Waraka wa Kibanda kabla ya kufikishwa mahakamani

Status
Not open for further replies.
Alipokuwa anaongea na wale anaowaita wazee wa Dar alikuwa muwazi kwamba atakuwa dikteta,haya ni matokeo ya alichokisema na bado tujiandae kuona na kusikia mengi,uswahili na uongozi haviendani jamani
 
Pasco unasema Tanzania hamna waandishi wachumia tumbo? I mean are you serious au unaona members wa JF ni mazezeta? Ukiona mwandishi yoyote bongo yuko introuble ujue tayari amechanganya interest za tumbo lake, au tutajie waandishi wasafi bongo ni nani?

- Halafu wewe si muandishi pia je msafi?
Mkuu WJM, sijasema Tanzania hamna waandishi wachumia tumbo, nimesema waandishi wachumia tumbo wapo mpaka makanjanja wapo, ila sio waandishi wote wa Tanzania, ni wachumia tumbo, tunao baadhi ya waandishi wazuri, wasafi, wenye wito ambao sio wachumia tumbo!.

Hili la kuwaona members wa jf mazezeta limetokea wapi?.

Mwisho mimi ni Pasco wa jf, hapa jf tukisha jitambulisha kwa pen names tunaishia hapa, zaidi ya hapa ni name calling!.
 
Huyo anatumiwa na Chadema hana lolote. Hatupo tayari kuvumilia uchochezi wa aina yoyote ile.

kweli ww ni mzee na hakika umejizeekea, hvyo ninachoona ni kwamba unasubiri kulala pema peponi amina.
 
nilijua watu kama ndugu yangu Pasco,kina mzee mtashabikia tu jambo hili,lakini nisema tu kwamba afadhali Pasco nakujua sisemi sana kwa huyo anaejiita mzee,nakuuliza hivi msukuma mwenzangu:
  1. Tangu lini majeshi yanapokea amri kutoka kwa raia?Mwigamba na Kibanda ni raia wala si wanajeshi-JW,si polisi,si KMKM wala askari Magereza.
  2. Majeshi yote yanapokea amri kutoka kwa wakuu wao na hata kama vyeo mnalingana basi amri inatoka kwa alie senior kwa jina
  3. Lini Mwigamba na Kibanda wamepewa hata kuongoza section,platoon au hata kikosi
  4. Ni askari gani yuko tayari kupokea order kutoka kwa raia eti tu kwa sababu ni mwandishi?
  5. Kwa taarifa yenu mgomo jeshini hakuna na kuna sheria imo kwenye zile volume za Jeshi nazungumzia JW kugoma amri halali adhabu yake ni risasi,kama kuna anaebisha akasome zile volume zilizoko jeshini-JW.
  6. Leo ni vipi mwandishi awachochee askari ambao wao amri ni mpaka hata ukiwa mitaani nje ya kazi order ziko pale pale?
  7. Ni kwa vipi uchochezi wa mwandishi unaweza kupelekea askari kutokutekeleza kazi yake?wakati huyo anaesadikiwa kuwachohea hafungamani na jeshi lolote?japo alielekea lakini akashindwa.
  8. Na kama ni uchochezi kwanini hatuzifungii ama kuwakamata walimu walioko vyuoni na mashuleni ambao wanfanya uchochezi wa kifikra kwa wanafunzi?maana uchochezi wa kifikra ndo hatari zaidi,unamfanya mtu kujua kipi ni kipi na wapi haki haitendeki.
  9. Nadhani kuna haja ya kutafakari ni wapi raia anaweza kumchochea askari au kumshawishiaskari aka-obey order ya raia na akaacha ku-obey order ya kazini kwake kama alivyofundishwa,askari huchochewa askari wenyewe wala sio raia,hata ule mgomo wa JW enzi zile haukuchochewa na waandishi,ni wao kwa wao na ndicho kilichopelekea hata kubadili jina na kuitwa JW.Tutafakari hapa juu ya huu uchochezi kwa majeshi
 
Nimekumbuka ile katuni ya kenya ikionyesha waandishi wa kibongo wakilamba viatu vya JK.

