Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Picha hii haihusiani na habari hii
Hivi inakuwaje?
Baadhi ya wanawake wanapowafanyia waume au wapenzi wao jambo zuri, hufanya hivyo huku wakihesabu na kutarajia wapenzi hao waone, watambue na pengine baadae kuwalipa kwa njia nyingine.
Kwa mfano.
Mke ana kawaida ya kumuwekea mume au mpenzi wake maji ya kuoga bafuni, anamwandalia chakula vizuri, anamnyooshea nguo zake au anazikagua nguo zake kwa umakini na kuzirekebisha pale zinapokuwa na kasoro na mengine yanayofanana na hayo. Badala ya kuchukulia au kujua kwamba huo ni wajibu wake, hufanya hivyo kama deni.
Mume anapomkosea, mke huacha kufanya au kumfanyia mumewe mambo hayo kwa maelezo kwamba, haoni sababu ya kufanya hivyo kwa sababu mumewe hana shukurani…………..
Nimekuwa nikisikia malalamiko mengi kutoka kwa baadhi ya wanaume wenzangu wakilalamikia jambo hili, na wanadai kwamba kwa upande wao hata wanapoudhiwa na wake zao kamwe hawasitishi utaratibu wao wa kuacha kodi ya meza lakini wanawake zao huwasulubu kweli kweli wanapoawakosea.
Hebu fungukeni hapa ili tujue namna nzuri ya kuwa-handle…………………