MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Wakiwa wamechoshwa na hali ya umasikini, ufisadi na wanasiasa wasiowajibika, na hasa kutokana na barabara mbovu isiyopitika, wanawake wa kijiji cha Barbacoas, Colombia, wameamua kuanzisha mgomo waliouita wa "Kubana miguu", wakimaanisha hawatashiriki katika ngono na waume/wanaume wao mpaka hapo barabara ya kijijini hapo itakapotengenezwa. "Hakuna barabara, hakuna mwanamke atakayepanua miguu yake" wamesisitiza wanamama hao wa Barbacoas. Baada ya siku tano tangu kuanza kwa mgomo huo, wanaume wamejibu mapigo kwa kutanganza mgomo wa kutokula. Nani ataibuka mshindi?
Chanzo: No Road, No Sex, Women Tell Town; Men Respond with Hunger Strike - Fox News Latino
Chanzo: No Road, No Sex, Women Tell Town; Men Respond with Hunger Strike - Fox News Latino