Waraka unaodaiwa wa Wabunge wa CCM kumpinga SIOI wasambaa Arumeru

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
Waraka wasambazwa

Watu wasiojulikana jana walisambazwa waraka ambao unadaiwa kuandikwa na wabunge wa CCM ambao wanapiga vita ufisadi wakitaka mgombea wa CCM, Sioi Sumari asichaguliwe kwani atawaongezea nguvu mafisadi kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Waraka huo ambao jana ulikuwa ukisambazwa katika mitaa mbalimbali ya Usa River na kwenye mikutano ya kampeni ya Chadema na CCM, una kichwa cha habari kisemacho "Chama cha Mapinduzi na Kamati maalum dhidi ya ufisadi."

Katika waraka huo ambao haujasainiwa na mtu yeyote unadaiwa kutumwa kwa wananchi wa Meru na wabunge wa CCM ambao picha zao zimeambatanishwa.

"Tunawaandikia waraka huu kwa kuwa tunaamini kabisa kwa kufanya hivyo tunamfurahisha Mungu na kuwanusuru na kiu ya damu ya baadhi ya viongozi wa nchi hii. Mafisadi hawa wameshindwa kabisa kuacha ufisadi na sasa wanatumia fedha walizowaibia Watanzania…" inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Kadhalika waraka huo unamtaja mmoja wa makada wakongwe wa CCM (jina tunalihifadhi) kwamba ameamua kutunisha misuli yake na kuhakikisha Sioi anashinda ubunge Arumeru, lengo likiwa ni kuonyesha kwamba ana nguvu zaidi kwa kutumia fedha zake.

Chadema jana walikana kuufahamu waraka huo na kusema kuwa wenye uzoefu wa kuandika nyaraka za aina hiyo ni CCM.

Mkuu wa operesheni wa uchaguzi huo wa Chadema, John Mrema alisema: "Sisi hatuwezi kuandaa waraka kama huu, haya ni mambo ya CCM wenyewe."

Meneja Kampeni wa CCM, Mwigulu Nchemba hakupatikana jana kuzungumzia waraka huo.


Source: Mwananchi.
 
Haingii akilini CCM waandike waraka huo wasiweke saini zao lakini waweke picha zao maana yake nini sasa? Hata mtoto mdogo lazima ajue kuwa hiyo ni njama na mwendelezo wa sisa za maji taka.
 
Haingii akilini CCM waandike waraka huo wasiweke saini zao lakini waweke picha zao maana yake nini sasa? Hata mtoto mdogo lazima ajue kuwa hiyo ni njama na mwendelezo wa sisa za maji taka.
Safari hii CCM imekuwa kwenye defenseve position mnakana kila kitu, kwa hiyo na ule waraka waliosambaza CCM kuwa CDM wamesema tayari wameshindwa nao ni wa uongo au ule ni kweli?
 
haya mashambulizi si ya kitoto, bado kidali po!!!!! hawatoki magamba this time.
 
Waraka huu ni dalili ya mfa maji, haachi kutapatapa, hata akiona chelewa, ataikimbilia kuidandia akijiaminisha inaweza kumuokoa!.
 
Waraka wasambazwa

Watu wasiojulikana jana walisambazwa waraka ambao unadaiwa kuandikwa na wabunge wa CCM ambao wanapiga vita ufisadi wakitaka mgombea wa CCM, Sioi Sumari asichaguliwe kwani atawaongezea nguvu mafisadi kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Waraka huo ambao jana ulikuwa ukisambazwa katika mitaa mbalimbali ya Usa River na kwenye mikutano ya kampeni ya Chadema na CCM, una kichwa cha habari kisemacho “Chama cha Mapinduzi na Kamati maalum dhidi ya ufisadi.”

Katika waraka huo ambao haujasainiwa na mtu yeyote unadaiwa kutumwa kwa wananchi wa Meru na wabunge wa CCM ambao picha zao zimeambatanishwa.

“Tunawaandikia waraka huu kwa kuwa tunaamini kabisa kwa kufanya hivyo tunamfurahisha Mungu na kuwanusuru na kiu ya damu ya baadhi ya viongozi wa nchi hii. Mafisadi hawa wameshindwa kabisa kuacha ufisadi na sasa wanatumia fedha walizowaibia Watanzania…” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Kadhalika waraka huo unamtaja mmoja wa makada wakongwe wa CCM (jina tunalihifadhi) kwamba ameamua kutunisha misuli yake na kuhakikisha Sioi anashinda ubunge Arumeru, lengo likiwa ni kuonyesha kwamba ana nguvu zaidi kwa kutumia fedha zake.

Chadema jana walikana kuufahamu waraka huo na kusema kuwa wenye uzoefu wa kuandika nyaraka za aina hiyo ni CCM.

Mkuu wa operesheni wa uchaguzi huo wa Chadema, John Mrema alisema: “Sisi hatuwezi kuandaa waraka kama huu, haya ni mambo ya CCM wenyewe.”

Meneja Kampeni wa CCM, Mwigulu Nchemba hakupatikana jana kuzungumzia waraka huo.

Source: Mwananchi.

Mosha huoshwa!
 