Waandishi wa kibongo wakawa mbogo not knowing that was 'honey moon' and honey moons never last long
 
Hivi mnajua adhabu ya hayo mashtaka?....... life imprisonment.

Na hii sheria imepitishwa na wabunge ambao wengi wenu mnawaona kama miungu yenu i.e wanaharakati.

Kaangaleni hansards za bunge halafu muwaulize kwanini hawakupinga sheria hii?

Na muwaulize hao waandishi kwanini walikaa kimya wakati hii sheria inapitishwa?... 2002.

Ndio maana mnaitwa wachumia tumbo, kwani mada zenu hazitumiki kama check n' balance..... Media is the fourth branch of any government/modern society.
 
Mhariri mtendaji wa Tanzania daima bw.Absalom Kibanda ataripoti tena polisi keshn na ikiwezekana ataburuzwa mahakamani.Huu ni muendelezo wa kesi inayoitwa ya"Uchochezi" kufuatia ile makala ya Samsoni Mwigamba kwa jeshi la polisi.Ikiwa imebaki masaa machache kabla ya kuripoti polisi Kibanda ameandika yafuatayo kwenye ukurasa wake wa facebook:


"Kesho saa 3:00 asubuhi natarajia kuripoti Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam tayari kwa lolote, kubwa likiwa ni kuburuzwa kortini Kisutu kusomewa shitaka la uchochezi. Hatua hii inakuja siku tatu tangu niliposhikiliwa , nikahojiwa, nikatoa maelezo yangu na kisha nikawekewa dhamana na rafiki na mdogo wangu, Saed Kubenea.
Taarifa tulizozipata kutoka kwa viongozi waandamizi serikalini ambao wanatutakia mema zinaeleza kwamba limekuwapo shinikizo kubwa kutoka kwa wakuu wa dola la kutaka mimi ambaye ni Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima nifunguliwe mashitaka ya Jinai kama njia ya kujibu hasira za wakubwa dhidiyangu binafsi na dhidi ya gazeti la Tanzania Daima ninaloliongoza.
Habari kwamba nilikuwa miongoni mwa wahariri waliokuwa wamewekwa katika orodha ya kufikishwa mahakamani kwa makosa ya jinai na siyo ya madai kama ilivyo ada tulielezwa miezi kati ya mitatu na minne iliyopita. Taarifa hizi zilitolewa na mmoja wa mawaziri kwa mmoja wa wahariri ambaye ni rafiki yake mkubwa.
Baya katika uamuzi huu si kwamba anayeshitakiwa ni Absalom Kibanda, ambaye ni Mhariri wa Tanzania Daima na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri la hasha, bali ni uamuziwa hatari wa baadhi ya viongozi wa serikali ambao wameamua kuminya uhuru wa kikatiba wa watu kutoa maoni yao.
Uamuzi huu wa sasa wa kuanzakuwashitaki wahariri kwa makosa ya jinai yanatukumbusha maneno ya Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye aliyetabiri kwamba kiongozi anayesaka umaarufu na ikulu kwa njia ya vyombo vyahabari akiingia madarakani atalinda himaya yake kwa risasi.Ni wazi kwamba dhamira ya kupambana na watu wanaokukosoa wewe binafsi au serikali yako kwa njia ya kuwakomoa au kuwaumiza si tu ni udikteta unaofanana kimantiki na wa zama za Adolf Hitler bali unadhihirisha namna tulivyo na madikteta wanaofichwa na uhuru wa kidemokrasia waliokuta ungalipo hata kabla hawajaingia madarakani.
Hatua ya kulitumia Jeshi la Polisi kukandamizi uhuru wa habari kwa kuwakamata waandishi wamaoni kama walivyofanya kwa Samson Mwigamba wiki iliyopita na wahariri wa magazeti kama inavbyofanyika kwangu haina budi kupingwa kwa matamko na kwa njia nyingine za kudai haki iliyowekwa rehani.
Hakika kama taifa tupo njia panda. Nimeamua kwa dhati kulitumia tukio hili kama somo kwa madikteta wa Tanzania na wengine wa Bara la Afrika. Nimehamasishwa kujitoa mhanga kuleta mabadiliko ya kweli ya uhuru wa habari na wawatu kutoa maoni yao pasipo kuvunja sheria. Ukisoma makalaambayo imewapotezea polisi, mahakama, magereza na wapendwa wetu muda adhimu huwezi ukaamini kwamba tuna viongozi wanaofikiri sawasawa.
Ni hatari kuwa na kiongozi mkuu aliye tayari kuumiza watu wadogo kama sehemu ya kupumua au kupunguza hasira na machungu yake moyoni ambayo yamesababishwa na kupwaya kwake au kushindwa kwake mwenyewe. Ni aibu kuwa na viongozi dhaifu ambaokwao kuumiza wengine ndiyo kipimo cha nguvu za kikatiba walizopata tena kwa njia ya sanduku la kura. Kama kweli tunalitakia mema taifa hili hatuna budi kuanzisha mapambano makali ya kupigania uhuru ambao sasa umewekwa rehani. Wanahabari na wanahabari tunapaswa kujitoa mhanga kuyaongoza mapambano haya mapya".

Nguza na familia yake bado wako ndani kisa kimada ndio rais wako huyo. Anatumia madaraka aliopewa na wananchi, ndio Tanganyika. Tangulia tu ila yana mwisho hata wao ipo siku wataonja jela hata ipite miaka 50 hakutakuwepo tena na kinga kwa vile wao ni rais. NASEMA YANAMWISHO VUMILIA MUNGU YUPO NAWE.
 
Kwa nyongeza hasa kwa wale wanaoshabikia kukamatwa kwa waandishi eti ni wachochezi kutokana na makala iliyowalenga majeshi,itoshe tu kusema kwamba kazi ya jeshi ni kazi ambayo iko tofauti sana na kazi zingine kama watu wanavyotaka kusadikishwa kupita kukamatwa kwa waandishi hawa,To be honest hakuna askari anaeweza kuchochewa na raia na kisha asitekeleze majukumu yake,na ndio maana hata hawa polisi (FFU) inapotokea migomo mfano vyuoni wakifika pale wanasubiri amri kutoka kwa mkuu wao na ikishatoka wanaanza kuitekeleza,kama ni mabomu haya,kama ni maji ya kuwasha haya,kama ni risasi za moto zote sawa,ila ikumbukwe kwamba katika wale wanaotekeleza amri iliyotolewa huenda kuna wawili au hata zaidi wana watoto wao pale na wamo kwenye mgomo,lakini kwa kuwa ni amri ya kazi yake,naye hana means nyingine ya kupata kipato inabidi aitekeleze tu,mengine yatajulikana baadae,iweje leo mwandishi tu awashawishi kutokutekeleza amri kwa kutoa mawazo tu kwenye gazeti?kwa upande wa JW part one order ikishatoka hakuna raia anaeweza kuipinga na wanajeshi wote wanaitii,asiefanya hivyo ujue hataki kazi na mwisho wa siku ataondoka na wengine wataingia kazi hiyo hiyo maana unaposema kazi mbaya wengine wanasema wataipata vipi,jeshini hakuna request kule ni order na ndio maana hakuna hata shikamoo bila kujali umri leo raia (mwandishi) atengue au atoe order kisha watu wagome,jamani ya wa wapi hiyo?hapa kuna mengine wala sio la uchochezi,hakuna raia anaeweza kugomesha amri za kijeshi hata kama ni mzazi wako au mkeo au mwanao
 
Uchumia tumbo mnaosema ni sawa wapo pia,lakini hapa mi nadhani hoja ni kipi kimepelekea wakamatwe,wahojiwe,na kisha watafikishwa mahakamani,ni uchumia tumbo au uchochezi kwa majeshi?maana tunaanza kujadili kitu tofauti na msingi wa kosa lenyewe,au mimi ndo sielewi,basi mnifahamishe
 
Nimekumbuka ile katuni ya kenya ikionyesha waandishi wa kibongo wakilamba viatu vya JK.

