'Wapiganaji' walioko CCM wanapigania nini hasa?

Asalaam wana jamvi:
Nimekuwa nikijiuliza maswali kadhaa juu ya mwenendo na harakati za chama cha mapinduzi (ccm) juu ya hali ya kisiasa,kiuchumi na kijamii,maswali yangu yanajikita kwa kundi linalojihita ni watetea haki na kupinga ufisadi na ukandamizaji wa haki za binadamu,samweli sita,mwakyembe,selelii na james lembeli na wafuasi wao ktk ccm je, wako wapi ktk matukio yafuatayo:-
(1).Moja mbinu chafu za kisiasa zinazofanywa na chama cha mapinduzi(ccm),kama propaganda kidini dhidi ya upinzani,kujihusisha na utengenezaji wa vidio feki na matukio mengine ya kinyama dhidi ya upinzani wanasimama upande gani ktk haya mambo?kauli yao ni ipi?
(2).kuporomoka kwa uchumi na kuinuka kwa mfumuko wa bei huku serekali na ccm ikilidhia kupandishwa holela kwa gharama za umeme,maji na usafiri bila kuangalio ongezeko la kipato cha wakulima na wafanyakazi,ipi kauli yao ktk hili?
(3).Ufisadi ulifanywa na chama chao wanachokitumikia ktk swala JITEGEMEE COMPANY na wao wakijipambanunua kama wapinga ufisadi je,wanaridhika na ufisadi huo?upi msimamo wao?
(4).Dhuluma za ardhi zinazofanywa na ccm na serekali huko ngorongoro dhidi ya wamasai huko ngorongoro,je,wapinga ufisadi na unyanyasaji wa raia wakina samweli sita ili wanalisemea vp?
(5)Kuporoka kwa kasi na janga la kufeli watoto wetu je,hili nalo wamelisemea wapi?
Samweli sita amekuwa akijipambanua kuwa yeye ndie mgombea wa urais mwema na mzuri kuliko wote ndani ya ccm mwaka 2015,bila kujitokeza ktk majanga kama haya mazito yanawatesa watanzania,ili linanifanya kupata majibu juu ya ili kundi la kina sita na wafuasi wake kuwa ni wanafiki na wazandiki wakubwa ambao hawastahili kujihita wateta raia huku wakiishi ktk chama fisadi(ccm) na kundi la wala rushwa wachafu wa matendo kama mwigulu nchemba, kama sita ni mstaarabu kwanini hawakemei watu kama wakina nape,wasira na mwigulu juu ya mataendo ya kikatili na machafu dhidi ya upinzani na raia kama kibanda?ccm imeoza hakuna msafi wote wachafu,hakuna mtetezi wa haki za binadamu na haki za raia ndani ya ccm....ccm ni kichafu kimekufa na kimeoza Sitta na kundi lake aache mara moja kujipambanua kuwa yeye ni mwanaharakati na mpinga ufisadi huku wakiuchekea ufisadi unaofanywa na ccm na ufedhuli wa dhidi ya upinzani.....ccm sio chama cha kisiasa tena ni kundi la wezi tu.

wamekaa kimya katika issue zote hizo muhimu wanasubiri uchaguzi ukaribie halafu ndio waamke na kudai walikuwa wanapinga hayo yote uliyoyataja utamsikia hata salim atadai alikuwa anapinga yote haya. kiongozi mzuri utamjua wakati dhuluma inafanyika na sio wakati wa uchaguzi.
 
Nimejaribu kujiuliza kuwa hawa ndugu zetu ambao wamebatizwa jina la “Makamanda” wa vita ya ufisadi walioko CCM wanachopigania hasa ni nini? Ujumbe wao unaotufanya tusimame nyuma yao na kuwaunga mkono hasa ni kitu gani? Kama kuna mtu ambaye bado ni dhaifu na hajaamua kuchagua upande hawa wapiganaji watamshawishi vipi ili awaunge mkono; wanamuahidi nini?

Ninajiuliza maswali hayo na mengine mengi kwa sababu ukiondoa madai makubwa mawili bado najaribu kutafuta ujumbe wa wapiganaji wetu ili niweze kuelewa kama wana nafasi ya kushinda au watakuwa na athari ya kuvutia mikutano na kuuza magazeti na majina yao kutangaa lakini itakapofika muda wa kura wakajikuta wanatupwa nje ya ulingo.

