Arusha Leo
Senior Member
- Mar 12, 2012
- 122
- 72
ZAIDI ya akinamama 300 kutoka jamii ya kifugaji katika kijiji cha Nadosoito kusini,kata ya Terat katika halmashauri ya jiji la Arusha,wameandamana katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha ,Magesa Mulongo wakiwalalamikia viongozi wao kushindwa kutatua kero mbalimbali zinazowakabili, likiwemo tatizo kubwa la uhaba wa maji ambalo ni la muda mrefu kijijini hapo,wakidai viongozi wa mkoa wameitenga kata yao kwani hata mbunge wao hawamfahamu.