Waandishi wa kibongo wakawa mbogo not knowing that was 'honey moon' and honey moons never last long
90cart01102006oo6.jpg
 
Mkuu WJM, sijasema Tanzania hamna waandishi wachumia tumbo, nimesema waandishi wachumia tumbo wapo mpaka makanjanja wapo, ila sio waandishi wote wa Tanzania, ni wachumia tumbo, tunao baadhi ya waandishi wazuri, wasafi, wenye wito ambao sio wachumia tumbo!.

Hili la kuwaona members wa jf mazezeta limetokea wapi?.

Mwisho mimi ni Pasco wa jf, hapa jf tukisha jitambulisha kwa pen names tunaishia hapa, zaidi ya hapa ni name calling!.
Lets hope you are not among of them.
90cart01102006oo6.jpg
 
Ukisoma alichoandika kibanda napata shida na Shaka kuamini Kama Mtu mzima kweli anaweza andika haya aliyoyaandika. Nilivyoelewa mimi ni kwamba kama amepatwa na uwoga vile au alikuwa hajuinkuwa muandishi kuandika,wananchi kusoma na vyombo vya usalama,kuuliza kama wanaona yaliyoandikwa yanahatarisha usalama wa nchi au yanachochea mambo fulani.

Kwanza kibanda angetuambia Ndani ya baraza hili Kama ni kweli kuwa ni yeye na gazeti lake ndiyo Walioandika haya. Maaana sina hakika Kama Jakaya na wenzake walimtuma akayaandike haya na baadae walimkataa katika Yale anayoyaita kuwa Watu wanatumia wamemfix. Au a nataka kutumia kuwa ndiyo mkuki umerudi kwa binaadamu.

Sidhani pia Kama kuna uhuru usio na mipaka.nifikiriavyo huu uhuru wa vyombo vya ulinzi na usalama kumuuliza Mtu yeyote na mahakamani ndiyo haki itakako patikana ndugu yangu na si katika mtazamo we kukandamiza uhuru wa vyombo via habari Kama ambavyo ndugu yangu Huyu anajaribu kuiambia dunia.nazungumza hili kwa kuwa umekuwa ni utamaduni sasa kwa vyombo vya habari kuzusha na kuandika mambo ya ajabu au habari za uzushi kwenye magazeti bila hata ya kuwa na uhakika wa habari hizo ,eti yote hayo ni katika yale wanayoyaita uhuru wa kutoa habari au maoni.maoni ya Namna gani haya ambavyo Ndani yake hayana hata chembe ya uzalendo,utu na uhalisia.nijuavyo mie ni kwamba kwa waandishi makini lazima ingefanyika research ya maana Sana kabl hamjaandika jambo au haya maoni Kama ambavyo anatuambia kibanda.haiwezi ikawa ndiyo jamii hii ambapo kila Mtu atandika tafsiri yake katika tukio Fulani ambavyo yeye kwa upande wake au kwa upande wake kisiasa au kihisia anaconda ndivyo ilivyo.

Tatizo ni kwamba wamezoea kuona mambo yakiharibika kwa upande mmoja na raha ikija kwa upande mwengine na sasa anatafuta sababu katika mwamvuli wa kukandamizwa kwa demokrasia wakijidai kuwa Watu wanatafuta umaarufu. Ahahah kaka kibanda toa wasi na yoga,ni utaratibu wa kawaida Sana kwa jeshi la polish au chombo cha usalama kumuuliza Mtu na pale linapoona kuwa kuna nia ya kufanya kesi basi watapeleka katika vyombo husika. Kama hivi ndiyo utaratibu, wapi ukandamizwaje wa uhuru.kama polisi hawakukuita na kumuuliza maws ali Yao hiyo Hali itapatikana vp Kamanda au umesahau Kazi za mahakama au umesahau zipo wapi? Billicanas.

