Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Mmmh; wacha nisiongee mengi, nimeikuta hii kitu hapa:
Source: HarusiYangu.com...Tanzania's Wedding Portal
Source: HarusiYangu.com...Tanzania's Wedding Portal
TOPIC: hivi kwa nini mnatutukana
Habari zenu wana HY, hivi kwanini wanawake wenzetu mlio katika ndoa mnatutukana sisi ambao hatupo katika ndoa na tunawanaume zenu, ikiwa mnafahamu fika kuwa sisi sio watongazi, na hatuna uwezo wa kufosi hao mnaowaita waume zenu kuacha nyumba zote na kuja kwetu?
Maana jamani mnatakiwa mkumbuke kuwa sisi ni binadamu kama nyinyi, na tuna mioyo kama nyinyi, tumetongozwa kama mlivyotongozwa nyinyi na tukapenda kama mlivyopenda nyinyi ndio maana tupo nao.
Sasa kwanini mnatuita majina yote hayo watoto wa wanawake wenzenu wakati mnajua fika kuwa na sisi tuna mioyo kama yenu. na sio kosa letu?