wanajifanya walemavu baada ya ndoa kila kitu wafanyiwe
Last edited by a moderator:
Hivi nyie wanaume kwanini mnafanana lakini??!??!!!!????!!!!mna maudhiiii, kwanza muache kuchanganya kitu kinaitwa WAJIBU na HIARI ndio tutaelewana.............hapo kwenye red huo sio WAJIBU wa mwanamke bali ni mapenzi/hiari ya huyo mwanamke kufanya hayo uliyoyataja na pengine kufanya zaidi ya hayo.
Niliwahi kuambiwa hivi we mwanamke kwanini leo hujanifulia boxers zangu unafikiri nilikutolea mahari ya nini???!!!!hivi kweli unafikiri mimi nitakua na moyo wa kuendelea kufanya hivyo tena wakati nilikua nafanya kwa mapenzi na sio lazima!!!!!
nyumba kubwa nimeshaitolea ufafanuzi hoja hiyo na pia nikaweka swali ambalo hadi sasa wanawake wanalikwepa kulijibu....Hata mi nimeshindwa kuelewa wajibu wa mwanamke wa dunia hii tunayoishi ni upi?? Mambo mengi yanafanywa kwa hiari ndo maana mke wako anachokufanyia si anachofanyiwa rafiki yako na mkewe. Sina nia ya kupinga tu lakini nasema ukweli wangu wajibu wangu siujuhi; tunafanya mambo kwa kushirikiana. Wakati mwingine mbona hubby ananiletea chai kitandani. Lol. Nao ni wajibu wake? Si amejisikia tu kunifurahisha.
The Boss hapa kinachobishaniwa ni neno linalowakilisha kile mke anachomfanyia mume kama sehemu ya kukamilisha madhumuni ya kuolewa kwake............... Ili kukata mzizi wa fitna tukubali kuwa ni hiyari yao kutekeleza majukumu hayo, lakini ikumbukwe kwamba hiyari si utumwa hivyo hiyari hiyo haiwezi kulazimishwa. lakini ikumbukwe kwamba mwanaume yeyote rijali amefundishwa kwamba ndiye mwenye wajibu wa kutunza familia na ndivyo ilivyo........
Swali: Kwa nini kwa mume iwe ni wajibu na kwa mke ni hiyari?
kwa hiyo mke hana 'wajibu wowote' kwa mume?
ni hiyari?
na mme nae ana wajibu au hiyari kwa mke?
kwa hiyo mke hana 'wajibu wowote' kwa mume?
ni hiyari?
na mme nae ana wajibu au hiyari kwa mke?
Mke anao wajibu ndani ya ndoa kama ilivyo kwa mume! Mapenzi yana uwajibikaji, hata kitandani kila mmoja atatakiwa kutimiza wajibu wake ndo iwe kwenye mambo mengine? Wajibu upo tu, na kama we mwanamke unadhani huna wajibu ndani ya ndoa then jiandae kusikia mumeo ana mwanamke anaejua wajibu wake na ndiye nyumba ndogo. We unafuga ng'ombe na kuku mwenzio anafunguliwa duka la sonara na botique! Kama hujui wajibu wako then huna sababu ya kuitwa mke, endelea kufanya hiari, wapo wanaojua nini cha kufanya katika mapenzi. Its like my wife, nimeweka utaratibu ambao umekuwa ni wajibu kwani ni lazima nimpigie mchana kumuuliza kama amekula lunch au nimfate ofcn tukale wote, jioni nampitia kurudi home hata kama nitarudi kwenye vikao vya bia na at least niwaone watoto, ni kwamba umekuwa ni utaratibu uliojengeka kuwa wajibu. Kama ulishakuwa unamfulia, unampikia kwani unataka kusema nae hakuna anavyotimiza kama mume? Wanawake wa siku hizi mzee wangu anasemaga vijana wa kiume tunakazi sana wakati wa kuchagua wa kuoa ndo maana vijana siku hizi wanaoa akiwa 30 -35! What a shame! Its true that NO WOMAN NO CRY!
itafikia mahali watu watakuwa wanatazamana tu usoni ndani ya nyumba - hakuna msosi, hakuna ada ya watoto, hakuna medical expenses, hakuna kupika, hakuna usafi, hakuna kuulizana kwa sababu kila kitu kinafanywa kwa hiari na hakuna anayewajibika ....
