Wanyakyusa, Wachaga na wahaya kuna nini?

Ukweli ni kuwa haya makabila yanabebana sana sana.

Hapa Sikonge, alikuwepo Abeid Katikaza kama MD wa NBC kama sikosei. Hakufanya lolote la maana huku Sikonge na kwa Wanyamwezi kwa ujumla. Baada ya yeye kuuguwa na kuachishwa kazi, ndipo akaingia Nsekela.

Amon Nsekela, aliwabeba Wanyakyusa si kawaida. Kazi zote za ujenzi akawa anapewa baba yake Dr. Mponjoli. NBC ikawa ikihema Kinyakyusa na Kinyakyusa ikawa kama lugha ya Taifa ndani ya NBC. Yule Boss wa Kipare pale Muhimbili na yeye alijaza Wapare kibao pale na siku aliondoka, Wapare walianza kunyanyaswa sana pale. Wachaga nafikiri tatizo lao si kubebana sana kama Wahaya ila wao wakifika sehemu, wanakomba pesa kama hawana akili nzuri. Ona Mramba na watu kama yeye.

Wahaya wengi story ni kama hizo hapo juu. Wakishajazana ofinisi, ndipo zinapoanza "usinigambire Shut up kuru-public lwa watu" yaani hapo itabidi tu ujifunze Kihaya ili uweze kufanya nao kazi.

Wanyamwezi/Wasukuma ni kabila ambalo lilikuwa limelala ila wako wengi sana. Mnyamwezi akishika kazi sehemu, basi Wanyamwezi wengine anawapishia mbali. Anaona hadi kinyaa kukaa nao kuongelea mambo ya kwao au kilugha. Atashirikiana na makabila mengine huku akiwakimbia wa kwake kama ukoma. Muone mtu kama Chenge na usomi wake. Jamaa alikuwa kwenye position ya kuwa hata Rais wa Tanzania ila ndiyo hivyo tena, akaanza KUFISADI na akina Lowassa na ndiyo mwisho wake.

Hili kabila Nyerere alilitakia kila la kheri katika usingizi wake. Usingizi wa hili kabila imekuwa heri ya CCM kwa miaka mingi sana. Tangu waanze kuamka, mabadiliko mengi sana Tanzania yanaanza kuonekana. Kwa sasa ni Mwanza imeamka ikifuatiwa na Shinyanga na nina imani siku Tabora nayo ikiamka, basi patakuwa hapatoshi.

Haya Makabila mengine kama Wachaga na Wanyakyusa, idadi yao si kubwa na hivyo hata kama wamesoma (zamani) kwa sasa hiyo haionekani sana. Sanasana wako mbele kipesa. Wengi wao sasa hivi wanajenga pwani au mbali na mikoa yao. Wanyamwezi/Wasukuma ndiyo kwanza wanaanza kurudi nyumbani maana sasa hivi wamechoka kuishi mbali na kwao wakishazeeka. Mtu kama Jaji Mfwalila ni mmoja ya mifano kuwa alipozeeka, karudi hapa Sikonge.

Kuamka kwa Kabila hili, inaweza kuwa ni habari njema na habari nzuri. Kutokana na ukubwa wake kihistoria, utakuta kuwa siku zote mikoa kama Mara na Bukoba huwa inaingia kwenye kundi hili na pia mkoa wa Rukwa huwa unaingia Tabora na hapo kulifanya hili kundi kuwa kubwa zaidi. Mji wa Mwanza ni kama vile umejengwa na makabila ya hiyo mikoa ya Mara, Mwanza na Bukoba na hii imejenga ushirikiano na ujirani mwema wa makabila ya hao watu.

Wingi wa watu wa mikoa hii Mitano, siku wakiungana, nina wasiwasi itatokea kama inavyotokea nchi kama Senegal ambako kuna kundi moja kubwa sana (Mouride brotherhood -Senegal's richest and most powerful Islamic brotherhood ) ambalo liko well organised na ndiyo wamempeleka jamaa yao hadi akawa Rais.

