Waraka Maalum kuhusu URAIS kwa Wajumbe wa Kamati Kuu CHADEMA

Tukubali kwamba kuwafahamu watu wanaoutaka urais mapema ni afya kwa maslahi ya taifa maana tutapata fursa ya kuwafahamu kwa undani, kuwafuatilia, kuwapima lakini pia kuhoji uhalali wao kabla. Ndiyo maana toka mwanzo kabisa mimi ni moja wa watu ambao naunga mkono hoja ya watu wenye sifa kwa mujibu wa katiba (Msisitizo wenye Sifa) kutangaza nia.

Kwa sasa CDM haina mfumo wa kikatiba wala wa kikanuni wa kutangaza nia ya kugombea urais (Kitila Mkumbo-Raia Mwema 10/10/2012) hivyo, yeyote anayefanya hivyo ukianza na John Magale Shibuda, Deogratius Mushi na Zitto Zuberi Kabwe hakiuki chochote na hivyo kuwa na defense dhidi ya maamuzi yoyote ya Kamati Kuu au vinginevyo. Kwa maneno mengine kuwapinga akina Zitto & Co na nia zao za kugombea urais ni kutumia upepo tu badala ya katiba na Kanuni za CDM.

Kwangu mimi, Shibuda na Mushi (Sifahamu exactly umri wa Mushi lakini nahisi atakuwa amefikisha miaka 40 mwaka 2015) wana haki zote za kikatiba kutangaza nia zao za kugombea urais kupitia CDM. Sioni sababu yeyote ya kuwapinga bali wanachama wa CDM wenyewe watachuja pumba na mchele. Lakini kwa Zitto Kabwe ni habari tofauti. Katiba kwa kigezo cha umri haitamruhusu kugombea urais hiyo mwaka 2015. Tegemeo lake ni majaaliwa ya Katiba mpya ambayo hatuna uhakika kama kweli itaaccomodate umri wake au laa. Huyu anaweza kupingwa, maana kuna grounds za kumpinga.

Hoja kwamba, kutangaza nia mapema ni kukigawa chama inategemea na utashi wa anayetangaza nia na nini analenga. Kama utashi, hitaji na busara zake zinamtuma kutangaza nia ya kugombea (na 'haoni' athari zozote ndani ya chama au malengo yake yatatimia) hakuna kitu kinachozuia maana hakuna atakachokiuka ndani ya chama. Katika hili la kutangaza urais ndani ya CDM ni utashi binafsi na si suala la kikatiba wala kikanuni.That is wahy Zitto alikuwa na nguvu ya kumjibu Mzee Edwin Mtei alipomkanya juu ya kutangaza kwake nia maana kwa mujibu wa utashi, busara na hitaji lake haoni tatizo katika hilo.

Swali moja la kujiuliza ni Je Kamati Kuu itawaonya au kuwaadhibu watu hawa wanaotangaza nia ya kugombea urais kwa kanuni zipi za Chama? Hili ndilo ombwe linalotumiwa na wanaotangaza nia.Sasa CDM walizibe? Nini hatma ya Demokrasia kama likizibwa?
 
Wahenga walisema "no reaserch no right to talk" sasa ndugu zanguni ni nani mwenye uhakika wa asilimia mia 100% kuwa Zitto anatumiwa na magamba? Tusimhukumu mtu bila kuwa na uhakika wa kujitosheleza. Pia kumbukeni Zitto ni kijana anayeweza kujenga hoja na mara nyingi anakuwa na uhakika wa kile anachokisema. Naamini kama Mtanzania na mwanachama halali wa CDM anayo haki kwa mujibu wa katiba ya nchi ambayo ni sheria mama ya nchi na hata katiba ya CDM. kitakachomzuia Zitto kwa sasa ni umri ambao katiba imesema ni kuanzia miaka 40. Ni ukweli usiopingika kuwa penye ukweli uongo hujitenga. na muda ni hakimu sahihi kabisa juu ya yote. kama kweli Zitto anatumiwa na magamba lazima ukweli utajidhirihisha. time will tell.
Kompis
 
Mimi naona kwa sasa ni bora kamati kuu ikae kimya kana kwamba hakuna kinachoendelea na ionekane kwamba kila mwanachama ana uhuru wa kutangaza kugombea ili mradi awe na sifa zinazotakiwa na katiba ya chama na ya nchi.

Mkianza kutafutana mtakuwa mna-play on ZZK tunes maana lengo la kujitangaza kwake ni kuleta mgogoro ili baadaye chama kisambaratike ijulikane kuwa akina Wassira ni watabiri kumbe ndio mastermind wa mpango mzima. Kwa CDM kukaa kimya inakuwa sawa na mwanaume anayemfumania mkewe halafu anakaa kimya hamsemeshi kitu na kumpa mate so makubwa ya kuwaza nini kitafuata. Zitto ametumwa na magamba kupeleka mgogoro ndani ya CDM na dawa yake ni kumchunia hivi hivi.

