavua ubunge wana CCM huko Sumbawanga na Igunga.

Naamini ili jeshi la polisi liweze kuendelea kulinda amani ndani ya nchi ni lazima tuliamini na lazima tujue kwamba lipo, likizuia jambo kwa mujibu wa sheria wote tuheshimu vinginevyo litakuwa halina sababu ya kuwepo. Si mara moja au mbili mamlaka za umma na vyombo vya sheria viliamua mambo muhimu katika maendeleo ya taifa, lakini yalipata upinzani hadi pale polisi ilipotumia nguvu kuhakikisha sheria inafuatwa na utekelezaji wake unatimia.

Je, kumfukuza waziri katika hafla ya kulaani mauaji na kumkaribisha mwana-CHADEMA Dk. Lweitama kuhutubia na kuilaani serikali ni sawa? Je, ni sawa kulilaumu jeshi zima la polisi kwa tatizo lililojitokeza sehemu moja ya nchi tena katika kutimiza wajibu wao? Kitendo cha kutowalaani walioanzisha uvunjaji wa sheria uliosababisha ndugu yetu Mwangosi kupoteza maisha katika umri mdogo kinaashiria nini kutoka katika taasisi zetu za habari?

Hapa ndiyo maswali mengine yasiyo na majibu yanapoanza, kwa nini tamko lililotolewa na CHADEMA na lile la wanahabari yanashabihiana. Kwa nini wanahabari hawakuilaumu CHADEMA hata mara moja kwa kutokutii sheria na kuanzisha ghasia zilizosababisha maafa ya ndugu yetu. Nadhani tunahitaji tafakuri pana zaidi. Je wametumwa? Wana hasira? au nao wameanza kushirikishwa katika ajenda za siri dhidi ya serikali na vyombo vyake?

Wote tumesikitishwa na msiba huu sidhani kama ni vyema kuendelea kushambulia jeshi la polisi bali kuangalia nani ameanzisha sokomoko ili awajibishwe kisheria, kama ikibainika aliyeua ni raia wa kawaida sheria ichukue mkondo wake, pia ikibainika muuaji ni askari akiwa katika kutimiza majukumu yake ni vyema taratibu za kijeshi na mahakama zitumike badala ya kuendeleza chuki zisizo na msingi.

Tusijisahau wote tunawahitaji polisi kama ambavyo tulikuwa tunamhitaji ndugu yetu Mwangosi nikiwemo mimi niliyeshirikiana naye katika shughuli mbalimbali. Tusiwe na hasira maana wahenga walisema hasira hasara. Tutafute suluhisho la yanayotokea yasijirudie.

Tambwe Hiza ni anaendeleza unafiki wa wanachama wengi wa ccm na viongozi wao. Tambwe anafahamu kuwa siku hiyo hiyo ya tarehe 2 ndio ccm walikuwa wanazindua kampeni za ubunge huko Bububu? Je Hiza anataka kutuambia kuwa Bububu hakukuwa na sensa au Bububu sio Tanzania? Labda pia atueleze kuwa zuio lililowekwa ili kuruhusu sensa liliihusu CHADEMA peke yake? Hiza anatambua kuwa harakati za uchaguzi wa wajumbe na wenyeviti wa mikoa wa ccm zilikuwa zikiendelea wakati wote wa sensa hata kufikia hatua ya kuhatarisha amani? (Kigwangala na Husein Bashe walifikia hatua ya kutishiana kwa risasi).

Kama Hiza anayafahamu haya yote lakini hakuyazungumzia anataka tuamini kuwa ana nia nzuri sana na amania ya nchi hii? Kama hawezi kuongelea pande zote zinazohusika (ccm na CHADEMA) anataka kuficha nini? Ni wazi tu kuwa huyu naye anacheza ngoma zile zile za ccm. Hana jipya. Sema ukweli ili uwe huru daima.
 
Back
Top Bottom