Wapenzi kufatiliana zero distance, hasara kubwa kwa faida ndogo.

Judgement

JF-Expert Member
Nov 13, 2011
10,327
4,779
Wiki moja nyuma, tukiwa tunasafiri, mimi na wenzangu wa5 , (wote wanaume)
safari tuliondoka asubuhi, na mpaka kufikia nyakati za adhuhuri, takriban wa5 kati yetu tulishapokea simu kadhaa za kupigiwa.
Mwenzetu mmoja hakua amepokea hata simu 1 tangia tumeanza safari.
Kwa kifupi ni kwamba mwenzetu huyu usiku wa kulalia safari, mkewe alitoa chip yake jamaa akaiweka kwenye simu yake na chip yake mke akamuwekea mumewe, kwa maksudi ya upelelezi.
Na kweli deal ya shemeji yetu ikazaa matunda kwani msgs mbili zilizotoka kwa No tofauti, ziliingia kwenye chip ya jamaa yetu.
Msg ya kwanza ikimuhimiza jamaa akamalizie kumlipia mtoto fees , na ya pili ikimlalamikia kama kashindwa kuitunza mimba, basi aliyeibeba ataitoa.
Niongeapo hapa mke karudi kwao na kuna kina dalili ya kuvunjika kwa ndoa.
Je?
Hii kufatiliana hapa si kumeleta hasara kubwa kuliko faida ?
Nawaasa wana wa Bodi tuache kuchunguzana kihivi.
 
Aisee hii mpya, l am sure wakaka na wadada humu wataijaribu!

Kwa swali lako, kwa muda sina comment.
 
tabu yote hiyo ya nini? at the end of the day, itasababisha maumivu zaidi kuliko kuleta faida
 
hizi ndo tabia za kike ambazo mimi huwa naziita a kishenzi, unamfuatilia wa nini? simu ya mumeo ya nini kuigusa? mwache aende zake adaiwe ada au hajalea shauri yake wewe songa na maisha yako. tena ukiw jeuri wa aina hii atafanya kwa kificho sana. ila ukiwa weak kumchunguza ndo sasa unayaona hadi ya wazi. Wanaume karibu wote ni wezi wa mapenzi nje ata akulambe mpaka .... lakini kuna pengine napo analamba ukisha jua hilo usitake kujua analamba wapi to hell with whatever business he has

binafsi hata ya kwangu asiguse manake kuna vile vi ofa vya zali vipo tu hivyo sasa asije kutana navyo bure.but ya kwake sitaki hata kuiona nisije pata jaka moyo na kufa mapema umwache yye akivuta raha. Si bora huo muda ungekwenda kutafuta kitu roho inapenda utie mbavuni kuliko kusumbuka na simu yake.
 
Aisee hii mpya, l am sure wakaka na wadada humu wataijaribu!

Kwa swali lako, kwa muda sina comment.

hicho ndio kitu cha kwanza kimenijia kichwani.........
lakini baada ya kuwaza na kuwazua....nimeona hapana......nisifanye hivyo......coz ni kujitakia presha zisizo za lazima.....
ila huyo jamaa yake na Judgement....mmmh....amezidi kucheza rafu......

 
Last edited by a moderator:
Eiyer my love, wea a yu tubadilishane sim card? Yaani ya kwangu SMS zitakazoingia ni mistari ya biblia tu, najua na yako pia!

Kuaminiana kwa waaminifu raha!
 
Last edited by a moderator:
tabu yote hiyo ya nini? at the end of the day, itasababisha maumivu zaidi kuliko kuleta faida

Umeiona eeh ? Alafu Mazee Curtura hua nakukubali sana kwa comments zako pande zile! Ntakustua tukigongana midamida.
 
Eiyer my love, wea a yu tubadilishane sim card? Yaani ya kwangu SMS zitakazoingia ni mistari ya biblia tu, najua na yako pia!

Kuaminiana kwa waaminifu raha!

Hebu jaribuni !
 
Last edited by a moderator:
ni vyema.....
Mke hawezi kutumia mbinu hiyo kama hajaona mabadiliko toka kwa mumewe, mapenzi yamepungua, matunzo yamepungua, sina hela imeongezeka....

Na kitendo cha kumimbisha hao wanawake inaonyesha kuwa mwanaume hajithamini wala hamthamini mkewe na haijali familia yaje ndo maana anacheza peku peku....

Kwa nini upate maradhi kwa starehe ya mtu mwingine?

Heri alivyosepa....
 
hicho ndio kitu cha kwanza kimenijia kichwani.........
lakini baada ya kuwaza na kuwazua....nimeona hapana......nisifanye hivyo......coz ni kujitakia presha zisizo za lazima.....
ila huyo jamaa yake na Judgement....mmmh....amezidi kucheza rafu......


Preta , just try badilishaneni na MC , uuone mziki wake unaimbika ama laa.
 
Last edited by a moderator:
hicho ndio kitu cha kwanza kimenijia kichwani..lakini baada ya kuwaza na kuwazua....nimeona hapana.nisifanye hivyo..coz ni kujitakia presha zisizo za lazima.ila huyo jamaa yake na Judgement....mmmh....amezidi kucheza rafu..

I know, ni ngumu sana. Nimebaki kuwish tu, l wish tungekuwa waaminifu, l wish.... I wish...

Kutendwa kama alivyofanyiwa huyo dada (yaani wanawake wa nje 2 halafu ni peku peku) bora mmama wa watu alivyojua. Na l think, alikuwa anatafuta proof tu. Sidhani kama things zinaenda vizuri angeenda that far!

Kwa upande mwingine, wanasema ukitafuta kosa utalipata kwani ni kama unatumia lens kukagua kama meza imefutwa vizuri. Kama things ziko okay (kwenye relationship) ni vizuri kutochunguza sana!
Njia anayoitumia gfsowin if l got her right, ni badala ya kutafuta mabaya anaconcentrate kwenye mazuri na with the right altitude unaweza mfanya mwenza kuacha/kupunguza mabaya na kuongeza mazuri kwani anakuwa rewarded kwa yale mazuri na sio reprimanded kwa mabaya!

Kazi mnayo, msio na the like of my Eiyer!
 
Last edited by a moderator:
Hili ni tatizo ambalo hufanywa na wake/waume ambao wanadhani wenza zao ni malaika sio bindadamu... hata kama sio cheating pekee, kuna mambo mwenza anaweza akawa anafanya ya kaku shock na kukulaza kitandani kwa pressure! sometimes anaweza akadhani anamkomoa mume kwa kuondoka, kumbe huyo mwanamme alimchoka na that is what he wanted toka kipindi... Sad.
 
I know, ni ngumu sana. Nimebaki kuwish tu, l wish tungekuwa waaminifu, l wish.... I wish...

Kutendwa kama alivyofanyiwa huyo dada (yaani wanawake wa nje 2 halafu ni peku peku) bora mmama wa watu alivyojua. Na l think, alikuwa anatafuta proof tu. Sidhani kama things zinaenda vizuri angeenda that far!

Kwa upande mwingine, wanasema ukitafuta kosa utalipata kwani ni kama unatumia lens kukagua kama meza imefutwa vizuri. Kama things ziko okay (kwenye relationship) ni vizuri kutochunguza sana!
Njia anayoitumia gfsowin if l got her right, ni badala ya kutafuta mabaya anaconcentrate kwenye mazuri na with the right altitude unaweza mfanya mwenza kuacha/kupunguza mabaya na kuongeza mazuri kwani anakuwa rewarded kwa yale mazuri na sio reprimanded kwa mabaya!

Kazi mnayo, msio na the like of my Eiyer!

you are very right Kaunga, binafsi sio mpempenzi sana wa kutafuta makosa ya mtu unless yajionyeshe waziwazi even to ma students, hidden atitudes huwa si deal nazo kabisa ila zile zinazojidhihirisha tu. Ukifanya haya hasa kwenye mahusiano utayaona maisha ni ya kawaida sana but ukianza kutafuta makosa utayakuta na hutoweza kuwithstand.

Yaani mm huwa napenda sana kujipa raha aisee, to the maximum. Sipendi vitu vya kuniumiza moyo. umechelewa kurud home navuta wine yangu taratibu nakula nalala. ukirud utakuta msosi wako nawe kula lala but umetoka wapi saa hizi siulizi utajijua mwenyewe bana this is life. Tena huwaga nasema kabisa ukificha moto kwa gunia lazima moshi utakuumbua tu. so sihitaj kujua utokapo kwani uovu utakao utenda huko ipo siku utafuka mosh tu. Na ikifika hapo pia sitashangaa life is full of alternatives bwana asikwambie mtu.
 
Last edited by a moderator:
hapa inaonesha waz mke ashamchoka mmewe,bas tu alikuwa anatafta uhakika na njia ya kuondoka. na kamchoka kwa tabia alizoziona kwa mumewe na mabadiliko kwan mke hawezi kukurupuka pasipo sababu kufanya hivo. ashaona dalili mbaya ndo mana akaamua kufanya uchunguzi. kha... me ctaki kufa haraka kwa magonjwa kisa mwanaume. cm yake yake na yangu yangu thou me binafsi najiamini hata Saint Ivuga anajua!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom