Wanaume wote wa JF someni hii,mmoja wenu ndo kafanya haya

makaburini

Member
Dec 14, 2011
19
22
wanaume wa jf someni hii thread,na kwa sababu muhusika yupo humu basi ujumbe wake utakuwa umemfikia. Wiki ilopita kulikuwa na kauhaba ka mafuta ambako hakakuchukua siku nyingi, nikiwa njiani narudi kazini alinipigia simu dada mmoja ambaye tunafahamiana naye pamoja na mumewe akiniomba nimsaidie sababu gari lake halina mafuta, na yupo somewhere Morogoro road akiwa anatokea kazini na sheli za karibu hazikuwa na mafuta.

Nikapitia kumnunulia sheli moja nilipata taarifa kuwa inauza mafuta na ndipo nilipompelekea sehemu alipo na kumkuta mwenye majonzi lakini alijitahidi kutabasamu baada ya kuniona na baada ya kumuwekea mafuta nilimuuliza mumewe aliko akajibu kwa unyonge yupo kazini!

Nikamuuliza tena kwa nini usimwambie kwa kuwa hapa ni karibu na ofisini kwake dada machozi yakaaza kumtoka nikaamua nimuache aende!

Baada ya siku chache nilimpigia kumuuliza akaniambia shemeji, naishi bila matumaini bora ya mgonjwa wa ukimwi! Akasema kuwa siku ile alimueleza mumewe tatizo hilo akamjibu" kwa hiyo.......unataka nikusaidiaje.....kwani mimi nauza mafuta ya gari???

Kama uliweza kununua gari iweje ushindwe kulihudumia, kwanza mimi nina kazi zangu ofisini sina muda .........dada akaamua akate simu maana angeendelea kumsikiliza angemuumiza maana maneno yaliyokuwa yanatoka kwa mumewe wa ndoa ni makali.

Najiuliza hivi sisi wanaume hawa wadada wa watu huwa tunawaoa ili kuwakomoa? Au hatujui maana ya ndoa? Au ni ushamba? Utoto? Au ni ukatili tu tunaamua kuwafanyia?

alitaka amwambie nani amsaidie kama si mumewe? why jamani tunakuwa wakatili hivi?? aghhhhhhhhh

Hebu wanaume wenye hekima jf tusaidiane kumshauri mwenzetu naona hajielewi na haelewi majukumu yake.
 
Loh ndoa hii lazima
1. Wamechokana
2. Wakati wa tukio kulikuwa na jiugomvi
3. Nyumba ndogo inahusika.

Pole dada ila kuna wanaume wenye majibu ya kuumiza!
 
Kuna mambo mengi hapo na sio ugomvi tuu wa mafuta
Kuna kitu kingine kipo nyuma ya pazia na walishagombana sana
hapo ugomvi wa mafuta ulikuw akikolezo tuu
na inawezekana hata hilo gari huyo mume wa huyo dada hataki alitumie na limeleta mgogoro toka liliponunuliwa
 
mwambie awe anapanda dala dala na hilo janaume ni lazima liwe na umeme na mwanamke ni gumegume..by khadija kopa
 
Mumewe ndie waubavu wake, sasa anapojibiwa vya kukatisha tamaa jamani ndo iweje na akasaidiwe na nani?? Mkuu yawezekana kuna kinagaubaga hapo kati kimefichwa, wao waseme tu ukweli!!! MJ1.....nakubaliana nawewe, yawezekana uloyataja yakahusu!!
 
Kuna mgogoro katika familia hiyo, sio rahisi mtu kumjibu hvyo Mrs wake kama wako katika good terms. Hatahivyo, umesikiliza upande mmoja, sio vizuri kutoa maamuzi kwa kusikiliza upande mmoja tu. Fanya mpango usikilize na upande wa pili yaana mwanaume ili kuona chanzo cha majibu mabaya.

Huenda huyo Bi. Dada hakumshirkisha mumewe wakati wa kukunua hilo gari, labda mwanaume alishtukia gari nje kuuliza kulikoni, kajibiwa...................au Mwanaume alishirkishwa lakini kwa wakati huo kukawa na jukumu lingine la kufanya na hiyo pesa kama vile karo kwa watoto, kujenga nyumba, kulipia pango nk.....(ni mawazo yangu tu).