Kwa mawazo yangu mie, kuna haja ya kuwa na kitu kiitwacho MADARAKA MIKOANI. Hii itafanya hii mikoa iwe ikishindana kwa maendeleo na siyo kama sasa hivi kuwa na Central Government. Kwa hali ilivyo sasa, ni rahisi sana siku moja akaja Mnyamwezi/Msukuma mwenye uwezo wa kuwaunganisha kama Mirambo, na akajenga kundi moja kubwa na lenye nguvu sana Tanzania na hapo kuanza kukandamiza makabila mengine ambayo kwa uchache wake, hawatakuwa na nguvu sana. Hii mikoa kwa kutumia madini yake, inaweza kuwa tajiri na kuanza kutawala wengine kwa nguvu hadi ikapelekea makabila mengine kutaka kujitenga na mwisho vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Ni jambo zuri kuliongelea na kuanza kutafuta solution mapema. Wachina wanasema "jasho jingi wakati wa amani, damu kidogo wakati wa vita". Tusiwe waoga kujadili tipic ngumu maana hali ikibadilika, tunakuwa tumejiandaa na tusiwe kama Mbuni kwa kuficha kichwa kwenye mchanga.

Please: Usiniite mie Mkabila. Maishani nimesaidiwa na watu wa makabila mengi sana na namba moja Wahaya.
Mkoa wa Bukoba uko nchi gani vile? Sikonge umeniangusha kwe..... kweli! kumbe kweli we mtu wa Tabora aiseeeee
 
Mkoa wa Bukoba uko nchi gani vile? Sikonge umeniangusha kwe..... kweli! kumbe kweli we mtu wa Tabora aiseeeee
Msamehe amepata ajali ya kuchanganya mikoa na miji yake mikuu. Kuna watu mikoa yao ni Sumbawanga,Songea, Bukoba, Moshi, Musoma.....
 
sahihisho DOUBLEOSEVEN, hakuna kabila linaloitwa wambulu, but Wairaqw, the cushites of East Africa anakotoka Dr
 
hawakutumikishwa na wakoloni wa kiarabu kwa kuwa ni makabila ya watu makini sana
na wanaojitambua, huku wakijitawala kifikra, vile vile haya makabira hayana dhana
ya ndiyo mzee, hata kwenye ujinga so mwalimu alipata upinzzani sana kutoka
kwa watu wa haya makabila, ukizingatia pia mfano Wanyakyusa walipata muamko
wa elimu mapema sana ukilinganisha na wayao, wamakua, wazaramo, wakwere,
wangindo, n.k

nawasilisha

Kwa kuongezea rejea. miaka ya mwanzo. Ni watu wa makabila gani walikuwa wa kwanza kufukuzwa TANU kwa misimamo yao.
 
Nilisoma kanda ya Ziwa kwa muda fulani na shule niliyosoma ilikuwa inachukuwa wanafunzi kutoka kanda ya ziwa tu. Hivyo nilipata bahati ya kusoma na watu wa makabila ya kutoka Shinyanga, Mwanza, Mara na Kagera. Na vilevile kulikuwa na wanafunzi wachache kutoka mikoa mingine.

Tofauti kubwa kati ya wahaya na watu wa makabila mengine ilikuwa ni income level. Mapato yanayotokana na kahawa yanawasaidia watu kwenda shule vizuri.

Hivyo basi suala la makabila haya kusoma aliingiliani kabisa na Mwarabu, Mjerumani au Mwingereza alitawala wapi. It's pure an economic issue. Huwezi kusomesha watu bila kuwa na engines za maendeleo.
 
Hebu wanaoyafahamu vizuri hayo makabila matatu watumegee sifa zao (nzuri na mbaya) - labda kuna kaukweli katika hiyo theory!
 
Nadhani topic hii karibu ipitwe na wakati. Wengi wa wasichana wa Kichagga, Kihaya na Kinyakyusa wanaolewa nje ya makabila yao na wanazaa WaTz. Wavulana wa makabila haya pia, hasa waliohamia mjini hawabagui.

Fikiria familia za wakubwa, hata wakati wa Nyerere. Wengi wao walizaa WaTz. Kwa hiyo hii topic ni out of date. Sisi ni Watanzania na tunataka tuwe hivyo.
 
Mod naomba uvumilie maana najua kuna vichwa maji wataijadili hii mada kwa mlengo wa ukabila. Lengo langu kujadili fumbo la haya makabila matatu kuonekana ni hatari kuongoza nchi hii,ni kuondoa dhana za kijinga tulizojipandikizia vichwani mwetu.

Watu wengi wanadai kwamba Mwalimu alishawahi kusema haya makabila hayafai kupewa nafasi ya kuwa Rais wa Tanzania. Lakini wengi wao ukiwauliza kuwa Mwalimu aliyasema maneno hayo akiwa wapi wanatangatanga nyikani kutafuta majibu.

Lakini kuna nini cha ajabu kwa makabila haya hadi wenzao wa makabila mengine waaminishwe kwamba ni hatari kuongoza nchi yetu. Ni nini kilitokea hadi haya makabila yawe hatari?

Mbona makabila makubwa ni wasukuma na wanyamwezi lakini hawaogopwi kama makabila haya yanavyoogopwa?


Enzi za mwalimu wasomi walikuwa Kilimanjaro, Mbeya na Kagera kwa ajili ya Seminary zilizojengwa wakati ule.
 
Nadhani topic hii karibu ipitwe na wakati. Wengi wa wasichana wa Kichagga, Kihaya na Kinyakyusa wanaolewa nje ya makabila yao na wanazaa WaTz. Wavulana wa makabila haya pia, hasa waliohamia mjini hawabagui.

Fikiria familia za wakubwa, hata wakati wa Nyerere. Wengi wao walizaa WaTz. Kwa hiyo hii topic ni out of date. Sisi ni Watanzania na tunataka tuwe hivyo.
Nakubali sisi ni watz ila tulio na makabila yetu kama wanyakyusa, wahaya, wachaga nk. Thats the fact.
 
Enzi za mwalimu wasomi walikuwa Kilimanjaro, Mbeya na Kagera kwa ajili ya Seminary zilizojengwa wakati ule.
Mwalimu alikuwa mzanaki wa butyama huko Mara. Yeye alisoma wapi kati ya hiyo mikoa 3??
 
You are vere vere true si unawaona kwenye kile chama chetu? wakwe watoto na pengine 2015 wajukuu watakuwa tayari wamefikisha miaka 18 watapata kula ndani ya chama hehehehe nawapenda sana wachagga zea vere smati.....

Sure very very smart and cooperative to their relatives!
 
haya makabila yalielimika miaka mingi ndo ilikuwa na shule mingi za secondari. Pia ni wa2 wa kuji2ma na wapenda mageuzi.pia wa2 na makabila yaliyozunguka ziwa wana uwezo wa kukaa darasani na kuelewa zaidi kutokana na vyakula bora
 
Hayo makabila yamejaa ubinafsi wa ari ya juu,1wao akiwa mkuu kitengo fulani basi ujue koo zote za kanyigo,katerero,kahongero,kakwizu,kazoba n.k zitalamba ajira eneo nyeti.
Mfano halisi ni ile iliyokuwa NIC ya hayati Mwaikambo,TRA n.k
 
Hao watu ni noma kwa kupendeleana na kubebana!

Hata kama ni kubebana ni katika misingi ya QUALITY sio kubeba tu hata wasiobebeka. Kubebana kupo kote duniani ila hatfumbi macho ili mradi kubaba kama afanyavyo mkwere JK.
 
Hii yote ni dhana ya vivu na kutojituma. kwa MTANZANIA wa kawaida hata haki yake ya msingi haijui, so lazima aliye na elimu lazima mazingira yajengwe watu waogope kumbuka wengi walioko na madaraka ni vihiyo vyeti vingi visivyo na reference na wengine wametuzwa na vyuo ambavyo credibility zake lazima utie shaka.
hii ni zana tu iliyo jengwa ya vihiyo wetu wa KIDUMU.
 
Ukiangalia maendeleo Tz kwa ujumla utaona hawa jamaa ndi wameendelea zaidi katika kila nyanja,pamoja na elimu hawa jamaa ni wachapa kazi wa kweli hawana mchezo na maisha.
 
Ukweli ni kwamba hawa jamaa wameenda vidato ile mbaya na isitoshe hakuna ubishi hao jamaa ni wakabila wa kutupwa sasa wakipewa nafasi kubwa wataharibu maana watabebana ile mbaya.
 
Ukweli ni kwamba hawa jamaa wameenda vidato ile mbaya na isitoshe hakuna ubishi hao jamaa ni wakabila wa kutupwa sasa wakipewa nafasi kubwa wataharibu maana watabebana ile mbaya.
 
Hiyo ni FOMOFOBIA, Hata mie huwa nausikia huu usemi na nimechunguza ila cjajua Mwalimu alisema wakati gani na akiwa wapi na alikuwa na maana gani. Vinginevyo naona ukabila wa CCM kama ulianzia kwa muhasisi wao tangu enzi na enzi. Otherwise makabila hayo ndio ukombozi wa Tanzania ya kesho maana wapo gado na ahakuna wanachohitaji zaidi ya maendeleo ya kweli. Ulikuwa woga wa mwalimu baada ya kukuta wapo waliosoma zaidi yake wakati ametoka Makerere akawa anadanganya yeye ndio Mtanzania wa kwanza mwenye Masters. Ipo siku ukweli utajidhihirisha
 
Back
Top Bottom