Kimbweka
JF-Expert Member
- Jul 16, 2009
- 8,597
- 1,683
Mtu mwenye nguvu kuliko watu wote katika historia ya dunia alikuwa Samson, kama ingekuwa leo basi Samson angeitwa John Cena n.k
Kama ni masumbwi basi Samson angebeba mikanda yote ya World Boxing Association (WBA) au World Boxing Council (WBC) au World Boxing Federation (WBF) au World Boxing Organization (WBO).
Hakuna cha akina Tyson wala Evander Holyfield au Wladimir Klitschko wote wangedundwa sekunde chache tu baada ya pambano kuanza.
Samson alikuwa shujaa (hero) kwa taifa la Israel, aliweza kuua simba kwa mikono mitupu, maelfu ya watu mikono mitupu pia na hata mageti ya vyuma yalishindwa kumfungia kwani aliyavunja bila huruma.
Samson alikuwa na ugonjwa na mabinti wa kifilisti (aliwapenda sana ingawa alionywa na kwake ikawa sikio lisiosikia...)
Mara ya kwanza alioana binti ambaye Biblia haimtaji jina na wengi huhisi hii ilikuwa ni Sababu tosha kwa Samsoni kuanzisha vita na wafilisti, ndoa haikudumu ilivurugika siku ya harusi hata hivyo Samson akampata mrembo mwingine kutoka kwa wafilisti, Delila ambaye hata hivyo wafilisti walimrubuni atafute siri ya nguvu za Samson.
Hata hivyo mke wa Samson yaani Delila alikuwa na nguvu kuliko Samson kama huamini subiri!
Huyu mwanamke alimaliza historia ya Samson na Samson akatoboa siri ya nguvu zake baada ya kuwekwa kufuani kwa Delila na matokeo yake akatobolewa macho na jina la kumchezea kama mdoli na kumpa kazi ngumu.
Habari hii inatuelimisha au kutukumbusha kwamba uwezo alionao mwanamke kwa mume wake ni mkubwa ajabu na anaweza kufanya lolote anataka akijua jinsi ya kuchezesha kalata zake hasa kwa kujua mume wake udhaifu wake upo wapi.
Wanawake wote wanauwezo mkubwa sana juu ya wanaume tatizo kubwa wanawake wengi wameshindwa kutumia uwezo wao, ushawishi wao kuhakikisha mume anamuweka sawa au kufanya vile anapenda kwa sababu hawajajifahamu.
Hapa ninazungumzia kufanya yale ambayo mwanaume anaamini mume wake anazembea kama vile kuiweka ndoa katika mstari sahihi.
Ni kawaida kuwa na Generals, au Governors au Rais au mawaziri wanaume hata hivyo wengi wao hujikuta wake zao wakiwa chimbuko la uongozi wao na kwamba huwa wanawasaidia kutoa maamuzi ya mambo mengi.
Kuna usemi kwamba:
A mans wife has more power over him than the state
Hata binadamu wa kwanza pale katika Bustani ya Eden alianguka baada ya shetani kumtumia Eva (mwanamke) kwa kumdanganya kula matunda na hatimaye amshawishi mume wake naye ale kwani alijua angemtumia mume ingekuwa ngumu sana mume kumshawishi mke akubali badala yake aliona mwanamke ni rahisi kumshawishi mume na akakubali.
Bottom line ni kwamba mwanamke anao uwezo mkubwa sana katika kuvumbua kile kilichomo ndani ya mume wake na kwamba mwanamke akitumia uwezo wake ambao Mungu amempa kuhusu mume basi anaweza kujenga mahusiano na ndoa imara na inayoridhisha.
Wapo wanawake kila kukicha ni kulalamika tu kwamba mume wangu mume wangu, acha kulalamika tumia uwezo wako wa kuwa mwanamke kumsaidia mume kuwa mume bora katika ndoa kwani Mungu amekupa uwezo wa ajabu ndani yako kiasi kwamba mume yeyote anaweza kumkubali kile mke anasema pale mke akitumia uwezo wake sawa na Mungu alivyompa Adam bustani yake akaikana.Mungu wake likatukanwa.
Delila alitumia uwezo wake kama mwanamke kumshawishi Samson atoboe siri ya nguvu zake ambayo ilikuwa ni nywele zake kutonyolewa tangu utoto wake.
Baada ya kutoboa siri tu wafilisti wakamshika, wakamtesa na wakamtoboa macho.
AMEN.......................
Kama ni masumbwi basi Samson angebeba mikanda yote ya World Boxing Association (WBA) au World Boxing Council (WBC) au World Boxing Federation (WBF) au World Boxing Organization (WBO).
Hakuna cha akina Tyson wala Evander Holyfield au Wladimir Klitschko wote wangedundwa sekunde chache tu baada ya pambano kuanza.
Samson alikuwa shujaa (hero) kwa taifa la Israel, aliweza kuua simba kwa mikono mitupu, maelfu ya watu mikono mitupu pia na hata mageti ya vyuma yalishindwa kumfungia kwani aliyavunja bila huruma.
Samson alikuwa na ugonjwa na mabinti wa kifilisti (aliwapenda sana ingawa alionywa na kwake ikawa sikio lisiosikia...)
Mara ya kwanza alioana binti ambaye Biblia haimtaji jina na wengi huhisi hii ilikuwa ni Sababu tosha kwa Samsoni kuanzisha vita na wafilisti, ndoa haikudumu ilivurugika siku ya harusi hata hivyo Samson akampata mrembo mwingine kutoka kwa wafilisti, Delila ambaye hata hivyo wafilisti walimrubuni atafute siri ya nguvu za Samson.
Hata hivyo mke wa Samson yaani Delila alikuwa na nguvu kuliko Samson kama huamini subiri!
Huyu mwanamke alimaliza historia ya Samson na Samson akatoboa siri ya nguvu zake baada ya kuwekwa kufuani kwa Delila na matokeo yake akatobolewa macho na jina la kumchezea kama mdoli na kumpa kazi ngumu.
Habari hii inatuelimisha au kutukumbusha kwamba uwezo alionao mwanamke kwa mume wake ni mkubwa ajabu na anaweza kufanya lolote anataka akijua jinsi ya kuchezesha kalata zake hasa kwa kujua mume wake udhaifu wake upo wapi.
Wanawake wote wanauwezo mkubwa sana juu ya wanaume tatizo kubwa wanawake wengi wameshindwa kutumia uwezo wao, ushawishi wao kuhakikisha mume anamuweka sawa au kufanya vile anapenda kwa sababu hawajajifahamu.
Hapa ninazungumzia kufanya yale ambayo mwanaume anaamini mume wake anazembea kama vile kuiweka ndoa katika mstari sahihi.
Ni kawaida kuwa na Generals, au Governors au Rais au mawaziri wanaume hata hivyo wengi wao hujikuta wake zao wakiwa chimbuko la uongozi wao na kwamba huwa wanawasaidia kutoa maamuzi ya mambo mengi.
Kuna usemi kwamba:
A mans wife has more power over him than the state
Hata binadamu wa kwanza pale katika Bustani ya Eden alianguka baada ya shetani kumtumia Eva (mwanamke) kwa kumdanganya kula matunda na hatimaye amshawishi mume wake naye ale kwani alijua angemtumia mume ingekuwa ngumu sana mume kumshawishi mke akubali badala yake aliona mwanamke ni rahisi kumshawishi mume na akakubali.
Bottom line ni kwamba mwanamke anao uwezo mkubwa sana katika kuvumbua kile kilichomo ndani ya mume wake na kwamba mwanamke akitumia uwezo wake ambao Mungu amempa kuhusu mume basi anaweza kujenga mahusiano na ndoa imara na inayoridhisha.
Wapo wanawake kila kukicha ni kulalamika tu kwamba mume wangu mume wangu, acha kulalamika tumia uwezo wako wa kuwa mwanamke kumsaidia mume kuwa mume bora katika ndoa kwani Mungu amekupa uwezo wa ajabu ndani yako kiasi kwamba mume yeyote anaweza kumkubali kile mke anasema pale mke akitumia uwezo wake sawa na Mungu alivyompa Adam bustani yake akaikana.Mungu wake likatukanwa.
Delila alitumia uwezo wake kama mwanamke kumshawishi Samson atoboe siri ya nguvu zake ambayo ilikuwa ni nywele zake kutonyolewa tangu utoto wake.
Baada ya kutoboa siri tu wafilisti wakamshika, wakamtesa na wakamtoboa macho.
AMEN.......................