kilema
Member
- Feb 23, 2009
- 59
- 0
Wanawake viumbe wa ajabu sana. Brother yangu alisoma STATES na aliporudi mwaka 1999 alioa mke kutoka kijijini katika familia fulani masikini. mkewe huyo hakuwa amesoma hivyo kaka yangu alijitahidi kumsomesha hadi akamaliza chuo kikuu mwaka 2008. wkati wote huu maisha yao yalikuwa bomba upendo full full. Baada ya kumaliza shule mama huyu alibahatika kupata kazi kampuni moja ya nje na kila wakati anasafiri kwenda ulaya juu ya hayo mshahara wake ni bomba. Bahati mbaya mume wake alipunguzwa kazi katika shirika fulani mwaka jana na anatafuta kazi. Kwa hiyo bread winner kwa sasa ni mama. Kwa hali hii basi mwanamke amejiona kijogoo mume hasikilizwi tena. na zaidi ya hao ni dharau na kejeli kibao. Wewe mwanamme nimekulea sana, hutaki kutafuta kazi umeridhika sana, na matusi kibao. Tayari amesahau alikotoka. Tuwasaidieje kuokoa ndoa hiyo?