Wapiga Kura waanza kufumbua macho

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Wananchi watoa masharti kwa wagombea ubunge
Merali Chawe, Mbeya
Daily News; Saturday,January 10, 2009 @20:06​

Baadhi ya wakazi wa Mbeya Vijijini, wamesema Mbunge atakayechaguliwa kuongoza jimbo hilo, anatakiwa kuhakikisha anatatua kero za msingi za wananchi zikiwamo za umeme, maji, barabara na madaraja kabla ya mwaka 2010.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na HabariLeo wakati wa mikutano ya wagombea ubunge wa CCM, CUF na SAU, walisema mgombea atakayeshindwa kutekeleza ahadi zake asijitokeze katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

William Nyomezi alisema kwa muda mrefu sasa wagombea wamekuwa wakitoa ahadi zisizotimizwa na mara baada ya uchaguzi hakuna kiongozi anayeonekana hadi uchaguzi mwingine unapokaribia, hali ambayo inakatisha tamaa wananchi.

Alisema aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Richard Nyaulawa, alijitahidi kutekeleza ahadi zake na kwamba wanaamini kuwa mbunge atakayechaguliwa safari hii, atakuwa na kipimo cha kutekeleza ahadi zake kabla ya mwaka 2010, ili wananchi waweze kumwamini na kumchagua tena.

Eliah Dafwile alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakipewa ahadi za kupewa umeme, maji, barabara na madaraja bila kutekelezwa."Ukizunguka hapa kuna nguzo za umeme zilizowekwa tangu mwaka 1999, lakini hadi sasa ikiwa ni miaka takribani tisa, hakuna umeme," alisema.

Alisema kipimo cha wagombea wa sasa ni jinsi watakavyoweza kutekeleza ahadi zao kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na kwamba atakayeshindwa kutekeleza ahadi zake, asitarajie kuchaguliwa tena katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Wakati huo huo, Mbunge wa Kuteuliwa, Tom Mwang'onda, amewataka wananchi kuchagua mgombea wa CCM, Mchungaji Luckson Mwanjale, kwa kuwa chama hicho ni imara na kwamba ndoa ya ASP na TANU iliyounda chama hicho haijavurugika hadi leo.Alisema vyama vya upinzani vimekosa msimamo ambapo ushirikiano wao unaelekea kuvunjika katika kipindi kifupi na kwamba wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi hawataweza.
 
Wakati huo huo, Mbunge wa Kuteuliwa, Tom Mwang'onda, amewataka wananchi kuchagua mgombea wa CCM, Mchungaji Luckson Mwanjale, kwa kuwa chama hicho ni imara na kwamba ndoa ya ASP na TANU iliyounda chama hicho haijavurugika hadi leo.Alisema vyama vya upinzani vimekosa msimamo ambapo ushirikiano wao unaelekea kuvunjika katika kipindi kifupi na kwamba wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi hawataweza.​


Akishinda mtu wa upinzani, wasahau, ndio Serikali itaweka ngumu. Akishinda wa CCM watadanganywa kuwa kipindi chake kilichobaki cha Ubunge ni muda mfupi, hivyo wapewe tena mwaka 2010 watatue hizo kero.

Mwang'onda anasema muungano wa ASP na TANU haujavunjika, hata CUF ilizaliwa kwa muungano. Ilikuwa chama kilichoongozwa na James Mapalala kiliitwa Chama cha Wananchi na Chama alichokuwa Maalim Seif KAMAHURU (Kamati Huru ya Mageuzi Zanzibar). Hawa jamaa wanaingia siasa hawaangalii historia, halafu wandanganya.​
 
Ndani ya mwaka mmoja mnataka mpate maji,umeme,barabara na madaraja wakati kuna mtu mlimchagua,aliwaahidi na ameshindwa ku deliver ndani ya miaka 9.
kazi kwelikweli!
 
Mwang'onda anasema muungano wa ASP na TANU haujavunjika, hata CUF ilizaliwa kwa muungano. Ilikuwa chama kilichoongozwa na James Mapalala kiliitwa Chama cha Wananchi na Chama alichokuwa Maalim Seif KAMAHURU (Kamati Huru ya Mageuzi Zanzibar). Hawa jamaa wanaingia siasa hawaangalii historia, halafu wandanganya.
Mkuu Mfumwa,hao ndo watoto wa leo(wala si wa jana), hawasomi hao wala hawana background ya kujua mambo muhimu katika Taifa.
 
Jamani hebu kwanza tuangalie nini kinajiri hapa, Magazeti ya Habari Leo, Daily News mmiliki wake nani hasa?, ukiisha jua hilo then connect the dots. Hizi ni Campaign za uchaguzi zikimaanisha kuwa ni chama Tawala pekee chenye uwezo wa kuleta maendeleo na wakichagua wapinzani wameliwa hiyo ndiyo maana halisi ya hii article hapa. Sasa tuchambue kwa kuangalia na upande wa pili wa sarafu. Nafikri nimeeleweka kidogo kama siyo sana.
 
Jamani huyo Tom namuonea sana huruma maana kila aongealo ni pumba tu sijui hana hata mshauri?inaonekana mvivu wa kufikiri...maana huwa hana jipya...kaka ushauri wa bure pendelea sana kusoma vitu mbali mbali upanue uwezo wako finyu....
 
Jamani huyo Tom namuonea sana huruma maana kila aongealo ni pumba tu sijui hana hata mshauri?inaonekana mvivu wa kufikiri...maana huwa hana jipya...kaka ushauri wa bure pendelea sana kusoma vitu mbali mbali upanue uwezo wako finyu....

Ni kweli kabisa mkuu. Huyu kila akifunua mdomo wake tu basi ni pumba za hali ya juu. Bora wamshauri asiseme chochote kile hata ndani ya bunge.
 
Back
Top Bottom