Haingii akilini CCM waandike waraka huo wasiweke saini zao lakini waweke picha zao maana yake nini sasa? Hata mtoto mdogo lazima ajue kuwa hiyo ni njama na mwendelezo wa sisa za maji taka.

Mkuki kwa nguruwe.............
 
Waraka huu ni dalili ya mfa maji, haachi kutapatapa, hata akiona chelewa, ataikimbilia kuidandia akijiaminisha inaweza kumuokoa!.
Pasco be specific nani mfamaji umesahau ulisema uchaguzi ulishakwisha Sioi anasubiri kuapishwa, mbona unaanza kuchanganya habari.
 
Pasco be specific nani mfamaji umesahau ulisema uchaguzi ulishakwisha Sioi anasubiri kuapishwa, mbona unaanza kuchanganya habari.
Mkuu Feedback niko pale pale niliposimama na msimamo ni ule ule, huyo mfa maji ni aliyeandika waraka ili uonekane ni wa CCM!.
 
yawezekana ni kweli umeandikwa na ccm kwani (1.) wana CCM wengi hawakumtaka siyoi, (2.) hata kampeni wanazopiga ni za kijinga na matusi hazionyeshi nia ya dhati ya kumsaidia siyoi ashinde.
 
yawezekana ni kweli umeandikwa na ccm kwani (1.) wana CCM wengi hawakumtaka siyoi, (2.) hata kampeni wanazopiga ni za kijinga na matusi hazionyeshi nia ya dhati ya kumsaidia siyoi ashinde.
Mkuu Angel Msoffe, kwani wanaochagua ni CCM au ni watu wa Arumeru?, kama uchaguzi wa mwaka 2010, mgombea fulani alishindana na mgombea wa CCM aliyekuwa hoi kitandani, CCM iukashinda!, what chances does does he stand kushinda, mgombea huyo huyo kishindana na mgombea ambaye yuko fit!. Kama umefanya experiment kwa kutumia the same reagents na the same conditions, usitegemee kuypata matokeo tofauti!. Sio hata angekuwa anasimama tuu na kusema, "jamani nipeni pole tuu kwa kufiwa na baba", bado anashinda kwa symphatetic votes!.
 
Mkuu Angel Msoffe, kwani wanaochagua ni CCM au ni watu wa Arumeru?, kama uchaguzi wa mwaka 2010, mgombea fulani alishindana na mgombea wa CCM aliyekuwa hoi kitandani, CCM iukashinda!, what chances does does he stand kushinda, mgombea huyo huyo kishindana na mgombea ambaye yuko fit!. Kama umefanya experiment kwa kutumia the same reagents na the same conditions, usitegemee kuypata matokeo tofauti!. Sio hata angekuwa anasimama tuu na kusema, "jamani nipeni pole tuu kwa kufiwa na baba", bado anashinda kwa symphatetic votes!.
Pasco, 2010 was then this is now, na Sumari sr alikuwa mwanasiasa Sioi si mwanasiasa kalazimishwa zione hizo tofauti. Kitu kingine ambacho hutaki kukiona ni kuwa Chadema ile si hii ya leo na CCM ile si hii ya waraka. Another think in mind 2010 Nassari alipigana peke yake na Lowassa hadi kupata >19,000 votes ambapo hakuwa hata na gari leo ana support ya timu nzima ya CDM can't you see the difference?
 
Kama ushindi ni makundi ya watu, au kubwebwa juu juu, basi Lyatonga angeshinda ile 1995!. Laiti huo umati ungewa ni umati wa wapiga kura!.

Angalizo: Msije kunifikiria mimi ndio naishabikia CCM ishinde, au namshabikia Sioi, no!, mimi nasimama kwenye ukweli, hata ukiwa ni mchungu kiasi gani, ukweli utabaki kuwa ni ukweli na ndio utakao simama!.

Endeleeni kujifariji na umati wa watu kwenye kampeni, mimi nilishuhudia haya kwa macho yangu kule Busanda na Biharamulo!. Sasa subirini matokeo Arumeru ndipo tutaeleweshana vizuri!.
No, tunaongea na facts, hata hivyo kuwa na washabiki wengi nayo ni factor mojawapo ya ushindi, washabiki wengi wana motivate undecided voters kukipenda chama, hizi ni kampeni za wazi kwa hiyo huwezi kuniambia uitishe mkutano wakusanyike watu 10 halafu useme chama kitashinda kwanza hata hao 10 si wote watakaokupigia kura.
 
Haingii akilini CCM waandike waraka huo wasiweke saini zao lakini waweke picha zao maana yake nini sasa? Hata mtoto mdogo lazima ajue kuwa hiyo ni njama na mwendelezo wa sisa za maji taka.
Ile picha maji marefu aliyopiga na Nassary inaingia akilini?
 
una taarifa za arumeru mashariki?
Jackbauer, sio taarifa za Arumeru, uchaguzi ulishafanyika kitambona matokeo ya Arumeru yalishatoka na nilishayatangaza huko nyuma. Kinachoendelea sasa ni kutimizwa tuu kwa matakwa ya sheria, taratibu na kanuni!.
 
Back
Top Bottom