Mshiiri
JF-Expert Member
- Jun 16, 2008
- 2,012
- 507
Ni muda mrefu nimekuwa nafanya utafiti katika hii kanda ya mapenzi na kugundua kuwa wanaume wengi hufa kabla ya wake zao hata kama wamezaliwa mwaka mmoja na kubaini kuwa tabia za wake zao huwafadhaisha na kuwafanya waishi maisha magumu sana na kupata yale maradhi ya kufisha kama HYPERTENSION, SAIKOSISI, STROKE N.K
Madhanio wakati wa utafiti ni kuwa je wanaume wasio katika ndoa je wanashambuliwa sana na magonjwa haya ya kufisha kama cohort wao walio katika ndoa? Hatimaye ikabainika kuwa wasio katika ndoa ni wachache sana karibu na hamna ila walio kwenye ndoa ni wote, kama sio aina moja ni nyingine. Hitimisho likawa wanawake huchangia vifo vya mapema vya wanaume katika ndoa.
Je, ni kwanini? Hii ni sehemu nyingine wazi ya utafiti.
Je. kuna aliyefanya utafiti binafsi kuhusu hili na nini hatima yake?
Nawasilisha!
=========
Chris Mauki anasemaje?
Madhanio wakati wa utafiti ni kuwa je wanaume wasio katika ndoa je wanashambuliwa sana na magonjwa haya ya kufisha kama cohort wao walio katika ndoa? Hatimaye ikabainika kuwa wasio katika ndoa ni wachache sana karibu na hamna ila walio kwenye ndoa ni wote, kama sio aina moja ni nyingine. Hitimisho likawa wanawake huchangia vifo vya mapema vya wanaume katika ndoa.
Je, ni kwanini? Hii ni sehemu nyingine wazi ya utafiti.
Je. kuna aliyefanya utafiti binafsi kuhusu hili na nini hatima yake?
Nawasilisha!
=========
Chris Mauki anasemaje?
(Kwanini wajane ni wengi kuliko wagane??)
Mtalaamu saikolojia na mahusiano Dk. Chris Mauki anatoa sababu zifuatazo:
1. Umri mdogo wa kikomo cha maisha ' life expectancy':
Kama unafahamu hili jambo linaloitwa 'life expectancy'; utakubaliana na mimi kwamba umri wa mwanaume wa kuishi ni mdogo sana ukilinganisha na mke wake, hususani kusini mwa jangwa la sahara. Kwa hiyo wanawake wanapewa nafasi kubwa ya kuishi muda mrefu kuliko waume zao.
2. Ugumu katika kufunguka:
Utakubaliana na mimi kwamba wanaume ni wagumu sana ten asana kufunguka na kushirikisha mambo yao, wao wako tayari wafe na tai shingoni wakijifanya hawaumii au hawasikii shida. Mkiwa na ishu kwenye ndo mkaitwa sehemu muyaongee yeye kamwe hamumpati, anakwambia mambo yetu tutasuluhisha wenyewe wakati ndani yanamla na kummaliza. Na kwa mtaji huu watakufa sana tu
3. Ugumu katika kusamehe:
Kusamehe sio tu kwa faida ya anayesamehewa bali pia kwa afya yaw ewe unayesamehe. Mzigo unaotokana na kusamehe hutuumiza sana mioyo yetu, hata kama mara nyingine tunajifanya hatuna shida yeyote. Unaposamehe unaachilia mzigo mkubwa, wanaume wao ni wagumu sna kusamehe. Wako tayari wakubebe moyoni miaka, na tena watakukumbusha uchungu wao kila wanapokuona. Hii inawala sana bila wao kujua.
4. Tabia hatarishi:
Wanaume wengi kwenye ndoa ndio wanaoongoza kushiriki tabia hatarishi kama vile ulevi, anasa, ngono holela na hii huwaweka karibu zaidi na jeneza kuliko wake zao waliowaacha nyumbani wakiwadanganya kuwa wako mkutanoni mkoani.