That is very true! Uwajibikaji katika mapenzi ni jambo la lazima. Usione mwanaume anahangaika kujiongezea kipato ili atunze familia, ule ni uwajibikaji. Ndo maana mwanamke akipata mwanaume asiejua nini maana ya kuwa baba ndani ya ndoa hukimbia ndoa. Mwanamke anaedhani akimfulia mwanaume ni utumwa angali mumewe huangaika kujituma kuleta mahitaji ya nyumbani, kusomesha wadogo zake, kuwatibu wazazi wa mke, michango mikubwa ya harusi na msiba wa mke then kupika uone ni hiyari! Hakuna ndoa siku hizi, hakuna wanawake, no wonder wanawake wa siku hizi mnataka kujifungua kwa operesheni kwa kuwa hata kuzaa ni hiari na si wajibu! Heri mama yangu alifariki kabla ya kushuhudia wanawake wa siku hizi wanaodhani kumpigia pasi nguo mumeo ni utumwa, hana wajibu ila mume ana wajibu wa kwenda supermarket kumletea sausages na baked beans! No wonder mnanenepeana sana na vitambi vya bia kama masanamu ya michelini na michirizi ya mikorogo na manywele feki hata hazikui kwa uvivu kila kitu afanye HOUSE MAID!
Hapo kwenye bold ningekupa credit kama ungefanya kwa hiari na si wajibu (ambao ni sawa na amri). Mi mwanaume anayenipigia simu kuniuliza kama nimekula in the name of responsibility not love ni sawa na asingepiga tu. I can imagine sauti ya anayepiga simu kwa sababu ni lazima apige. Lol.
baba hapa umeuwaaa.....That is very true! Uwajibikaji katika mapenzi ni jambo la lazima. Usione mwanaume anahangaika kujiongezea kipato ili atunze familia, ule ni uwajibikaji. Ndo maana mwanamke akipata mwanaume asiejua nini maana ya kuwa baba ndani ya ndoa hukimbia ndoa. Mwanamke anaedhani akimfulia mwanaume ni utumwa angali mumewe huangaika kujituma kuleta mahitaji ya nyumbani, kusomesha wadogo zake, kuwatibu wazazi wa mke, michango mikubwa ya harusi na msiba wa mke then kupika uone ni hiyari! Hakuna ndoa siku hizi, hakuna wanawake, no wonder wanawake wa siku hizi mnataka kujifungua kwa operesheni kwa kuwa hata kuzaa ni hiari na si wajibu! Heri mama yangu alifariki kabla ya kushuhudia wanawake wa siku hizi wanaodhani kumpigia pasi nguo mumeo ni utumwa, hana wajibu ila mume ana wajibu wa kwenda supermarket kumletea sausages na baked beans! No wonder mnanenepeana sana na vitambi vya bia kama masanamu ya michelini na michirizi ya mikorogo na manywele feki hata hazikui kwa uvivu kila kitu afanye HOUSE MAID!
nyumba kubwa acha awape vidonge vyenu, nimesoma wadada na wamama wengi hapa walikuwa wanawashambulia wanaume wakati mtoa mada alitaka ufafanuzi wenuTaratibu, maana naona umekariri; wengine mamodo humu. Lol. Nikirudi kwenye uzi wako wa hapo juu; ungekuwa unampenda mkeo usingeandika uliyoandika kwenye bold. Maana sidhani kama una refer kwa mke wa jirani na kumuita michelini na maandishi mengine yenye kila dalili za hasira, ni obvious una m-describe mkeo.
wapo wanaokuwa wapole na wanatimiza wajibu wao bila taabu
lakini dah.....revenge yake iko kwa kukutafutia vidumu tu
so bora wanaogoma na kununa
angalau utajua 'now kakasirika umbembeleze'
Taratibu, maana naona umekariri; wengine mamodo humu. Lol. Nikirudi kwenye uzi wako wa hapo juu; ungekuwa unampenda mkeo usingeandika uliyoandika kwenye bold. Maana sidhani kama una refer kwa mke wa jirani na kumuita michelini na maandishi mengine yenye kila dalili za hasira, ni obvious una m-describe mkeo.
nyumba kubwa acha awape vidonge vyenu, nimesoma wadada na wamama wengi hapa walikuwa wanawashambulia wanaume wakati mtoa mada alitaka ufafanuzi wenu
Najua kuna vimodo bana, na mke wangu sio kimodo wala si michelini, anajua ana wajibu wake. Namshukuru mungu anajua uwajibikaji kwenye ndoa. Hawezi kuacha kunichagulia suit ya kuvaa ninapoenda ofisini, na hajawahi kuacha wajibu wake kwangu na mtoto wetu hata tukiwa tumetofautiana kamwe sijaliona hili toka mwaka 2008 tulipoamua kuwa mwili mmoja. Jitahidi uwajibike mama utabaki kusema we ndiye nyumba kubwa wakati wenzio wanakusaidia majukumu. kalagabaho!