Feedback
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 7,988
- 4,507
Alikwambia anataka kujaribu udikteta kidogo kwa hii miaka mitatu aliyobakiza akinogewa anaongeza mingine mitano kama alivyofanya Museven lets get prepared.NDUGU ZANGU WATANZANIA, KATIBA SI MILIKI YA MTU AU TAASISI MOJA HATA KUKASHAWISHIKA KUHODHI UUNDWAJI WAKE: DALILI ZOTE HIZI ZA HAPA MWISHONI NI DHAHIRI IKULU KUNA TATIZO TENA ZITO SANA!!!
Watanzania enzangu,
tangu hii timua timua kiholela holela katika vyuo vikuu vyetu kote nchini, kamata kamata ya sauti pinzani kila mkoa na hivi sasa bambika bambika ya hizi kesi za kuchonga kuminya zaidi sauti huru kusikika na wananchi kudai uhuru wa kujitungia katiba, wazee wote tunatahadharisha hapa kwamba pale Magogoni kuna tatizo tena lisiloweza kupatiwa ufumbuzi kivile.
Kila mmoja anayeweza leo hii tunaamkia Mahakama ya Kisutu na ni huko huko ndiko kutakakokua huko! Kama Kisutu ndio karamuni wavujajasho tunakoshereheshwa kila tunapolilia HAKI nchini, hebu sasa twendeni karamuni tukasheherekee tangu asubuhi ya saa tatu vile.
Ndugu zetu Kibada na Mwigamba waonekana ni wahalifu hata kabla ya kesi kufunguliwa shauri tu ya kulilia katiba mpya; sote kote twendeni karamuni sasa!!