Waraka wa waislam, tumeyataka wenyewe na tujiandae kwa vurugu hizi. Maaskofu, hawakuangalia mbali kuona wanaanzisha vurugu kubwa. Kila dhehebu likitoa waraka na mwongozo wa namna ya kufanya uchaguzi, hatuwezi kufika! Ni wazi utakuja na waraka wa wapagani, waraka wacommunist nk.
Hizi ni dalili tosha kuonyesha kwamba Hekima na busara zimekwenda likizo. Dini zikianzisha vurugu, haina mwisho. Bahati mbaya au nzuri, waumini wa Afrika wanaamini kiushabiki. Labda ni umaskini wa mali na fikra. Hivyo tutachinjana wenyewe kwa wenyewe kulinda waraka kutoka kwa viongozi wetu wa dini.
Katika mambo ya siasa, hakuna haja ya kuwa na waraka kutoka madhehebu mbali mbali. Mwongozo wa kuchagua viongozi utolewe na serikali. Dini zinaweza kusaidia kwa kuhakikisha watanzania wana roho ya Kimungu.
Ni lazima tuwe makini kabisa, vinginevyo tunaweza kuwa kama Somalia na nchi nyingine za Afrika zinazopigana vita ya kudumu. Ni lazima watanzania tusimame kwa pamoja kukemea mtido wa viongozi wa dini kutoa waraka kuwaelekeza waumini wao namna ya kuchagua. Tukichelewa na kuliacha hili likapiti; majuto ni mkuuu!
Hizi ni dalili tosha kuonyesha kwamba Hekima na busara zimekwenda likizo. Dini zikianzisha vurugu, haina mwisho. Bahati mbaya au nzuri, waumini wa Afrika wanaamini kiushabiki. Labda ni umaskini wa mali na fikra. Hivyo tutachinjana wenyewe kwa wenyewe kulinda waraka kutoka kwa viongozi wetu wa dini.
Katika mambo ya siasa, hakuna haja ya kuwa na waraka kutoka madhehebu mbali mbali. Mwongozo wa kuchagua viongozi utolewe na serikali. Dini zinaweza kusaidia kwa kuhakikisha watanzania wana roho ya Kimungu.
Ni lazima tuwe makini kabisa, vinginevyo tunaweza kuwa kama Somalia na nchi nyingine za Afrika zinazopigana vita ya kudumu. Ni lazima watanzania tusimame kwa pamoja kukemea mtido wa viongozi wa dini kutoa waraka kuwaelekeza waumini wao namna ya kuchagua. Tukichelewa na kuliacha hili likapiti; majuto ni mkuuu!