Ndg zangu mie bado ninatafakari habari za wa 16. Wazo langu ni kwamba huko. Tuliko tuhakikishe basi tunafanya kazi ya kufa na kupona kwa kukuwa mabalozi wazuri kwenye zoezi la kusimamia uhesabuji wa kura. Tukifanya hilijukumu vizuri tutakuwa tumefanya kazi kubwa yumkini kuliko kura moja tutakayo kuwa tumepoteza. Najua mgombea wetu mpaka sasa bado anakubalika vilivyo na bado tutaona moto siku zilizobaki! Shughuli kubwa sana sasa ninamna ya kulinda hizi kura. Kampeni tumepiga sana ila bado kuanza mbio si hoja tutakavyomaliza ndipo mchezo ulipo. Km nyerere alivyokomboa taifa hili kutoka kwa wa koloni nasi lazima tulikomboe kutoka kwa mafisadi wa ccm! Hamasisha vijana kujitokeza kusimamia na kulinda kura na fika ofc za chadema huko uliko saidia kutathmini hali na uwetayari kujitoa kusaidia organazesheni. Nawasilisha! Hatutalala mpaka kieleweke!!!!!!