Wanawake na kupenda wanaume wenye hela...

Tatizo kubwa linalotukabili wanaume wengi ni kumtambua mwanamke anayekupenda kwa dhati ya moyo wake.

Kuna wanawake wamefuzu chuo cha sanaa, yaani wanajua kujivika ngozi za kondoo huwezi amini, anakuwa mpoleee lakini akitaka kuvuna anajua tu atakukamatia wapi. wanawake wako tayari kuficha tabia zao halisi hata kwa miaka kadhaa ilimuradi watimize malengo. mwingine atakupeleka mpaka utamuoa akijua kwamba kwakuwa umemuoa basi utakuwa umeridhika kwamba anakupenda. Akishatimiza malengo yake hapo sasa anaanza kuchomoa makucha yake.

Kuna jamaa yangu alipatwa na huo mkasa kaoa mwanamke baadae mwanamke kaanza kuzimikia masharobaro wa mjini wanaopata hela kwa msimu na magari ya kuazima akaacha ndoa yake baada ya masharobaro kumtumia vya kutosha wakaachana nae na huku aliishaachana na mumewe kisa hana hela na wala hajamnunulia gari bahati nzuri jamaa akapata kazi nzuri na akawa anawasaidia ndugu wa mwanamke bila kinyongo na bila mwanamke kujua.

Ndugu wa huyo mwanamke wakawa wanamlaumu kweli huyo mwanamke siku ya siku mwanamke anaenda kuomba kazi hiyo sehemu anakuta mtu ambaye anapswa kumfanyia interview ni the same X-Husband alipata mshtuko sana kiasi kwamba alishindwa kuamini nafikiri interview yenyewe hakufanya kutokana na aibu
 
asante michell natamani wangeelewa ..... ingesaidia sana wale ambao ni waaminifu kwenye hilo kuaminika. wanaume inabidi wabadili mitazamo na kujua kuna wanawake wapo kwa penzi la dhati na si mifuko yao hii huwafanya nao kupoteza muelekeo na kukosa penzi la kweli walinalo dada zetu waaminifu

Asante kwa mawazo yako.....naona ume-generalize sana kuwa ni mazungumzo yote ya wadada yanaelekea kuchuna tu....labda unaozungumza nao....wengi siku hizi wameamka,ni wachache sana wanakalisha makalio kusubiri wanaume wa kuchuna na hata kupata mwenye hela ni matokeo pia....anaweza asije ukapata asiye nazo..... ni vizuri kujitegemea na kufanya kazi kwa bidii kwa wale ambao hawafanyi hivyo......

Wanaume wanapaswa kujua si kila mwanamke anawapendea hela zako,wengi wamejiwekea kuwa wanapendewa hela zao hata kama ninachopenda ni utu wako na ulivyo...wajiamini,wachukue muda kuangalia kama mapenzi ni genuine si kukaa na kusema tunawapendea hela...na wao pia wawe na bidii hakuna anayetaka mzigo wa mume na baba watoto....
 
michelle nikiangalia avatar yako najihisi kuogopa kwa mbali manake kuna mahala tutatofautiana.
 
Siku hizi naona kupewa gari na wanaume imekuwa issue kubwa.......kiasi kwamba kuna wakati hoja inajadiliwa mtu labda ana tatizo...mtu anaweka comment za ajabu kwamba wasichana wa siku hizi mnafuata hela na mnadanganywa na magari sijui nyumba na vitu kama hivyo.........ndo maana mnateseka............Au mtu umepata mwanaume mwenye uwezo watu wanakukatisha tamaa,mara hawajatulia,atakudharau mara sijui nini.......

Na wasichana tumekuwa tukijaribu kubisha hilo au kusema si wote.........

Nafikiri wote tunapenda maisha mazuri,hayaletwi na hela bali hela ni sehemu tu ya kuwa na maisha bora na yenye furaha.....

Nikiangalia dunia ya sasa,na hasa jamii inayonizunguka siioni tofauti ya kimatendo na kimaadili ya mwanaume mwenye hela na maskini......wanaume asilimia kubwa ni waongo na wanatoka nje ya ndoa na wengine wanashindwa hata kutimiza wajibu wao kama baba na kama mume.........mimi siamini kwamba ukiwa na hela kiasi au usipokuwa nazo inakufanya wewe uwe mwema sana au mwenye upendo wa kweli....