Pamoja na hili Mbona mwenzake alipoitwa kuhojiwa na polish ali toa ushirikiano na hakulalamika.hebu angalia alivyo pews Chumba hotelini na Kesha yake asubuhi baada ya mahonia no akapelekwa mahakamani Kama haya kosa mdhamini na outings jela.nini wasi wasi wako kwani inamaana haujui kuwa hapo polish ni kuandika maelezo na kushirkiana naomkujua au kupelekwa sababu za Msingi zilipelekea wewe kuandika article.Huu umekuwa ni utaratibu we kawaida. Haya Sasa SWAZI langu, bwana kibanda alitaka polisi wafanye nini na huyu anayemsema kuwa alitafutanumaarufu kwa magazeti na sasa anatumia dola kulinda mamlaka yake alitaka afanyaje?

Nionavyo Mimi, vyombo vinatimiza wajibu wake. Iwe wewe Mimi au Yule, nifikiriavyo ukikosea jambo au pale vyombo vinapoona kuwa hili lililotendeka si jambo la kawaida ni wajibu wao kutumia na kumuuliza Mtu yeyote na Kama adhabu itatolewa na mahakama. kwa kufanya hivi muandishi mkongwe kibanda unataka nini Kama sio Kuwa unajitoa akili Angaki unajua kuwa polisi agungwi Mtu kwa upande mmoja na pili kwamba kazi yako ilikwisha baada ya makala kutoa na watu kununua kwa wingi na baadae kuingia mtaani na kuona kwamba ulichoandika ni taarifa sahihi,huku vyombo vikisoma na kuangalia uzuri aw maneno yako ambayo Leo katika maandishi yako,unasema yalikuwa maoni.

Pole brother, umetimiza wajibu wako kama muandishi,umeweza.
Polisi wamekuita ili watimize wajibu wao,toa ushirikiano hakuna ugomvi
Wananchi tutaliongea na matarajio yetu Kama utajibu Maswali ya wahusika vizuri na sio kutumia forum zenu kulalamika.

Pole Sana MPIGANAJI, kaza moyo mapambano yanaendeleaje,waache wafanyaje kasi Yao Acha uwoga. Fanya kama upo chumba cha habari billicanas pale.
 
NDUGU ZANGU WATANZANIA, KATIBA SI MILIKI YA MTU AU TAASISI MOJA HATA KUKASHAWISHIKA KUHODHI UUNDWAJI WAKE: DALILI ZOTE HIZI ZA HAPA MWISHONI NI DHAHIRI IKULU KUNA TATIZO TENA ZITO SANA!!!

Watanzania enzangu,

tangu hii timua timua kiholela holela katika vyuo vikuu vyetu kote nchini, kamata kamata ya sauti pinzani kila mkoa na hivi sasa bambika bambika ya hizi kesi za kuchonga kuminya zaidi sauti huru kusikika na wananchi kudai uhuru wa kujitungia katiba, wazee wote tunatahadharisha hapa kwamba pale Magogoni kuna tatizo tena lisiloweza kupatiwa ufumbuzi kivile.

Kila mmoja anayeweza leo hii tunaamkia Mahakama ya Kisutu na ni huko huko ndiko kutakakokua huko! Kama Kisutu ndio karamuni wavujajasho tunakoshereheshwa kila tunapolilia HAKI nchini, hebu sasa twendeni karamuni tukasheherekee tangu asubuhi ya saa tatu vile.

Ndugu zetu Kibada na Mwigamba waonekana ni wahalifu hata kabla ya kesi kufunguliwa shauri tu ya kulilia katiba mpya; sote kote twendeni karamuni sasa!!
 
Vita dhidi ya fikra ni vita ambavyo ni vigumu sana kuvishinda na hasa pale jambo lenyewe linapogusia haki ya wengi!!!!!!
 
I can't believe kama hii ni post yako ya 3 toka 2006 lazima kuna kitu in common..

MREKEBISHARIKA
Junior Member
Join Date : 4th December 2006
Posts : 3
Rep Power : 0
 
Ukisoma alichoandika kibanda napata shida na Shaka kuamini Kama Mtu mzima kweli anaweza andika haya aliyoyaandika. Nilivyoelewa mimi ni kwamba kama amepatwa na uwoga vile au alikuwa hajuinkuwa muandishi kuandika,wananchi kusoma na vyombo vya usalama,kuuliza kama wanaona yaliyoandikwa yanahatarisha usalama wa nchi au yanachochea mambo fulani.

Kwanza kibanda angetuambia Ndani ya baraza hili Kama ni kweli kuwa ni yeye na gazeti lake ndiyo Walioandika haya. Maaana sina hakika Kama Jakaya na wenzake walimtuma akayaandike haya na baadae walimkataa katika Yale anayoyaita kuwa Watu wanatumia wamemfix. Au a nataka kutumia kuwa ndiyo mkuki umerudi kwa binaadamu.

Sidhani pia Kama kuna uhuru usio na mipaka.nifikiriavyo huu uhuru wa vyombo vya ulinzi na usalama kumuuliza Mtu yeyote na mahakamani ndiyo haki itakako patikana ndugu yangu na si katika mtazamo we kukandamiza uhuru wa vyombo via habari Kama ambavyo ndugu yangu Huyu anajaribu kuiambia dunia.nazungumza hili kwa kuwa umekuwa ni utamaduni sasa kwa vyombo vya habari kuzusha na kuandika mambo ya ajabu au habari za uzushi kwenye magazeti bila hata ya kuwa na uhakika wa habari hizo ,eti yote hayo ni katika yale wanayoyaita uhuru wa kutoa habari au maoni.maoni ya Namna gani haya ambavyo Ndani yake hayana hata chembe ya uzalendo,utu na uhalisia.nijuavyo mie ni kwamba kwa waandishi makini lazima ingefanyika research ya maana Sana kabl hamjaandika jambo au haya maoni Kama ambavyo anatuambia kibanda.haiwezi ikawa ndiyo jamii hii ambapo kila Mtu atandika tafsiri yake katika tukio Fulani ambavyo yeye kwa upande wake au kwa upande wake kisiasa au kihisia anaconda ndivyo ilivyo.

Tatizo ni kwamba wamezoea kuona mambo yakiharibika kwa upande mmoja na raha ikija kwa upande mwengine na sasa anatafuta sababu katika mwamvuli wa kukandamizwa kwa demokrasia wakijidai kuwa Watu wanatafuta umaarufu. Ahahah kaka kibanda toa wasi na yoga,ni utaratibu wa kawaida Sana kwa jeshi la polish au chombo cha usalama kumuuliza Mtu na pale linapoona kuwa kuna nia ya kufanya kesi basi watapeleka katika vyombo husika. Kama hivi ndiyo utaratibu, wapi ukandamizwaje wa uhuru.kama polisi hawakukuita na kumuuliza maws ali Yao hiyo Hali itapatikana vp Kamanda au umesahau Kazi za mahakama au umesahau zipo wapi? Billicanas.

Pamoja na hili Mbona mwenzake alipoitwa kuhojiwa na polish ali toa ushirikiano na hakulalamika.hebu angalia alivyo pews Chumba hotelini na Kesha yake asubuhi baada ya mahonia no akapelekwa mahakamani Kama haya kosa mdhamini na outings jela.nini wasi wasi wako kwani inamaana haujui kuwa hapo polish ni kuandika maelezo na kushirkiana naomkujua au kupelekwa sababu za Msingi zilipelekea wewe kuandika article.Huu umekuwa ni utaratibu we kawaida. Haya Sasa SWAZI langu, bwana kibanda alitaka polisi wafanye nini na huyu anayemsema kuwa alitafutanumaarufu kwa magazeti na sasa anatumia dola kulinda mamlaka yake alitaka afanyaje?

