Wapinzani waandaa hoja: Wamtaka Pinda kujiuzulu

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Well... ndani ya mwaka mmoja tunaweza kuwa na Waziri Mkuu mwingine aliyejiuzulu? Well.. wapinzani inaonekana wanataka iwe hivyo. Wengi wamefikia hilo baada ya kusoma makala ya The Citizen la leo kuwa Pinda alimaanisha alichosema kuwa wananchi wawaue papo hapo wanaowatuhumu kuwa ni wauaji wa albino.

Kesho kwenye kipindi cha maswali na majibu wabunge wanasubiri kwa hamu kusikia kama PInda atathubutu kutetea msimamo wake huo Bungeni au atakanusha. Kuna kundi la wabunge wa CCM ambao nao wanasubiri kusikiliza kuwa alimaanisha nini hasa (sijui kama bado kuna utata hapo)
 
Hivi waTanzania tumefikia kiwango cha kutupa sahani iliyojaa 'wali' just because tumekuta jiwe moja katika wali huo?Im doubtin dat ze wapinzani are over-reacting on the matter.
 
Ukimuua albino, tutakuua tu. Na hili wala halikuhitaji Waziri Mkuu kulisemea ... Kwa mliotarajia "kula" kwa kuandika habari za mauaji ya albino, sasa subirini kuandika habari za kuuwawa kwa "wauaji wenyewe".

Hapo hakuna cha haki za binadamu wala nini. Ukiondoa uhai wa "albino", haki yako ya ubinadamu inaishia hapo hapo.

Acha Pinda ajiuzulu, lakini sisi tutawaua tu, kama ambavyo tumekuwa tukifanya kwa majambazi, n.k.

Ikionekana kuna wanaotetea wauaji wa albino, kama hao viongozi (wanasiasa) wa NCCR, nao tutawajumuisha kwenye list ya wauaji ... hii ni vita, si siasa!!!

Ole wenu!!
 
Unajua Mkuu MM, kama Mheshimiwa akiendelea kutetea hoja yake Bungeni, na waBunge wakiwa wakali, anaweza kabisa kutakiwa kujiuzulu. Kwa maana atakuwa anajiweka katika mambo makubwa mawili. Moja ni kutetea uvunjaji wa Katiba na sheria za nchi (ambapo kuua ni kosa la jinai) na yeye kama kiongozi mkubwa wa nchi, kutetea kwake mauaji ni kosa pia. La pili, ni kuhatarisha usalama wa Taifa. Maana watu wakianza kuuana, si rahisi kwa serikali iliyoshindwa na kuchoka kutetea/kulinda na kuzuia mauaji ya Albino ikaweza kuzuia mfumuko huo wa mauaji ya kimbari yatakayoweza kuanzishwa kutokana na kauli yake hiyo. Inachotakiwa ni yeye kufafanua kwa kukanusha matamshi yake (kama alivyofanya mwandishi wake). Hata kama itaeleweka vibaya kiasi gani, haitamuweka pabaya sana.
 
Well... ndani ya mwaka mmoja tunaweza kuwa na Waziri Mkuu mwingine aliyejiuzulu? Well.. wapinzani inaonekana wanataka iwe hivyo. Wengi wamefikia hilo baada ya kusoma makala ya The Citizen la leo kuwa Pinda alimaanisha alichosema kuwa wananchi wawaue papo hapo wanaowatuhumu kuwa ni wauaji wa albino.

Kesho kwenye kipindi cha maswali na majibu wabunge wanasubiri kwa hamu kusikia kama PInda atathubutu kutetea msimamo wake huo Bungeni au atakanusha. Kuna kundi la wabunge wa CCM ambao nao wanasubiri kusikiliza kuwa alimaanisha nini hasa (sijui kama bado kuna utata hapo)

Utata upo kwenye 'wapinzani', ni kina nani hao'? Isije kuwa ni vyama vya upinzani vinavyojulikana kama 'ntoke vipi', wamepata style ya kutokea. Tunataka watoke na style ya kushinda uchaguzi mwakani baada ya style ya ufisadi kuenda arijojo.
 
Unajua Mkuu MM, kama Mheshimiwa akiendelea kutetea hoja yake Bungeni, na waBunge wakiwa wakali, anaweza kabisa kutakiwa kujiuzulu. Kwa maana atakuwa anajiweka katika mambo makubwa mawili. Moja ni kutetea uvunjaji wa Katiba na sheria za nchi (ambapo kuua ni kosa la jinai) na yeye kama kiongozi mkubwa wa nchi, kutetea kwake mauaji ni kosa pia. La pili, ni kuhatarisha usalama wa Taifa. Maana watu wakianza kuuana, si rahisi kwa serikali iliyoshindwa na kuchoka kutetea/kulinda na kuzuia mauaji ya Albino ikaweza kuzuia mfumuko huo wa mauaji ya kimbari yatakayoweza kuanzishwa kutokana na kauli yake hiyo. Inachotakiwa ni yeye kufafanua kwa kukanusha matamshi yake (kama alivyofanya mwandishi wake). Hata kama itaeleweka vibaya kiasi gani, haitamuweka pabaya sana.

hawezi kukanusha kwani anajua anachezea hisia za watu. Nakumbuka alipoapa aliapa kulinda hisia, vionjo, na machungu ya Watanzania! Hivyo anatekeleza wajibu wake.
 
Hivi waTanzania tumefikia kiwango cha kutupa sahani iliyojaa 'wali' just because tumekuta jiwe moja katika wali huo?Im doubtin dat ze wapinzani are over-reacting on the matter.

Mwakyj, I disagree, kazi ya upinzani ni to keep the government on its toes and to hold it accountable at every possible turn. Unafikiri hii ingetokea Marekani, Obama akatamka kitu kama hiki Republicans wangesema eti amekosea let's forget about it? umesahau Clinton's Lewinsky case and his near impeachment?
Sorry, waziri mkuu Pinda amesema kitu ambacho ni unacceptable kutoka kiongozi wa nchi kwani he has flaunted the rule of law and has encouraged people to take justice into their own hands, also can be deemed as instigating murder, incitement etc. Ni maneno mazito sana aliyoyatamka and it is time we hold our leader's feet to the fire.
 
Hivi waTanzania tumefikia kiwango cha kutupa sahani iliyojaa 'wali' just because tumekuta jiwe moja katika wali huo?Im doubtin dat ze wapinzani are over-reacting on the matter.

Totally agree.

While i think Pinda's statement is not beffiting a prime minister, i think these people are overeacting.
 
Tatizo la uongozi wa Tanzania siyo elimu, umri, kabila wala dini ni uwezo.
By M.M. Mwanakijiji Jan. 2009
 
Nafikira Pinda aliteleza ulimi..akubali kuwa aliteleza ulimi bahati mbaya!

Mkuu, hili litakuwa jambo gumu sana kwa kiongozi wa Bongo! but that would be the right thing to do not to defend a position and to continue digging a hole!
 
Alitaka awe shujaa wa karne labda ingefuta kabisa mauaji ya albino na yeye kuwa shujaa pole sana Pinda
 
Kesho kwenye kipindi cha maswali na majibu wabunge wanasubiri kwa hamu kusikia kama PInda atathubutu kutetea msimamo wake huo Bungeni au atakanusha.

Wapinzani wanaanda hoja dhidi ya Pinda au wanasubiri kwa hamu kusikia kama kuna utetezi na kanusho?

Pinda katoa li gaffe la mwaka, kama kawaida yake, li gaffe liko crystal clear, watu wakadai Pinda eti mwenyewe ndio awape nakala ya alichokisema. Pinda katuma msemaji karudia kile kile, watu wakasema hajafafanua vizuri. Pinda akaona nakala za hotuba za nini, akaenda gazetini kuongea kwa mdomo, akarudia kile kile, mara ya tatu, halafu tunaambiwa wapinzani wanasubiri tena kuambiwa mengine.

Sijui tatizo ni wapinzani au ni tunachoambiwa kinaendelea au ni mimi ambae ndio sielewi haya maluelue.
 
Wapinzani wanaanda hoja dhidi ya Pinda au wanasubiri kwa hamu kusikia kama kuna utetezi na kanusho?

Pinda katoa li gaffe la mwaka kama kawaida yake, li gaffe liko crystal clear, watu wakadai Pinda eti mwenyewe ndio awape nakala ya alichokisema. Pinda katuma msemaji karudia kile kile, watu wakasema hajafafanua vizuri. Pinda akaona nakala za hotuba za nini, akaenda gazetini kuongea kwa mdomo, akarudia kile kile, mara ya tatu, halafu tunaambiwa wapinzani wanasubiri tena kuambiwa mengine.

Sijui tatizo ni wapinzani au ni tunachoambiwa kinaendelea au ni mimi ambae ndio sielewi haya maluelue.

Kuhani mkuu, nadhani watu wanampa nafasi tena na tena Waziri mkuu ajirekebishe au aombe radhi kwa tamko lake ambalo ni kosa kisheria. Lakini jamaa kama tulivyoona anazidi kujichimbia mtaro mkubwa zaidi!
 
... Well.. wapinzani inaonekana wanataka iwe hivyo. Wengi wamefikia hilo baada ya kusoma makala ya The Citizen la leo kuwa Pinda alimaanisha alichosema kuwa wananchi wawaue papo hapo wanaowatuhumu kuwa ni wauaji wa albino.

Kwamba wapinzani waandaa hoja. Mimi bado sijaelewa, kwamba wamekubaliana kwa pamoja (ikiwamo CUF na CHADEMA) au mleta hoja amepata ujumbe kutoka katika vyama mbalimbali vya upinzani separately?
 
Wapinzani wanaanda hoja dhidi ya Pinda au wanasubiri kwa hamu kusikia kama kuna utetezi na kanusho?

Wapinzani wameshasikia ya kutosha wao wanaendelea mbele na hilo. Wabunge wengine wengi (hasa wa CCM) wanasubiri kesho kabla ya kuform their opinion.

Pinda katoa li gaffe la mwaka, kama kawaida yake, li gaffe liko crystal clear, watu wakadai Pinda eti mwenyewe ndio awape nakala ya alichokisema. Pinda katuma msemaji karudia kile kile, watu wakasema hajafafanua vizuri. Pinda akaona nakala za hotuba za nini, akaenda gazetini kuongea kwa mdomo, akarudia kile kile, mara ya tatu, halafu tunaambiwa wapinzani wanasubiri tena kuambiwa mengine.

soma vizuri basi...

Sijui tatizo ni wapinzani au ni tunachoambiwa kinaendelea au ni mimi ambae ndio sielewi haya maluelue.

Tatizo yawezekana ni wewe kusoma kisichoandikwa.
 
Sometimes mtu unafanya kosa kubwa hasa pale unaporuhusu hisia kufanya kazi sehemu ambako brain inatakiwa ifanye kazi.

Kwa kusema kweli Huyu PM mimi namsujudia sana but sometimes hayuko makini.huwa anasolve rational problems emotionally.

I dont think if he will be able to clarify or to defend himself regarding this matter.Pinda kwa kweli hakutakiwa kutamka yale aliyotamka,ku-justify watu kujichukulia sheria mkononi?It's a crime.Kwa hiyo no rule of law,and i think huyu jamaa ni mwanasheria kitaaluma.Hapo hajatofautiana na Ole Sendeka.

Hili suala la albino linaudhi na linaumiza Roho kwa kweli.But pm hawezi kuhalalisha wauaji nao wauwawe by any means.


Tukifanya hivyo mbona Watanzania watauawa wengi sana,watauawa hata innocent people kwa visingizio au kutokana na chuki binafsi tu.Natamani moyo wake ungewachukia walioiba pesa zetu kama ulivyochukia wauaji wa Albino.

Akijiuzulu sasa sijui Jk atamteu Mwakyembe,atampandisha Membe,Anne kilango au atakua nani tena
 
Back
Top Bottom