Na, je huyo mwanaume yeye ana usafiri?
 
wanaume wa jf someni hii thread,na kwa sababu muhusika yupo humu basi ujumbe wake utakuwa umemfikia.
wiki ilopita kulikuwa na kauhaba ka mafuta ambako hakakuchukua siku nyingi,nikiwa njiani narudi kazini alinipigia simu dada mmoja ambaye tunafahamiana naye pamoja na mumewe akiniomba nimsaidie sababu gari lake halina mafuta, na yupo somewhere morogoro road akiwa anatokea kazini na sheli za karibu hazikuwa na mafuta,nikapitia kumnunulia sheli moja nilipata taarifa kuwa inauza mafuta na ndipo nilipompelekea sehemu alipo na kumkuta mwenye majonz,i lakini alijitahidi kutabasamu baada ya kuniona na baada ya kumuwekea mafuta nilimuuliza mumewe aliko akajibu kwa unyonge yupo kazini! nikamuuliza tena kwa nini usimwambie kwa kuwa hapa ni karibu na ofisini kwake dada machozi yakaaza kumtoka nikaamua nimuache aende!

Baada ya siku chache nilimpigia kumuuliza akaniambia shemeji,naishi bila matumaini bora ya mgonjwa wa ukimwi!
akasema kuwa siku ile alimueleza mumewe tatizo hilo akamjibu" kwa hiyo.......unataka nikusaidiaje.....kwani mimi nauza mafuta ya gari???
kama uliweza kununua gari iweje ushindwe kulihudumia,kwanza mimi nina kazi zangu ofisini sina muda .........dada akaamua akate simu maana angeendelea kumsikiliza angemuumiza maana maneno yaliyokuwa yanatoka kwa mumewe wa ndoa ni makaln Najiuliza hivi sisi wanaume hawa wadada wa watu huwa tunawaoa ili kuwakomoa?au hatujui maana ya ndoa?au ni ushamba?utoto?au ni ukatili tu tunaamua kuwafanyia?alitaka amwambie nani amsaidie kama si mumewe? why jamani tunakuwa wakatili hivi?? aghhhhhhhhh
Hebu wanaume wenye hekima jf tusaidiane kumshauri mwenzetu naona hajielewi na haelewi majukumu yake.
KUna uwezekano kuwa kweli mumewe alimjibu hivyo... lakini pia kuna uwezekano pia kuwa unategwa wewe
 
Kuna mambo ya kwenye ndoa ukiyasikia hata kutamani ndoa inakuwa vigumu sana. Hivi hata kama mmegombana ndio mwenzio anapokuwa na shida huwezi kumsaidia hata mawazo tu? Inawezekana kweli asingeweza kumsaidia labda yupo kazini lakini hata maneno ya kutia moyo kidogo hakuna?????? Khaaaaaaaaaa!!!!!
 
upuuzi mtupu .yaani niishi kwa matumaini kisa wese? daladala zimeisha? je bajaji? je bodaboda? je punda? wanawake wengi wanaishia kujiuza kisa tu waonekane wanadrive
mtu anakuwa na wanaume kibao kisa gari
switi wa mafuta.
honey wa service
darling wa leseni
angel wa insurance nk nk
huyo jamaa yako yuko right kabisa ukinunua gari ujue na jinsi ya kulihudumia maana sio kitu cha muhimu sana hiyo ni luxury thing.kama huna huwezo achaaaaaaaaaaaaaa.
 
Mwanamke atakuwa kachuja tayari kwa mwanaume hapo hakuna jinsi ni kurenew tena penzi aanze utotoni kama mwanzo.
 
upuuzi mtupu .yaani niishi kwa matumaini kisa wese? daladala zimeisha? je bajaji? je bodaboda? je punda? wanawake wengi wanaishia kujiuza kisa tu waonekane wanadrive
mtu anakuwa na wanaume kibao kisa gari
switi wa mafuta.
honey wa service
darling wa leseni
angel wa insurance nk nk
huyo jamaa yako yuko right kabisa ukinunua gari ujue na jinsi ya kulihudumia maana sio kitu cha muhimu sana hiyo ni luxury thing.kama huna huwezo achaaaaaaaaaaaaaa.

Huwa nakupendaga sana kwa kuwapaga mashosti ukweli
hilo gari wakati anajinunulia mbona hakuombaga msaada si alijinunulia mwenyewe?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom