Waraka wa Hamani

Hakuna sababu za kuogopa jumuiya ya afrika ya mashariki kwa ujumla mimi nimesoma Kenya kwa kipindi kirefu nimefanya kazi kule kidogo na mpaka sasa hivi nina ushirikiano na watu wengi wa huko , hakuna sababu ya kuogopa kufanya nao kazi au chochote tunaweza kushindana kwa lolote endapo tunaamua kwa dhati kwa mtu mmoja mmoja au wote kwa ujumla tuache unafiki na wivu usio na mipango
 
Pana makala ya Boaz Boaz iliyoainisha kwa kina namna Watanzania wenye inferiority complex wanavyoamua kuunga mkono EAC kama njia mojawapo ya kuonyesha wao "sio waoga", kisha "wamesoma". Kana kwamba haitoshi, watu hao wenye kutaka kujithibitisha walivyo 'wamekucha' huwaita "waoga" Watanzania wenzao wote wanaokataa EAC.

Kwa kawaida hawana uwezo, au kwa sababu nyingine, hawawezi kuchangia mada inayozungumzwa.

Watu hawa ni wa kupuuzwa.

Hoja ipo palepale, Waraka Hamani umesainiwa, Watanzania tufanyeje kuinusuru nchi yetu?
 
Hakuna sababu za kuogopa jumuiya ya afrika ya mashariki kwa ujumla mimi nimesoma Kenya kwa kipindi kirefu nimefanya kazi kule kidogo na mpaka sasa hivi nina ushirikiano na watu wengi wa huko , hakuna sababu ya kuogopa kufanya nao kazi au chochote tunaweza kushindana kwa lolote endapo tunaamua kwa dhati kwa mtu mmoja mmoja au wote kwa ujumla tuache unafiki na wivu usio na mipango

Yap, hakuna sababu ya kuwaogopa, pamoja na kwamba, hata tukiingia kwenye jumuiya ya africa mashariki, bado tunatakiwa kuwa watanzania, si waafrica mashariki.

Cha muhimu ni kujiunga na hawa jamaa ni mambo ya uchumi peke yake, kwa habari ya mambo mengine yote, hatuko pamoja na mioyo yao huwa iko negative against us, so we better be careful katika ushirikiano. a

Another fact ni kwamba, kitendo cha wao kujiona wana akili kuliko sisi hata katika ordinary things mtaani tu, ni cha kuogopa, wengi mliokaa Kenya, tunajua kuwa wengi wa wakenya wana myth kuamini kuwa watz hawana akili, na ni wajinga kishule. Hii huwa ni impression utakayoikuta wakati wowote hata katika ushirikiano mbalimbali.

Napenda sana East African Communtiy, lakini sipendi kutukanwa, sipendi kudharauliwa, sipendi ku be taken advantage, sipendi mtu aamini kuwa siwezi. Kama tutaungana kwa kuheshimiana sisi kwa sisi basi hapo hamna shida.
 
Pana makala ya Boaz Boaz iliyoainisha kwa kina namna Watanzania wenye inferiority complex wanavyoamua kuunga mkono EAC kama njia mojawapo ya kuonyesha wao "sio waoga", kisha "wamesoma". Kana kwamba haitoshi, watu hao wenye kutaka kujithibitisha walivyo 'wamekucha' huwaita "waoga" Watanzania wenzao wote wanaokataa EAC.

Kwa kawaida hawana uwezo, au kwa sababu nyingine, hawawezi kuchangia mada inayozungumzwa.

Watu hawa ni wa kupuuzwa.

Hoja ipo palepale, Waraka Hamani umesainiwa, Watanzania tufanyeje kuinusuru nchi yetu?

Things fall apart
 
Makala ya Boaz Boazi hii hapa!

Nukuu (mkolezo wa wino umeongezwa):

"Hata Watanzania wanaounga mkono shirikisho wamekuwa wakiwaeleza Watanzania wenzao wanaopinga shirikisho kuwa ni watu waoga au watu wasiojiamini.

Lakini kwa mtazamo wangu, katika Tanzania naona suala la kutojiamini lipo hasa kwa wasomi wanaounga mkono shirikisho."


"Kuna kundi la wasomi wameamua kuunga mkono shirikisho au kunyamaza kabisa kwa sababu inadaiwa hawataki waonekane wao ni duni, waoga na hawajiamini mbele ya wasomi wenzao wa Uganda na Kenya, ambao wako mstari wa mbele kuunga mkono shirikisho."

"Kwa hiyo njia ya haraka ya kujipambanua kuwa wewe ni msomi unayejiamini na si mwoga wa ushindani na huna hofu ya eti ya kunyang’anywa kazi na Wakenya au Waganda ni kuunga mkono shirikisho hilo. "
 
Mikataba ya EAC imeshasainiwa na inaendelea kusainiwa kwa kasi mpya.

"Waraka wa Hamani" ushasainiwa.

Jamani, lipi la ziada tunaloweza kulifanya kuliokoa taifa letu dhidi ya maangamizi?

Mlenge

Wewe unataka nini?

a) Tuvunje muungano kwa sababu sio waoga!
b) Tuweke ulinzi wa sungusungu Wakenya wasije iba rasilimali zetu?
c) a na b yote sahihi
Chagua jibu sahihi
 
Wewe unataka nini? [/SIZE]
a) Tuvunje muungano kwa sababu sio waoga!
b) Tuweke ulinzi wa sungusungu Wakenya wasije iba rasilimali zetu?
c) a na b yote sahihi
Chagua jibu sahihi

Tatizo nafikiri ninyi mnafikilia kwamba wakenya watakuja kuchukua mali ama watatu piku ktk ajira lakini sivyo.

Wewe utafanye je biashara na adui yako?? na hata hivyo utaungana vipi na jamaa ambaye kwake instability ndo mwake?? sio kenya tu Tanzania nchi inazoungana nazo zote zina historia nzuri sana ktk vita na wala sio historia ni kitu inayoendelea
 
mkuu ,Mlenge naomba msaada,naona umeniacha kidogo
Waraka wa Hamani" ushasainiwa...,kilichojiri kwenye waraka huo ni kipi?na kwa nini ukaitwa waraka wa hamani?
naomba ufafanuzi kidogo,samahani kwa usumbufu
 
Bawa Mwamba,

Waraka wa Hamani uliandikwa huko Uajemi ili kuwaangamiza watu wote wa taifa fulani waliokuwako Uajemi.

Mwenye kuuandika alikuwa anaitwa Hamani.

Mara baada ya waraka kuandikwa kwa huo Waraka wa Hamani, waliotakiwa kuangamizwa waliamua kuchukua hatua.

Sasa hivi Tanzania imeridhia na kusaini mikataba inayosema Tanzania ambayo ilikuwa mali yetu peke yetu watu milioni 40, sasa hivi itakuwa pia ni mali ya watu wengine milioni mia moja.

Watu hao hawaamini kwamba Watanzania ni binadamu wenye stahili ya kuishi au kuwa na maisha, kujipatia riziki, na kadhalika.

Wanaamini kwamba Watanzania ni wajinga, mazuzu, wavivu na ambao hawafai kuwepo duniani hapa. Imani yao inapata ushahidi kwa vile ambavyo Bunge letu, Rais wetu pamoja na Serikali, siyo tu vinaridhia mikataba ya kuachia madaraka waliyokuwa nayo, bali pia wanaigawa nchi kana kwamba hatuwezi kujitawala wenyewe.

Imebaki miezi miwili ili ile siku ya 'maangamizi' itimie.

Je, pana tunaloweza kulifanya, zaidi ya kuchapa masikitiko na mshangao wetu mtandaoni?

Mlenge
 
Mikataba ya EAC imeshasainiwa na inaendelea kusainiwa kwa kasi mpya.

"Waraka wa Hamani" ushasainiwa.

Jamani, lipi la ziada tunaloweza kulifanya kuliokoa taifa letu dhidi ya maangamizi?

Mlenge

Kuna watu wajinga wamekalia ati Watanzania ni waoga huo uoga umeanza lini? Tanzania ni taifa kubwa la kuheshimika limewang'oa masultani na wakoloni itakuwa hawa manyang'au. Kikwete sio kiongozi ni mzuka tu wakati wake utapita kama vumbi na huu unaoangaliwa kama protocal etc itakufa kifo cha mende, tumeona mengi itakuwa hii ya kuja kujitwalia rasilimali ambazo sio zao? Viongozi wengi hawana uhakika na waliyotenda kwa nchi zao ndio sababu ya kukurupuka na kufikiri watajificha kwenye jumuiya tutawasaka kama panya ili waje wajibu ubaradhuli wao.
 
Wacha1,

I can understand your pain. But please refrain from using the N* word.

It is not justified under any circumstances to use that word.

I can tell you, there are no people who are born evil. This fight is not against group of people of other countries. It is to preserve our country for ourselves, the citizens of the country.

It is not against Kenyans, Rwandese, Ugandans or Burundians.

If our leaders come back to their senses and withdraw Tanzania from EAC, we Tanzania will not be enemy country to those our good neighbors.

I know evil Tanzanians beyond measure. I know good-hearted Kenyans, Rwandese, Ugandans, and Burundians.

Again, this got nothing to do with unjust generalization like use of N* word.

I know Wacha1 you are better than that.

Now let's go on to protect our beloved country.

Let us not give the enemy of our cause a 'red-herring' to divert the real issue at stake here.

Regards,

Mlenge
 
Mlenge acha uoga na mawazo finyu siku zote muungano ni nguvu , usilete propaganda ambazo hutoweza kuzitetea siku moja. Nadhani kama una mambo yako binafsi ya wakenya basi weka wazi lakini waache watanzania wazalendo waungane na wao katika kujiletea maendeleo na kutetea maslahi yao eneo zima la Afrika haswa hili la Afrika ya Mashariki.

Huko nyuma nchi yetu imewahi kuwa mkombozi wa mataifa mengi sana Afrika karibu yote lakini ona sasa tulivyo kisa ni kama hivi uoga uoga, kutokujiamini na propaganda zingine kama hizo zako hapo juu .

Mimi nasema hatuna sababu ya kuachia nafasi hii lazima tujiunge kwenye ushindani, lazima tuendeleze nchi zote kwa ujumla, lazima Afrika ya Mmashariki ing'ae, kama ilivyo Jumuiya ya Maendeleo ya Afrika ya Magharibi na sehemu nyingine zilizokubaliana kuungana.

Amani mie nimesoma Kenya kwa muda mrefu sana tu na sasa hivi niko njiani naelekea huko huko pamoja na Juba ntarudi Jumapili.
 
Back
Top Bottom