5. Ugumu katika kujali afya:
Ni rahisi sana mwanaume akajisikia vibaya lakini asiende hospitalini kuangalia afya, hata pale anapohimizwa kwenda bado anaweza kukwepa au kubisha au hata kusema kuwa ameshakwenda au ameshakunywa dawa kumbe mwongo. Wako pia ambao wanaweza kupewa dawa na wasizitumie.
6. Msongo wa mawazo:
Wanaume ndio wabebaji wakubwa wa shehena za msongo wa mawazo 'stress' ingawa kwa nje wanajitahisi sana kuonyesha kuwa mambo yako shwari wakati wanatafunwa ndani. Kaulize hospitalini, wanaokufa kwa presha ya kupanda au ya kushuka, stroke, kusimama kwa moyo, kupasuka kwa mishipa ya damu, matatizo ya mifupa, au kuumwa sana kichwa, halafu uliza ni jinsia gani.
Maisha sio mabaya kiasi hicho, maisha ni mazuri. Chagua kuishi
Chriss Mauki
Pamoja na kwamba wanawake ndiyo wamekuwa wakielemewa na majukumu mengi na mazito kimaisha, lakini ni hao hao ambao wamethibitika kuishi kwa muda mrefu kuliko wanaume.
Kulingana na jarida la Human Nature la huko nchini Marekani ni kwamba tofauti hiyo ya umri wa kuishi kati ya wanaume na wanawake haikuanza jana wala juzi bali ni ya siku nyingi sawa sawa na historia ya binadamu mwenyewe.
Kwa hiyo ni suala la maumbile. Katika utafiti uliowahi kufanywa ulibaini kwamba tabia iliyopindukia mipaka ya kujihatarisha na kukandamiza mihemko ya kihisia kwa upande wa vijana wa kiume, inahusiana moja kwa moja na vifo vya mapema vya wanaume vijana na hata kupunguza umri wao wa kuishi ukilinganisha na wanawake.
Tabia nyingine ambazo pia zinawaweka wanaume kwenye hatari ya kufa mapema ni pamoja na uvutaji sugu wa sigara, ulevi, uendeshaji mbaya wa magari na vurugu nyingine.
Wanaume wengi wana maradhi ya kihisia kuliko wanawake, pamoja na kwamba inaonekana wanawake hukabiliwa sana na sononi za kimaisha.
Hebu chunguzeni kisha mniambie, ni akina nani wenye Kisukari, shinikizo la juu la damu, matatizo ya moyo, matatizo ya kiakili na mengine yanayofanana na hayo, kati ya wanaume na wanawake?
Kama mkifanya utafiti wenu kwa makini mtabaini kwamba ni wanaume.
Hebu niwaulize, hivi ni akina nani wanaokufa kwa kutafuta fedha au umaarufu kati ya wanaume na wanwake?
Jibu liko wazi. Ukisikia mwanamke ni jambazi utashngaa, ukisikia mwanamke ni tapeli, lazima utashangaa, ukisikia mwanamke mdhulumu mirathi, pia utashangaa. Kitakahokushangaza ni ugeni wa wanawake kwenye aina hiyo ya maisha.
Wanaume wengi wanaingia kwenye shughuli au tabia hizo hufanya hivyo kwa sababu wanataka kuthibitisha kwamba, wanaweza, wamefanikiwa na kuonesha tofauti yao na wanawake ambao hawajaweza. Wanataka kuwaonesha wanawake kwamba wamemudu.
Mwanaume huwa na umri mfupi kuliko mwanamke kwa sababu anataka kuwa mkuu, anataka kushinda na anataka kuonesha jamii kwamba, anastahili kuliko wengine.
Anaposhindwa kuonesha ndipo pale anapoingia kwenye tabia mbaya zaidi kama ulevi wa pombe, uvutaji bangi,utumiaji dawa za kulevya, na kupata sononeko na kusongeka kiakili. Yote haya yana madhara makubwa kwa afya na usalama wake. Yote haya yanamfupishia maisha yake. Anakuwa amechagua kuishi kwa muda mfupi kwa hiyari yake.