Zafanana
Kitu kimoja hata hivyo naweza kukisema kwa uhakika zaidi ni kuwa kuna mfanano wa ajabu kati ya wanasiasa watetezi wa mafisadi (makuwadi wa ufisadi) na wale wanasiasa wanaowapinga mafisadi (wapinagaji). Kufanana huku ni muhimu kukuelewa kwani kimsingi kabisa kunafanya wapiganaji wawe na kazi kubwa zaidi ya kuushawishi umma kuhusu lengo na madhumuni yao hasa ni nini.

Wanafanana kwani makundi yote mawili yako kwenye chama kimoja; CCM imekuwa kama tenga lililobeba ndani yake matunda mabivu na matunda ambayo hayajaiva na pamoja na hao matunda wadudu wa kila aina wanaofuata uchafu. Makundi yote mawili yako kwenye tenga moja na hivyo moja linaweza kubeza jingine kuwa halijaiva sana au bado ni bichi au limeoza na lile jingine likalalamika kuwa linaonewa na kuwa kinachofanyika ni “chuki binafsi”. Lakini ukweli unabakia hadharani kuwa wote wawili wako kwenye tenga moja.

Wanafanana kwa sababu wote wanagombania nafasi ndani ya chama hicho hicho kimoja. Tumeshuhudia Dodoma wiki chache zilizopita jinsi gani makundi haya mawili yako kwenye muelekeo wa kugongana kusikoepukika. Lakini pamoja na mgongano huo tunaona kuwa makundi yote mawili yanagombania zaidi nafasi zao ndani ya chama. Hadi hivi sasa kundi la watetezi wa watuhumiwa ufisadi linaonekana kuongoza na kupata mashabiki wengi zaidi.

Ni nani kati yao atakayeweza kuwa na nafasi ya kutengeneza wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi hususan kwenye Ubunge ifikapo 2010? Itakuwaje kama kundi la makuwadi litapata kuunga mkono zaidi ndani ya chama na kundi la wapiganaji likajikuta linaungwa mkono zaidi nje ya chama? Jibu ni jepesi; makuwadi watakuwa na wagombea wengi zaidi chamani na hivyo kutuamulia viongozi wetu wajao ni kina nani.

Hata hivyo kufanana ninakozungumzia mimi siyo kufanana kwa aina hiyo. Ni kufanana kwa kile wanachogombania mwakani ni nini hasa. Makundi yote mawili yanagombania kuchaguliwa tena.

Baada ya matukio ya kihistoria ya Februari 2008 yaliyosababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kwa kuhusishwa na kashfa ya Richmond mpasuko mkubwa umetokea ndani ya CCM. Mpasuko ambao hauwezi kuisha kwa vikao, mazungumzo, makubaliano au muafaka wa aina fulani. Mpasuko huu ni mkubwa sana kwani makundi mawili yanayoshindana hayawezi kurudi nyuma hata kidogo kwani kufanya hivyo itakuwa ni sawa na kujitia kitanzi wao wenyewe.

Kundi la watetezi wa Lowassa haliwezi kurudi nyuma kwani hawa wanaamini kabisa kuwa kitendo cha Lowassa kubanwa na kamati teule ya Bunge kilikuwa kimekusudiwa, kupangwa na kufanikishwa na watu mbalimbali miongoni mwao ni Spika wa Bunge la Muungano Bw. Samweli Sitta na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo teule Dr. Harrison Mwakyembe pamoja na wajumbe wengine wa kamati hiyo.

Hivyo kundi hili la Lowassa, mashabiki wake, wanufaika wa utawala wake, mashabiki na marafiki wake wa karibu waliapa toka wakati ule kulipa kisasi na kuhakikisha kuwaangusha wahusika wote na hatimaye kusababisha mchakato mpya utakaomsafisha Lowassa na wenzake na kitendo kile wanachoamini kuwa ni cha “uonevu mkubwa”. Kama nilivyodokeza siku chache baada ya matukio yale kundi hili halitokoma mpaka Lowassa atakaposimama tena akiwa safi na akiwa kiongozi. Chini ya hapo hakuna mapatano.

Kundi la kina Mwakyembe linaamini kabisa kuwa lilifanya kazi yake kwa uadilifu na weledi na halikumuonea mtu yeyote na zaidi kuwa wangeweza kufanya makubwa zaidi kama wangetaka. Hawa wamejipanga wakati wowote kumwaga “mchele kwenye kuku wengi” endapo itabidi iwe hivyo hasa pale hatima yao ya kisiasa itakapokuwa mashakani. Kundi hili linaamini kabisa kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ilihusika moja kwa moja na suala la Richmond na kwa hilo hawako tayari kumuomba msamaha mtu yeyote.

Hawa nao mashabiki wao, wapambe wao na wale wanaowaunga mkono hawako tayari kurudi nyuma wala kusalimu amri. Sasa hawa wamepania kabisa kutetea viti vyao vya Ubunge na nafasi zao katika chama.

Hivyo basi tunaweza kuona kuwa pande hizi mbili haziwezi kupatana kwa kadiri ya kwamba kila moja inaamini kuwa iko sahihi katika mtazamo wake wa matukio ya Februari 2008. Hawawezi kukaa meza moja; hawawezi kujadili sera pamoja na kwa hakika kwa upande wao hakuna mapatano yoyote na wale wa utetezi wa kundi la ufisadi isipokuwa ushindi tu.

Ushindi hauji chee
Hapo kwenye ushindi ndio tatizo. Kama nilivyoanisha katika makala zangu kadhaa zilizopita ni kuwa vitani ushindi hauji mezani bila kumlazimisha adui kusalimu amri. Ushindi katika vita unakuja kwa kumzidi adui uwezo na kumuweka kama kwenye kabali hivi na kumlazimisha anyanyue mikono kuomba radhi na kuingia katika meza ya makubaliano ya kusitisha vita kwa kusalimu amri.

Ili upande mmoja ushinde ni lazima uwe na ujumbe, mbinu, na zana na utaalamu wa kutosha kumshinda adui. Nasikitika kusema kuwa upande wa watetezi wa Lowassa na wale wanaowatetea mafisadi (kama wanaomtetea Mkapa) umejipanga vizuri zaidi, ujumbe wake unagusa wanufaika wengi wa ufisadi na kwa hakika wana uwezo na zana za kuwamaliza wapinzani wao.

Ndio maana hapa nimeuliza hawa wapiganaji wetu wao wanaujumbe gani zaidi ya zile mbili tulizozizoea na ambazo ukweli wake unakubalika katika akili za Watanzania wengi? Ni zipi unauliza..?

Kwanza kuna ujumbe kuwa mafisadi wanaeneza fedha na mikakati ya kuwang’oa katika viti vyao vya Ubunge. Hili tumelisikia kwa muda na lina mantiki ndani yake. Kwamba, wale walioathirika wanataka kuwaangusha wale waliowaathiri ni sehemu ya siasa. Ninachokiona ni kuwa watetezi wa ufisadi wanatumia sayansi na sanaa ya siasa kuwaangusha wabaya wao. Katika hili mbinu na njia mbalimbali zitatumika hata zile ambazo ni kinyume cha sheria.

Sasa wapiganaji wetu wamekuwa wakilia na kulalamika juu ya hili. Lakini wataendelea kulia lia huku hadi uchaguzi mkuu utakapofika ili kiwe nini? Sawa mafisadi wanataka kuwaangusha kwenye majimbo ya uchaguzi wao walitarajia nini? Hivi walifikiri baada ya matukio ya Februari wangetumiwa zawadi ya maua na keki kutoka kwa walioangushwa kwa fedheha na aibu?

Wanachofanya makuwadi wa mafisadi si kingine bali kutumia siasa kulipa kisasi na Dodoma ilikuwa ni mwanzo tu. Watapiga tena.

Ujumbe wao wa pili ni kuwa kuna mafisadi na mafisadi ni lazima washindwe. Sasa ukweli wa huu tunaujua kuanzia enzi za kipindi cha “Mikingamo” na matangazo ya “Liangalieni limbukeni hili”. Mafisadi wamekuwepi nchini kwa muda mrefu na wamekuwepo ndani ya CCM kwa muda mrefu (na siyo wanne tu kama mmoja alivyotaka tuamini).

Sasa kutuambia kuwa mafisadi wanasambaza fedha na vipeperushi n.k kwenye majimbo katika mbinu ya kuwaangusha wapiganaji kunaweza kutufanya tuwaonee huruma lakini hiyo ni sehemu ya siasa. Kama watetezi waliweza kujipanga vizuri hadi kuweza kuleta hoja nzito dhidi ya Spika kwenye mkutano wa Halmashauri Kuu na kwa kutumia njia za kisiasa basi hatuna budi kukubali kuwa hii ni sehemu ya siasa na makuwadi wa ufisadi wako tayari kutumia mchakato wa kisiasa kutimiza malengo yao.

Pia kutuambia ukweli kuwa ufisadi na mafisadi wapo na wana nguvu na wako tayari kufanya lolote ni ukweli ambao wengi wetu tunaufahamu.

Wananchi wanahitaji na wanastahili zaidi ya jumbe hizo mbilli. Watanzania wanataka kujua hawa wapiganaji zaidi ya kupigana ili kuokoa meli zao kabla ya uchaguzi ni kitu gani kingine ambacho ni kikubwa na wanakipigania ambacho kitawafanya wananchi wawaunge mkono na kuwarudisha Bungeni?

Je, wao wapiganaji wanatumia vipi mchakato wa kisiasa kuwazidi kete makuwadi wa ufisadi? Je wanafanya kila kinachowezekana kuhakikisha kuwa makuwadi wa ufisadi na wenyewe hawarudi Bungeni na kushika nafasi mbalimbali?

Ninaamini katika mvutano huu ni ushindi wa upande mmoja tu utakaosababisha mjadala kuisha ndani ya CCM. Hadi hivi sasa wanaoelekea kushinda ni watetezi wa ufisadi na dakika ni hizi za majeruhi. Je, wale wapiganaji wetu zaidi ya kuhutumia mikutano ya kutupa jumbe zao mbili wana kitu gani zaidi wanachogombania ndani ya CCM na kwenye Taifa ambacho kitatufanya tuamini kuwa kitu hicho ni cha thamani zaidi kuliko fedha na ahadi za makuwadi wa ufisadi?

Ni kitu gani wapiganaji wetu wanagombania hasa ukiondoa wao kuchaguliwa tena kwenye Bunge la 2010?

Mkuu Mwanakijiji

Tafakuri yako jadidi mpaka leo haijapata jibu sahihi.

Pengine, tusubiri kwa miaka mingine minne ndipo tutajua wapinaji waliopo CCM wanapigania nini hasa...!
 
hiki ni kikundi kilichojipambanua kupambana na ufisadi ndani ya ccm na kiliongozwa na samweli sitta akisaidiwa na anna klango, harison mwakyembe,kangi lugola, lukasi sellelii na aloyce kimaro wa vunjo moshi bila kumsahau nape na kinana/mukama.la kujiuliza leo ni kuwa kundi lile limetowekea wapi?je ajemda ya ufisadi ndani ya ccm ndo imefungwa?mbona watuhumiwa bado wapo na wanadunda mitaani?hivi wale walikuwa wakipinga ufisadi kwakwa wanauchhukia au waliwachukia mafisadi kwa sababu zao nyingine?hivi walikuwa wazalendo wa kweli au wapiga kelele?tusaidiane kuliuliza swali hili kila inapowezekana kwa mustakbali mwema wa taifa letu.
 
Unajua CCM wana msemo kuwa "mchawi mpe mwanao akulelee" Sita kapewa wizara katulia pia alikuwa na nguvu pale alipokuwa spika,, akawa kama aliyekuwa anaupinga ufisadi..Alipotolewa kwenye USPIKA akawa kama samaki aliyetolewa kwenye maji,, sawa na nape na Mwakyembe.Walipopewa wizara na kutolewa pale walipokuwa wakijipambanua kama wapinga ufisadi waliweka kipaumbele kwenye wizara zao..Kinachonipa shida na mimi kuwaona nao ni wapinga ufisadi ni pale wanapomkosoa anayepita makanisana kufanya kampen na wao pia wakapita humohumo lakini kwa namna nyingine kuponda na kufanya kampeni ya kundi lao.
 
Mtu kama Nepi sio mpinga ufisadi ila analifanyia kampeni kundi lake la kina Six na Mzee wa kyela kwa kuwachafua wengine walio tishio kwao..HAKUNA msafi hata mmoja ndani ya CCM.
 
Watasikikaje ili hali watanzania tunapenda kitu kidogo, Wananchi kwasasa wanafagilia watu wenye pesa, kama huamini angalia kwenye harambee na makongamano wanaalikwa akina nani kama wageni rasmi.

hiki ni kikundi kilichojipambanua kupambana na ufisadi ndani ya ccm na kiliongozwa na samweli sitta akisaidiwa na anna klango, harison mwakyembe,kangi lugola, lukasi sellelii na aloyce kimaro wa vunjo moshi bila kumsahau nape na kinana/mukama.la kujiuliza leo ni kuwa kundi lile limetowekea wapi?je ajemda ya ufisadi ndani ya ccm ndo imefungwa?mbona watuhumiwa bado wapo na wanadunda mitaani?hivi wale walikuwa wakipinga ufisadi kwakwa wanauchhukia au waliwachukia mafisadi kwa sababu zao nyingine?hivi walikuwa wazalendo wa kweli au wapiga kelele?tusaidiane kuliuliza swali hili kila inapowezekana kwa mustakbali mwema wa taifa letu.
 
Hii thread ni mwiba mkali mno na mchungu sana kwa magamba Hahaha hahaha hahaha hahaha hahaha
 
that is a rhetorical question, wanachopigania ni matumbo. nao huvuma kama pepo za kusi.....
 
Walifanya walioyafanya kwaajili ya umaarufu sasa wamepata vyeo so mission acomplished


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Wakuu zangu,
Waacheni wapiganaji waifanye kazi yao..mimi sioni tatizo liko wapi..Yawezekana mimi nakosea lakini ndivyo vita inavyopigana..Mafisadi wanahitaji mashambulizi toka pande zote nje na ndani ndipo tunaweza kufanikiwa kwani hasira ya wananchi sio kwa chama CCM kama chama, isipokuwa viongozi wabovu waliomo ndani ya chama CCM...Chama ni watu.

Tukumbuke tu kwamba hata wakati wa kumwonda Hitler kulikuwepo na wapiganaji toka ndani ya utawala wake wakiitwa resistance group, hawa ndio waliofanya kazi kubwa ya kumwangusha Hitler ktk kila utawala alochukua iwe France, Urusi, na kwingineko.. Majeshi ya nchi za nje yalipokuwa yakiingia yalipata taarifa na sehemu na nyaraka za siri za Hitler hivyo kurahisisha mashambulizi.. kazi ambayo imekuwa ikifanyika kwa muda mrefu sasa hivi nyumbani kiasi kwamba Mafisadi wanahaha!.

Binafsi Mwanakijiji kama mpiganaji akijiunga na CCM na kuahidi kuwaangusha Mafisadi nitamtazama sawa na mgombea mwingine maadam imani yangu ni huyu mwanakijiji na kile anachokisimamia. Chadema, TLP au CUF haina maana hakuna mafisadi ndani ya vyama hivyo, wapo wengi tu isipokuwa tunachoomba ni utawala mzima kutokuwa wa kifisadi hivyo agenda za watu binafsi zitakosa nafasi.

Tumeyaona nchi za jirani kama Zambia, Malawi na Kenya ambako mafisadi wametokea vyama ambavyo havikutegemewa kabisa kwani fisadi ni mtu sio chama. Kwa maana kubwa nasema hivi mchafu wa tabia ni binadamu sio dini yake. Mkandara hapa kam ni jambazi basi nafanya Ujambazi sii kwa sababu mimi ni mkristu au Muislaam ati nilibadili dini nitabadilika...hjapana kinachotakiwa ni mimi kuokoka na kazi kubwa ya jumuiya ni kumweka Lupango Mkandara iwe hata ndugu yangu akipiga simu Polisi nikakamatwa huo ndio uzalendo.

Mafisadi ni WATU, tafsiri nyingine nje ya imani hiyo mimi siikubali pamoja na kwamba naweza kuwa nimekosea sana. Sidhani kama CCM inawafundisha wanachama wake kuubeba Ufisadi ila kuna kundi la watu ndani ya CCM wanaoukumbatia.. na hakuina njia bora zaidi ya kuwakosesha nguvu hawa jamaa ila kuwaondoa ktk madaraka, kesho watajipanga upya wakifahamu sababu iliyowaangusha. Tumeyaona KANU, ZAPU, na vyama vinginevyo vilivyotangulia ktk nchi za jirani.
chama kinaweza kuwa mtambo wa kuzalisha mafisadi hasa hasa pale unapoamua kuangalia sura ya mtu na si sheria inavyotaka-refer Tz na ccm.Kosa kwa Y ni kosa kwa X ni halali
 
Nimejaribu kujiuliza kuwa hawa ndugu zetu ambao wamebatizwa jina la "Makamanda" wa vita ya ufisadi walioko CCM wanachopigania hasa ni nini? Ujumbe wao unaotufanya tusimame nyuma yao na kuwaunga mkono hasa ni kitu gani? Kama kuna mtu ambaye bado ni dhaifu na hajaamua kuchagua upande hawa wapiganaji watamshawishi vipi ili awaunge mkono; wanamuahidi nini?

Ninajiuliza maswali hayo na mengine mengi kwa sababu ukiondoa madai makubwa mawili bado najaribu kutafuta ujumbe wa wapiganaji wetu ili niweze kuelewa kama wana nafasi ya kushinda au watakuwa na athari ya kuvutia mikutano na kuuza magazeti na majina yao kutangaa lakini itakapofika muda wa kura wakajikuta wanatupwa nje ya ulingo.

Zafanana
Kitu kimoja hata hivyo naweza kukisema kwa uhakika zaidi ni kuwa kuna mfanano wa ajabu kati ya wanasiasa watetezi wa mafisadi (makuwadi wa ufisadi) na wale wanasiasa wanaowapinga mafisadi (wapinagaji). Kufanana huku ni muhimu kukuelewa kwani kimsingi kabisa kunafanya wapiganaji wawe na kazi kubwa zaidi ya kuushawishi umma kuhusu lengo na madhumuni yao hasa ni nini.

Wanafanana kwani makundi yote mawili yako kwenye chama kimoja; CCM imekuwa kama tenga lililobeba ndani yake matunda mabivu na matunda ambayo hayajaiva na pamoja na hao matunda wadudu wa kila aina wanaofuata uchafu. Makundi yote mawili yako kwenye tenga moja na hivyo moja linaweza kubeza jingine kuwa halijaiva sana au bado ni bichi au limeoza na lile jingine likalalamika kuwa linaonewa na kuwa kinachofanyika ni "chuki binafsi". Lakini ukweli unabakia hadharani kuwa wote wawili wako kwenye tenga moja.

Wanafanana kwa sababu wote wanagombania nafasi ndani ya chama hicho hicho kimoja. Tumeshuhudia Dodoma wiki chache zilizopita jinsi gani makundi haya mawili yako kwenye muelekeo wa kugongana kusikoepukika. Lakini pamoja na mgongano huo tunaona kuwa makundi yote mawili yanagombania zaidi nafasi zao ndani ya chama. Hadi hivi sasa kundi la watetezi wa watuhumiwa ufisadi linaonekana kuongoza na kupata mashabiki wengi zaidi.

Ni nani kati yao atakayeweza kuwa na nafasi ya kutengeneza wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi hususan kwenye Ubunge ifikapo 2010? Itakuwaje kama kundi la makuwadi litapata kuunga mkono zaidi ndani ya chama na kundi la wapiganaji likajikuta linaungwa mkono zaidi nje ya chama? Jibu ni jepesi; makuwadi watakuwa na wagombea wengi zaidi chamani na hivyo kutuamulia viongozi wetu wajao ni kina nani.

Hata hivyo kufanana ninakozungumzia mimi siyo kufanana kwa aina hiyo. Ni kufanana kwa kile wanachogombania mwakani ni nini hasa. Makundi yote mawili yanagombania kuchaguliwa tena.

Baada ya matukio ya kihistoria ya Februari 2008 yaliyosababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kwa kuhusishwa na kashfa ya Richmond mpasuko mkubwa umetokea ndani ya CCM. Mpasuko ambao hauwezi kuisha kwa vikao, mazungumzo, makubaliano au muafaka wa aina fulani. Mpasuko huu ni mkubwa sana kwani makundi mawili yanayoshindana hayawezi kurudi nyuma hata kidogo kwani kufanya hivyo itakuwa ni sawa na kujitia kitanzi wao wenyewe.

Kundi la watetezi wa Lowassa haliwezi kurudi nyuma kwani hawa wanaamini kabisa kuwa kitendo cha Lowassa kubanwa na kamati teule ya Bunge kilikuwa kimekusudiwa, kupangwa na kufanikishwa na watu mbalimbali miongoni mwao ni Spika wa Bunge la Muungano Bw. Samweli Sitta na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo teule Dr. Harrison Mwakyembe pamoja na wajumbe wengine wa kamati hiyo.

Hivyo kundi hili la Lowassa, mashabiki wake, wanufaika wa utawala wake, mashabiki na marafiki wake wa karibu waliapa toka wakati ule kulipa kisasi na kuhakikisha kuwaangusha wahusika wote na hatimaye kusababisha mchakato mpya utakaomsafisha Lowassa na wenzake na kitendo kile wanachoamini kuwa ni cha "uonevu mkubwa". Kama nilivyodokeza siku chache baada ya matukio yale kundi hili halitokoma mpaka Lowassa atakaposimama tena akiwa safi na akiwa kiongozi. Chini ya hapo hakuna mapatano.

Kundi la kina Mwakyembe linaamini kabisa kuwa lilifanya kazi yake kwa uadilifu na weledi na halikumuonea mtu yeyote na zaidi kuwa wangeweza kufanya makubwa zaidi kama wangetaka. Hawa wamejipanga wakati wowote kumwaga "mchele kwenye kuku wengi" endapo itabidi iwe hivyo hasa pale hatima yao ya kisiasa itakapokuwa mashakani. Kundi hili linaamini kabisa kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ilihusika moja kwa moja na suala la Richmond na kwa hilo hawako tayari kumuomba msamaha mtu yeyote.

Hawa nao mashabiki wao, wapambe wao na wale wanaowaunga mkono hawako tayari kurudi nyuma wala kusalimu amri. Sasa hawa wamepania kabisa kutetea viti vyao vya Ubunge na nafasi zao katika chama.

Hivyo basi tunaweza kuona kuwa pande hizi mbili haziwezi kupatana kwa kadiri ya kwamba kila moja inaamini kuwa iko sahihi katika mtazamo wake wa matukio ya Februari 2008. Hawawezi kukaa meza moja; hawawezi kujadili sera pamoja na kwa hakika kwa upande wao hakuna mapatano yoyote na wale wa utetezi wa kundi la ufisadi isipokuwa ushindi tu.

Ushindi hauji chee
Hapo kwenye ushindi ndio tatizo. Kama nilivyoanisha katika makala zangu kadhaa zilizopita ni kuwa vitani ushindi hauji mezani bila kumlazimisha adui kusalimu amri. Ushindi katika vita unakuja kwa kumzidi adui uwezo na kumuweka kama kwenye kabali hivi na kumlazimisha anyanyue mikono kuomba radhi na kuingia katika meza ya makubaliano ya kusitisha vita kwa kusalimu amri.

Ili upande mmoja ushinde ni lazima uwe na ujumbe, mbinu, na zana na utaalamu wa kutosha kumshinda adui. Nasikitika kusema kuwa upande wa watetezi wa Lowassa na wale wanaowatetea mafisadi (kama wanaomtetea Mkapa) umejipanga vizuri zaidi, ujumbe wake unagusa wanufaika wengi wa ufisadi na kwa hakika wana uwezo na zana za kuwamaliza wapinzani wao.

Ndio maana hapa nimeuliza hawa wapiganaji wetu wao wanaujumbe gani zaidi ya zile mbili tulizozizoea na ambazo ukweli wake unakubalika katika akili za Watanzania wengi? Ni zipi unauliza..?

Kwanza kuna ujumbe kuwa mafisadi wanaeneza fedha na mikakati ya kuwang'oa katika viti vyao vya Ubunge. Hili tumelisikia kwa muda na lina mantiki ndani yake. Kwamba, wale walioathirika wanataka kuwaangusha wale waliowaathiri ni sehemu ya siasa. Ninachokiona ni kuwa watetezi wa ufisadi wanatumia sayansi na sanaa ya siasa kuwaangusha wabaya wao. Katika hili mbinu na njia mbalimbali zitatumika hata zile ambazo ni kinyume cha sheria.

Sasa wapiganaji wetu wamekuwa wakilia na kulalamika juu ya hili. Lakini wataendelea kulia lia huku hadi uchaguzi mkuu utakapofika ili kiwe nini? Sawa mafisadi wanataka kuwaangusha kwenye majimbo ya uchaguzi wao walitarajia nini? Hivi walifikiri baada ya matukio ya Februari wangetumiwa zawadi ya maua na keki kutoka kwa walioangushwa kwa fedheha na aibu?

Wanachofanya makuwadi wa mafisadi si kingine bali kutumia siasa kulipa kisasi na Dodoma ilikuwa ni mwanzo tu. Watapiga tena.

Ujumbe wao wa pili ni kuwa kuna mafisadi na mafisadi ni lazima washindwe. Sasa ukweli wa huu tunaujua kuanzia enzi za kipindi cha "Mikingamo" na matangazo ya "Liangalieni limbukeni hili". Mafisadi wamekuwepi nchini kwa muda mrefu na wamekuwepo ndani ya CCM kwa muda mrefu (na siyo wanne tu kama mmoja alivyotaka tuamini).

Sasa kutuambia kuwa mafisadi wanasambaza fedha na vipeperushi n.k kwenye majimbo katika mbinu ya kuwaangusha wapiganaji kunaweza kutufanya tuwaonee huruma lakini hiyo ni sehemu ya siasa. Kama watetezi waliweza kujipanga vizuri hadi kuweza kuleta hoja nzito dhidi ya Spika kwenye mkutano wa Halmashauri Kuu na kwa kutumia njia za kisiasa basi hatuna budi kukubali kuwa hii ni sehemu ya siasa na makuwadi wa ufisadi wako tayari kutumia mchakato wa kisiasa kutimiza malengo yao.

Pia kutuambia ukweli kuwa ufisadi na mafisadi wapo na wana nguvu na wako tayari kufanya lolote ni ukweli ambao wengi wetu tunaufahamu.

Wananchi wanahitaji na wanastahili zaidi ya jumbe hizo mbilli. Watanzania wanataka kujua hawa wapiganaji zaidi ya kupigana ili kuokoa meli zao kabla ya uchaguzi ni kitu gani kingine ambacho ni kikubwa na wanakipigania ambacho kitawafanya wananchi wawaunge mkono na kuwarudisha Bungeni?

Je, wao wapiganaji wanatumia vipi mchakato wa kisiasa kuwazidi kete makuwadi wa ufisadi? Je wanafanya kila kinachowezekana kuhakikisha kuwa makuwadi wa ufisadi na wenyewe hawarudi Bungeni na kushika nafasi mbalimbali?

Ninaamini katika mvutano huu ni ushindi wa upande mmoja tu utakaosababisha mjadala kuisha ndani ya CCM. Hadi hivi sasa wanaoelekea kushinda ni watetezi wa ufisadi na dakika ni hizi za majeruhi. Je, wale wapiganaji wetu zaidi ya kuhutumia mikutano ya kutupa jumbe zao mbili wana kitu gani zaidi wanachogombania ndani ya CCM na kwenye Taifa ambacho kitatufanya tuamini kuwa kitu hicho ni cha thamani zaidi kuliko fedha na ahadi za makuwadi wa ufisadi?

Ni kitu gani wapiganaji wetu wanagombania hasa ukiondoa wao kuchaguliwa tena kwenye Bunge la 2010?
ACHA WAFU WAZIKE WAFU WAO-Tanzania bila CCM inawezekana!
 
We are all work for the own benefits first, and even if you contribute to other you depending something later and new reset after misevaluate focus beyond the untouchable target. By mayala masuka
 
Mzee Mwanakijiji, hao makamanda dhidi ya ufisadi wamegawanyika makundi mawili, miongoni mwao wamo wanapinga ufisadi kwa sababu wanauchungu wa dhati na umasikini wa Watanzania ambao ufisadi umechangia kuongezeka kwa umasikini na unaendelea kuitafuna nchi na utaendelea kwa miaka kadhaa ijayo.

Kundi la pili ni la wapinga ufisadi wanaopigania nafsi zao, wanahasira kwa sababu nao wanataka share yao kwenye huo mkate na nafasi zikiwakalia vazuri, nao watafisidi vile vile hivyo nawaweka kundi moja na mafisadi tuu.Kwa mtazamo huo kuna makamanda wenye uchungu na makamanda mafisadi.

Swali ni jee ndani ya CCM, wanapigania nini?. Jibu langu la jumla ni kuwa wanapigania nafsi zao just for survival na wakishapata uhakika wa survival baada ya 2010, mtawashuhudia nao wakifisidi ushahidi ni 'time will tell'.

watatumia formular ya 'if you can't beat them, join them' watajiunga nao na wote wakuwa kwenye tenga moja la samaki, na wote watakuwa ndio hao hao.
With 7 days to go, najikumbusha tuu, hili ni bandiko la 2009 kwenye uzi huu wa Mkuu Mzee Mwanakijiji,

Nilisema kuna makamanda wa aina mbili, makamanda wa kweli, wanaopigania taifa lao, na makamanda njaa, wanaopigania nafsi zao, na matumbo yao!.

Hata sisi humu jf, tulikuwa na makamanda wetu, tukiwadhania ni makamanda kweli, na makamanda wapiganaji wa kweli, yaani ni wenzetu, kumbe sii wenzetu bali ni wenzao ambao nao ni makamanda njaa tuu ambao wao pia wanapigania matumbo yao kwa formular ile ile ya 'if you can't beat them, join them!, sasa wamejiunga nao, ni wamoja na lao ni moja!.

Jumapili Njema.
Pasco

 
With 7 days to go, najikumbusha tuu, hili ni bandiko la 2009 kwenye uzi huu wa Mkuu Mzee Mwanakijiji,

Nilisema kuna makamanda wa aina mbili, makamanda wa kweli, wanaopigania taifa lao, na makamanda njaa, wanaopigania nafsi zao, na matumbo yao!.

Hata sisi humu jf, tulikuwa na makamanda wetu, tukiwadhania ni makamanda kweli, na makamanda wapiganaji wa kweli, yaani ni wenzetu, kumbe sii wenzetu bali ni wenzao ambao nao ni makamanda njaa tuu ambao wao pia wanapigania matumbo yao kwa formular ile ile ya 'if you can't beat them, join them!, sasa wamejiunga nao, ni wamoja na lao ni moja!.

Jumapili Njema.
Pasco


Mungu akubariki Pasco jumapili yetu hii imeanza vizuri kwa kuuweka ukweli hadharani, tunakushukura. Ngoja tufanye mengine kwanza kisha tutarudi. Ila nadhani hii itakuwa thread of the day
 
Last edited by a moderator:
Wanapigania matumbo yao maana ikulu ni tyamu sana kwao na wamefadi kwa mika mingi na hawapendi kuachia ndi maana kuna kaul;i za goli la mkono, ushindi ni lazima
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom