Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Jana nilikua natazama program ya mikas eatv.Wageni walikua Nakaaya na Nancy Sumary Nancy aliulizwa kuwa,ni kwa nini wanamitindo wengi boyfriend zao ni na wazungu,hakutoa jibu la kueleweka,lakini pia hata dada yake,Nakaaya ikaonekana ana kidume mweupe,kwani alipoulizwa alijiumauma. Serena Williams aliwahi kusema kuwa wanaume weusi hawajui mapenzi,hawajiamini na wana wivu wa kijinga.Mshirik wa BBA revolution,Mtanzania Elizabeth Gupta,aliwahi kuwaponda wanaume au vijana weusi,akadai hakuwahi kuwa na kidume mweusi,lakini nashangaa ameolewa na Kevin ambae ni mweusi! Hivi ngozi inaweza ikaathiri tabia ya mtu au ni ujinga wa hawa wanawake?Kuna ushahidi wowote wa kisansi wa kuthibitisha hili?Naomba ieleweke kwamba hao niliowataja hapo sio kipimo cha ufahamu au wao ni bora,hapana.Nimewatumia kama mifano kuelezea tatizo la kutokujitambu tulilonalo!