"mwanagu ni mbishi na hashauriki" nanukuu kauli ya mama yake mzazi wa Zitto. Kizuri tutakachopata toka kwa Zito akiwa rais ni First Lady Wema Sepetu lakini maendeleo tusahau kwani mafisadi wanaomtumia hawana nia na maendeleo ya hii nchi.

Well said mkuu!na nafikiri hiyo ndo ndo njia pekee ya kuwapotezea,manaake malumbano c mazuri kwa chama chetu
 
Kila siku nasema ni wakati muafaka wa kung'oa magugu maji ndani ya CDM ambao ni shibuda,zitto na rose kamili.
 
Zitto anakula mshiko wa maana sana kutoka ccm na usalama wa taifa .......................is a very dangerous kijana....uzuri wake ni kuwa inteligensia ya cdm ni zaidi ya ile ya serikali ndiyo maan serikali ya dr.slaa ina uwezo wa kuibua mambo mazito ambayo serikali ya kikwete/maga,ba kamwe hawawezi
 
Mkuu waraka huu umeshawekwa hapa na watuwameshakujadili sana hata hivyo tunatumia simu za kawaida tunashidwa upata ni vema wanoweza wakaukopy na kuuweka hapa
 
Molemo,,angalia post ya Ulukolokwitanga, Imemaliza kila kitu. Hapana haja kuanza kutoana macho,unataka kamati kuu iingize kwenye katiba kuzuia watu kutangaza nia? Imeshafahamika wazi hawa wanaotangazatangaza wakati wenzao wanaimarisha mshikamano kichama kuelekea 2015 wanatumiwa tu na hakika hawana nia ya urais wala urahisi. Hakuna haja kuanza kujibizana nao! Its ur good observation,lkn namna nzuri ni kuachana nao na kuendelea na mikakati ya kusamabaza elimu kwa raia
 
Ushauri mzuri sana.Cha msingi Kamati Kuu itoe mwongozo ili kuepuka kuchanganya wanachama.
 
Kila siku nasema ni wakati muafaka wa kung'oa magugu maji ndani ya CDM ambao ni shibuda,zitto na rose kamili.

Aaaargh!!!!! Umenikata stimu. Watu wanajadili issues, wewe unajadili Watu. Hebu nenda kajojoe ulale wakubwa tujadili issues .
 
Eti "wanachama wadogo" hivi ndani ya chadema kuna wanachama wakubwa ee? Ikiwa kina zitto hawajavunja katiba sasa hiyo kamati kuu itawajadili kitu gani? Kwa nia njema tu na kwa ajili ya kujiimarisha ktk lengo lake ambalo ni halali kwa mujibu wa kanuni za chama ubaya u-wapi mtu kujiandalia mtandao wa ushindi mapema? Chadema inapaswa kuwa makini ktk mwenendo wake ili kisiwe chama ambacho hakina uhuru ndani yake, kumsakama zzk wakati hajavunja kanuni ni kujirudisha nyuma kutoka ktk harakati za ukombozi wa kweli
 
Mkuu Molemo
Leo umekiri waliotangaza urai hawajafunga kipengele cha katiba ya Chadema; bado sijaelewa hawa wanachama wa Kishapu uliokuwa umewanukuu wanaona chama kitaharibika kwa misingi ya watu watatu kutangaza nia yao au kwa misingi ya Chadema kuheshimu Demokrasi? Bado hujafunguka kinaogopwa kitu gani

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Ccm ikishirikiana na usalama wa taifa inampa zitto pesa nyingi ili kujenga mtandao ndani ya cdm ili kukivuuga chama zito ni janga kwa maendeleo ya m4c
 
Kweli kabisa kwa sababu mwanzo wa matatizo katika vyama ni kutotolea kauli juu ya jambo linaloonekana kuguza hisia za watu wengi, twakushukuru kwa waraka wako bora hasa kipindi hiki kigumu cha vuguvugu la mabadiliko kichama sehemu mbalimbali.
 
Wahenga walisema "no reaserch no right to talk" sasa ndugu zanguni ni nani mwenye uhakika wa asilimia mia 100% kuwa Zitto anatumiwa na magamba? Tusimhukumu mtu bila kuwa na uhakika wa kujitosheleza. Pia kumbukeni Zitto ni kijana anayeweza kujenga hoja na mara nyingi anakuwa na uhakika wa kile anachokisema. Naamini kama Mtanzania na mwanachama halali wa CDM anayo haki kwa mujibu wa katiba ya nchi ambayo ni sheria mama ya nchi na hata katiba ya CDM. kitakachomzuia Zitto kwa sasa ni umri ambao katiba imesema ni kuanzia miaka 40. Ni ukweli usiopingika kuwa penye ukweli uongo hujitenga. na muda ni hakimu sahihi kabisa juu ya yote. kama kweli Zitto anatumiwa na magamba lazima ukweli utajidhirihisha. time will tell.
Kompis

Usiwe kama robbot si kweli kila kitu mtu anachotakiwa kusema lazima afanye research, research inafanyika kwa vitu so challenging that no exact answer.kwani zitto kukamatwa mawasiliano yake na zoka kunahitaji research.wewe vipiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!
 
Back
Top Bottom