Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,884
- 6,885
Watumishi watano wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete wamesimamishwa kazi wakidaiwa kujihusisha na masuala ya siasa kinyume na kanuni za kudumu za utumishi wa umma. Watendaji hao ni kutoka idara ya mipango, idara ya maji na watendaji watatu, wakiwemo wawili wa kata na mmoja kutoka ngazi ya kijiji. Watumishi hao kwa pamoja, wakiwa kila mmoja katika eneo lake la kazi, wanatuhumiwa kufanya shughuli za kisiasa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Kufuatia tuhuma hizo, Halmashauri ya Wilaya ya Makete imewasimamisha kazi na kuwapa nafasi ya siku 14 za kujieleza kwa maandishi kuthibitisha kama madai hayo yana ukweli au la. Uchunguzi wa NIPASHE uliofanyika wilayani hapa, umebaini kuwa waliokumbwa na kadhia hiyo ni pamoja na mtumishi wa idara ya mipango Barton Sinene, Naumu Tweve kutoka idara ya maji na Clemence Sanga ambaye ni Ofisa Mtendaji Kata (WEO) ya Bulongwa. Wengine ni Yusti Konga, Ofisa Mtendaji (WEO) wa Kata ya Mlondwe na Happy Mahenge ambaye ni Ofisa Mtendaji wa Kijiji (VEO). Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Imelda Ishuza alipotafutwa na NIPASHE kutoa ufafanuzi kuhusiana na sakata hilo, alikiri kuwa watumishi hao watano wamesimamishwa kazi na kupewa siku 14 za kujieleza kwa maandishi.
Ni kweli tuliwapa barua za kuwasimamisha na kuwataka wajieleze kimaandishi ndani ya siku 14 ambazo hata hivyo bado hazijaisha Hawa wanatuhumiwa kujihusisha na mambo ya siasa kinyume na kanuni za kudumu za utumishi wa umma,alisema Mkurugenzi huyo. Sisi tunafanya uchunguzi wetu na kwakweli hatuna tatizo na wao ila tukibaini hawakufanya hivyo watarejea kazini kuendelea na majukumu yao,alisema mkurugenzi huyo.
Kutokana na hali hiyo, NIPASHE ilitaka kujiridhisha kuhusiana na sakata hilo na kufanya mahojiano na Ofisa Utumishi wa Halmashauri hiyo, Pius Gerace ambaye alikiri kuwa watumishi hao wamesimamishwa kazi kwa mujibu wa kifungu cha 21 (f) cha sheria ya mwaka 2009 ya kanuni za kudumu za utumishi wa umma.Hii sheria tuliyotumia kuwapa mapumziko wakati ambapo Halmashauri inafanya uchunguzi wa kina kuhusiana na tuhuma hizo inaitwa Standing Order for Public Service,alisema Gerace.
Nipashe
Kufuatia tuhuma hizo, Halmashauri ya Wilaya ya Makete imewasimamisha kazi na kuwapa nafasi ya siku 14 za kujieleza kwa maandishi kuthibitisha kama madai hayo yana ukweli au la. Uchunguzi wa NIPASHE uliofanyika wilayani hapa, umebaini kuwa waliokumbwa na kadhia hiyo ni pamoja na mtumishi wa idara ya mipango Barton Sinene, Naumu Tweve kutoka idara ya maji na Clemence Sanga ambaye ni Ofisa Mtendaji Kata (WEO) ya Bulongwa. Wengine ni Yusti Konga, Ofisa Mtendaji (WEO) wa Kata ya Mlondwe na Happy Mahenge ambaye ni Ofisa Mtendaji wa Kijiji (VEO). Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Imelda Ishuza alipotafutwa na NIPASHE kutoa ufafanuzi kuhusiana na sakata hilo, alikiri kuwa watumishi hao watano wamesimamishwa kazi na kupewa siku 14 za kujieleza kwa maandishi.
Ni kweli tuliwapa barua za kuwasimamisha na kuwataka wajieleze kimaandishi ndani ya siku 14 ambazo hata hivyo bado hazijaisha Hawa wanatuhumiwa kujihusisha na mambo ya siasa kinyume na kanuni za kudumu za utumishi wa umma,alisema Mkurugenzi huyo. Sisi tunafanya uchunguzi wetu na kwakweli hatuna tatizo na wao ila tukibaini hawakufanya hivyo watarejea kazini kuendelea na majukumu yao,alisema mkurugenzi huyo.
Kutokana na hali hiyo, NIPASHE ilitaka kujiridhisha kuhusiana na sakata hilo na kufanya mahojiano na Ofisa Utumishi wa Halmashauri hiyo, Pius Gerace ambaye alikiri kuwa watumishi hao wamesimamishwa kazi kwa mujibu wa kifungu cha 21 (f) cha sheria ya mwaka 2009 ya kanuni za kudumu za utumishi wa umma.Hii sheria tuliyotumia kuwapa mapumziko wakati ambapo Halmashauri inafanya uchunguzi wa kina kuhusiana na tuhuma hizo inaitwa Standing Order for Public Service,alisema Gerace.
Nipashe