Nionavyo Mimi, vyombo vinatimiza wajibu wake. Iwe wewe Mimi au Yule, nifikiriavyo ukikosea jambo au pale vyombo vinapoona kuwa hili lililotendeka si jambo la kawaida ni wajibu wao kutumia na kumuuliza Mtu yeyote na Kama adhabu itatolewa na mahakama. kwa kufanya hivi muandishi mkongwe kibanda unataka nini Kama sio Kuwa unajitoa akili Angaki unajua kuwa polisi agungwi Mtu kwa upande mmoja na pili kwamba kazi yako ilikwisha baada ya makala kutoa na watu kununua kwa wingi na baadae kuingia mtaani na kuona kwamba ulichoandika ni taarifa sahihi,huku vyombo vikisoma na kuangalia uzuri aw maneno yako ambayo Leo katika maandishi yako,unasema yalikuwa maoni.

Pole brother, umetimiza wajibu wako kama muandishi,umeweza.
Polisi wamekuita ili watimize wajibu wao,toa ushirikiano hakuna ugomvi
Wananchi tutaliongea na matarajio yetu Kama utajibu Maswali ya wahusika vizuri na sio kutumia forum zenu kulalamika.
Pole Sana MPIGANAJI, kaza moyo mapambano
yanaendeleaje,waache wafanyaje kasi Yao Acha uwoga. Fanya kama upo chumba cha habari billicanas pale.[/QUIOTE]



Inaonyesha ni jinsi gani usivokuwa makini. Bila shaka utakuwa mbwa mmoja wa TISS waliogeuzwa sasa mbwa wa viongozi na kuchumia tumbo. Sasa kama hujui kama habari iliandikwa kwenye gazeti la Absalom unajuaje habari yenyewe na kuiandikia maneno marefu yasiyokuwa na chembe ya umakini?
Ukweli ni kuwa huo ni ukandamizaji wa uhuru wa habari. Mwandishi mwigamba aliwaandikia maaskari kwa kuwarudisha kwenye mstari walipo wananchi badala kuwa kama mbwa anayetupiwa nyama na viongozi na kusahau kuwa wanapaswa kuwatumikia wananchi si kutumikia amri za kukandamiza haki zinazotolewa na viongozi walioshindwa wajibu wao. Kama wewe ni mmoja wa viongozi hao unafaidika na ufirauni wa viongozi wetu ujue sisi wananchi tuko nyuma ya watu kama Absalom na Mwigamba. Mnachokifanya ni kuwa mnatumia dola kukandamiza sauti ya wanyonge inayopazwa na kina Absalom ila amini usiamini ipo cku kama sio sisi basi watoto wetu watashindwa kuvumilia na kuwatia bunduki matakoni kama Ghadafi. Salama yenu ni pale tu mtakapo acha kubughudhi sauti ya umma na kuvitungia kesi sizo na kichwa kama hizo za kina Absalom na kuacha wananchi waamue hatima
yao.
Hiyo mipaka ya uhuru ni wapi? Kutogusa maovu ya viongozi? Kutowaambia maaskari wasiwapige wananchi wanaoandamana kwa amani badake wawaunge mkono? Kaandika kitu kinachoaribu amani ya nchi au kuhatarisha usalama? La hasha! Kaandika makala inayotishia usalama wa viongozi wabovu. Ni ujumbe mahsusi wa kizalendo. Vipi Pinda na bibi Kiroboto wa Bungeni walioandikiwa posho ya laki2.8 na Jairo kuwahonga? Nani alistahili kuwa wa kwanza mahakamani? Vipi kuhusu Ngeleja na Naibu wake wanaojilipa posho ya Mil4 kwa siku? Hawakustahili kuitwa polisi na kuhojiwa? Uovu wa nchi ulikofika ni hatua ya mwisho kwa tawala dhalimu iliyopo kuachia ngazi. INA MISUKOSUKO KAMA ILIVOANZA SASA, waandamanaji kupigwa risasi, wanafunzi kufukuzwa chuo kwasabu ya siasa, kuwafungilia watu kesi za kichochezi na uhaini ila uzuri hapo ndipo inapoishilia. Mola akurehemu uyashuhudie hayo machungu kwa wezi na waharibu nchi CCM.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom