Songambele
JF-Expert Member
- Nov 20, 2007
- 4,695
- 2,553
Makamanda dhamira yao haiweleki kisawa sawa na binafsi nawaona wanawoga nikiwalinganisha na Dr. Slaa au Zitto. Hii inatia wasi wasi zaidi ya kushindwa vita ambayo kwa ukweli waasisi ni JF na Dr. Slaa isipokuwa walidandia kwa mbele na kulinda maslahi yao kisiasa zaidi. Mwanzoni ilionekana kama kuzima ushindi wa wapinzani ili ionekane na CCM pia kunawapiganaji.
Inaweza nia yao njema lakini muda hauko upande wao na wanachopigania hakionekani wazi, manake miaka minne imepita hawajakamata wala kutaja Fisadi hata mmoja zaidi ya kuuza magazeti na kulalamika kama wananchi wengine ambao hawana siti mjengoni. Ni vyema wakaamua kutoka katika chama na kuanzisha chama chao au kuungana na vyama vingine nje ya CCM. Vinginevyo wanauza sura tu na hakuna mabadiliko yeyote watakayoleta na majimboni kwao hakuna walichofanya zaidi ya kutafuta huluma kwa kisingizio cha kupingwa na mafisadi.
Inaweza nia yao njema lakini muda hauko upande wao na wanachopigania hakionekani wazi, manake miaka minne imepita hawajakamata wala kutaja Fisadi hata mmoja zaidi ya kuuza magazeti na kulalamika kama wananchi wengine ambao hawana siti mjengoni. Ni vyema wakaamua kutoka katika chama na kuanzisha chama chao au kuungana na vyama vingine nje ya CCM. Vinginevyo wanauza sura tu na hakuna mabadiliko yeyote watakayoleta na majimboni kwao hakuna walichofanya zaidi ya kutafuta huluma kwa kisingizio cha kupingwa na mafisadi.