Wapangaji wa nyumba jagwani wanandaa maandamano ya kumpinga mkuu wa mkoa dar es salaam

Bata batani

JF-Expert Member
Nov 11, 2011
3,182
3,547
Taarifa za kiitelinjisisia nilizozipata jana ya kwamba watu waliokuwa wapangaji nyumba za jagwani wanandaa maandamano ya kupinga tamko la mkuu wa mkoa said mech said ya kwamba waliopanga nyumba hizo
hawatalipwa chochote na wanatakiwa kuhama jagwani bila kulipwa chochote
 
kati ya mali na uhai bora kipi? hawa si binadamu wenzetu wana mapungufu kichwani. walipewa viwanja na Mwinyi na Mkamba wakauza na kukataa kuhama. Kikwete kasema atawapa viwanja bila kujali walioza au ambao hawajawahi kupata. viwanja viko magwe pande bunju.
 
kwa nini nasema hawa hawana akili za kibinadamu kwa sababu sisi watoto wa upanga, osyterbay, kindondoni na viunga vyake tuliokulia karibu na mabonde tumeondoka kwa wazazi wetu na kujenga nje ya mji. Mabonde hayo tuliyaona tangu tukiwa watoto lakini utu wetu ulitambua hatari yake wao kwa nini hata wakipewa viwanja wanauza na kurudi tena huko huko mabondeni?
 
hakuna fungu la hazina ya taifa kwa ajili ya kuwalipa wavunja sheria au bunge lipitishe sheria hiyo ili kutenga fungu kwa ajli hilo. Tumeshihudia wengine wakibomolewa nyumba zao baada ya kujenga kwenye hifadhi ya barabara lakini hawakupata fidia iweje leo fidia inabagua watanzania wanaovunja sheria wengine walipwe na wengine wasilipwe? sheria au utaratibu wenye kubagua ni kinyume cha katiba
 
Tusiwe wepesi wa kutetea maovu ya watanzania wenzetu wanaovunja sheria kwa sababu tu ya kuifanya nchi isitawalike. Makosa ya serikali tutaiambia na makosa ya hawa waliogoma kutoka mabondeni tutawaambia. Hawa walipewa viwanja wakauza bado tutasema serikali haina huruma kwa wananchi.
 
Je, nchi hii ina sheria ya kumjengea nyumba mtu aliyevunja sheria? kama haipo serikali itatumia kanuni ipi kuhalalisha matumizi hayo nje ya bunge?
 
Hao bado hawajajitambua inaonesha wazimu wao kichwani ni mwingi.
Viwanja wamepewa bure lakini hawataki kuhama ujinga huo walionao.
Serikali iwamishe kwa nguvu ndio kilichobakia.
 
Back
Top Bottom