Nafikiri maisha ni kuchagua na bahati, mwanamke ukipata mwanaume mwenye hela nyingi manake hata mwenye mia mbili atasema anazo.... kama UNAMPENDA, mchunguze, chukua muda tafuta ufahamu wa kile anachokifanya kumpatia kipato...... ukimuona anakufaa nenda,ishi maisha yako,Sali,lea watoto wako na kuwa mvumilivu,zaidi jitahidi kuwa wa manufaa kwa jamii yako na wenye shida.

Ukiwezeshwa nawe kaza buti,jijenge,fanya kazi usiwe tegemezi.......na zaidi kuwa msaada kwa mumeo na furaha yake ili aendelee kufanikiwa zaidi na zaidi mkumbushe kuwasaidia wasio na uwezo.

.............................Pole sana Dada Michelle,
 
Kuna jamaa yangu alipatwa na huo mkasa kaoa mwanamke baadae mwanamke kaanza kuzimikia masharobaro wa mjini wanaopata hela kwa msimu na magari ya kuazima akaacha ndoa yake baada ya masharobaro kumtumia vya kutosha wakaachana nae na huku aliishaachana na mumewe kisa hana hela na wala hajamnunulia gari bahati nzuri jamaa akapata kazi nzuri na akawa anawasaidia ndugu wa mwanamke bila kinyongo na bila mwanamke kujua.

Ndugu wa huyo mwanamke wakawa wanamlaumu kweli huyo mwanamke siku ya siku mwanamke anaenda kuomba kazi hiyo sehemu anakuta mtu ambaye anapswa kumfanyia interview ni the same X-Husband alipata mshtuko sana kiasi kwamba alishindwa kuamini nafikiri interview yenyewe hakufanya kutokana na aibu

Tamaa mbaya kaka,siku zote tenda wema na timiza wajibu wako.....malipo ni hapa hapa huyo kaka alitimiza wajibu kadri ya uwezo wake, dada ahkuona...sasa ataishi maisha ya kujutia mpaka basi,ndo tunaambiwa tujifunze kutafuta zetu na kuwa msaada kwa waume zetu wafanikiwe lakini haya ya kufuata ving'aavyo ndo maana wadada wengi tunaumizwa vibaya.......
 
Ahsante michelle.
Watu hawajui hata hao wanaume wenye hela, hela zao hazina raha kama hawatapata wapenzi wenye kuwajali na kuwapenda.
Dharau ni tabia ya mtu tu. Wangapi hawana hela ila wana dharau na mashauzi kibao.
 
michelle nikiangalia avatar yako najihisi kuogopa kwa mbali manake kuna mahala tutatofautiana.

Marytina nishakuambia mimi napenda challenge,ningekuwa naziogopa singeweka hii thread hapa.....nitafurahi na kuzidi kukupenda ukitofautiana na mimi.....ndo kuwa great thinker huko......please.....
 
Hata tusijidanganye, Pamoja na yote money ni kila kitu.
Binafsi mbali na vigezo vingine, mwanaume anaponitokea ni lazma pia niangalie na status yake kiuchumi.
Mapenzi bila pesa mh! is nothing.
 
.............................Pole sana Dada Michelle,

Asante Mwenzetu,kudanganywa ni sehemu ya maisha ya mwanamke na mwanaume....tunasamehe,kuchukua hatua,tunasonga mbele tukiwa makini zaidi na kumuomba Mungu.....am a better person kwa kuwa nimedanganywa na nikajifunza mengi......
 
Kuna jamaa yangu alipatwa na huo mkasa kaoa mwanamke baadae mwanamke kaanza kuzimikia masharobaro wa mjini wanaopata hela kwa msimu na magari ya kuazima akaacha ndoa yake baada ya masharobaro kumtumia vya kutosha wakaachana nae na huku aliishaachana na mumewe kisa hana hela na wala hajamnunulia gari bahati nzuri jamaa akapata kazi nzuri na akawa anawasaidia ndugu wa mwanamke bila kinyongo na bila mwanamke kujua.

Ndugu wa huyo mwanamke wakawa wanamlaumu kweli huyo mwanamke siku ya siku mwanamke anaenda kuomba kazi hiyo sehemu anakuta mtu ambaye anapswa kumfanyia interview ni the same X-Husband alipata mshtuko sana kiasi kwamba alishindwa kuamini nafikiri interview yenyewe hakufanya kutokana na aibu

wanawake wa design hiyo ndio wengi siku hizi.
wanatafuta short cuts, hawataki kuumiza vichwa wala kusumbua akili zao.
we chukulia mfano wasichana wanaosoma vyuo vikuu siku hizi, pamoja na elimu zao lakini wengi wao ndio hopeless kabisa.
Kuna mmoja tulisoma nae tena mke wa mtu, alifunga ndoa tukiwa bado chuoni, lakini huwezi kutamani kuoa kwa mambo anayofanya.
Mme wake akija chuoni kumsalimia, watu wanamsikitikia lakini hawawezi kumwambia.
 
Ahsante michelle.
Watu hawajui hata hao wanaume wenye hela, hela zao hazina raha kama hawatapata wapenzi wenye kuwajali na kuwapenda.
Dharau ni tabia ya mtu tu. Wangapi hawana hela ila wana dharau na mashauzi kibao.

Asante mamii,nao pia ni binadamu wenye mapungufu na wanastahili kupendwa kama wanaume wengine......hilo la dharau,kuna wanaume jamani......niishie hapo kwa sasa......l.o.l
 
Hata tusijidanganye, Pamoja na yote money ni kila kitu.
Binafsi mbali na vigezo vingine, mwanaume anaponitokea ni lazma pia niangalie na status yake kiuchumi.
Mapenzi bila pesa mh! is nothing.

Usipompata mwenye hela utafanyeje???
 
hivi jaman tuwe wakweli tuache dead theories, hapa mjini hamna shamba la kulima mihogo na ndizi shamba ni ATM, hata uwe na misuli kama ARNOLD au handsome kivipi hamna show game wala huruma kuoneana in life.
 
Asante sana dada yangu,mawazo mazuri sana na yenye hekima....

Just a comment and not a critism!!!
Asante sana na wewe dada Michelle! Ningelipenda uniite Kaka, Baba au Babu yangu. Jina la Mammamia halina uhusiano wowote na jinsia yangu bali ni "interjection" ya Kitaliana yenye maana ya "Mama yangu!!!!". Tafadhali ingia kwenye Account yangu kwa maelezo zaidi.
 
hivi jaman tuwe wakweli tuache dead theories, hapa mjini hamna shamba la kulima mihogo na ndizi shamba ni ATM, hata uwe na misuli kama ARNOLD au handsome kivipi hamna show game wala huruma kuoneana in life.

Nafikiri unamaanisha kuwa ukiwa mjini kusiko na shamba then mwanaume lazima awe na hela......hakuna kuoneana huruma Marytina,issue hapa kwanza umpende mtu,na uangalie je anaweza kubadilika na kuwa na hizo fedha kama wengine,ana bidii na malengo sahihi kwenye maisha......mimi personally siwezi mpenda mtu kwa kigezo cha hela pekee,siwezi kuwa na Governor wa benki kuu mlevi,mzinzi au mgomvi...ila naweza kuwa na mtu alomaliza shule,anayejua alipo na anapotaka kwenda na ambaye nina uhakika tutasikilizana na atakuwa baba mzuri na mume.....again,siwezi kuwa na mwanaume tegemezi,labda awe anatafuta namna ya kuondokana na huo utegemezi nimsaidie kwanza.
 
Just a comment and not a critism!!!
Asante sana na wewe dada Michelle! Ningelipenda uniite Kaka, Baba au Babu yangu. Jina la Mammamia halina uhusiano wowote na jinsia yangu bali ni "interjection" ya Kitaliana yenye maana ya "Mama yangu!!!!". Tafadhali ingia kwenye Account yangu kwa maelezo zaidi.

Am sorry,maelezo yako yalinipa picha wewe ni mdada....samahani.
 
Back
Top Bottom